Sehemu YA kwanza
*(Uandishi wangu si mzuri sana)
Jina langu ni Vintage1q. Nimezaliwa mwishoni mwa miaka YA themanini na kukulia ughaibuni kwa takribani miaka 12. Nimezaliwa katika familia YA hali YA chini kabisa na mimi nikiwa ndo mtoto wa kwanza wa kiume.
Kukulia na kuishi ughaibuni kwa miaka yote 12 ilikuwa kama zali tu(nitaelezea siku nyingine). Baada ya kurudi nyumbani, mwishoni mwa miaka ya tisini, nikaangalia uhalisia wa mazingira niliyozaliwa, hakika niliumia sana. Mama yangu mzazi siku moja alinishika mkono na kuniambia kwamba jambo pekee litakalotukomboa katika hali ya umaskini, ni wewe kusoma kwa bidii. Niliamua kwenda shule na kusoma kwa bidii. Mimi ni miongoni mwa wanafunzi pengine wachache ambao nimesoma kuanzia darasa la kwanza mpaka kidato cha nne nikishika namba moja pekee.
Baada ya kusoma na kumaliza kidato cha sita, wakati fulani nikiwa katika makambi ya wasabato, siku ya jumamosi, nilipokea ujumbe kwenye karatasi ndogo iliyokunjwa ukiniomba nikutane na dada mmmoja ambae alitaja jina Lake kama(hapa nintatumia Upendo). Baada ya ibada alinifuata na kunisalimia. Alikuwa bado mgeni machoni pangu. Baada ya maongezi, alinifahamisha kwamba wakati mimi nipo kidato cha nne yeye alikuwa kidato cha pili katika shule ile ile. Upendo alikuwa mrembo sana. Aliniambia dhahiri kwamba alikuwa anani-admire sana ila alikuwa anashindwa kuwa na ukaribu na mimi kwa sababu muda wote nilikuwa busy na masomo.
Baada ya mazungumzo marefu, Upendo aliniambia kwamba hata hivyo Ana bahati mbaya kwa sababu hajafanya vizuri kwenye masomo yake na hakuona nafasi ya kuwa na mimi tena kwani wanaume wengi waliosoma, wanapenda wanawake wenye hadhi yao(alipata division IV-28). Kwa utani, nilimuahidi kwamba ningemuoa na akaniomba twende nyumbani kwao kuwasalimia wazazi wake(si mbali na pale mahubiri yalikuwa yakifanyika). Tulikwenda na akanitambulisha kwa wazazi wake kwamba mimi ni rafiki yake. Wiki chache baadae matokeo ya kidato cha sita yalitoka na nilikuwa nimefaulu vizuri. Niliomba chuo na nikawa nimepata nafasi katika mojawapo ya vyuo vikubwa hapa nchini.
Nilijiandaa na hatimae kwenda kuanza masomo ya chuo kikuu. Upendo nae alipata nafasi ya kwenda kusoma chuo cha ualimu wa msingi. Baada ya kufika chuoni, niliugua sana. Nilikuwa nikivimba miguu na mikono. Nilishindwa kutembea kabisa. Kadili siku zilivyosonga, nikienda hospital na kwa wachungaji kuombewa bila nafuu, hali ilikuwa inazidi kuwa mbaya sana. Hatimae nilipata wazo la kuahirisha masomo. Niliwasiliana na Upendo na kumueleza adhima yangu hiyo. Alinisihi sana nisiache masomo na yeye alikuwa tayari kuacha masomo na kuja kuishi na mimi hadi nitakapo pata ahueni. Niliona ni jambo gumu lakini kesho yake alisafiri na kuja mpaka chuoni akapokelewa na rafiki yangu akamleta ghetoni tulipopanga.
Upendo alinisaidia sana. Ndio alikuwa mtu pekee wa kunisapoti upande ambao ulikuwa na madhara zaidi na kunikokota hadi chuoni. Baadhi ya walimu wangu walimpenda sana. Wakawa wanamsihi kukaa hadi muda wa vipindi unapokwisha. Akinisaidia kutoka lecture room moja kwenda nyingine. Wazazi wake walikasirika sana. Wakamuambia kwamba si mtoto wao tena. Alikuwa akilia sana. Lakini muda wote alikuwa akiniambia kwamba faraja yake ni mimi. Alinionesha mapenzi ya dhati sana.
*(Uandishi wangu si mzuri sana)
Jina langu ni Vintage1q. Nimezaliwa mwishoni mwa miaka YA themanini na kukulia ughaibuni kwa takribani miaka 12. Nimezaliwa katika familia YA hali YA chini kabisa na mimi nikiwa ndo mtoto wa kwanza wa kiume.
Kukulia na kuishi ughaibuni kwa miaka yote 12 ilikuwa kama zali tu(nitaelezea siku nyingine). Baada ya kurudi nyumbani, mwishoni mwa miaka ya tisini, nikaangalia uhalisia wa mazingira niliyozaliwa, hakika niliumia sana. Mama yangu mzazi siku moja alinishika mkono na kuniambia kwamba jambo pekee litakalotukomboa katika hali ya umaskini, ni wewe kusoma kwa bidii. Niliamua kwenda shule na kusoma kwa bidii. Mimi ni miongoni mwa wanafunzi pengine wachache ambao nimesoma kuanzia darasa la kwanza mpaka kidato cha nne nikishika namba moja pekee.
Baada ya kusoma na kumaliza kidato cha sita, wakati fulani nikiwa katika makambi ya wasabato, siku ya jumamosi, nilipokea ujumbe kwenye karatasi ndogo iliyokunjwa ukiniomba nikutane na dada mmmoja ambae alitaja jina Lake kama(hapa nintatumia Upendo). Baada ya ibada alinifuata na kunisalimia. Alikuwa bado mgeni machoni pangu. Baada ya maongezi, alinifahamisha kwamba wakati mimi nipo kidato cha nne yeye alikuwa kidato cha pili katika shule ile ile. Upendo alikuwa mrembo sana. Aliniambia dhahiri kwamba alikuwa anani-admire sana ila alikuwa anashindwa kuwa na ukaribu na mimi kwa sababu muda wote nilikuwa busy na masomo.
Baada ya mazungumzo marefu, Upendo aliniambia kwamba hata hivyo Ana bahati mbaya kwa sababu hajafanya vizuri kwenye masomo yake na hakuona nafasi ya kuwa na mimi tena kwani wanaume wengi waliosoma, wanapenda wanawake wenye hadhi yao(alipata division IV-28). Kwa utani, nilimuahidi kwamba ningemuoa na akaniomba twende nyumbani kwao kuwasalimia wazazi wake(si mbali na pale mahubiri yalikuwa yakifanyika). Tulikwenda na akanitambulisha kwa wazazi wake kwamba mimi ni rafiki yake. Wiki chache baadae matokeo ya kidato cha sita yalitoka na nilikuwa nimefaulu vizuri. Niliomba chuo na nikawa nimepata nafasi katika mojawapo ya vyuo vikubwa hapa nchini.
Nilijiandaa na hatimae kwenda kuanza masomo ya chuo kikuu. Upendo nae alipata nafasi ya kwenda kusoma chuo cha ualimu wa msingi. Baada ya kufika chuoni, niliugua sana. Nilikuwa nikivimba miguu na mikono. Nilishindwa kutembea kabisa. Kadili siku zilivyosonga, nikienda hospital na kwa wachungaji kuombewa bila nafuu, hali ilikuwa inazidi kuwa mbaya sana. Hatimae nilipata wazo la kuahirisha masomo. Niliwasiliana na Upendo na kumueleza adhima yangu hiyo. Alinisihi sana nisiache masomo na yeye alikuwa tayari kuacha masomo na kuja kuishi na mimi hadi nitakapo pata ahueni. Niliona ni jambo gumu lakini kesho yake alisafiri na kuja mpaka chuoni akapokelewa na rafiki yangu akamleta ghetoni tulipopanga.
Upendo alinisaidia sana. Ndio alikuwa mtu pekee wa kunisapoti upande ambao ulikuwa na madhara zaidi na kunikokota hadi chuoni. Baadhi ya walimu wangu walimpenda sana. Wakawa wanamsihi kukaa hadi muda wa vipindi unapokwisha. Akinisaidia kutoka lecture room moja kwenda nyingine. Wazazi wake walikasirika sana. Wakamuambia kwamba si mtoto wao tena. Alikuwa akilia sana. Lakini muda wote alikuwa akiniambia kwamba faraja yake ni mimi. Alinionesha mapenzi ya dhati sana.