Maisha halisi ya Watanzania waishio hapa Afrika Kusini

Ontan katika uhalisia wake...ushanidaka mkuu nikiona bandiko lako tu lazima nilipitie....makes clap!
 
Stippers ninao wakubali ni wale wa the summit,wengine wote tupa kule! Wabongo waliotusua wapo kibao pia ila ni wale wenye shughuli rasmi zinazofahamika.
Boss! Nakubaliana na wewe, sikatai kua hao wapo. Lkn tuwe wakweli SA si pa kuenda mzima mzima.

Mimi I'm being honest, kuna sehemu nilienda panaitwa White House hotel, mtaa wa Main street, Town. Kuna dogo ni mwafrika kusini pure, nilikutana nae ana degree ya metallurgy engineering na bado alikua ni bar waiter.

Alikua anatamani sana kuzamia kuja Bongo, alinambia ana rafiki zake wamekuja Bongo na wakala mashavu migodini. Sasa, nafikiria mwenyeji anahenya hivi, vipi kuhusu mgeni anayekuja huku hajui kuzungumza Tswana, Zulu, Khoxa, Ndebele, Swati wala Tshonga na hata kingereza chenyewe mtu hawezi kuongea dakika 3 bila kunywa maji.

Huko ni pagumu sana km hauna pa kuanzia.
 
KATIKA HILI HAKUTUTENDEA HAKI HUYU MHESHIMIWA, ALIYO YA ZUNGUMZA MENGI NI SAHIHI ILA SI KWAMBA WOTE TULIO HAPA TUPO HIVYO INAWEZA LIKAWA NI KOSA LA MWENYEJI WAKO AU NI MAKUSUDI TU! 0733318248 TUWASILIANE UJE NYUMBANI TAFADHALI.
Unaishi wapi boss, weekend nakuja Honey Dew kuna ishu nafata.
 
Duh hii movie Nilitamani isiishe nzuri sana sana sana booonge la documentary hongera sana Mdau,binafsi kwetu Green City aka Mby ni njia panda ya kwenda RSA,zamani ilikuwa ni ndoto yangu kwenda kuishi kule sababu Brothers wakipiga picha Wamenenpa na wamependeza kwa mavazi Nilijua maisha huko ni rahisi tu mpaka siku Moja Jamaa mmoja alisema siwezi kuruhusu ndugu yangu kuishi South kuuana ni dakika moja bora Nibaki sokomatola au Mbata kuliko RSA!
 
Pia ufike cape town. Na ukifika Johannesburg fanya mawasiliano tukukutanishe na watanzania wenye maisha yao. Mana kuwajumlisha wote kisa umeona maisha ya mateja. ... da!
Boss siwezi kugeneralize kuwa Wabongo wote ni mateja hahahaa. Pia weekend nakuja Jozi maeneo ya Honey Dew, from Rustenburg, ntakua nalala Home Stay Hotel hapo Roodpoort.

Boss nimefika Cape town. Huko si Africa, si Africa Kabisa. Nilifika Western Cape, kisha nikakaa V & A Waterfront. Huko sijawahi kuona hata dalili ya wabongo. Yani niseme mpaka Mbongo anafika Cape, basi huyo katoka Bongo anajua route yake mwanzo hadi mwisho. Maana ukiangalia hata flight distance tu kutoka O.R Tambo hadi Cape Town Airport bi sawa na O.R Tambo hadi Dar.
 
Natoka chafu pozii...asant sana mkuu.ila ntaisoma asbuh,ilo neno juu ndo nimeliona harak na pich y ilo eneo.
 
Ontan katika uhalisia wake...ushanidaka mkuu nikiona bandiko lako tu lazima nilipitie....makes clap!
Thanks my main man. Tupo pamoja sana askari wangu.
 
Mkuu mbona tupo wengi tu na wengine wametusua hapahapa wakasonga mbelembele huko na wanafanya vizuri tu spain, sweden, Belgium, Holland, Italy nk..

Karibu maeneo yetu sandton tuchome nyama Mandela square hapo.. ..
 

David Treziguet a.k.a Trezgoals hahaha... Huyu jamaa haki ya nani wataliano hawawezi msahau, umenifanya nikumbuke the luckiest France!! ilikuwaga ina bahati sana miaka hiyo, miss that golden era.

In blue, umeongea kitu cha msingi saaaana ambacho nilitaka nikiandike hata kwenye reply iliyopita ila nikaona nisubiri kwanza ni muone gani hasa ulio nao... Huyo mwalimu amekanyaga bondeni kwa mara ya kwanza 2009 nadhani ilikuwa ni baada tu ya Xenophobic attack ile ya kwanza, alikuwa ana kielimu chake kiana alichotoka nacho hapa bongo amefika kule amefanya kazi hizi hizi za hohe hahe ila upate kula tu, baadae akaona arudi class kwenye hiyo hiyo aridhi ya madiba... Amemaliza course kapata internship na internships za kule sio za kishamba kama huku eti hata nauli hupati, kule unapata allowance una sahau kama unajitolea.

Hakuchukua muda akapata shavu, sasa hivi nakula zake ZR20k+ ambozo ni zaidi ya Tsh.4.4m. Na maisha yanasonga.

Ukweli ni kwamba unapoenda kwenye nchi za watu kama hauna shule, hauna fani wala kipaji chochote hata cha kuendesha maringi yaani wewe ni bashite type na kibaya zaidi hata lugha nayo iwe ni tatizo ....haaaa hapo lazima usage meno na utajikuta umekuwa kibaka automatically.

If you don't know the way, then the way itself will take you anywhere.
 
Kiongozi Ongera sna karibu sna kifupi maisha uliozungumzia hata nyumbani bongo yko kupanga ni kuchagua hao uliwakuta wanaishi maisha hayo ndio maisha walio chagua ila tupo tunao jielewa na maisha yanakwenda...
 
Thanks my main man. Tupo pamoja sana askari wangu.
HATA BONGO WAPO<br />Mi nampongeza sana mtoa mada. Nafikiri ni muandishi. Na nimuandishi mzuri kwa kweli. <br /> Ameeleza kwa ufasaha sana Yale aliyoyaona. Na amejitahid kuyapigia rangi inayompendeza. Lakin kamlipia mtu hotel ambae aliachwa hotel na mtu asiejulikana (kama kweli) mtanzania alieachwa kwenye mataa hotel, simkazi wa afrika kusini. Ni mtu alietumwa Afrika kusini akaachwa solemba. Je mtu aliemtuma kutoka bongo hakumpa japo pesa kidogo ya kijikwimu? Shida imeanzia bongo.<br /> Mana nadhani kama aliondoka bila kuchukua walau nusu ya malipo yake ya kazi yake kazi ipo hapo. Sijui kama Hilo lina uhusiano wowote na maisha ya south Africa au ni tabia tu ya hao watu alofanya nao biahara. <br /> Kisha akaenda mjini. Cbd. Kama nimesoma vizuri akaona vibaka wa ndole. Tena mateja. Je ndo utapima maisha ya watanzania wanaoishi Afrika kusini kwa kiwaangalia hao. <br /> Alienda kunyoa. Akaona vinyozi na baadhi ya watanzania wasio na kazi wamekaa hapo. Je ni maisha ya watanzania wote afrika kusini. <br /> Maisha yote uliyafanikiwa kuyaona Afrika kisini. HATA bongo yapo. Wapo watanzania wanaoishi maisha hayo ndani ya Tanzania. Ila si maisha ya watanzania wote. <br /> Maisha ya watanzania ndani ya afrika kusini hayana tofauti maisha ya watanzania ndani ya Tanzania. Wapo wanaoishi vizuri sana. Wapo wanaoishi maisha ya kati. Wapo wanaoishi maisha ya kawaida. Wapo wanaoishi maisha dhalili sana. Na aina yote hii ya watu, Hata bongo wapo. Nimesema.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…