Mahojiano yangu na washirika wa FDLR kuhusu uhasama wao na RPF- Inkotanyi

Mahojiano yangu na washirika wa FDLR kuhusu uhasama wao na RPF- Inkotanyi

Mpunguze ujuaji humu huyu jamaa asipopost mimi na wanangu huwa tunamfuata mpaka anaposhindia kubishana huko jukwaa la hezbooolah na kina Hamas ,akija hapa mtu anaanza kutoa vitisho mara utauliwa mara hiki ina maana huyu jamaa kwa taarifa hii anayotoa hapa hajui kama kuna madhara? Muacheni atiririke na hajapost mpaka muda huu subirini hapa hapa najua alipo
We usikae unatisha watu humu,we nani kwanza?
Unaweza kufikiwa kabla hujaanza hizo ujinga ujinga,jibu hoja kwa hoja humu.
 
We usikae unatisha watu humu,we nani kwanza?
Unaweza kufikiwa kabla hujaanza hizo ujinga ujinga,jibu hoja kwa hoja humu.
Unatumia nini kufikiri wewe? Wapi nimetisha mtu hebu toka hapa mimi ndio nimeandika watu waache vitisho "anko " atiririke unaleta ujuaji wako hapa kuwa na adabu wewe tena ukiniquote tena kwa upuuzi puuzi wako huo
 
INAENDELEA..........!

Ukiwa nchini Rwanda mwaka 1987 kuna usemi mkubwa ulikua unaenea miongoni mwa vikosi vya wanajeshi wa jeshi la serikali kwa mujibu wa afande ""F"" nao usemi huo ulikua unasema kua Wafaransa wanataka kuigawa nchi kwa watusi na ikumbukwe kua asilimia 100% ya wanajeshi walikua ni wahutu na jambo hili lilikua linaondoa weledi wa kijeshi kwa jeshi la Rwanda na kuleta ukabila kwa mujibu wa afande""F"".

Afande ""F""ambae alikua na cheo cha ukanali anasema baada ya kuwasilisha ripoti yake ya kijasusi mbeke ya komandi kuu ya kijeshi, alitoa pia ripoti ya mapendekezo kuhusu nini kifanyike ili kuweka mambo sawa mahali palipoyumba.

Na alisisitiza kua jeshi lisichanganywe na siasa za nchi husika. Baada ya hapo afande ""F""alirudi mpakani mjini Katuna kuendelea na kazi yake ya kulinda mpaka wa nchi ya rwanda.

DECEMBER 14 1987 KATUNA RWANDA.
Ilikua usiku mida ya saa nne na robo wakati ambao kanali afande""F"" alikua ndio anamalizia mlo wa chakula cha usiku ili akatazame ripoti ya ulinzi afu apumzike,alipopokea simu ya upepo (Radio call) ikimueleza kua kuna magroup ya vikundi vya watu wenye silaha wamevuka mpakani upande wa Uganda kitongoji cha kihunda na wameingia ndani ya aridhi ya rwanda wakiwa na maguruneti ya kurusha kwa mkono na maroketi ya kutungulia ndege na maroketi ya kuzuia vifaru na ni watu ambao kwa idadi yao hawazidi watu 800.

Afande "F" aliamka akavaa mkanda wake wa risasi za akiba kiunoni na akaijibu ile redio upepo kua kila komandi iandae ambushi au shambulio la kuvizia kama wale watu watavuka kilometa tatu kutoka mpakani na wawazingire kutokea upande wa mlimani wa kihunda na wasiwashambulie mpaka akitoa idhini.

Yeye binafsi alipanda Jeep ya kijeshi na kuifanya iwe komandi station yake kufuatilia hali yote nzima,,na kuripoti pia katika kamandi kuu mjini Kigali.

Kulikua na ukimya mkubwa ila baada ya dakika ishirini na saba ,,alipokea tena simu ya upepo ikisema upande ule wa kihunda mlimani kua wapo katika mfululizo wa mashambulizi ya risasi na roketi na maguruneti kutoka kwa vikosi vilivyoripotiwa mwanzo kuingia na vilikua vimevaa sare za jeshi la uganda,na walikua wanaacha maeneo yao na kurudi nyuma ili kuzuia maafa zaidi maana walikua wanazidiwa nguvu na wale watu waliowavamia.

""""""Namnukuu Afande F """"""
Hali ilikua tete maana vile vikosi vilivyovuka mpaka kutokea uganda vilikua na silaha bora na uzoefu wa kupigana milimani kuliko vijana wetu tuliokua tumewaweka jeshini mwaka huo na wengi wao hawakupata mafunzo ya kutosha kuhusu mapambano ya uwanja wa vita,bali mafunzo ya kulenga shabaha tu na mafunzo ya utimamu wa mwili na akili kama wanajeshi.

"""""Nimemaliza kunukuu"""""""
Afande F akaamua aombe usaidizi wa kikosi anga cha jeshi la Rwanda kikichokua kipo uwanja wa ndege kigali na pia kwenye uwanja wa ndege wa kijeshi katika kambi ya kijeshi ya Kamina ili apatiwe helikopta za mashambulizi ya angani na ndani ya lisaa limoja zaidi ya helkopta 11 zilikua tayari zipo uwanja wa mapambano kwenye mlima kihunda zikiwashambulia watu waliovuka mpaka kuishambulia rwanda kutokea Uganda na wakafanikiwa kuwarudisha nyuma na kuua wengi kati yao,,ila na wao walikua wamepata hasara za kutosha za maisha ya watu na mali katika post zao za mpakani upande ule wa mpakani ambapo mashambulizi ndipo yalipotokea.

Ikumbukwe kua kama anavyosema afande""F"" zile helikopta zote za kufanya assaulting zilikua zinaendeshwa na marubani wa kifaransa kutoka katika jeshi la anga la ufaransa lililokua na kituo katika uwanja wa ndege wa Kigali.

Afande ""F""anasema cha ajabu aliambiwa hili tukio asilitangaze kwa mtu yoyote yule na iwe siri raia wasijue kama habari rasmi bali uvumi.

Kwa mara ya kwanza hiyo December 14 1987 ndio kanali au afande""F"" alipambana na wanaharakati wa rwanda patriotic front wakitokea ndani ya jeshi la uganda waliojaribu kijeshi na kwa mapambano ya kurushiana risasi kuvuka mpaka na kuingia nchini rwanda wakitokea uganda kwa upande ule.Walikua wamejizatiti kwelikweli na haikua rahisi kuwarudisha nyuma bila msaada wa wanajeshi wa jeshi la anga la ufaransa.

PAULO JACOB KAGAME!
Huyu alikua ni nani na movement yake ya TWEHEZA ilikua inahusu nini na kwanini alikua na mahusiano ya karibu na serikali zote tatu za Uganda na Zaire na Rwanda kwa wakati ule.Na kwanini alikua mshirika mwaminifu wa afande""F"" katika medani ya ujasusi kwa kipindi cha miaka tisa mpaka mwaka 1990 walipokorofishana.

Paulo alikua mfanyabiashara na mwanajeshi pia na jasusi pia na mwanasiasa pia kwa wakati huo huo.
Paulo alikua mtu wa kuzitazama fursa kwa jicho la mbali na kuzikimbila. Paulo alikua mshirika aliyeaminika wa CIA na MOSSAD na M-15 na kuna nyakati alishirikiana na KGB na TISS kama. double agent.

Paulo aliweza kujinasibu kama mtu wa kuaminika wa serikali ya Rwanda toka mwaka 1982.Ni yeye pekee tu aliyekua na acsess ya kupata direct instructions kutoka kwa raisi,akiwazidi hata wale majasusi waliokuepo ndani ya serikali na aliaminiwa na jeshi hadi mwaka 1990 alipowasaliti kwa mujibu wa afande""F""

Tutaijadili movement ya TWEHEZA huko mbele ili tuifahamu. Baada ya tukio lile la mwezi December tarehe 14 mwaka huo 1987 basi hali ya mpakani mwa uganda na rwanda ikabadilika na kukawa na ongezeko la vikosi vya wanajeshi wenye uzoefu na vifaa katika mpaka huo hasa upande wa rwanda.
Katika mahojiano yetu afande""F""anasema kua wakati yeye yupo jeshini,pia kulikua na hisia za ukabila za hali ya juu baina ya jamii mbili kubwa za Watusi na Wahutu.

Na hili lilichangiwa na wanasiasa wa kinyarwanda waliokua na uchu wa madaraka.

ITAENDELEA....!
Safi sana,historia nzuri hasa.
 
KAMEMBE NEAR LAKE KIVU.......!!!
NAENDELEA.........!!!
Afande"f" anasema kua aliona hakuna maisha tena Rwanda kwa wakati ule,maana uwepo wa wanajeshi wa umoja wa mataifa na wanajeshi wa ufaransa na wa uganda na ushindi wa vikosi vya RPF ulimfanya plan A aliyokua nayo aachane nayo na afuate plan B.
Toka mjini Kamembe plan ikawa ni kuvusha magari yote ya kijeshi na vifaru na yale marolo ya logstic kwa kupitia njia isiyo rasmi ya Cyangugu,ila wale wanajeshi kikosi kizima wakavuka upande ule wa ziwa mpaka upande wa pili wa nchi ya Zaire.
Shughuli hii nzito ilimchukua wiki nzima kuhakikisha kila kitu kinaenda sawa na wakati huo huo alikua anazuia askari wa RPF wasiweze kumsogelea mjini Kamembe na alituma vikosi vya asikari kulinda barabara kuu ya kuingia mjini Kamembe mpaka pale atakapomaliza kuvivusha vikosi vyake na silaha salama mpaka upande wa pili wa ziwa Kivu hadi mjini Bukavu.
Na ikumbukwe kwa wakati huo Zaire ndio ilikua inaongoza afrika kwa kua na mtandao wa barabara mbovu sana kuliko maelezo.
Na kutokea upande ule wa kusini mwa ziwa Albert vikosi vya afande""f""_vilijisogeza mpaka upande wa Zaire katika mji wa Bukavu.
Na alipofika mjini Bukavu akawakuta wakuu wake wa kijeshi,chini ya serikali ya mpito iliyokua inaongozwa na raisi aliyepinduliwa na RPF Theodore Sindikubwabo.
Mzee Sindikubwabo mpaka anafariki yeye alikataa kabisa kukubali kua yale mauaji ya watusi yalikua genocide.Bali yeye anadai ilikua self defence ya wahutu.
Alikua ni bingwa wa kufanya mahojiano na alikua mtaalamu wa kukwepa maswali magumu na bingwa wa kuhalalisha chochote kile ambacho serikali yake ya mpito ilikifanya nchini Rwanda na hakujutia kwa lolote lile kwa kumaanisha
Maana alikua anapenda siasa za kinafiki sababu ya uchu wa madaraka
THEODORE SINDIKUBWABO
Mzee Theodore Sindikubwabo yeye alishiriki na kuandaa mikakati ya kuua watusi na alishirikiana na tajiri mkubwa mjini Chigali (Kigali) enzi hizo aitwae Felix Kabuga.
Hawa kwa kushirikiana na watu wengine wenye ushawishi kama Mama Agatha the first lady.
Mzee Sindikubwabo alikua na roho ya kikatili sana ,sababu alishuudia mauaji ya raia hasa watusi mjini Gitarama na mjini Kigeme,lakini yeye kama raisi wa mpito hakuwakemea intarehamwe waache kuua watu bali aliwachochea.
Na hii ndio ilifanya na wanajeshi wa RPF kua wanawaua wahutu kwa kulipiza kisasi,kwao ule mwaka waliochukua nchi kila muhutu alikua Intarehamwe,haijalishi ni mtoto au mtu mzima.
Huyo ndio mzee Theodore Sindikubwabo mwanasiasa aliyekimbilia Bukavu na serikali yake ya mpito na ambae afande""f"" anasema hakumuamini kabisa katika lolote ila halimueshimu kama mkuu wake wa kiheshi.
MAMA AGATHA.
Huyu alikua ndio mratibu wa mipango yote ya wanasiasa wenye misimamo mikali ambao walikataa kabisa kufikiria au kuwaza kua ipo siku watakuja kuondolewa madarakani na mahasimu wao kijeshi.
Alipanga na kuandaa mengi since 1987 na 1992.
Aghata alikua mwanamke anayependa madaraka kuliko hata familia yake binafsi,na alikua ni milionea kwa kujilimbikizia mali binafsi kwa wingi katika nchi ya ubelgiji na ufaransa,miaka yote ambayo famikia yake ilikua madarakani nchini Rwanda.
Na kwenye baraza la mawaziri la mumewe alikua na influence kubwa mno mpaka mwaka 1994.
FELIX KABUGA""DON KING""
Huyu alikua ndio mfadhili mkubwa wa shughuli za mama Aghata na Mzee Theodore.
Na aliitwa Don king kwa sababu alikua tajiri na alikua na pesa.Everyone in rwanda politics kipindi hicho walitegemea msaada wake kufanya mambo yao.
Alikua tycoon mfanyabiashara mkubwa na mtu wa watu.
Cha ajabu yeye binafsi alihusika na mauaji ya watu zaidi ya elfu nane na wote walikua ni jamii ya watusi,na alifadhili vipindi vya redio na magazeti ya kibaguzi vilivyochochea mauaji ya kimbari mwaka 1994 nchini Rwanda.
Nimewataja hawa watu wawili sababu wamehusiana kwa ukubwa na Mzee Theodore na huwezi kumtaja Mzee Theodore bila kuwataja wao.
Sasa nadhani umejua kwanini afande""f"" alikua hamwamini kabisa mzee Theodore Sindikubwabo kisiasa.
AFANDE""F"""
Afande"" f""anasema alikua hawaamini kabisa viongozi wake hao sababu walishiriki mauaji ya watusi wasio na hatia kwa tamaa zao za kisiasa.
Vilevile serikali ya Zaire ilikua inawapa presha waondoke maeneo ya Bukavu na kuelekea kaskazini zaidi.
Serikali ya Zaire haikutaka hali ya usalama iliyokua tete kivu ya kusini iendelee kua tete.
Maana katika kivu kusini tayari kulikua na makundi yanayoipinga serikali ya Mobutu japokua hayakua na nguvu kubwa za kijeshi.
Hapa nazungumzia makundi ya kikabila ya wabangu bangu na walende na wa mulenge.
Serikali ya Zaire chini ya mpambe wa Mobutu ambae alikua Kenge wa Dondo ilikua haina stratigic za kijeshi za kuweza kuzuia kuenea kwa huo uasi uliokua unamea taratibu na haikua tayari kupokea mzigo mwingine kutoka kwa banyarwanda,wakati wao masuala yao ya ndani nchini Zaire yalikua yanawaelemea na siasa zao za ndani toka ule uasi wa wanajeshi mjini kinshasa mwaka 1992 na 1993
Na vilevile serikali ya Zaire haikutaka kuingia katika ugomvi na mshirika wake mkubwa kibiashara,,hapa namaanisha serikali ya Uganda ambayo alikua ni mshirika mzuri kiusalama kwa eneo la mashariki mwa Zaire ya wakati huo chini ya Mobutu.
Ndio maana ilikua inawasukumiza waende kivu ya kaskazini na kuweka makambi yao huko karibu na kambi za kubwa za wakimbizi karibu na mji wa Goma na mpakani na Rwanda
Afande f anasema,kwa mara ya kwanza ndio alianza maisha ya ukimbizini huku akiwa kama mwanajeshi na sio raia.
Aliondoka mjini Bukavu na kusogea mjini Kalehe ambapo ndipo alijiandaa na mpango kazi wa kufungua kambi zake za kijeshi maeneo ya karibu na Goma.
ITAENDELEA............!!!!
 
Mpunguze ujuaji humu huyu jamaa asipopost mimi na wanangu huwa tunamfuata mpaka anaposhindia kubishana huko jukwaa la hezbooolah na kina Hamas ,akija hapa mtu anaanza kutoa vitisho mara utauliwa mara hiki ina maana huyu jamaa kwa taarifa hii anayotoa hapa hajui kama kuna madhara? Muacheni atiririke na hajapost mpaka muda huu subirini hapa hapa najua alipo
Nipo na ndugu yangu Maralia 2,
Mpalestina mweusi 🤣🤣🤣
 
Nyamwasa bado yuko SA? Bado yuko na zile harakati zake
Siku hizi analindwa na serikali ya Afrika kusini baada kunusurika kuuawa na wale wabongo wakiokodiwa kumuua ila walikamatwa na alishawaomba radhi watu wote aliowakosea wakati akiwa kwenye harakati za kijeshi.
Uungwana ni vitendo.
*Mwenzake aliuawa kikatili sana kwenye korido za hoteli ya Sandton kisha wakamtupia chumbani kwake pale pale Jozi
 
Siku hizi analindwa na serikali ya Afrika kusini baada kunusurika kuuawa na wale wabongo wakiokodiwa kumuua ila walikamatwa na alishawaomba radhi watu wote aliowakosea wakati akiwa kwenye harakati za kijeshi.
Uungwana ni vitendo.
*Mwenzake aliuawa kikatili sana kwenye korido za hoteli ya Sandton kisha wakamtupia chumbani kwake pale pale Jozi
Kifo cha mwenzake na kikumbuka
 
Back
Top Bottom