Maisha ya Afrika Kusini siyo poa

Maisha ya Afrika Kusini siyo poa

Kule ni kama vile Dar kuna masaki, Mwananyamala, Sinza etc. - Johanesburg Hillbrow mfano ni kama Mwananyamala (roba za mbao n.k) Sandton ni kama Masaki- full kamera na doria za Police- ukionekana unatembea kwa miguu tu Police lazima wakusimamishe wajue unaenda wapi na ni nani wewe! Na barabara za kuingia sehemu za wanaokaa matajiri kuna road block zinazohamishika kila dakika. Ukifikia Mashenzini kweli utaiona Sauz ni ya kikatili na Umalaya kama vile Wageni (wakongoman na Wanaijeria wanaoishi Kinondoni na Mwananyamala) daima watasema Dar apafai!
Masaki na Sandton ni kama kifo na usingizi mkuu, Sandton pazuri sana
 
Uhalifu unakomeshwa kwa kutumia bunduki, ni kuwasaka wakuu wa magenge ya uhalifu na kuwatupa tu baharini. Jinsi ya kuwapata viongozi wao ni kuwasaka wahalifu na kuwapa mateso wanataja baada ya kutaja wanapigwa risasi kisha wanafatwa wengine hivyo hivyo ndani ya miezi 3 wote wameisha ndicho walivyofanya Rwanda.
Huwezi mpeleka mwizi jela utegemee abadilike jela zenyewe ni kama paradise halafu abadilike. Mwizi ni shetani na shetani asikii neno ila bunduki. Wezi wote mtaani wanajulikana na police. Waganga wote uwajua wachawi wote mtaani.
 
Umesahau na rape, hii kule wahalifu wanaona ni kawaida kubaka.
South carjacking, house robbery, murder and rape ujitayarishe navyo.
Sehemu salama kwako, labda uende sehemu za utalii. Kidogo huko polisi wanapalinda sana.

Sababu ya crime kuwa juu, South Africa. Wanasema baadhi tu ni Unemployment, Ufisadi mkubwa wa Serikali, hawajali tabaka la chini na Alcohol.
Binasfi naona ukiondoa Mandela na Mbeki , marais waliofaata ZUMA na RAMAPHOSA ni majambazi tu , criminals!!!!!!!!
 
Shida ni income disparity-Nelson Mandela watu wanamuona shujaa kutokana na kuwakumbatua makaburu lakini kwa sisi wabobezi wa mambo hapo ndio tunaona alichemka.

S.A means of production zote zina milikiwa na makaburu na mbaya zaidi wameenda mpaka level ya chini-unategemea watu wako wataishi vipi?

Hata hapa Tanzania ni bahati tu kuwa ardhi getu ni mkubwa kuliko population tuliyonayo-subiri baada ya miaka 30-50 ijayo hiyo crime rate ya South itakuwa cha mtoto.
Nchi zote za africa ukiacha za kiarabu zina uchumi unaomilikiwa na mabepari au wahindi.

Uchumi wa Tz unamilikiwa na wahindi kwa zaidi ya 70%.
 
Matola, Hillbrow Kuna mchezo mchafu unaochezwa hasa na Zimbabweans wa kuteka nyumba na kuishi bure bure.... ndiyo maana ukipita hapo Sasa hivi maghorofa mengi yametelekezwa. Mengi hayana umeme n.k.

Wamiliki wamesha give-up. Operation Dudula imeshindwa kufanya kazi sababu kubwa Wasouth wamegawanyika. Malema anaichukua hii opportunity to gain political popularity.... nothing else.

City center ya Jozi Ina megeni mingi kuliko wazawa... ukiniuliza data sina. Kwa report tu iliyofanyika siku Moja waligundua wageni wanaopita Beitbridge kwa siku ni mia mbili lakini sitini wanarudi. 140 hubaki ndani ya South Afrika.

Nikirudi kwenye mada... Uhalifu wa SA unasababishwa na wageni kwa asilimia nyingi nyingi saana.
Daah hizi data za wapi wageni wapite kama bus saba tuu hapo Messina aisee kazi ipo...na unaandika maandishi marefu kwa kwa taarifa hii..
 
Sasa mkuu unasema baada ya hiyo miaka 30-50 crime rate ya Tanzania itakuwa kubwa na ya South itakuwa cha mtoto...!

maana yake crime rate ya South yenyewe itakuwa imeganda tu au ina decline? Kwamba rate yao haiongezeki ila ya Tanzania ndio inaongezeka tu hadi kupita crime rate ya South?
Huwa inatokea raia wanachoka kabisa na uhalifu, wanampigia kura mtu anayeahidi kupambana na uhalifu kwa mkono wa chuma, kama Durtete vile. Huko mbeleni unaweza kupungua. uliberali huaga si mzuri kwa usalama wa nchi.
 
Sasa Pagad sio Wauzaji wa Madawa, Pagad sio Gang Crew, Pagad ni Waislam ambao waliamua kupambana na hayo Magenge ya Kihuni, Member alikua anauliza kuhusu 26, nikaamua nipe info japo kwa uchache kuhusu hizo number, hakukuwa na sehemu ningeweza kuwazungumzia Pagad, labda siku nikizungumzia Historia ya haya Makundi, then Pagad wana nafasi ya kuzungumziwa.
Pagad ni genge la wauza madawa waliojificha kwenye kimvuli cha waislamu, Wamorocco wengi ni members wa kundi ka Pagad.

Huwezi kuliweka kundi la Kigaidi kama Pagad kwamba ni la kidini, hakuna dini inayobariki kutega mabomu ili kuuwa watu.

Ugomvi wa Pagad wao ndio wanataka kudhibiti biashara ya Dawa za kulevya at the same time wanajificha kwenye kimvuli cha waislamu kujifanya wanapiga vita biashara ya Dawa za kulevya.

Nimeishi Bookap nawajuwa vizuri Pagad.
 
Nafikilia kuanzisha Uzi hapa kuzungumzia nguvu ya hizi numbers kwenye Maisha ya kila siku ya SA, Mitaani na Gerezani...!

26 ni Gang crew, kama ilivyo 27 na 28, hizo numbers zina nguvu sana Gerezani, Maisha yako yatakua ya dhiki kubwa kama ukienda Jela hafu ukawa sio member wa hizo numbers, japo huku Mtaani number zinageuka na kuwa na Majina ya Crew, miongoni mwa kundi Hatari na kubwa hapa Cape town, ni Americano, Mongolos, Yankees, School Boy etc.

Hawa wanauana dairy kwa kutafuta himaya ya kuuza Madawa, Wanaiba, wanakaba mtaani na kila aina ya Ufedhuri, Mf. Ndani ya Americano kuna 26, 27 na 28 wanapambana na Mongolos yenye 26, 27 na 28 pia, ila wakienda Jela, hakuna Americano, hakuna Mongolos wala majina mengine, ila wanaishi pamoja kwa numbers zao!
Japo kwenye Jela moja kubwa inaitwa Possmall, kuna mtu hatari sana, anamiliki Number 28 anaitwa John Mongol, ambaye ndo mwanzirishi wa kundi la Mongolos ambalo linasebenza Mtaani, huyu Mtu ni mtu ambaye sio mtu mzuri hata ukimtizama.

Wana salamu zao za ishara, means mtaani mtu akikusalimia unajua huyu ni 26, 27 au 28, wanaenda mbali wana Lugha yao wanaelewana wenyewe, inaitwa Sabela, hakuna mtu anaelewa hiyo Lugha zaidi yao wenyewe.

Member wa kundi lolote hajakukaba au kukuibia mpaka ajitamburishe kuwa yeye anamiliki number ipi, atapiga mguu chini, salamu ikiambatana na Kujitamburisha kwake kwako na Lugha yao ya Sabela, kama wewe unamiliki namba pia means utajibu na yeye atajua huyu ni mwenzagu, kama katika kusalimiana anatambua wewe ni mkubwa kuliko wewe, atapiga Saluti, otherwise, utaenda kuhadithia Nyumbani.
(Wako vyeo vyao ambavyo wanajichora kama Tatoo)

26- Ni Watu watafutaji pesa, Brothermen wanapenda kupendeza na wanajua kutafuta pesa.

27. Ni Wauaji straight, akipewa Amri akuue, harudi nyuma, mpaka akuue, na ni mbaya kama amri ikitoka Jela, coz asipokuua atauwawa yeye, na yeye hawezi kukubari kufa kwa ajiri yako. Kuua kunampa Cheo zaidi kwenye Crew aliyopo.

28. Wanajihusisha na Mapenzi hata ya jinsia Moja, lakini pia anaweza kuua....

Hawa ndo wanaifanya SA iwe na Ushenzi tunaousikia, Hawa wanauza Madawa straigjt kwa watu wao, lipo kundi moja lipo Cape town, town kabisa, linaitwa UnderWorld Cape gang, hili kundi lina Connection mpaka na makundi Makubwa ya kuuza Unga toka Latin America, linaingiza madawa Cape town tokea Brazil....!

Sawa Wabongo wanauza madawa, na Wanigeria pia, ila Wabongo wengi na Wanigeria wengi ni kama Machinga wa madawa mbele ya hawa Raia wa Kirangirangi.

Wageni wanaofanya kazi halali ni wengi kuliko wanaofanya Mazabe.
umedadavua vizuri, Asante sana kwa maarifa.
 
Ukienda tour hata hayo matukio ya South Africa utaishia kuyasoma mtandaoni tu na kuona kwenye TV Tu.

Cape town inapokea watalii wengi sana kila mwaka kutoka duniani na hakuna mtalii añapata tatizo lolote.
Najua. Nina wadogo zangu walisoma University of Cape Town bado kidogo tu niwatembelee.

I am just protesting the widespread xenophobia there.
 
Usijidanganye kwenda bondeni kutafuta maisha kama huna msingi, wala kibali. Kama unaweza kulipa nyumba Milioni kwa mwezi hapa Tanzania basi unaweza kuishi huko.

Kama unaweza kuishi Masaki na Mbezi beach basi unaweza kuishi huko sababu tabia za huko mazoea ya uswahilini hakuna, ukiweza kuishi South Africa na ndio umeweza kuishi nchi yoyote iliyopo Ulaya na pengine.

South Africa gredi ya uhalifu ni kubwa sana, kesi za kufa watu zipo nyingi kuliko kesi nyengine, ingekuwa tz kila siku kamanda wa polisi anatangaza mwisho hata choka.

Ngono kule ni kitu cha kawaida yani unatongoza mchana usiku unapewa, sio huku kwetu mpaka uchunwe kwanza.

Ukiwa na misosi ya kutosha na nyumba utachagua wanawake mpaka UKIMWI ukufikie, wanathamini kula sana maana maisha magumu kwao. Wezi, wauza madawa, wakwepa kodi na n.k wanaogopa kuweka pesa zao benki sababu benki za huku ni kama TRA kukuchunguza, Rais Ramaphosa ni mfano tosha.

Wizi wa magari ni kama wizi wa simu, gari nyingi zinazoingia hapa kwetu nyingi za wizi zinatoka huko. Vigogo wakubwa na wauza ngada hapa Tz wanaishi huko au kuwa na makazi ni wengi tu.

Msidanganye na wasanii wanasema wamenunua nyumba bali kule nyumba unaweza kununu tena nzuri ila ni kama umekodi, tofauti ya tanzania ardhi ina bei utadhani unanunua madini.

Kuvamiwa ni jambo la kawaida, wezi wakule usumbufu hawataki unaenda kwa order ukileta ubishi ni kugusa kaburini.

Huwezi kuchezea simu ovyo maana mitaa yote kuna wahalifu usipo kuwa makini unaweza kuona benzi kali inapita kumbe wapo wezi, ukifika nyumbani kama kuna geti lazima uchunguze mbele na nyuma nani anakufata ijalishi gari au mtembea miguu na hatua kidogo kabla ujafika getini, unaingia nao.

Vijana wetu waliozamia ukiona kaenda karudi katoboa maisha, mawili ni mchomoko au madawa.

Mchomoko ni kuvizia nyumba wenyewe hawapo tena nyumba hizi kama nilivosema wanaoweka pesa za kutakatisha.

South sio poa.
mwandende
 
Usijidanganye kwenda bondeni kutafuta maisha kama huna msingi, wala kibali. Kama unaweza kulipa nyumba Milioni kwa mwezi hapa Tanzania basi unaweza kuishi huko.

Kama unaweza kuishi Masaki na Mbezi beach basi unaweza kuishi huko sababu tabia za huko mazoea ya uswahilini hakuna, ukiweza kuishi South Africa na ndio umeweza kuishi nchi yoyote iliyopo Ulaya na pengine.

South Africa gredi ya uhalifu ni kubwa sana, kesi za kufa watu zipo nyingi kuliko kesi nyengine, ingekuwa tz kila siku kamanda wa polisi anatangaza mwisho hata choka.

Ngono kule ni kitu cha kawaida yani unatongoza mchana usiku unapewa, sio huku kwetu mpaka uchunwe kwanza.

Ukiwa na misosi ya kutosha na nyumba utachagua wanawake mpaka UKIMWI ukufikie, wanathamini kula sana maana maisha magumu kwao. Wezi, wauza madawa, wakwepa kodi na n.k wanaogopa kuweka pesa zao benki sababu benki za huku ni kama TRA kukuchunguza, Rais Ramaphosa ni mfano tosha.

Wizi wa magari ni kama wizi wa simu, gari nyingi zinazoingia hapa kwetu nyingi za wizi zinatoka huko. Vigogo wakubwa na wauza ngada hapa Tz wanaishi huko au kuwa na makazi ni wengi tu.

Msidanganye na wasanii wanasema wamenunua nyumba bali kule nyumba unaweza kununu tena nzuri ila ni kama umekodi, tofauti ya tanzania ardhi ina bei utadhani unanunua madini.

Kuvamiwa ni jambo la kawaida, wezi wakule usumbufu hawataki unaenda kwa order ukileta ubishi ni kugusa kaburini.

Huwezi kuchezea simu ovyo maana mitaa yote kuna wahalifu usipo kuwa makini unaweza kuona benzi kali inapita kumbe wapo wezi, ukifika nyumbani kama kuna geti lazima uchunguze mbele na nyuma nani anakufata ijalishi gari au mtembea miguu na hatua kidogo kabla ujafika getini, unaingia nao.

Vijana wetu waliozamia ukiona kaenda karudi katoboa maisha, mawili ni mchomoko au madawa.

Mchomoko ni kuvizia nyumba wenyewe hawapo tena nyumba hizi kama nilivosema wanaoweka pesa za kutakatisha.

South sio poa.
Nadhani huu Uzi una mwendelezo Kuna mengi ya kujifunza apa
 
Back
Top Bottom