Maisha na mikasa ya safari yangu nchini DR Congo miaka ya 2000's hadi kutaka kupigwa risasi hadharani


 
Inaendelea sehemu ya nne...

Ndugu nilikuwa napata Iftari kidogo nikawa nimesitisha kidogo kuandika kama mmnavyojua bado tuko ndani ya mwezi mtukufu wa ramadan ishallah tunaendelea kuwa pamoja .

Naomba nishauri kitu kimoja kwa wafutiliaji wa hii story ndugu ili uweze kusoma kitu na kujifunza au hata kupata burudani ni vyema ukapata story hiyo kwa hatua ili nawe uweze kutafakari mafunzo yaliyomo ndani yake hivyo basi kwa wale ambao wanafikiri kuwa kuandika tu story mwanzo mwisho ndo ujanja basi hakuna sababu ya kuifuatilia hii story mpite tu .kama nilivyosema mwanzo lazima niimalizie yote .


Twende kazi sasa wakati jamaa yule aliedandia pale nyuma anaendelea kuhangaika pale juu mara paapp akateleza bwana hadi chini kama unajua tulikuwa tumepakia mazulia na mahema ya wale jamaa nafikiri aliteleza kutokana na utelezi wa zile turubai aise jamaa akaanguka mzima mzima hadi katika ya lami mimi niko nyuma nikamkwepa kwa pembeni nikawa niko upande wa kulia cha kushangaza yule jamaa kumbe wakati anapanda alikuwa na simr anajaribu kutoboa zile turubai ndo kushikashika akajikuta ameteleza hadi chini.

Aise ghafla tu nikashangaa rama amesimama na akapiga revasi akarudi nyuma kumlenga yule jamaa pale chini na kumgonga kwa nyuma yanii gari ikapita juu yake yote halafu akarudia tena kwa mbele halafu akatoa kalele na vishindo vya maumivu ya yule binadamu nilivyokuwa navisikia nikiwa kwenye gari aise mwili mzima ulinisisimka yani unaona kabisa binadamu anamuua binadamu mwenzi wazi wazi tena kwa kumfinyanga na gari kwa maksudi kabisa nikiwa naangalia kwenye site mirror rama akanipa ishara ya tuendelee na safari tukaenda kidogo hadi mbele kama kilometer tano tukapaki akatoa maji ya chupa akaanza kusafisha damu kwenye plate namba na maeneo mengine ya mbele na nyuma hakika chini gari ilijaa damu tupu baada usafi tukaendelea na safari..

Mpaka boda hiyo saa kumi na moja ndo tumefika boda KASUBALESA.

Turudi nyuma kidogo pale jamaa yangu alipoua mtu.....tulivyofika boda
Rama ananihadithia kwa kunionyesha kovu upande wa kushoto wa jicho lake na kuniambia kovi hilo alolitoa hapo wakati akiwa tanboy wa magari makubwa alikuwa akifika maeneo hayo basi dereva anamwambia apende juu na panga kulinda wezi maeneo hayo kuna kilima flani hivi ambapo gari kubwa ikifika lazima ipande taratibu hivyo hao wezi walikuwa wanatumia mwanya kukata turubai na kuvunja kufuri kuiba bidhaa mbalimbali zinaelekea congo na humtanguliza moja akifanikiwa kukudhibiti linatokea kundi la wezi polini linakomba kila kitu unaambiwa vikundi hivyo hufadhiriwa na wafanyabishara wa mji mdogo wa Ndola kuiba na kwenda kuwauzia wao bidhaa za wizi kwa bei ya kutupa.
Sasa rama anahadithia kuwa kipindi gari lake lilivyofika tu pale yeye akakwea juu kama kawaida kumbe alikuwa na usingizi, kijiusingizi kikampitia bwana njemba ikapanda kustuka njemba ipo juu nae yupo juu ndo mapambano yakaanza lakini pamoja na kumshinda alimwachia majeraha kadha a yaliyomweka hospitali week nzima ndo akajiaza kuwa iwe isiwe siku ikitokea maeneo hayo likatokea tukio lolote likamuhusu lazima alipize kisasi na ile ndo akawa amelipizia kisasi siku .

Sasa tupo boda tunafanya mawasiliano.na wenyeji tumefika boda waje wachukue mzigo wao sisi tugeuke .maboss kubigiwa simu kuambiwa gari zao zipo salama wakafurahi sanaa wakaagiza kwa jamaa yao moja anauwezo flani pale kwa boda atuchukue kwake tukale na kulala yule jamaa akaja mpaka tulipo tulikopaki magari yetu boda na askali akapewa chake alinde magari ,sasa pale kuna
Askali analipwa na boda lakini usipompa chochote unaweza ibiwa na ukienda kulalamika hakuna wa kukusikiliza watu wako busy aise. Tukaenda kulala kwa ajili ya kuwa asu uhi kuonana na wenyeji wetu tuwakabidhi mali zao sisi turudi zetu home. Tukawa tunasikilizia pia lile tukioa la kuua kule. madereva wakija wanatoa taarifa ya maiti kwa askali sisi tukawa tunasikilizia tu hadi tulipochukuliwa na jamaa kulala hadi kesho.

LEO TU NIMEWEKA EPISOD NNE NAOMBA KWA USIKU NIWAACHIE HII NIPUMZIKE KESHO TUTAENDELEA NA ZINGINE ISHALLAH HADI TUMALIZE
 
Aah, Mzee Baba vp.....!?
Angalia usije kutulisha kiporo....

Mambo ya kesho hatutaki....😅😂🤣
 
Malizia hata moja shekhe mbona bado mapema Sana!
 
[emoji28]kwaiyo mkuu auta jibu comment zetu maana mmh
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…