Maisha bila kafara hii ngoma haiendi, utaishia kusindikiza wenzako

Maisha bila kafara hii ngoma haiendi, utaishia kusindikiza wenzako

Acha ujinga,Bill gate,Dangote wanatoa kafara gani?
Diamond,Alikiba,Vunja bei,wanatoa kafara gani?Donald Trump ametoa kafara gani?
Chapa kazi wewe,acha janja janja
Ona kenge hii uyo tajir ninae kwambia ana petro station Tanzania nzima na wilaya zake na kata zake mahali popote pale wew diamond ni bwana yako unajua mambo yake au uyo billgate ulishawahi kumuona au kuishi nae wew vp?

Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
 
Hayo maji yenyewe ya baraka unajua wanapoyatoa,watu wangu wanaangania kwa kukosa maarifa,laiti km ungefuatilia hayo maji yanapotoka usingethubutu kuandika hivy,hayo maji ni zaidi ya zam zam zaidi yavushetani ,yanatoka kwa kina lucifer wenyewe,unashindwaje kuomba na kufunga mwenyewe au upate msaada wa maombi hadi utumie maji,chumvi,jasho nk nk sio kila asemaye bwana bwana,,chunguzeni maandiko
huku kwetu tunakemeaa "shindwa kwa jina la Yesu" "damu azizi/takatifu ya Yesu takasa biashara yanguu" kisha unamwaga maji ya baraka
Aa
 
Nawasalimu kwa jina la Jamuhuri

Wakuu nimeunganisha doti za sehemu tofauti tofauti ambazo either nimefanya kazi au biashara nimegundua karibu wote wenye mafanikio wanatoa kafara kwa shetani.

Mfano 1: Kuna Wachina niliwahi fanya nao kazi miaka kumi iliyopita ya barabara jamaa walikua kila hatua ya utengenezaji wanachinja mbuzi au kondooo.

2. Tukiachana na Wachina nikaja Dar kuna waturuki walikua maeneo ya Mwenge pale wanafanya decoration na finishing kwenye majumba niliwahi fanya kazi pale nao ilikua ikifika mwisho wa mwezi wanachinja mbuzi mlangoni pa kuingilia ofisini kisha wanapika nyama watu wanakula.

3. Mbali na hao Waturuki kuna kampuni moja kubwa sana ya mafuta mi nilijua maboss awana muda na izi mambo wana petrol station kibao za blue wao kila mwisho wa mwezi wanaboost na Ng'ombe kisha nyama wanapika wanapewa wafanyakazi.

Mwisho nikagundua kama wewe sio mshirikina sali sana unless or otherwise mafanikio utaishia kuyasikia tu kwa wenzako .

Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
Usishangae mkuu, wewe angalia wabunge na mawaziri wetu walivyo washirikina.....HAKUNA mbunge wala waziri asiye mshirikina hapa Tanzania.
 
Wanasiasa wameshawatoa wanyonge kafara kitambo sana.

Yaani wanawatumikisha tu na hakuna mwenye uthubutu wa kuhoji.

Mfano hivi majuzi mmoja wao bila aibu kabisa anadai mshahara wao wa mamilioni na posho kedekede eti hazitoshi.
 
Hahaha endelea kujidanganya dogo..

Unadhani Gates amekaa kihasarahasara, hayo ma ebola ma ukimwi, ma kansa na ma saratani na chanjo zao watu wanapewa wanakufa unadhani ni kwa bahati mbaya,
.
Endelea pia kuwaamini motivation speakers akina vunjabei wakiongea kwenye ma tv mnakua na muwashawasha kudhani mtakua kama wao kwa kudhani mtaanza na jeans moja then kiwanda cha jeans
Mtu mweusi bwana akishindwa kukifafanua kitu,atakiita uchawi,
Kansa,ebola,ukimwi,ni magonjwa,Dunia ya leo,sayansi ina uwezo wa kutengeneza ugonjwa,au kirusi kama silaha,au Ili kutengeneza pesa kwenye Tiba,
Lakini kusema kwamba watu wamekaa sehemu wakatengeneza ukimwi Ili uue watu,Ili baadae watu wapige pesa kwenye Tiba,hizi ni "conspiracy theory"zisizo na ushahidi.
Naweza nikaamini,nchi za Ulaya na US,wanaweza wakaanzisha vita,mashariki ya Kati,Ili wauze siraha,na viwanda vyao vipate mapato,
Kipindi Cha Mkapa,UK walituuzia rada kwa bei kubwa,Tena tukashinikizwa tuinunue,Ili kuokoa ajira za wazungu kwenye kiwanda huko UK,sasa hapa,aliyetolewa kafara kwa kukosa huduma ni mbongo,aliyetoa kafara Ili apate mali ni serikali ya TZ,au UK?
Hizi ni mbinu za kiuchumi,na kijasusi,
Wakenya walipocheza ujasusi wakaua kiwanda Cha general tyre,Ili wao wazalishe tairi,sisi tulikosa ajira,wao wakapata,hiyo ndio kafara?
Hakuna ushahidi Dangote,au Bill gate,alienda makaburini,akacheza ngoma usiku,akamtoa mwanae kafara,au akalala na mama yake,au dada Ili kupata mali!!
Tuambie Bakheresa kamtoa nani kafara?!!
Maana usichanganye social responsibility ya makampuni kutoa kwa jamii,na kutoa kafara kwa mizimu,
Hizi story Zenu za makafara huwa hazifiki mbezi beach,zinaishia Tandale,
Haya Mond alikuwa fukara choka mbaya,kamtoa nani kafara Kufika hapo,
Shida mkishindwa kuelezea mtu kafikaje hapo na kuwaacha chini,mnamchukia na kuzusha story,ohhh anatembea na mama yake,,au anatembea na Dada yake.
Na wewe tembea na Dada yako upate mali.
Akili chafu kabisa,
Nenda kasome historia ya kampuni ya Benz,MTU,MAN,Caterpillar,zilianzishwa 1890+kwa watu kufsnya kazi,sio kuwaza kama wanga.
 
Kafara ya mbuzi sijui ng’ombe eti unaita KAFARA!!
 
Hata kwa mungu kuna kutoa sadaka ili ufanikiwe , uwezi jua labda dini zao ndoo utaratibu huo
 
Nawasalimu kwa jina la Jamuhuri

Wakuu nimeunganisha doti za sehemu tofauti tofauti ambazo either nimefanya kazi au biashara nimegundua karibu wote wenye mafanikio wanatoa kafara kwa shetani.

Mfano 1: Kuna Wachina niliwahi fanya nao kazi miaka kumi iliyopita ya barabara jamaa walikua kila hatua ya utengenezaji wanachinja mbuzi au kondooo.

2. Tukiachana na Wachina nikaja Dar kuna waturuki walikua maeneo ya Mwenge pale wanafanya decoration na finishing kwenye majumba niliwahi fanya kazi pale nao ilikua ikifika mwisho wa mwezi wanachinja mbuzi mlangoni pa kuingilia ofisini kisha wanapika nyama watu wanakula.

3. Mbali na hao Waturuki kuna kampuni moja kubwa sana ya mafuta mi nilijua maboss awana muda na izi mambo wana petrol station kibao za blue wao kila mwisho wa mwezi wanaboost na Ng'ombe kisha nyama wanapika wanapewa wafanyakazi.

Mwisho nikagundua kama wewe sio mshirikina sali sana unless or otherwise mafanikio utaishia kuyasikia tu kwa wenzako .

Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
Kutoa Kafara/sadaka sio ushirikina.
 
huku kwetu tunakemeaa "shindwa kwa jina la Yesu" "damu azizi/takatifu ya Yesu takasa biashara yanguu" kisha unamwaga maji ya baraka
Pumbaf kabisa yesu mzungu haji ng'oo'oo'o! utasubiri sana!! halafu itakuwa vice versa!!! walio toa wataenda amabo hamkutoa! mototni!!! Mark my words!!
 
Back
Top Bottom