Maisha na mikasa ya safari yangu nchini DR Congo miaka ya 2000's hadi kutaka kupigwa risasi hadharani

Maisha na mikasa ya safari yangu nchini DR Congo miaka ya 2000's hadi kutaka kupigwa risasi hadharani

jioni?? embu kua serious mzee baba atleast unge weka hata episode 2 au kaa uandike ukimaliza ndo uanze kupost hvo vipande vipande kuliko kutusubirisha
Washakutengenezea kiu hapo kuwa na subira tu MKUU
 
Ukimaliza kuandika story yote nitag nianze kuisoma.
 
[emoji848][emoji848][emoji848][emoji848]
 
Nawasalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Ndugu zangu bila shaka mwenyezimungu anaendelea kutupigania hadi sasa.

Ndugu leo naona nilete story kidogo kuhusu safari yangu moja hivi nchini DRC mikasa na visa mbali mbali kwa kipindi chote cha safari wakati napambana na maisha kwenye udereva ili niweze kuishi kama mnavyojua maisha ni popote na kujaribu ni muhimu kuangalia kila sehemu ili uweze kutoka ukinzingatia kuwa wengine shule yetu ni kidogo hivyo ni muhimu kijipambania kwa kila hali ili uweze kujikimu kimaisha tukawa tunashike hili na lile ili mrasi tuweze kuishi.

Story yangu ni ndefu kigodo ila ntajitahidi niimalize kwa wakati ili kuepuka zile maneno za kakimbia sijui nini ila naomba tuwe na uvumilivu tu kwani swala la kuandika nalo ni mtihani ukizingalia device tunazo tumia sio rafiki .kwa wale wasio wavumilivu naomba tupite tu hakuna haja ya kulalamika.

Story inaanzia hapa...

Miaka 2000's kulitokea wimbi kubwa la usafirishaji wa magari kutoka bandarini Dar kwenda DRC kipindi kicho ikitwa congo (kama sijakosea) kipindi hicho nilikuwa najishughulisha na udereva taxi pale Mapambano kijitonyama nikipindi ambacho biashara ya taxi ilikuwa na hela kiasi kwani biashara ya Bajaji na bodaboda ilikuwa bado na watu walikuwa hawajazoea kupanda vyombo hivyo, basii maisha yakawa yanasonga mbele kama sijasahau mwishoni mwa miaka ya 2001 ndo vita congo ilikuwa imepowa japo nilikuwa siwahi kufika huko hata mara moja.

Kijiweni kulikuwa kuna mshikaji alikuwa anaitwa Rama kwanza nikili kuwa huyu jamaa alikuwa mjanja kupitiliza na alikuwa anasafiri sanaa inasemekana hata nganda alikuwa anabeba japo tulikuwa wote pale pale kijiweni nae ana kigari chake mwenyewe anabeba abiria ndipo akanipa mchongo wa kusafiirisha magari ya wa kongo kwenda Congo kipindi hali haikuwa nzuri kwakweli hivyo madereva wengi walikuwa hawapendi kwenda huko japo wacongo walikuwa wanapanda offer ya mpaka dolla 250 kuifikisha gari KASUBALESA boda ya Congo na zambia then unamwachia anamilizia kipande chake.

Hapo ndipo jamaa yangu Rama alipopata hiyo fursa kwa jamaa yake alieoko pale bandarini ambae alikuwa na kampuni yake ya clearing na fowarding pale bandarini na kumwambia kuwa kuna wacongo wanahitaji magari yao yafike lumbumbashi then wao watayasafirishi kwa ndege kwenda kinshasa ila wao hawapandi hizo gari wao tutakutana lumbumbashi sehemymu moja sehemu moja kunaitwa KOTA naona nikaribu na soko kubwa la Lubumbashi mjini katikati.

Cha ajabu jamaa walitoa pesa yote kwa jamaa yao wa pale bandarini na kampuni ndo ilitakiwa isimamie kila kitu hapo ndipo mwanangu Rama akanitustua nakumbuka ilikuwa ni kati ya mwezi wa tano kwenda wa sita. Mvua zinanyesha Dar hakuna mfano abiria hakuna nikaona bora nitoe gari kwa jamaa nikimbize IT kwanza nami nipate uzoefu.

Baada ya jamaa yangu kuweka mambo sawa ikiwemo kupata passport ya karatasi na chanjo ya homa ya manjano mzes mzima siku ikawadia jamaa yule akatupa dolla 100 advance, 50 maillage na 50 ya barabarani nikiongea bararani mnilewe hiyo ya wazee .Gari mpya kutoka kiwandani yani bado zina makaratasi mitusubishi dabo cibin mpya kabisa wazee tukawekewa full tank. Zikabandikwa number za IT .siku ya j2 ndo safiri ikawa imeanza rasmi mara ya kwanza kusafiri na magari ya IT ila mwenzangi rama yeye alikuwa mzoefu hata kwa njia hio pia alikuwa anaijua vizuri na alikuwa anajua hata kizambia kidogo na kikongo kisawahili chao kile cha kuya Papa uko na makuta ngapi? Hhhhaaaa...

Safari imeanza.

ITAENDELEA JIONI...
Inaendelea sehemu ya tatu ..

Basii safari ikaanza asubuhi na mapema aise hapo tunaitafuta MPika hapo Rama anaamsha mashine vibaya nami nipo nyuma yake ,kama unakumbuka aliniambia nikiamasha nawe amsha hakuna kuniacha hata kwa mita ishirini chuma zinatembea baridi kali unawasha heater ya gari lakini wapi baridi inapenya hadi kwenye vitundu vidogo vya madilrisha aise selenji hapana si kwa baridi ile

Baada ya mwendo kama nusu saa hivi karibia na kilima kwenye kona nilishuhudia kitu cha ajabu sanaa kinatokea angani upande wa kulia kwanza mimi sikutambua chochote niliona mfano wa kimombo hivi unaanguka kutoka juu kuja chini kumbuka mimi nipo nyuma ya Rama chuma tumeziachi la vibaya yani hata mashimo tulikuwa tunafukia kumbe bwana rama ile michezo ya wazambia kurusha mawe anaijua ndo maana aliniambia nikitoka speed nawe kanyaga mafuta hadi mwisho kumbe garii ikiwa speed kukadiria uangushaji wa jiwe kutoka kilimani unakuwa mgumu kwani speed ya gari na jiwe unakuwa tofaouti sasa hakuniambia ila baadae aliniambia ningekuambia ungejawa na hofu hivyo ungepoteza comfidance ndo maana akakaa kimya kwani matokeo hayo huwa hayatokei mara kwa mara huwa wanakuwa na timing ya wa watu wao kutoka boda kuwatonya na ndo maana kule boda jamaa alivyotwambia tuvuke boda j3 Rama alikataa akataka tuvuke j4 tu kama tulivyokubaliana ,ndugu tembea uone yani unakuta jitu lipo customer pale na tai shingoni na simu kubwa kumbe ni informer wa majambazi njiani.

Sasa tuongee kidogo kuhusu huu uhuni wa kurusha mawe kwenye hicho kipande kuna vishimo vishimo hivi sasa kama wewe mgeni unapofika lazima utembee mwendo wa wastani sasa ukitembea mwendo huo ndo unawapa mwanya wale wezi kukurushia jiwe kubwa zaidi mara nyingi huwa hawakosei lazima likupate kama kawaida ukipigwa lile lazima uyumbe utasimama tu hapo hapo waliochini wanakuvaa unaporwa kila kitu na hata kukua hapo hapo barabarabi ndani ya dakika hilo gari linabaki na chasisi wanang'oa kila kitu.na maeneo hayo machuma ya magari kibao yaliyoungua moto.

Basi bana tupo mia ishirini fukia shimo likarushwa jiwe mara gafla nikaona kama Rama anatoka barabarani gafla kwa speed kali yani akawa anaendesha gari kwa pembeni huku anapiga honi kali kumbe ananipa ishara nami nitoke katikati ya barabara niendeshe pembeni mara ya kwanza nikajua labda anasinzia likini alivyozidi kukaa pembeni bila kuingia polini akili kengere ikalia kichwa ni nikakumbuka rama aliniambia kila nachokifanya nawe nifuate hivyo nami nikatoka road nikawa upande wa barabara pembeni barabara za zambia nyingi ni pana sanaa nikaona ameacha kupiga honi sasa mara nikaona jiwe kubwa kwa mbele linakatiza ktk ya barabara mara ghafla rama akarudi road chap chap nami nikarudi chap jiwe litapita vuuuupp niseme tu ukweli lile jiwe ni kubwa na kama lingetupata hiyo gari haiwezi kuwa gari tena sasa ngoma hapo niseme tu ukweli sijawahi kukimbia na gari katika maisha yangu kama tulivyokimbia kile kipande cha selenji - Mpika tulikimbia na zile gari yani kama tupo kwenye mashindano hapo uoga wote umeisha yani unaona kama umenusurika kifo kwente tundu la sindano.

Tukaendesha kwa speed kubwa sanaa tunakaribia mji wa kapili mposhi ndo nikaona rama anawasha indicator kuonyesha ishara ya kusimama pembeni mwa barabara tukapaki hapo mzee tukapumzika kidogo ndoa akawa ananipa story ya lile eneo aise kwa kweli niliogopa sanaa mbaya zaidi akaniambia alishampotezaka rafiki yake eneo lile na mbaya zaidi wale wezi baada ya kulipiga gari walimchoma moto ndani ya gari ili ionekane ni ajari tu ali kupoteza ushahidi aise kwakweli niliogopa sanaa ila Rama alikuwa jasiri aise usiombe, akagundua hilo akanipa moyo na maneno ya ujasiri ya hapa na pale tukatulia tukaanza safari ya kuukaribia mji wa wa kapiri mposhi saa nne asubuhi hiyo tukafika kwa mama msomali tukaagiza wali na nyama tukala unajua ukiwa mgeni wa safari unaweza dhani watu wanakosea kupika kumbe zambia wakipika waLi badala ya kuweka chumvi wao wanaweka sukari aisee nilishanga sanaa nikamuuliza rama akaishia kucheka na kunitania vijimaneno vya hapa na pale ..tukacheka pale akaniambia nimfuate tukapaki magari yetu maeneo hayo hata maroli huwa yanapaki akampa.kijana moja kwacha kidogo naona nikijana wa mama wa hotel wa kisomali akaniambia nimfuate nikamfuata tukavuka barabara hadi nyuma ya msikiti ndo tukamkuta mzee moja akamsalimia kumbe wanafahamiana akumuomba tuoge tukaingia pale bafuni zipo nyingi tukaoga safiii kabisa tukarudi kujipumzisha pale hotelini rama ananiambia safari tunaendelea saa nane mchana sasa tutulie tu tuzicheki cheki chuma kutoka pale hotelini mbele kidogo kuna shell mara nikaona kuna jamaa wawili wanakuja na madumu ya mafuta petrol sijui walitokea wapi rama akaniambia hao ndo tulikuwa tunawasubiri tukajaza mafuta tena top zile gari unajaza full tank halafu inakijitank kingine pembeni cha akiba mafuta ya kiisha unabonyeza batani u akitumia kama dharura unaweza tembea kilomita hata 50 .

Basi kufika saa nane safari ikaanza mdogomdogo rama mbele mimi nyuma tunauacha mji wa kapili.mposhi taratibu speed ya wastani tukachapa gia hadi njia panda kuelekea njia kuu ya Lusaka na boda ya LUBUMBASHI-ZAMBIA wanakuita KASUBALESA. Yanii hapo ndo safari yetu ilitakiwa iishie kulingana na makubaliano ya awali ila wakati tunafika boda kukutana na jama mpokeaji tukalizimike kuambiwa lazima tuingie lumbumbashi kabisa waliotakiwa kuja wameshimdwa kutokana mapigani ya waasi katikati barabara kuu ya lumbumbashi Tobaaa nyongeza dola 75. Mara ya kwanza nilimbishia sanaa Rama tuachane na huo mpango lakini Rama aligoma kabisa lazima atoboe hata kama vipi pale kuna kama 12okms hivi ntaelezea mbele nini kilitokea pale boda hadi mimi na Rama tukataka kuhitirafiana nafsi ilishahisi hatari mbeleni..tuendelee.

Na safari yetu tukakunja barabara kuu tukawa ndo tunaiacha kapili mposhi rasmi hapo tunaitafuta barabara ya kuu ya mwelekeo wa mji wa NDOLA nyiee ukifika ndola unaweza dhani upo masaki ni kamji kadogo kazuri sanaa halafu wageni wengi na supermerket kibao aise tukapita pale jamaa akaniambia tuchepuka barabara kuu twende ndola kidogo tukasuuze macho wenzetu wazambia namba za IT Hazina shida ukichepuka barabara kuu tofauti na sisi yaniii utoke bandarani na namba za IT wende masaki kutoka barabara kuu . lazima njau wakudake zambia unaweza tembea na namba zai IT mtaani hata siku mbili mle mle ndani...

Basi tukaelekea ndola bana huko tulienda kusuuza macho tukakaa kama masaa mawili tukarudi njia kuu kuelekea boda kuna sehemu kunaitwa CHILABOMBWE kilomita 30 kutoka boda rama alifanya kitu ambacho kilinifanya hata mimi nianze kumuogopa aise .....wakati tunaendelea na safari taratibu nikashaanga kuna mtu katokea tu polini ghafla kuna mtu karukia nyuma ya gari la Rama nikampigia honi...rama badala ya kupunguza mwendo yeye akaongeza kumbuka tuko porini hapo na tulikuwa mwendi mdogi wa wastanii kabisaa..


Itaendelea ......
 
Back
Top Bottom