Maisha halisi ya Watanzania waishio hapa Afrika Kusini

Umeandika upuuzi tu

Ulikuwa unataka tujue tu kama na wewe ulienda kwa mzee madiba basi hizo nyingine zote ni porojo tu umegoogle mapicha ili kuufanya uwongo wako uwe kweli.
 
ONTARIO uliwahi kukutana na Sandile Mantsoe yule jamaa aliyemuua girlfriend wake halafu akamchoma moto kabla hajakamatwa wiki iliyopita?
 


mkuu wacha nikuache kwa hiki kitu labda usiku wako wa leo utakua mzuri "Nigeria's journey to Olympic Football gold"

Tukirud kwenye mada, bwana ONTARIO kajaribu kuleta kitu muhimu sana hapa cha kujifunza. Natumai wengine watajifunza kupitia hapa. Si vema kukurupuka na kwenda kuhangaika na kutaabika ugenini. Pia na wale walioko huko abroad na hawana green pasture as they expected nadhani ni time ya kujikusanya na kurudi nyumbani na kuanza moja. Tutawaelewa na kuwapokea tukifahamu fika juhudi zao hazikufanikiwa. Wahenga wanasema "lake mtu halimtapishi bali humchefua." Asante kwa mara nyingine bwana ONTARIO kwa kushea na wadau.

"Over the fence is not always ever green"
 
Mkuu K_dizle umetisha sanaa mazee kwa kuleta hii kitu ya akina Nwanko Kanu na amokach, true super eagles.
 
ONTARIO uliwahi kukutana na Sandile Mantsoe yule jamaa aliyemuua girlfriend wake halafu akamchoma moto kabla hajakamatwa wiki iliyopita?
Sandile Mantsoe sijakutana nae, japo skendo yake imepata sana headlines huku. Kila kituo cha habari wanamjadili yeye, hasa ukizingatia mwanzoni alikua ana image fulani hapa SA kupitia biashara yake ya options.
RIP Karabo.
 
Kama kuna mtu alete Habari za wabongo wanaoishi Ghanzou.
 
Umeandika upuuzi tu

Ulikuwa unataka tujue tu kama na wewe ulienda kwa mzee madiba basi hizo nyingine zote ni porojo tu umegoogle mapicha ili kuufanya uwongo wako uwe kweli.
wewe na jamaa nani mpuuzi
upuuzi wako wewe hujui kutumia jamii forum app na kila siku tunasema jambo hilohilo
7bu umekuja mbio mbio mipovu inakutoka kama ndo wewe ulokuwa umebeba mboks wa sabufa wa wizi baada kuona ALLY katusua maisha yamekushinda huko kwa madiba na kuja kuquote thread nzima
kutupa shida tuu wenzako tunaotumia simu
 

Mwaka 2004 hadi 2005 nilikaa hapo Cape Town nikiwa ' napiga ' Kozi moja UCT ( University of Cape Town ) na nilikuwa naishi karibu tu hapo na Chuo mtaa wa Rondebosch jirani kabisa na Supermarket yao kubwa ya Pick & Pay. Wabongo walikuwepo hasa akina Hamidu na Kundi lake na kama ukiwataka sana Wabongo rudi nyuma kama unakwenda Hospital kubwa ya Jiji la Cape Town ya Grooteskil utakutana nao wengi sana. Ila eneo kubwa ambalo utakutana sana na Wabongo ni kule ' uswahilini ' mwa Jiji la Cape Town maeneo ya Langa na Gulu.
 
Mmh. Mkuu sijui hasa lengo la huu uzi. Ila wabongo wanaojielewa ni wengi tu afrika kusini. Na pia hapo water front ulipokua kuna zaidi ya wabongo kumi(ninaowajua mimi) wanamiliki maduka. Wabongo wengi tu wanaishi mjini cbd Na wana biashara tofauti.
Sijui picha inayoingia akilini kwa mtu ambae hajaingia Africa kusini unaposema langa Na hiyo uloandika "gulu" labda ulikusudia guguletu kua ni uswahilini. Sijui picha gani wanapata.
Wabongo kadhaa wanaishi na wengi wanafanya biashara na si kuishi humo kutokana na mazingira ya usalama. Cape Town ina watanzania wengi Mkuu. Na wengi wanaheshimiwa kutokana na mchango wao wa kutoa ajira kwa wazawa na watanzania na wazimbabwe.
Zaidi maisha ya afrika kusini yapo tofauti sana na Tanzania. Tanzania mwenye pesa yupo tofauti sana na asiye nazo. afrika kusini hutaona maendeleo ya mtu kwa kuangalia chakula, nguo, au sehem anyoishi. mfumo wa biashara pia ni tofauti. Muuza matunda Tanzania na afrika kusini ni watu tofauti sana. Muuza samaki Tanzania na afrika kusini ni watu tofauti sana. Kinyozi Tanzania na afrika kusini ni watu tofauti sana. Mziba pancha Tanzania na afrika kusini ni tofauti. Afrika kusini Kila kazi ina heshima na kipato stahiki.
kazi zinaheshimiwa hapa. Kila kazi. Na ukumbuke pia. Wengi ya watanzania walio hapa ni wale ambao hawakwenda sana shule. Maisha ya kwao yalikua magumu mno. Kwao hapa wamepata nafuu sana ukilinganisha na walivyokua au kama wangekua wanaishi bongo.
Ndio maana angalia watanzania walioanzisha biashara za kutuma pesa wamepata pesa sana kutokana na vijana kujitahidi kutuma pesa japo kidogo kwao. labda kwako mtoa mada waoza usione kutokana na kujaaliwa kua na pesa nyingi. Ila kwa sisi tuliotoka kwenye maisha duni tunaona tofauti.
Ndugu kuna maisha yote afrika kusini kwa watanzania. Na wanaishi sehem zote pia. tuna watanzania ambao ni milionea afrika kusini.
Mkuu cha kufanya ni ukija tena. Usipite tu mitaani na kutegemea kuona maisha halisi ya watanzania afrika kusini. Labda yatafute. Au watafute.
 
mkuu sasa kama wapo Watanzania wenye maisha mazuri ni jukumu lako sasala kutueleza wako wapi na mafanikio yao ni kiasi gani na wanafanya shughuli gani.....usimlaumu mtoa mada yeye ametembea na Watanzania aliokutana nao ndio hao choka mbaya wauza matunda, waosha magari na machangudoa.....sasa ulitaka asifie Watanzania wana maisha mazuri wakati hajawaona hao wenye maisha mazuri?........Njoo na thread ya kuonyesha hao Watanzania wenye maisha mazuri na shughuli wanazofanya acha bla bla
 
Ningekuwa na nauli ningeenda nikaanzishe kijiwe cha kubrashi viatu mbona kwenye uzi huu hajaongelea inamaana watakuwa hawapo

Wapo wengi sana mazee, hata hao vinyozi aliowaongelea huwezi ukawalinganisha na wa huku bongo kwa kipato. Watu wanajichanga hadi wanafungua Berbershop zao wenyewe kikubwa discipline tu. Usiogope kuchukua uamuzi kama umedhamiria kwa hicho utachotaka, hata wamarekani wenyewe wapo wanaoendega Mexico kutafuta life sembuse wewe mbongo unaoishi dunia ya 3.


Hapo nilipokazia na blue, nifupishe tu kwa kusema informal sector ya Afrika kusini kamwe haiwezi kufanana na iliyopo Tanzania, they are way up our league in all spheres! na hii ndio sababu kuu ya msingi ni kwanini mtu anaweza kuacha kazi ya u-bank teller akaenda kule akapiga hata udereva tax tu na baada ya miaka mitano mambo yake yakawa super kuliko hata angeendelea kubaki huku kwa hiyo miaka mitano.

Hapo kwenye kazi na hadhi tofauti huwa inaonekanaga tu siku zote, ila kwa south ni tofauti na bongo... Bongo mtu ukimiliki gari tu wengi wanakuangalia kwa jicho la umeshatoboa tayari au bado kidogo. Lakini hii yote ni kwa sababu ya umasikini tulio nao, wewe kama Tanzania nzima tunaambuliwa ina magari laki 7 kwenye taifa la watu 50.7m wakati huo Johannesburg tu peke peke yake ina magari zaidi ya milioni 2, kwanini Tanzania mtu mwenye gari asijulikane na yeye mwenye kujiona yuko well off na wakati huo huko Johans unashindwa kujua mwenye gari ni yupi na asiye na gari.
 
Sandile Mantsoe sijakutana nae, japo skendo yake imepata sana headlines huku. Kila kituo cha habari wanamjadili yeye, hasa ukizingatia mwanzoni alikua ana image fulani hapa SA kupitia biashara yake ya options.
RIP Karabo.

Jamaa alikuwa ni trader na mentor mzuri sana wa FOREX, alikuwa anajiita binary option master. Ana mkwanja hatari halafu bado chalii tu wa miaka 27 ila ndio hivyo tena kashapotea life sentence inamuhusu. Lakini hivi kweli unaanzaje kumuua na kumchoma moto huyu mtoto!?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…