Maisha bila Mungu yamekuwa ya amani na furaha

Maisha bila Mungu yamekuwa ya amani na furaha

Katika mambo ambayo nimejifunza kwenye kitabu cha Philosophy of Religion ni kwamba mafundisho ya dini na dini kwa ujumla yanaweza kuwafanya watu wengi kushindwa kutumia uwezo wao wa kufikiri na hivyo kushindwa kujua ukweli na kujua kuamua au kufanya mambo bila kukosea.

Hilo linaonekana katika vipindi mbalimbali jinsi jamii za wanadamu walivyokuwa wakiamini kuhusu Mungu na au hata sababu za kutokea kwa hali mbalimbali.

Unaweza ukasema kuwa mtu hana uwezo wa kufikiri unaomuezesha kujua na kujua kuamua au kufanya mambo bila kukosea.

Lakini ninataka kukuuliza swali.

Je! Suala la uvumbuzi wa maarifa ya kujua kutengeneza magari au mitambo, uwezo huo ni wa nani?

Na uvumbuzi huo au uwezo huo una makosa gani ukiacha makosa yanayotokana na matumizi?

Na Je! Kufikiri maana yake ni nini? Na kati ya mnyama na mtu, mwenye uwezo wa kufikiri ni nani?
Unafanya kosa la logical fallacy, logical non sequitur.

Kwa kuwa tu, watu wana uwezo fulani wa kufanya maamuzi fulani kufanya mambo bila kukosea, hilo halina maana watu wananuwezo wa kufikiri na kufanya mambo bila kukosea.

Unaelewa tofauti?

Yani ni hivi, mtu akiweza kufanya hesabu za kujumlisha za namba 1 mpaka 10 bila kukosea, hilo halimaanishi kuwa mtu anaweza kufanya hesabu bila kukosea.

Wewe unachokosea ni kwamba, unaangalia mfano wa mtu anayeweza kufanya hesabu za kujumlisha namba 1 mpaka 1 bila kukosea, halafu unahitimisha kuwa huyu mtu ana uwezo wa kufanya hesabu bila kukosea.

Wakati kuna ma polynomial equation na ma Riemann Zeta Function hujayaangalia huko.

Ushaona unapokosea hapo?

This is a non sequitur logical fallacy.

This is a hasty generalization logical fallacy.
 
1. Ukiona unachoita uumbaji, unajuaje ni matokeo ya Mungu na si kingine chochote? Unathibitishaje hilo?

2. Ukiona unachoita meno, unajuaje ni matokeo ya Mungu na si kingine chochote? Unathibitishaje hilo?

3. Ukiona unachoita roho mtakatifu, unajuaje ni matokeo ya Mungu na si kingine chochote? Unathibitishaje hilo?

Hujathibitisha , hujathibitisha hata hiyo roho kwamba ipo.
Kama unataka kuthibitisha kwa vigezo vyako unavyovijua wewe ni sawasawa na unakataa kuthibitishiwa,

kwasababu ninakupa vigezo vya uhakika hauvitaki,

Kigezo kikuu ni imani. Kama huamini! basi umekataa mwenyewe kuthibitishiwa!

IMANI
 
Hapana, haipo. Usinilazimishe.

Hujaeleza inapimwaje.

Hujathibitisha ipo.

Unalazimisha tu.

Hapana, haipo. Usinilazimishe.

Hujaeleza inapimwaje.

Hujathibitisha ipo.

Unalazimisha tu.
Mimi sikulazimishi jamaa
Na unasema wewe uko huru lakini bado unaishi kwa kufuata sheria na Katiba ya nchi yako, hauoni kwamba hauna uhuru kabisa bado uko kwenye dini
Kwa sababu hizo Sheria unazozifuata za nchi yako ni copy and paste ya amri KUMI za Mungu wa wayahudi
 
Mimi sikulazimishi jamaa
Na unasema wewe uko huru lakini bado unaishi kwa kufuata sheria na Katiba ya nchi yako, hauoni kwamba hauna uhuru kabisa bado uko kwenye dini
Kwa sababu hizo Sheria unazozifuata za nchi yako ni copy and paste ya amri KUMI za Mungu wa wayahudi
Wapi nimesema niko huru? Ni mimi nimesema au ni wewe unafikiri nimesema bila ya mimi kusema?

Hizo sheria unazosema ni amri kumi za Mungu unajuaje hazikuwapo kabla ya hizo amri kumi za Mungu?

Unaweza kuthibitisha huyo Mungu yupo? Usije kuziita amri kumi za watu amri kumi za Mungu.

Unajuaje hizo unazoziita amri kumi za Mungu ni za Mungu kweli, na si za watu tu?
 
Kama unataka kuthibitisha kwa vigezo vyako unavyovijua wewe ni sawasawa na unakataa kuthibitishiwa,

kwasababu ninakupa vigezo vya uhakika hauvitaki,

Kigezo kikuu ni imani. Kama huamini! basi umekataa mwenyewe kuthibitishiwa!

IMANI
Imani si uthibitisho, imani ni kukosa uthibitisho.

Kuamini kitu ni kukubali kitu bila ya kuwa na uthibitisho, hiyo ndiyo definition ya imani.

Ila wewe unaandika kuhusu imani bila kujua hata definition ya imani.

Na ninachotaka mimi si uthibitisho kwa vigezo vyangu.

Ninataka uthibitisho kwa vigezo vya mantiki, kwa logical consistency, bila contradiction, vigezo vilivyokuwepo maelfu na maelfu ya miaka kabla sijazaliwa, hivyo si vigezo vyangu.
 
Kwa kuwa tu, watu wana uwezo fulani wa kufanya maamuzi fulani kufanya mambo bila kukosea, hilo halina maana watu wananuwezo wa kufikiri na kufanya mambo bila kukosea.

Unaelewa tofauti?

Yani ni hivi, mtu akiweza kufanya hesabu za kujumlisha za namba 1 mpaka 10 bila kukosea, hilo halimaanishi kuwa mtu anaweza kufanya hesabu bila kukosea.

Wewe unachokosea ni kwamba, unaangalia mfano wa mtu anayeweza kufanya hesabu za kujumlisha namba 1 mpaka 1 bila kukosea, halafu unahitimisha kuwa huyu mtu ana uwezo wa kufanya hesabu bila kukosea.
Hoja yako inaepuka ukweli au msingi kwamba mtu ana uwezo wa kufikiri ambao unamwezesha kujua na kujua kuamua au kufanya mambo bila kukosea.

Na badala yake inajikita kwenye sababu zinazofanya mtu ajuwe kwa kiwango kidogo na asijuwe kwa kiwango kikubwa na au asijuwe kabisa.

Na hivyo unahitimisha kwamba mtu hana uwezo wa kufikiri unaomuezesha kujua na kujua kuamua au kufanya mambo bila kukosea.
 
Huyo mnyama 666 hajawahi kuwepo, hayupo na hata uwezekano wa kuwepo kwake Haupo.

Mnatunga tunga dhana zenu uchwara zisizo na uthibitisho wowote ule.

Jehanam haijawahi kuwepo, haipo na hata uwezekano wa kuwepo kwake Haupo.

Hakuna Mungu wala Shetani.

Hakuna pepo wala jehanam.
Yani Mungu aumbe JUA/SUN jinsi lilivyo na moto mkala kama likishuka kidogo litachoma Dunia yote na kubakisha majivu alafu ndio ashindwe kuumba Jahannam?

Kweli nyinyi makafiri mnashida
 
Hoja yako inaepuka ukweli au msingi kwamba mtu ana uwezo wa kufikiri ambao unamwezesha kujua na kujua kuamua au kufanya mambo bila kukosea.

Na badala yake inajikita kwenye sababu zinazofanya mtu ajuwe kwa kiwango kidogo na asijuwe kwa kiwango kikubwa na au asijuwe kabisa.

Na hivyo unahitimisha kwamba mtu hana uwezo wa kufikiri unaomuezesha kujua na kujua kuamua au kufanya mambo bila kukosea.
Mtu hana uwezo wa kufikiri na kuamua bila kukosea kwa sababu hana habari zote.

Maamuzi yote, hata yale ambayo anapatia na kufanya bila kukosea, ni matokeo ya maamuzi ambayo kimsingi hayana uwezo wa kuamua bila kukosea.

Tuchukue mfano wa mtu anayeamua kwamba achukue mwamvuli au asichukue mwamvuli kwenda kazini siku tatu zijazo.

Mtu huyo ataangalia utabiri wa hali ya hewa aone kama mvua itanyesha.

Utabiri wa hali ya hewa utatoa makisio ya asilimia fulani ambazo mvua inawezekana kunyesha, hautoi habari yenye uhakika wa 100% kwamba mvua itanyesha au la.

Hivyo, uamuzi wowote atakaofanya, kwamba achukue mwamvuli au asichukue, utatokana na maamuzi yanayofanywa kwa kufikiri kwa kuangalia habari z amakisio, probability, kwa asiimia.

Hivyo, hata kama kukiwa na utabiri wa mvua kuwepo, utabiri wa 99%, inawezekana mvua isinyeshe.

Mamuzi yetu yote ya mambo yajayo yako hivyo. Hakuna uamuzi wenye uhakika wa 100%.


Na kwa sababu hiyo, hutakiwi kusema kuwa mtu ana uwezo wa kufikiri na kufanya maamuzi bila kukosea.

Ndiyo maana hata hayo magari unayosema watu wana design na kutengeneza, baada ya miaka kadhaa utasikia kuna kifaa kimefanyiwa recall kwa sababu wamegundua kina tatizo fulani katika design yake.
 
Inawezekana science na ulimwengu wa roho vinazungumza lugha moja ila ina apply katika mazingira tofauti 👇🏻

Atheist

What is Newton's Third Law? Newton's third law simply states that for every action there is an equal and opposite reaction. So, if object A acts a force upon object B, then object B will exert an opposite yet equal force upon object A.

KARMA (Asians)

in Hinduism and Buddhism) the sum of a person's actions in this and previous states of existence, viewed as deciding their fate in future existences.
"a buddha is believed to have completely purified his karma"

What Goes Around comes Around (Wazungu)

the consequences of one's actions will have to be dealt with eventually

Malipo ni hapa hapa duniani (Waswahili)

Ukimtendea mwenzako ubaya, utalipwa sawa sawa kwa ubaya ulio mtendea


Sioni kama kuna sababu ya kutumia nguvu nyingi kila mtu abaki na mtazamo wake
 
Mtu hana uwezo wa kufikiri na kuamua bila kukosea kwa sababu hana habari zote.

Maamuzi yote, hata yale ambayo anapatia na kufanya bila kukosea, ni matokeo ya maamuzi ambayo kimsingi hayana uwezo wa kuamua bila kukosea.
Kusema kwamba mtu hana uwezo wa kufikiri na kuamua bila kukosea kwa sababu hana habari zote ni hoja isiyozingatia akili.

Mtu ana habari zote na mtu hana habari zote.

Fikiria kwa mfano, habari za fizikia, habari za baiolojia, jiografia, habari za hisabati, kemia, habari za saikolojia, habari za elimu ya anga za mbali, teolojia na kadhalika. Habari hizo mtu anazitoa wapi kama hana habari zote?

Kwa kufikiri mtu anapata habari zote na kwa kutofikiri hana habari zote.

Unaweza ukajua mvua itanyesha katika siku tatu zijazo kwa akili; au unaweza usiwe na hizo habari.

Kila mtu ana uwezo wa kupata habari zote. Ni mtu mwenyewe aamuwe kutafuta hizo habari au aache.
 
Yani Mungu aumbe JUA/SUN jinsi lilivyo na moto mkala kama likishuka kidogo litachoma Dunia yote na kubakisha majivu alafu ndio ashindwe kuumba Jahannam?
Hakuna Mungu aliyewahi kuumba Jua.

Hakuna Mungu aliyewahi kuumba kitu chochote kile.

Huyo Mungu hajawahi kuwepo hayupo na hata uwezekano wa kuwepo kwake Haupo.
Kweli nyinyi makafiri mnashida
Wavaa kobazi mna ufinyu wa fikra.
 
Kusema kwamba mtu hana uwezo wa kufikiri na kuamua bila kukosea kwa sababu hana habari zote ni hoja isiyozingatia akili.

Mtu ana habari zote na mtu hana habari zote.

Fikiria kwa mfano, habari za fizikia, habari za baiolojia, jiografia, habari za hisabati, kemia, habari za saikolojia, habari za elimu ya anga za mbali, teolojia na kadhalika. Habari hizo mtu anazitoa wapi kama hana habari zote?

Kwa kufikiri mtu anapata habari zote na kwa kutofikiri hana habari zote.

Unaweza ukajua mvua itanyesha katika siku tatu zijazo kwa akili; au unaweza usiwe na hizo habari.

Kila mtu ana uwezo wa kupata habari zote. Ni mtu mwenyewe aamuwe kutafuta hizo habari au aache.
Habari zozote utakazozipata zina mapungufu.

Kwanza kifizikia, habari zote utakazozipata ni za dunia iliyopita, ziko limited na the speed of light or electromagnetic waves.

Ukiliangalia jua sasa hivi, unajidanganya kwamba unaliangalia jua kama lilivyo sasa hivi. Lakini, ukweli ni kwamba, ukiliangalia jua sasa hivi, unaliona jua kama lilivyokuwa takriban dakika nane na sekunde ishirini zilizopita. Maana yake ni kwamba, jua likizimika sasa hivi, hatutajua kwamba jua limezimika mpaka dakika nane na sekunde ishirini zipite.

Jua ni nyota ya karibu tu, ukienda kwenye nyota inayofuatia, Proxima Centauri, ikizima leo, tutaendelea kuiona kwa takriban miaka 4.2 bila kujua kwamba imezimika. Kuna nyota ambazo tunaziona leo lakini zimeshazimika mamilioni ya miaka iliyopita.

Kwa nini? Kwa sababu ujuzi wetu umewekewa kikomo na speed of light.

Pili, kuna habari hazijulikaniki kwa kuwa ziko beyond the Planck Scale, hazijakidhi kubanwa kama ni wave au particle katika wave particle duality, haziwezi kujulikana vizuri velocity na position yake kwa wakati mmoja kw akufuata Heisenberg's Uncertainty Principle.

Unavyozidi kusoma, ndivyo unavyozidi kujua kuwa habari za dunia, kimsingi, zina ukomo, na kuna kiasi fulani tu tunachoweza kukijua
 
Hakuna Mungu aliyewahi kuumba Jua.

Hakuna Mungu aliyewahi kuumba kitu chochote kile.

Huyo Mungu hajawahi kuwepo hayupo na hata uwezekano wa kuwepo kwake Haupo.

Wavaa kobazi mna ufinyu wa fikra.
Kwahiyo Kwa maelezo haya ndio tuungane na wewe kukubali kuwa hakuna Mungu?

Au unayo maelezo mengine na evidence ya kuthibitisha kuwa Mungu hayupo?
 
Kwahiyo Kwa maelezo haya ndio tuungane na wewe kukubali kuwa hakuna Mungu?
Hata usipokubali kwamba Mungu hayupo.

Ukweli na uhalisia utabaki palepale, Huyo Mungu hajawahi kuwepo hayupo na hata uwezekano wa kuwepo kwake Haupo.

Kama huyo Mungu yupo ajitokeze hadharani mwenyewe ajidhihirishe yupo kama ana huo uwezo.

Mnahangaika sana kumwelezea na kumuongelea huyo Mungu kwa vile hajawahi kuwepo na hayupo kujiongelea mwenyewe na kujidhihirisha mwenyewe.

Mnatetea fictional character.
Au unayo maelezo mengine na evidence ya kuthibitisha kuwa Mungu hayupo?
Anayedai Mungu yupo ni mimi au wewe?

Yani unaleta habari na madai yako ya kwamba Mungu yupo, Halafu unataka mimi nikuthibitishie madai yako?

Wewe unayedai huyo Mungu yupo ndio umthibitishe yupoje ili tuweze kumjua yupo.

Ukishindwa kuthibitisha, Ni kwamba madai yako ya uwepo wa huyo Mungu ni madai ya UONGO na huyo Mungu HAYUPO.

Unafosi mawazo yako uchwara yasiyo na uthibitisho wowote ule.
 
Back
Top Bottom