Maharage wa TANESCO atimuliwa kwenye kikao cha Waziri Mkuu Majaliwa na Naibu Waziri Mkuu Biteko. Apewa siku tatu

Atumbuliwe tu. Kwa nini walimtoa mtangulizi wake yule aliyekuwa anafanya vizuri. Asipotumbuliwa hatutamuelewa mteule wake.
 
Yaani hawa jamaa wamefanya nimeua vifaranga wengi sana kwa kujipa moyo umeme utarudi muda si mrefu

Hizi hasara ilitakiwa shirika liwe linazibeba ili wawe makini kwenye majukumu yao.

Haiwezekani changamoto ni zile zile miaka na miaka huku watu wakiingia hasara kubwa
 
Kipindi cha Prof Muhongo, umeme ulikoma kabisa kukatika na ulikuja kuanza kukatika tena baada ya Muhongo kumaliza muda wake. Ushahidi wa hili upo kwa sababu Muhongo yupo kule Bungeni

Kipindi cha Muhongo umeme ulikatika pale mwanzoni tu wakati akiwa bado ni mgeni, baada ya hapo hizo stori zilikoma kabisa.

Kwa hiyo Waziri akiwa mkali, umeme haukatiki, na akiwa mpole, umeme unakatika
 
Safi sana anapata wapi nguvu x kukaa High table wakati Nchi iko gizani. Kweli maharage uyo kama maharage yenyewe Takataka tu
 
Hivi akitimuliwa anaendelea kuwa mtumishi wa UMMA? hivi kazi za uteuzi kutoka nje ya Utumishi wa UMMA inampatia sifa ya moja kwa moja kuwa mtumishi wa UMMA baada ya uteuzi wake kukoma? Naomba kujua.
 
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ hiyo ya kulegeza tai imenivunja mbavu

Nimependa hicho alichofanyiwa yeye kama Mkurugenzi anakula tai anapenda kikaoni anakula per Diem huku watanzania wanahangaika na maisha umeme hamna biashara hawawezi kufanya

WATANZANIA tunataka umeme hatutaki bla bla za vikao waingie field wafanye kazi tuone matokeo
 
Hiki unachokisema kinawezekana endapo umeme utakua wireless!! Haya magunzo na manyaya ya TANESCO moja yanatukera, je yakiwa 5 times??
 
Dr magufuli ndio aliweza kumudu Hili la umeme msoga hi wizara hawaiwezi wao wanawaza kula na kuiba tu
 
Vitendea kazi hana tangu 2021 anafanya nini ofisini? Analipwa mshahara wa nini? Aachie nafasi
Aachie nafasi kwanini wasiachie nafasi CCM ambao wamekuwepo madarakani kwa muda wa miaka60 na wameshindwa kutatua matatizo ya nchi ikiwa ni pamoja na hili la umeme?.
 
Wewe acha ujinga umeme kukatika katika mara kwa mara unaona sawa?
Wewe acha upumbavu, si support hata kidogo kukatiwa umeme, Maharage ni kafara mmoja tu. Shughulisha akili yako ku pinpoint the point. Miaka hii kwa hatua ambayo dunia imefikia maendeleo ya kiteknolojia ni aibu kwa taifa kuwa na mgao wa umeme!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…