Maisha ya ndoa na familia

Maisha ya ndoa na familia

Sehemu ya saba
Baada ya kunicheka aliniuliza kama ananitumia kwa ile namba. Akatuma elfu 10 na kisha akanitumia ujumbe kwamba yupo na mpenzi wake kwahiyo nisiwe nampigia simu. Nilimshukuru na kumtakia maisha mema. Nilimuomba anisaidie nyaraka zangu za kitaaluma na akanielekeza sehemu ambapo nitazipata.

Nipokea nyaraka zangu. Wakati huu nilikuwa nimechoka. Nilikonda na kuwa mtu wa ajabu kabisa. Kutoka kuvaa suti karibia siku tano za wiki na kufikia kuwa katika mavazi machafu yasiyoelezeka. Nilivaa ndala zilizofungwa na kamba.

Wakati fulani nikiwa katika mawazo mazito, niliamua kutaka kujiua lakini kwanza nikatafuta simu niongee na mtoto wangu niliezaa na Upendo. Mtoto wangu alinisalimia kisha akaniambia kwamba, "Dad, you promised to come back for me. Please remember that I miss you". Nililia sana siku ile na nikaamua kuendelea kupambana.

Nitawataja watu wachache hapa maana najua ni kwa nia njema. Wakati nahangaika, nilitafakari kukutana na kaka yangu mmoja hapa JF. Sikuwahi kuwasiliana nae kabla lakini moyo ulinisukuma kuongea nae. Nilitamani anisaidie viatu ili nipate kwenda kwenye sehemu moja ambayo nilialikwa kwa ajili ya interview. Nilimu-pm akaniomba tuonane kibada. Nilitembea kutoka rangi tatu hadi kibada kwa mguu.
Ilikuwa bahati mbaya maana siku ile hakunipa viatu kama nilivyoomba. Alinitazama kisha akanipa elfu 10. Nilikuwa na njaa sana. Nilikuwa sijapata chakula kwa muda mrefu. Nilitumia ile pesa kiasi kupata chakula pale kibada. Baada ya kuwasiliana tena, aliniomba nifike kibaha. Nilitembea tena kwa mguu hadi kibaha. Nilichoka sana. Alinipa nguo pamoja na viatu. Brother Jr., asante sana na Mungu akubariki.

Nilikuwa na jamaa yangu mwingine yupo humu anaitwa clearmind. Nilisoma nae na alikuwa mtu wangu wa karibu sana. Nakumbuka kipindi anataka kunisaidia aligombana sana mchumba wake na kwa bahati mbaya wakaachana. Niliumia sana nikaogopa kuendelea kumuomba msaada.

Nilipona msongo wa mawazo. Nipo Dar napambana. Sipo kama nilivyokuwa japo hali bado ni ngumu sana. Nina imani nitarejea tena upya. Yaliyotokea yote katika maisha yangu nayaangalia kama changamoto mpya zinazonijenga kuelekea kwenye hatima yangu iliyo njema zaidi. Nimejisikia amani kushea nanyi safari yangu hii ambayo imekuwa na matukio mengi ya kuumiza. Asanteni sana na Mungu awabariki.
Vintage1q.
Enjoy your life to the fullest today because tomorrow's never promised!
Pole na hongera ndugu.
Endelea kupambana.
 
Pole sana braza Kwa mapito yako magumu lakini naimani umeyaweka hapa ili tujifunze.
Kuna vitu tunavifanya kama wanaume vinakuja kuwa bakora maisha yetu yote. Kosa la kwanza umelifanya kipindi upo na pendo ni kumuonesha kuwa Kuna mtu unamjali na kumthamini kuliko hata yeye na wazazi wako.
Kipindi umemsimasha asiende nyumbani kwenu aanze Kwa rafiki Dodoma umemfanya apate interest yakutaka kujua ananini haswa kuwa mtu muhimu kiasi hiko akajikuta anaanguka kwenye zinaa, kosa limeanzia kwako.
Kosa la pili ni Kwa yasinta, kwanza naona alikubali kuoleea na wewe baada ya kuona upo desperate na ndoa, pia unapesa. Kitendo Cha wewe kukubali masharti yake Yani kubadili dini na kimfuata manyara ulikuea umeingia kwenye mtego wake na kukuona anaweza kukuongoza sio wewe kumuongoza yeye.
Mwanaume lazima uwe na misimamo yako. Mwenye kuweza kuifuata tunaanza kumconsider.
 
Pole sana braza Kwa mapito yako magumu lakini naimani umeyaweka hapa ili tujifunze.
Kuna vitu tunavifanya kama wanaume vinakuja kuwa bakora maisha yetu yote. Kosa la kwanza umelifanya kipindi upo na pendo ni kumuonesha kuwa Kuna mtu unamjali na kumthamini kuliko hata yeye na wazazi wako.
Kipindi umemsimasha asiende nyumbani kwenu aanze Kwa rafiki Dodoma umemfanya apate interest yakutaka kujua ananini haswa kuwa mtu muhimu kiasi hiko akajikuta anaanguka kwenye zinaa, kosa limeanzia kwako.
Kosa la pili ni Kwa yasinta, kwanza naona alikubali kuoleea na wewe baada ya kuona upo desperate na ndoa, pia unapesa. Kitendo Cha wewe kukubali masharti yake Yani kubadili dini na kimfuata manyara ulikuea umeingia kwenye mtego wake na kukuona anaweza kukuongoza sio wewe kumuongoza yeye.
Mwanaume lazima uwe na misimamo yako. Mwenye kuweza kuifuata tunaanza kumconsider.
Ni kweli, nilifanya makosa kadhaa. Nina imani kuna jambo la kujifunza kwa wengine na ndio maana nimeshea hapa. Asante sana.
 
Asante! "Makambi 2024 nitakwenda mimi na familia yangu". Rudi kundini mkuu.

Turudi kwenye mada, Jipange upya mkuu ukizingatia una binti anayekutegemea. Na kamwe usikubali mwanamke akuamulie mambo kama ilivyotokea kwa Yasintha.
 
Nilidhani ni story ya kutunga hadi ulipowahusisha member wa humu jukwaani, na nilitamani iwe ya kutunga kwa vile inaumiza sana mtu kupitia yote haya.

Mkuu, pole sana. Itunze imani yako, siku yako yaja na haya yote yatabaki historia badala ya maumivu.
 
Nilidhani ni story ya kutunga hadi ulipowahusisha member wa humu jukwaani, na nilitamani iwe ya kutunga kwa vile inaumiza sana mtu kupitia yote haya.

Mkuu, pole sana. Itunze imani yako, siku yako yaja na haya yote yatabaki historia badala ya maumivu.
Hii ni sehemu tu kati ya mengi. Nawashukuru sana wachache walionifikia.
 
Sehemu ya saba
Baada ya kunicheka aliniuliza kama ananitumia kwa ile namba. Akatuma elfu 10 na kisha akanitumia ujumbe kwamba yupo na mpenzi wake kwahiyo nisiwe nampigia simu. Nilimshukuru na kumtakia maisha mema. Nilimuomba anisaidie nyaraka zangu za kitaaluma na akanielekeza sehemu ambapo nitazipata.

Nipokea nyaraka zangu. Wakati huu nilikuwa nimechoka. Nilikonda na kuwa mtu wa ajabu kabisa. Kutoka kuvaa suti karibia siku tano za wiki na kufikia kuwa katika mavazi machafu yasiyoelezeka. Nilivaa ndala zilizofungwa na kamba.

Wakati fulani nikiwa katika mawazo mazito, niliamua kutaka kujiua lakini kwanza nikatafuta simu niongee na mtoto wangu niliezaa na Upendo. Mtoto wangu alinisalimia kisha akaniambia kwamba, "Dad, you promised to come back for me. Please remember that I miss you". Nililia sana siku ile na nikaamua kuendelea kupambana.

Nitawataja watu wachache hapa maana najua ni kwa nia njema. Wakati nahangaika, nilitafakari kukutana na kaka yangu mmoja hapa JF. Sikuwahi kuwasiliana nae kabla lakini moyo ulinisukuma kuongea nae. Nilitamani anisaidie viatu ili nipate kwenda kwenye sehemu moja ambayo nilialikwa kwa ajili ya interview. Nilimu-pm akaniomba tuonane kibada. Nilitembea kutoka rangi tatu hadi kibada kwa mguu.
Ilikuwa bahati mbaya maana siku ile hakunipa viatu kama nilivyoomba. Alinitazama kisha akanipa elfu 10. Nilikuwa na njaa sana. Nilikuwa sijapata chakula kwa muda mrefu. Nilitumia ile pesa kiasi kupata chakula pale kibada. Baada ya kuwasiliana tena, aliniomba nifike kibaha. Nilitembea tena kwa mguu hadi kibaha. Nilichoka sana. Alinipa nguo pamoja na viatu. Brother Jr., asante sana na Mungu akubariki.

Nilikuwa na jamaa yangu mwingine yupo humu anaitwa clearmind. Nilisoma nae na alikuwa mtu wangu wa karibu sana. Nakumbuka kipindi anataka kunisaidia aligombana sana mchumba wake na kwa bahati mbaya wakaachana. Niliumia sana nikaogopa kuendelea kumuomba msaada.

Nilipona msongo wa mawazo. Nipo Dar napambana. Sipo kama nilivyokuwa japo hali bado ni ngumu sana. Nina imani nitarejea tena upya. Yaliyotokea yote katika maisha yangu nayaangalia kama changamoto mpya zinazonijenga kuelekea kwenye hatima yangu iliyo njema zaidi. Nimejisikia amani kushea nanyi safari yangu hii ambayo imekuwa na matukio mengi ya kuumiza. Asanteni sana na Mungu awabariki.
Vintage1q.
Enjoy your life to the fullest today because tomorrow's never promised!
Asante utafanikiwa sana
 
Pole sana mkuu kwa maswaibu unayopitia..but kosa kubwa unalofanya ww ni kuwapa kipaumbele sana wanawake kuliko kusudi la maisha Yako..

Nimekunote umesafiri mara kadhaa kufata mwanamke badala yy ndio akufate... unawezaje kuhama mji kufata mwanamke badala yy ndio akufate... unawezaje kubadili dhehebu kufata la mwanamke...

Sikia nikwambie unauza mamlaka Yako uliyopewa na Mungu ya uongoz na utawala kwa wanawake kisa mapenz,, hvo Mungu hawez kukusaidia kwa chochote sabb badala ya kumsikiliza yy unasikiliza wake zako...kama esau na yakobo,,esau kauza baraka zake sabb ya msosi alipokuja kuzililia halikuwezekana..

Sanduku la pesa I mean hazina Yako ilikuaje unamkabidhi mke na nyaraka zako pia...inafikirisha sana!!

Simamia kama mwanaume acha hayo mambo ya kupetpet mwanamke...

Mwisho uligundua mke anakusalit na kiongozi wa kanisa asa ulikua unasubir nn kumlima talaka.. mwanamke msaliti hasameeki never ever!!!!
 
Man utakua tajiri na kiongozi mkubwa sana!

Hope tutakuja kufanya KAZI office Moja na tutakua team wazalendo!

Nadhani utaniunga mkono kwenye dhamira yangu ya kupunguza mapesa mengi kulipa wanasiasa mishahara na maposho kibao wakati huduma za kijamii zinalega lega!!

Paulo mtume anaandika"najua kushiba na kuona njaa" akielezea Kwa kina mapito yenye maumivu meengi!

Tunapitia nyakati kama hizo maishani ili tukipata tuelewe Hali zote wanazopitia watu wote Ili tuwe msaada!!

See you at the top!! Trust me nitakutafuta ngoja kwanza litimie neno fulani!!
Hivi ni kweli ID yako inasadifu dhamira yako? I wish to work with you. If you don't mind pm me..
 
VINTAGE, unahisi ulikosea wapi kama Mwanaume?

Ungependa vijana wa kiume ambao bado hawajaoa wajifunze nini kwenye story ya maisha yako ?
 
Pole sana mkuu kwa maswaibu unayopitia..but kosa kubwa unalofanya ww ni kuwapa kipaumbele sana wanawake kuliko kusudi la maisha Yako..

Nimekunote umesafiri mara kadhaa kufata mwanamke badala yy ndio akufate... unawezaje kuhama mji kufata mwanamke badala yy ndio akufate... unawezaje kubadili dhehebu kufata la mwanamke...

Sikia nikwambie unauza mamlaka Yako uliyopewa na Mungu ya uongoz na utawala kwa wanawake kisa mapenz,, hvo Mungu hawez kukusaidia kwa chochote sabb badala ya kumsikiliza yy unasikiliza wake zako...kama esau na yakobo,,esau kauza baraka zake sabb ya msosi alipokuja kuzililia halikuwezekana..

Sanduku la pesa I mean hazina Yako ilikuaje unamkabidhi mke na nyaraka zako pia...inafikirisha sana!!

Simamia kama mwanaume acha hayo mambo ya kupetpet mwanamke...

Mwisho uligundua mke anakusalit na kiongozi wa kanisa asa ulikua unasubir nn kumlima talaka.. mwanamke msaliti hasameeki never ever!!!!
How a man can place his purpose above his woman?

Je maumivu ya kufeli biashara yako yanaweza kuwa makubwa kuliko ku divorce na mke wako?

Nifundishe mimi nipo tayari kupokea ushauri wako.
 
Back
Top Bottom