Mahojiano yangu na washirika wa FDLR kuhusu uhasama wao na RPF- Inkotanyi

Mahojiano yangu na washirika wa FDLR kuhusu uhasama wao na RPF- Inkotanyi

Kama mwandishi wa habari huru nilikua nachunguza viini vya migogoro katika maeneo ya ukanda huu wa maziwa makuu.

Nilibahatika kufanya mahojiano ya kina na washirika wa iliyokua serikali ya Rwanda kabla ya kupinduliwa mwaka 1994.

Watu wengi hawawezi kujua kua,karibia majenerali wote wa iliyokua serikali ya Rwanda mwaka 1994 walikimbilia nchi ya Zaire kabla ya baadhi yao kwenda ughaibuni kuishi.

Nilibahatika kufanya nao mahojiano kuhusu kupinduliwa kwao na wanajisikia vipi kupinduliwa na kuishi ukimbizini.

Niliwauliza je wanajihisi vipi na wao kufukuzwa kwa mtutu wa bunduki hadi ukimbizini na wale watu waliokua nao wamekimbizwa ukimbizini kwa mtutu wa bunduki.

Niliwauliza kuhusu mauaji ya kimbari na kikabila dhidi ya watusi wengi na wahutu wachache.

Niliwauliza kuhusu chuki waliyokua wanaipandikiza kama watawala kwa wananchi ili kuleta machafuko.
Niliwauliza kuhusu ukabila baina ya watusi na wahutu na wakati wote wanaongea lugha moja kinyaruanda.
Niliwauliza kuhusu mipango yao baada ya kupinduliwa ipoje.

Niliwauliza kuhusu wanajisikiaje wanapotuhumiwa kama wapangaji wa mauaji ya kimbari dhidi ya binadamu wenzao.
Niliwauliza kuhusu vikosi vya wanamgambo makatili na wauaji wa intarehamwe.

Niliwauliza kuhusu mahusiano yao kisiasa na nchi jirani.

Nitakua nawaletea kwa vipengele hayo mahojiano yangu yote na vizazi vya wanajeshi wa iliyokua RAF (Rwanda Armed forces) kabla ya kupinduliwa na RPF forces mnamo mwaka 1994.

Mahojiano yanajumuisha mambo mengi ya kiuchumi na kisiasa na kitamaduni.

Na kuna ukweli ambao watu wengi hawaufahamu na hata kama unafahamika basi watu hawapendi kuuzungumza.

KABLA YA MFULULIZO WA MAHOJIANO YANGU NA WASHIRIKA WA FDLR NITAANZA NA HISTORIA FUPI YA MUHUSIKA MMOJA KAMA ALIVYONIADITHIA.

June 16 saa tatu usiku kwenye eneo la Gatuna au kwa kinyarwanda Katuna mpakani mwa Uganda na Rwanda 1987.

Kulikua na mkutano wa nje ya kambi kwenye upande ule wa mlimani kwenye mji ule wa mpakani.Na mkutano wenyewe ulikua wa makanali wa jeshi na wanajeshi wa vyeo vya chini waliokua wanaifuatilia hali ya wasiwasi mpakani katika mji wa Gatuna upande wa mpaka wa Uganda.

Taarifa za kijasusi za jeshi la Rwanda zilikua zinasema kua,wakimbizi wa kinyarwanda waliokua upande wa nchi ya Uganda walikua wanajiandaa kuivamia nchi ya Rwanda.Taarifa zilisema kua wanyarwnda ambao wamesajiliwa katika jeshi la NRM la Uganda walikua wanaondoka jeshini kwa kasi na kuenda kuunda vikosi vya kijeshi ili kuishambulia Rwanda.

ITAENDELEA.............!!!!!!
ushauri aliotoa kikwete ndio ulikuwa the best. FDLR ni wanyarwanda, huwezi kuwafukuza nchini wakae uhamishoni milele kama kagame alivyoishi uhamishoni zaidi ya 30 years, halafu ukasema upo salama. kuna siku tu wao au watoto wao au wajukuu zao watakuja kukurudia na wewe unaweza kufukuzwa ukaishi uhamishoni miaka hiyo vilevile. la maana aliloshauri kikwete lilikuwa ni wakutane, wasameheane, waishi pamoja kama wanyarwanda, hiyo haingempunguzia chochote kagame kwasababu tayari yeye ni rais. maadamu wapo msitu wa congo ambako kuna waasi kibao na kagame mwenyewe alishaishi msitu wa congo, watoto wao watakuwa wazoefu wa vita sana huko kwa waazi na kuna siku watarudi rwanda kwa kishindo. sema kagame anafadhili m23 ambao ni watusi wenzie ili wawe wanapunguza nguvu, sasa hatujui kama m23 watadumu milele na kama hatatokea nchi yeyote duniani adui wa kagame akafadhili FDLR ili kumkomesha kagame. amevaa mabom bila yeye kujua.
 
SASA TUENDELEEE...................!!!
SAFARI YA KANALI""F"" KURUDI NYUMA MPAKA MJI WA KAMEMBE NEAR ZIWA KIVU.
Haikua kitu rahisi kwa kanali f kurudi nyuma mpaka mji wa Kamembe.
Kwanza alikua na uchungu mkubwa moyoni katika vitu vikuu vitatu.
MOSI: Yeye aliamini kua rwanda imetumbikizwa kwenye vita na mauaji na wanasiasa wenye uchu wa madaraka.Na aliamini kabisa wakuu wake wa kijeshi walimgeuka hasa katika yale makubaliano ya Arusha Tanzania ya kusitisha vita.
PILI: Kanali au afande"f"aliamini kua waasi wa RPF wamemsaliti kwa yale yote waliyokubaliana mwaka 1987 na 1992 na nia yao ilikua ni kuchukua nchi na kumfukuza yeye na wahutu wwngine nao wakaonje adha ya kua wakimbizi ughaibuni.
TATU: Aliamini wafaransa walihusika na kupanga mauaji ya kimbari kwa kuwashawishi wakuu wake wa kijeshi kutekekeza mauaji hayo na vivile walihusika na kumuua raisi Juvenal ambae alikua bosi wake na alikua anamlinda mpaka siku ile aliyosafiri kwenda nchini Tanzania.
NB: KUMBUKA YEYE KANALI ALIKUA ANAMLINDA RAISI AKIWA ARDHINI NA SIO ANGANI...JUKUMU LA KUMLINDA RAISI AKIWA ANGANI HALIKUA LAKE YEYE.
Anasema raisi Juvenal alimwambia maneno haya kabla hajapanda ndege kwenda mjini Dar es salaam nchini Tanzania.
""""""""NAMNUKUUU""""""""""""""
JUVENAL : Kanali kama unavyoona hii hali ya kivita sio nzuri upande wetu na hata hawa wanajeshi 600 wa RPF waliopo hapa Kigali mimi siwaamini kabisa katika lolote,,,,maana wapo karibu na uwanja wa ndege,hivyo wanaweza kuniua wakati wowote.
AFANDE""F"": Mkuu najua na ningekushauri ukirudi kutoka Tanzania basi makao yako makuu yahamishie mjini Gitarama.
JUVENAL: Sawa Kanali nimekuelewa na nikirudi tutajadili hili suala kwa kina.
AFANDE""F"": Nikutakie safari njema mkuu
JUVENAL: Ilinde familia yangu kwa gharama yoyote ile Kanali sawa.
JUVENAL: Ni aibu sisi kushindwa na RPF na sura yangu nitaiweka wapi.
JUVENAL: Tafadhali Kanali ilinde familia yangu kwa gharama yoyote ile.
JUVENAL: Najua wewe na Aghata mna tofauti zenu,,lakini usisahau yule ni mke wangu na usisahau pia wewe ni mdogo wangu Kanali.
JUVENAL: Na tumetoka mbali sana mdogo wangu toka nilipokutoa jeshini miaka ile
AFANDE""F"": Sawa Mkuu (copied) huku akipiga saluti na hiyo ndio ilikua saluti yake ya mwisho na mazungumzo yake ya mwisho na raisi Habyarimana akiwa hai ikulu.
Afande anasema na hili lilikua linamuuma sana sababu alijua mkuu wa vikosi vya kulinda wanadplomasia wa RPF waliokua Kigali kwa mujibu wa makubaliano ya amani ya Arusha.
Brigedia Rwegema alihusika na mauaji ya Rais Juvenal.
NB: Brigedia Rwegema na yeye aliuawa katika mazingira ya kutatanisha wakati waasi wa RPF wanaichukua na kuidhibiti Kigali.
Basi afande""f""aliendelea na utaratibu wa kujihami huku akirudi nyuma mpaka mji wa Kamembe akiwa na askari makomandoo 1800 na malori ya kijeshi 116 na magari ya deraya 66 na maroli ya kawaida 75 na vifaru 14 na askari wa miguu wasiokua makomandoo zaidi ya 3000,hapa ukijumuisha na vikosi vya wanamgambo wa kiraia ambao ni tofauti na intarehamwe militias.
Hakutaka kupigana au kuzuia waasi wa RPF kuchukua miji ya Rulamba na Kitabi sababu aliona hakuna sababu ya kupoteza nguvu kazi kwa jambo lisilowezekana kwa namna yoyote ile iwe kiualisia au kidhaaniana maana tayari kimahesabu walikua wameshashindwa vita na RPF.
Mnamo tarehe 26 january 1994 ilimkuta afande ""f"" akiwa mjini Kamembe akiwa amechoka na amepoteza mawasiliano kati yake na wakuu wake wa kijeshi.
NA WAZO KUU LILIKUA NI KUVUKA ZIWA KIVU NA KUINGIA ZAIRE NA KUJIPANGA UPYA KIJESHI NA KUANZISHA UPYA MAPIGANO ILI KURUDISHA NYUMA VIKOSI VYA RPF VILIVYOKUA VIMETAMALAKI NCHI NZIMA YA RWANDA MPAKA WAKATI HUO JANUARY 26 1994
Na alichukua simu ya upepo na kumpigia rafiki yake wa zamanj na adui yake kwa sasa PAULO mjini Kigali na kusema maneno haya.
AFANDE: PAULO UMENISALITI
PAULO: KANALI WALIOKUSALITI NI RDF WOTE KWA KUSHINDWA KUPIGANA KWENYE UWANJA WA MAPAMBANO NA KUISHIA KUUA RAIA WA KITUSI
AFANDE: HUKUTIMIZA WAJIBU WAKO
PAULO: NI KWELI ILA NDIO SIASA HIZO
AFANDE: NA ULIBUNI MAUAJI YA HALAIKI
PAULO: UNA USHAHIDI KANALI??
AFANDE NDIO PAULO NINAO
PAULO:UR DEAD KABLA HAUJAONEKANA
AFANDE: NIFE MARA NGAPI PAULO?
PAULO: UNANIJIBU KWA UJEURI SABABU YA HUYO MZEE MOBUTU?
NINA VIKOSI HUKO KIVU NA VINASUBIRI TU AMRI YANGU KUMSHAMBULIA HUYO MZEE MLA RUSHWA
AFANDE: WE ARE ENEMIES NAKUJIBU HOW I FEEL TOWARDS YOU
AFANDE: KWA SABABU ULINISALITI BASI HAUTOKAA KWA AMANI TAKE THAT CARD YOU PLAYED ONCE.
PAULO: HABARI ZA RWEGEMA UNAZO?
PAULO: BAS NA WEWE UTAISHIA HIVYO
AFANDE: NIMEKUPIGIA SIMU KUKUAMBIA BADO SIJAFA NIPO NA NINAONDOKA NDANI YA RWANDA KWA SASA ILA NITARUDI MDA SI MREFU NA WEWE UNAJUA HILO.
NA KAMA ULIMUUA REGWEMA,HUO NI UOGA WAKO NA TAMAA ZAKO ZA MADARAKA PAULO NA MIMI HILO HALINIHUSU.
BAS AFANDE"F""AKAKATA SIMU YAKE YA UPEPO NA IKUMBUKWE HAPO ALIKUA MJINI KAMEMBE NJE KIDOGO YA ZIWA KIVU NA HIYO ILIKUA JANUARY 26 1994.
NA HII SIKU NDIO WAZO LA FDLR LILIPOZALIWA KICHWANI MWA KANALI AU AFANDE""F"""
ITAENDELEA...............!!!!!!!!!!
Hahahahah, nice , paul vs afande F ,hongera Jacob kwa uzi mzuri
 
ushauri aliotoa kikwete ndio ulikuwa the best. FDLR ni wanyarwanda, huwezi kuwafukuza nchini wakae uhamishoni milele kama kagame alivyoishi uhamishoni zaidi ya 30 years, halafu ukasema upo salama. kuna siku tu wao au watoto wao au wajukuu zao watakuja kukurudia na wewe unaweza kufukuzwa ukaishi uhamishoni miaka hiyo vilevile. la maana aliloshauri kikwete lilikuwa ni wakutane, wasameheane, waishi pamoja kama wanyarwanda, hiyo haingempunguzia chochote kagame kwasababu tayari yeye ni rais. maadamu wapo msitu wa congo ambako kuna waasi kibao na kagame mwenyewe alishaishi msitu wa congo, watoto wao watakuwa wazoefu wa vita sana huko kwa waazi na kuna siku watarudi rwanda kwa kishindo. sema kagame anafadhili m23 ambao ni watusi wenzie ili wawe wanapunguza nguvu, sasa hatujui kama m23 watadumu milele na kama hatatokea nchi yeyote duniani adui wa kagame akafadhili FDLR ili kumkomesha kagame. amevaa mabom bila yeye kujua.
Sasa kuna kizazi cha 1994 nacho kipo uhamishoni wanataka kurudi ,wkt huo Paulo anataka kutoa madaraka kwa kizazi cha umri huo lkn kilichotoka uhamishoni
 
ushauri aliotoa kikwete ndio ulikuwa the best. FDLR ni wanyarwanda, huwezi kuwafukuza nchini wakae uhamishoni milele kama kagame alivyoishi uhamishoni zaidi ya 30 years, halafu ukasema upo salama. kuna siku tu wao au watoto wao au wajukuu zao watakuja kukurudia na wewe unaweza kufukuzwa ukaishi uhamishoni miaka hiyo vilevile. la maana aliloshauri kikwete lilikuwa ni wakutane, wasameheane, waishi pamoja kama wanyarwanda, hiyo haingempunguzia chochote kagame kwasababu tayari yeye ni rais. maadamu wapo msitu wa congo ambako kuna waasi kibao na kagame mwenyewe alishaishi msitu wa congo, watoto wao watakuwa wazoefu wa vita sana huko kwa waazi na kuna siku watarudi rwanda kwa kishindo. sema kagame anafadhili m23 ambao ni watusi wenzie ili wawe wanapunguza nguvu, sasa hatujui kama m23 watadumu milele na kama hatatokea nchi yeyote duniani adui wa kagame akafadhili FDLR ili kumkomesha kagame. amevaa mabom bila yeye kujua.
Upo sahii mkuu
 
Mkuu kwanza FDLR NI SEHEMU YA VIKOSI VYA WANAJESHI WA SERIKALI YA RWANDA ILIYOPINDULIWA.
RPF MWAKA 1996 WALIVAMIA ZAIRE NA KUANZA KUUA WAHUTU WAFUASI WA FDLR NA IKABIDI FDLR WAJIHAMI KWA KUUA WATUSI WA VILIMA VYA MULENGE.
KATIKA SIASA HAKUNA ADUI WA KUDUMU NDIO MAANA FDLR WALIUNGANA NA MZEE KABILA AMBAE MWAKA 1996 -1999 ALIKUA ADUI YAO
NB:ALIR NI TAWI LA WALIOJITENGA NA FDLR NA HII NI HABARI NDEFU SANA INAHITAJI UZI WAKE PEKEE
NB: ASKARI WOTE WA KIHUTU WALIOJIUNGA NA RPF HAWAKUA NA MAISHA MAREFU JESHINI.
Mkuu ina maana RPF ni jeshi la Watusi pekee?
 
Mkuu kwanza FDLR NI SEHEMU YA VIKOSI VYA WANAJESHI WA SERIKALI YA RWANDA ILIYOPINDULIWA.
RPF MWAKA 1996 WALIVAMIA ZAIRE NA KUANZA KUUA WAHUTU WAFUASI WA FDLR NA IKABIDI FDLR WAJIHAMI KWA KUUA WATUSI WA VILIMA VYA MULENGE.
KATIKA SIASA HAKUNA ADUI WA KUDUMU NDIO MAANA FDLR WALIUNGANA NA MZEE KABILA AMBAE MWAKA 1996 -1999 ALIKUA ADUI YAO
NB:ALIR NI TAWI LA WALIOJITENGA NA FDLR NA HII NI HABARI NDEFU SANA INAHITAJI UZI WAKE PEKEE
NB: ASKARI WOTE WA KIHUTU WALIOJIUNGA NA RPF HAWAKUA NA MAISHA MAREFU JESHINI.
Hawakuwa na maisha marefu jeshini kwanini? Waliuwawa? Au walifukuzwa?
 
NB:ALIR NI TAWI LA WALIOJITENGA NA FDLR NA HII NI HABARI NDEFU SANA INAHITAJI UZI WAKE PEKEE
Hizo sababu za wao kujitenga na Fdlr unaweza kututajia kwa uchache ?


ASKARI WOTE WA KIHUTU WALIOJIUNGA NA RPF HAWAKUA NA MAISHA MAREFU JESHINI.
Baada ya Rpf kudhibiti nchi, Kuna uasi bado uliendelea hivyo baadhi ya askari wa jeshi la Habyarimana waliingizwa kwenye vikoai vya Rpf na kupewa vyeo ili kuzima huo uasi, vipi sasa hawakudumu?

Bizimungu alikuwa mhutu mwenye cheo ndani ya Rpf, kipi kilimsibu mpaka kutofautiana na makamu wake mwenye nguvu ?

zitto junior
 
Back
Top Bottom