Mahari ni biashara ya utumwa. Kwanini dunia ipo kimya?

Mahari ni biashara ya utumwa. Kwanini dunia ipo kimya?

Unamaanisha nini kusema "ualisia" wa kibinadamu?

Mimi nasema katika Uislam, mahari ukiangalia maana yake na mafundisho kuhusiana nayo kisha ukaangalia mafundisho na Sharia kuhusu Ibada nzima ya ndoa, mahari sio biashara ya utumwa.

Sijui kwenu mahari ni nini. Lakini katika Uislam mahari ni zawadi anayopewa mwanamke na mwanaume anayetaka kumuoa ili kuonesha ukweli wa kutaka kwake kumuoa na ni jambo la wajibu lililowekwa na Allah katika Qur'an kama haki ya mwanamke. Na haisihi ndoa katika Uislam bila ya mahari.


وآ توا النساء صدقاتهن نحلة

“Na wapeni wanawake mahari yao…” (An-Nisaa: 4)

يا أيها النبي إنا أحللنا لك أزواجك اللاتي آتيت أجورهن

“Ewe Nabii! Tumekuhalalishia wake zako uliowapa mahari yao…” (Al-Ahzaab: 50)


فما استمتعتم به منهن فآتوهن أجورهن فريضة

“ … basi wale mnaowaoa miongoni mwao wapeni mahari yao yaliyolazimishwa…” (An-Nisaa: 24)


Na mahari haina kiwango maalum ni makubaliano ya wao wawili (akitaja mwanamke au mwanaume aki offer kisha mwanamke akakubali kwa hiyari yake) na ni haki ya mwanamke mwenyewe sio wazazi au walezi. Inaweza kuwa Mali au jambo jengine. Sio pesa tu na ng'ombe. Inaweza kuwa ni vitu mbali mbali kulingana na ada na makubaliano. Na ni mwanamke mwenyewe ndie anataja na kuridhia. Na ikapendekezwa mahari iwe ndogo

Kuna ambao wanatoa Pete kama mahari, kuna ambao walioa na mahari yao ilikuwa ni kile walichokihifadhi katika Qur'an (yaani kiwango walichohifadhi katika Qur'an ) ndio ilikuwa mahari nk.

Ngoja nikupe mfano mmoja tu kutoka zama za Mtume kukuonesha; wakati wa Mtume(SwallaAllahu 'Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam) kulikuwa na Swahaba anaitwa Abu Talha (Radhwiya Allahu 'Anhu), Abu Talha alitaka kumuoa Umm Sulaym (Radhwiya Allahu 'Anha), lakini wakati Abu Talha anamposa Umm Sulaym, alikuwa sio Muislam. Umm Sulaym akamuambia Abu Talha; "Wa Allahi, mtu mfano wako harejeshwi, ila wewe sio muislam na mimi ni muislam, na haiwi halali kwangu kuolewa nawe, ukisilimu hiyo ndio mahari yangu na sitotaka kengine zaidi ya hilo". Abu Talha akasilimu na kule kusilimu kwake ndio ikawa ni mahari ya Umm Sulaym (Allah awe radhi nao wote wawili).

Kuna ambao mahari waliyoiridhia ilikuwa ni viatu (ndala mbili) kama yule mwanamke kutoka kabila la Bani Fazara na Mtume akamuuliza kama ameridhia hilo, akamjibu kuwa karidhia.

Sijui nikufafanulieje mimi sio fasaha sana, ila elewa kuwa katika Uislam mahari ni tofauti na unavyoelewa wewe.

Kazakh destroyer




Allah anajua zaidi.
umemaliza yote akhy, hawa watu kwa kule kuwa wanapumua na wanapata rizki zao basi kunawapa kiburi cha hali ya juu mpaka wanaanza kuhoji taratibu alizoziweka allah kwa waja wake, sasa wameanza kuwaonea wivu wanawake kwenye mahari sijui wanataka wapewe wao?.
 
katika vijana wa hovyo huyu naye ni mmoja wao.

hii kitu hata vitabu vya dini vinakubali kuonesha kwamba ina uthamani sana kwa wote wawili.

kama hujui hilo mwanamke ambaye hujaenda kwao ukatoa mahari hata hawezi kukuheshimu kama mume wake sana sana kila ukikoroma atakuuliza umenitolea mahari ?

katika mada na mawazo ya kijinga toka mwaka umeanza hii kwangu ni namba moja
 
katika mada na mawazo ya kijinga toka mwaka umeanza hii kwangu ni namba moja
Kuliku hakuna sababu ya msingi ya wewe kushiriki katika mada hii, kama umeiona haina maana.
 
Uzuri hailazimishwi, ukishindwa unaachana nayo.

Sina hakika sana kama mwanaume aliyetimia sawasawa akishindwa kutimiza utaratibu wa kuoa anawezaje kuwajibika kwa familia?

Kuoa sio kuwa na uwezo wa kudindisha. Kuoa ni zaidi ya majukumu ya kifamilia.

Mwenyezi Mungu akujaalie watoto wa kike uwakuze wakifika wakati wa kuolewa wagawe bure bure tu.
Safi Sana [emoji2958][emoji2958]apime Kwa mizani kabisa aangalie na upande wake[emoji3577][emoji3577][emoji3539][emoji3539][emoji3539]
 
Mimi ni mwanamke, ila napinga sana swala la mahali! Namshukuru marehemu Baba yangu aliyekataa kutoza mahali akisema mwanangu siuzi! Mpaka kesho nitamuhsehimu kwa hilo! Kutoa mahali, tena wakati mwingine kubwa sana, haina maana kuwa mke ataheshimika; na kutotoa mahali, haimaanishi mke atadharauliwa, hakuna uhusiano wowte!
 
Kwa hiyo ndugu wazungu na waarabu walikuwa sawa kushirikana na machifu kuuza mababu zetu kwa kuwa thaminisha kwa viwango vya kifedha/mali kutokana na maumbile yao na nguvu walizo kuwa nazo ?
Kwani wazungu na waarabu hawana mahari?
 
Mimi ni mwanamke, ila napinga sana swala la mahali! Namshukuru marehemu Baba yangu aliyekataa kutoza mahali akisema mwanangu siuzi! Mpaka kesho nitamuhsehimu kwa hilo! Kutoa mahali, tena wakati mwingine kubwa sana, haina maana kuwa mke ataheshimika; na kutotoa mahali, haimaanishi mke atadharauliwa, hakuna uhusiano wowte!
Hakika wanawake aina yako ni wachache sana kwenye jamii, wenda wengi wao wana uelewa finyu wa mambo au malezi yame changia kuwa hivyo? sifahamu kwa kweli.

Kuna safari ndefu sana kupingana na hili jambo kwa kuanzia kwa waathirika wakubwa wa hili jambo ambao ni wanawake, wa napaswa kwa asilimia kubwa waji tafakari namna utu wao unavyo dharilika kupitia swala la mahari wenda tu hawa fahamu.
 
Utashangaa india wahindu wanawake ndio hulipa mahari,
Mahari ni zaidi ya ufikiriavyo wewe, hununui wala hakuna kuuzwa ndio maana mkishindwana anarudi kwao yaani mnaachana na wengine wanatengana
Jitahidi kusoma, kusoma ni kuelimika
 
Utashangaa india wahindu wanawake ndio hulipa mahari,
Mahari ni zaidi ya ufikiriavyo wewe, hununui wala hakuna kuuzwa ndio maana mkishindwana anarudi kwao yaani mnaachana na wengine wanatengana
Jitahidi kusoma, kusoma ni kuelimika
Moja wa msingi wa elimu kwangu ni kuya tafakari mambo mbali mbali kwenye jamii kwa kina zaidi tofauti na jamii inavyo yatafakari na kuya tafsiri kwa hiyo usitilie shaka kuhusu swala la mimi kujielimisha maana ndio kitu nachopenda sana maishani.

Swala la mahari nimeli tafakari kwa kina kuliko unavyo dhani ndio maana maoni yangu yamekuwa tofauti kwa asilimia kubwa na jamii inavyo lichukulia jambo kiwepesi.
 
S
Moja wa msingi wa elimu kwangu ni kuya tafakari mambo mbali mbali kwenye jamii kwa kina zaidi tofauti na jamii inavyo yatafakari na kuya tafsiri kwa hiyo usitilie shaka kuhusu swala la mimi kujielimisha maana ndio kitu nachopenda sana maishani.

Swala la mahari nimeli tafakari kwa kina kuliko unavyo dhani ndio maana maoni yangu yamekuwa tofauti kwa asilimia kubwa na jamii inavyo lichukulia jambo kiwepesi.
Sawa, hongera kwa kusoma, labda hujasoma quran na biblia,
Wala usingehangaika na suala la mahari lisingekusumbua

Au freemanson?
 
S

Sawa, hongera kwa kusoma, labda hujasoma quran na biblia,
Wala usingehangaika na suala la mahari lisingekusumbua

Au freemanson?
Asante kwa mchango wako, kuhusu freemason jibu ni hapana sifungamani na huo upande.
 
naona unanipangia cha kufanya sasa baada ya kuninunulia bundle 😀
Hakuna mahali nilipo kupangia wewe matumizi ya data zako lakini kwa busara zaidi kulikuwa hakuna ulazima wa wewe kushiriki kwenye hii mada ya kijinga.
 
Back
Top Bottom