Maisha haya aisee, jana ilikuwa harusi leo imekuwa msiba

Maisha haya aisee, jana ilikuwa harusi leo imekuwa msiba

Nilikuwa nafuatilia interview ya marehemu Professor. Matthew Luhanga iliyofanyika miezi michache kabla ya umauti kumfika aisee , alikuwa anaonekana amechoka sana(72 by then). Anaulizwa Hali yake akasema "Hali yangu inaendana na umri wangu, hivyo sina malalamishi makubwa.." 😥kwa tone ya kuonyesha he's no more happy, ni vile tu bado pumzi ipo
We acha tu yaani!! kwamba hata tufurukute tuna mwisho na ukiishi na miaka mingi ni mateso kwa nn tudharauliane? Hii dunia tu
 
Wakuu, hapa mtaani kwangu kuna ndugu yetu nyumbani kwake kulikuwa na harusi(mtoto wake alikuwa anaoa). Ndoa imefungwa vizuri kabisa,
watu tumekula ubwabwa mpaka basi, na wanywaji wamekula bia mpaka basi.

Cha kusikitisha leo asubuhi mzee wa watu kaenda Kibaoni kununua pumba za kuku wake, akagongwa na gari na kupoteza maisha hapo hapo.

Watu tunamalizia kuosha vyombo vya harusi, zinakuja taarifa za msiba.

So sad kwakweli.
Fumbo la maisha halina ufumbuzi
 
Nilikuwa nafuatilia interview ya marehemu Professor. Matthew Luhanga iliyofanyika miezi michache kabla ya umauti kumfika aisee , alikuwa anaonekana amechoka sana(72 by then). Anaulizwa Hali yake akasema "Hali yangu inaendana na umri wangu, hivyo sina malalamishi makubwa.." [emoji26]kwa tone ya kuonyesha he's no more happy, ni vile tu bado pumzi ipo.
Dah,Mzee aliongea maneno yakufikirisha sana,maneno mazito sana, nimejisikia huzuni sana!Mungu ana siri nzito mno.
 
We acha tu yaani!! kwamba hata tufurukute tuna mwisho na ukiishi na miaka mingi ni mateso kwa nn tudharauliane? Hii dunia tu
Hatari sana, muhimu kuishi kwa upendo... Tukipata nafasi ya kufurahi unafurahi!
“Kisha nikaisifu furaha, kwa sababu mwanadamu hana neno lo lote lililo jema chini ya jua, kuliko kula, na kunywa, na kucheka; na yakuwa hilo likae naye katika amali yake, siku zote za maisha yake alizompa Mungu chini ya jua.

— Mhubiri 8:15
 
Maisha ni f*keni
4775795-Tupac-Shakur-Quote-Why-am-I-dying-to-live-if-I-m-just-living-to.jpg
 
Dah,Mzee aliongea maneno yakufikirisha sana,maneno mazito sana, nimejisikia huzuni sana!Mungu ana siri nzito mno.
Tuishi kwa upendo! ndio maana Mhubiri anasema yote ni ubatili.
“Maana hakuna kumbukumbu la milele la mwenye hekima, wala la mpumbavu; kwa sababu siku zijazo wote pia watakuwa wamekwisha kusahauliwa. Na mwenye hekima, jinsi gani anavyokufa sawasawa na mpumbavu!

— Mhubiri 2:16
 
Maisha ni Fumbo,,Kuna ndugu yangu mwezi wa sita kafunga ndoa takatifu na tukasherehekea Kweli kweli,,jana usiku Amefariki..yani ndoa haijatoboa hata miezi miwili [emoji24][emoji24][emoji24]
 
Aisee

Kweli tuishi Ila tusimsahau muumba.wetu

Maisha ni tafakuri nzito yenye kujaa mafumbo na Siri

Wachache wanaijui siri hii
 
Shemeji yangu wa kike ni shabiki wa simba lia lia,humwambii kitu kuhusu hiyo timu

Tarehe 13 mwezi huu alikuwepo uwanja wa taifa kushuhudia ngao ya jamiii,mpira umekwisha yanga 2-1

Kwakuwa ni mtu wa majigambo na tambo nyingi,tukawa tunamsubiri kwa hamu arudi home tumshambulie kwa kejeli. ( sisi yanga)

Akawa harudi...tukampigia simu haipatikani,tukajua kwasabu timu yake imefungwa kaamua kuzima simu kwakuwa anakwepa utani wa jadi.

Kumbe bhana pikipiki aliyopanda iligongwa na gari maeneo ya kwa musuguri,walipoteza maisha palepale.

Kupata taarifa hata hatukuamini yani,shemeji yangu amekwenda kiutani namna hiyo,tumeumia sana.

Apumzike kwa amani
Mkuu poleni sana
 
Au unakuta anaiba mapesa na kuwapa mke na wanawe madaraka utadhani wataishi milele.
At the end wajukuu zake wanakuja kuwa masikini.Thus watawala wa kizungu wao waliona ni upumbavu kuiba madarakani ni SAwa na kujiibiia mwenyewe maana hata ukiiba zaidi labda watafaidi wanao je kizazi cha wanao je si kitaishia kuwa masikini,wao waliona jibu jepesi ni kuboresha maisha ya jamii nzima,yakiwa bora na vizazi vyao vitafaidi.Afrika mtu anaiiba pesa anaenda fadhili timu ya mpira kwa kodi zetu.
Mtu anapewa tenda ya kusambaza maji vijijini anazipiga kwa kushirikiana na watendaji kisha anaenda zifanyia biashara ya mabus huku Jamii ikiteseka na maji
 
Yeah!
Duniani tupo ili tuvunje sheria, duniani tupo ili tufanye dhambi.
Hapana. Ndugu yangu kwenye hii Dunia jitahid kuishi maisha ya kumpendeza Mungu. Maisha ni mafupi sana Tena yamejaa taabu na shida
 
At the end wajukuu zake wanakuja kuwa masikini.Thus watawala wa kizungu wao waliona ni upumbavu kuiba madarakani ni SAwa na kujiibiia mwenyewe maana hata ukiiba zaidi labda watafaidi wanao je kizazi cha wanao je si kitaishia kuwa masikini,wao waliona jibu jepesi ni kuboresha maisha ya jamii nzima,yakiwa bora na vizazi vyao vitafaidi.Afrika mtu anaiiba pesa anaenda fadhili timu ya mpira kwa kodi zetu.
Mtu anapewa tenda ya kusambaza maji vijijini anazipiga kwa kushirikiana na watendaji kisha anaenda zifanyia biashara ya mabus huku Jamii ikiteseka na maji
Hao wezi ndio hawakutaka kuona kiongozi anayehakikisha kila mtu ananufaika na miradi ya maendeleo.

Kwa ubinafsi wao wanaona ni sahihi kabisa na haki kwao kujilimbikizia mapesa ya wananchi wao na familia zao.

Ni jambo la kishetani mno kuwa na watu wa aina hii wenye tamaa iliyopitiliza ya pesa na mali.

Mtu yupo tayari kuona watu wanakosa barabara au hospital yenye vifaa na madawa lakini mwanae akasome ulaya na kutibiwa huko.
 
Hao wezi ndio hawakutaka kuona kiongozi anayehakikisha kila mtu ananufaika na miradi ya maendeleo.

Kwa ubinafsi wao wanaona ni sahihi kabisa na haki kwao kujilimbikizia mapesa ya wananchi wao na familia zao.

Ni jambo la kishetani mno kuwa na watu wa aina hii wenye tamaa iliyopitiliza ya pesa na mali.
Pesa za wizi huwa hazitoshi,kadri upatavyo na ndivyo idadi ya vimada inaongezeka
 
Yaani haya maisha kama uwezo wa kula bata unao, wewe kula bata tu.
Mhubiri 8:8
Hakuna mwenye uwezo juu ya roho aizuie roho; Wala hana mamlaka juu ya siku ya kufa; Wala hakuna kuruhusiwa katika vita vile; Wala uovu hautamwokoa yule aliyeuzoea
 
Had it been clearly posted kabla haujazaliwa na tukawa na option za kuchagua tuzaliwe ama la , ningeamua kutozaliwa.

Huwa napita makaburini na kushangaa kwa masikitiko , hayaonyeshi tofauti ya nani alikuwa hodari au maarufu, kaburi la profesa aliyestruggle na elimu akajifunza kusoma hadi kuaandika thesis , linalingana sawa tu na la marehemu babu yangu ambaye hata kusoma hakujua!

Why woud someone create a wolrd so unfair like this ? Soma unavyojua kusoma pata pesa unavyojua kupata ukifa ndo kila kitu kimeishia hapo. And I, sincerely hate this idea
Sayansi hapa inasema ulichagua kuishi, ktk sperm kuna mamilioni ya sijui chromosome/gene hushindana mbio kuingia kwenye yai la mwanamke, so mbio zako zilikuponza, make uliwazidi wale wengine milioni kadhaa.
 
Kuna mwanangu wa 9 years huwa ananiambia "la vie n'a pas de sens "Yaani maisha hayana maana,kama tulikuwa ni wa kufa kwa nini sasa tulizaliwa?Si Bora hata tusingekuwepo kabisa likajulikana moja. Huwa ninamjibu maisha yana maana. Tunakufa ili tubalance écosystème. Dunia hii ni ndogo sana watu wasingekufa isingekalika.Maisha yana kupanda na kushuka,kuna kuzeeka. Hivyo kufa ni sehemu ya maisha.
Mwanao anaongea mantiki na wewe unaongea siasa , ati ecosystem balance! , aliyeeumba huo ulimwengu hakujua kwamba tutazaliana ? Alikuwa na kila kitu at disposal kwa nini aumbe kifo ?, shetani alikuwa na ulazima gani kuumbwa?: Kwan hata angeumba bao moja tu ndo litoe mtoto baada ya hapo yanayofuata ni kwa ajili ya burudani , mbona tungezaliana kwa wastani tu .
 
Back
Top Bottom