Maisha ya ndoa na familia

Maisha ya ndoa na familia

How a man can place his purpose above his woman?

Je maumivu ya kufeli biashara yako yanaweza kuwa makubwa kuliko ku divorce na mke wako?

Nifundishe mimi nipo tayari kupokea ushauri wako.
Mwanaume ameumbwa na kupewa mission maalum hapa dunian kutimiza,,beside amepewa mwanamke pemben wa kumsaidia..

Mwanaume kama mbeba maono anatakiwa a stick na mission aliyopewa kwa nguvu zote na kutoa maelekezo kwa mwanamke nn anatakiwa kufanya na kumsimamia..

Mungu akiona upo hvo anakubless na kukulinda hata bila ya ww kumwomba sabb kile alichokutuma ndio umestic kukitekeleza..

Tatizo ni pale ww mwanaume uliepewa maono,, unaacha pambania maono Yako unahangaika kufurahisha na kumsikiliza msaidizi wako(mke) Ambae kiuhalisia yy hata hajui ww upo kwa ajili gan..anashangaa na ww unamfata wakat hajui hata anapoenda..hapo lazima akudharau na kukupiga chini na kwenda tafuta mwanaume mwengine anayejua anachotakiwa kufanya...

Na uyo Mungu atakupotezea tuu sabb yy ana protect na kusupport mwanaume anayetimiza mission aliyomtuma and not other wise...
 
Pole ,Sasa umefanikiwa kurejea maisha yako ya wastani au bado ? Una taaluma gani ? Achana na mapenzi jitafute kwanza utunze wanao
 
VINTAGE, unahisi ulikosea wapi kama Mwanaume?

Ungependa vijana wa kiume ambao bado hawajaoa wajifunze nini kwenye story ya maisha yako ?

Pole ,Sasa umefanikiwa kurejea maisha yako ya wastani au bado ? Una taaluma gani ? Achana na mapenzi jitafute kwanza utunze wanao
Bado nahangaika sana mkuu ila naamini nitasimama.
 
VINTAGE, unahisi ulikosea wapi kama Mwanaume?

Ungependa vijana wa kiume ambao bado hawajaoa wajifunze nini kwenye story ya maisha yako ?
Will Jr., jambo kubwa ambalo ningependa kushauri ni, kuchukua muda zaidi kujifunza kwa kina tabia za mwanamke unaemhitaji katika mahusiano ya ndoa kabla ya kuamua kuishi pamoja.
 
Pole sana mkubwa, hii story imenifundisha kuwa Wanawake sio watu wa kuamini. Nimeongeza asilimia tisini zaidi
 
Wanawake wana roho mbaya sana... Msitongozeke mkiwag kwa mahusiano
 
Sehemu ya saba
Baada ya kunicheka aliniuliza kama ananitumia kwa ile namba. Akatuma elfu 10 na kisha akanitumia ujumbe kwamba yupo na mpenzi wake kwahiyo nisiwe nampigia simu. Nilimshukuru na kumtakia maisha mema. Nilimuomba anisaidie nyaraka zangu za kitaaluma na akanielekeza sehemu ambapo nitazipata.

Nipokea nyaraka zangu. Wakati huu nilikuwa nimechoka. Nilikonda na kuwa mtu wa ajabu kabisa. Kutoka kuvaa suti karibia siku tano za wiki na kufikia kuwa katika mavazi machafu yasiyoelezeka. Nilivaa ndala zilizofungwa na kamba.

Wakati fulani nikiwa katika mawazo mazito, niliamua kutaka kujiua lakini kwanza nikatafuta simu niongee na mtoto wangu niliezaa na Upendo. Mtoto wangu alinisalimia kisha akaniambia kwamba, "Dad, you promised to come back for me. Please remember that I miss you". Nililia sana siku ile na nikaamua kuendelea kupambana.

Nitawataja watu wachache hapa maana najua ni kwa nia njema. Wakati nahangaika, nilitafakari kukutana na kaka yangu mmoja hapa JF. Sikuwahi kuwasiliana nae kabla lakini moyo ulinisukuma kuongea nae. Nilitamani anisaidie viatu ili nipate kwenda kwenye sehemu moja ambayo nilialikwa kwa ajili ya interview. Nilimu-pm akaniomba tuonane kibada. Nilitembea kutoka rangi tatu hadi kibada kwa mguu.
Ilikuwa bahati mbaya maana siku ile hakunipa viatu kama nilivyoomba. Alinitazama kisha akanipa elfu 10. Nilikuwa na njaa sana. Nilikuwa sijapata chakula kwa muda mrefu. Nilitumia ile pesa kiasi kupata chakula pale kibada. Baada ya kuwasiliana tena, aliniomba nifike kibaha. Nilitembea tena kwa mguu hadi kibaha. Nilichoka sana. Alinipa nguo pamoja na viatu. Brother Jr., asante sana na Mungu akubariki.

Nilikuwa na jamaa yangu mwingine yupo humu anaitwa clearmind. Nilisoma nae na alikuwa mtu wangu wa karibu sana. Nakumbuka kipindi anataka kunisaidia aligombana sana mchumba wake na kwa bahati mbaya wakaachana. Niliumia sana nikaogopa kuendelea kumuomba msaada.

Nilipona msongo wa mawazo. Nipo Dar napambana. Sipo kama nilivyokuwa japo hali bado ni ngumu sana. Nina imani nitarejea tena upya. Yaliyotokea yote katika maisha yangu nayaangalia kama changamoto mpya zinazonijenga kuelekea kwenye hatima yangu iliyo njema zaidi. Nimejisikia amani kushea nanyi safari yangu hii ambayo imekuwa na matukio mengi ya kuumiza. Asanteni sana na Mungu awabariki.
Vintage1q.
Enjoy your life to the fullest today because tomorrow's never promised!
Maana halisi ya hustle 🫡🫡
 
Sehemu ya Tatu

Baada ya kupata majibu ya kukatisha tamaa kutoka kwa wazazi wa Upendo, niliamua kutoendelea kuwapa taarifa kuhusu maendeleo ya Upendo. Nilibaki kuwa faraja kubwa kwake pamoja na mtoto wetu. Tuliishi kwa furaha na upendo mkubwa sana. Wakati mwingine tulikuwa tukitoa machozi tukikumbuka nyakati ngumu zilizopita.

Katika mwaka wangu wa mwisho wa masomo, nilimuomba Upendo afunge safari kuelekea nyumbani kwetu ili nipate nafasi ya kupambana na kumaliza mwaka wa mwisho salama maana ulikuwa na programs nyingi sana. Mpenzi wangu Upendo alikubali na wazazi wangu walikuwa na shauku kubwa ya kumuona. Wakati akiwa safarini, niliwasiliana na rafiki yangu ambae alikuwa akiishi Dodoma akifanya kazi. Rafiki yangu huyu tulisoma pamoja na kiukweli alikuwa kama ndugu. Mpenda dini sana. Katika kipindi chote ambacho nilimfahamu hakuwahi kuwa kwenye mahusiano na binti yoyote. Nilimueleza kuhusu mpenzi wangu kurudi nyumbani.

Rafiki yangu aliniomba Upendo wangu apite nyumbani kwake amsalimie kabla ya kuelekea nyumbani kwa wazazi wangu, Mwanza. Ilinilazimu nimtaarifu mama yangu kwamba Upendo angechelewa maana anapita Dodoma kwa rafiki yangu Charles kumsalimia. Mama alishtuka kisha akaniuliza kama Charles Ana nyumba nyingine ya Upendo kufikia. Nilimuuliza Charles akanijibu kwamba nisiwe na shaka nyumba ipo na mimi sikuwa na wasiwasi juu ya Charles. Baada ya majadiliano hayo, nilimpigia simu Upendo akiwa safarini na kumuelekeza ateremke Dodoma kumsalimia shemeji yake.

Alifika salama na kupokelewa na Charles. Baada ya siku tatu, nilimpgia simu Upendo nikimuelekeza aelekee mwanza. Baadae kidogo rafiki yangu Charles akanipigia simu akinisihi Upendo asielekee Mwanza kwamba angekwenda kuwasumbua wazazi tu na hali ngumu iliyopo nyumbani. Tuliongea mengi na kisha nikamuuliza Upendo kama alikuwa huru kuendelea kukaa pale. Alinijibu kwamba hapakuwa na shida.

Ajabu ni kwamba, siku ile usiku nilikuwa naota Upendo akiwa anafanya mapenzi na rafiki yangu. Nilifadhaika mno. Asubuhi nikampigia simu kumuuliza kama alikuwa salama, akanijibu kwamba hapakuwepo na shida. Ndoto ile iliendelea kwa siku tatu mfululizo. Niliumia sana. Nikawa mtu mwenye mawazo sana chuoni. Nilijipa moyo na kuendelea na masomo. Baada ya kumaliza chuo, nilikuwa na barua mkononi nikihitajika kwenda kufanya kazi singida katika kampuni fulani. Niliomba udhuru wa siku kadhaa kwenda kumufuata mke wangu. Nilisafiri hadi Dodoma na kufika kwa rafiki yangu. Upendo alifurahi sana kuniona laikini alikuwa mwenye mashaka. Rafiki yangu pia hakuwa na ule uchangamfu nilio uzoea. Baada ya mazungumzo mafupi, nilikaa na Upendo kwa mazungumzo. Nikamueleza kuhusu ile ndoto. Nikamkumbusha mambo mengi tuliopitia katika maisha. Kisha nikamuomba anieleze ukweli na akanithibitishia kwamba, rafiki yangu alikuwa akimuingilia kwa nguvu usiku wa manane na kweli mlango ule haukuwa unafungwa.

Sikumhoji Upendo mambo mengi. Nikajua mimi ndie mwenye makosa. Nikamuomba tuondoke pamoja na mtoto wetu. Rafiki yangu Charles, aliomba kuondoka nasi pia ili akaone tunapoishi. Tulisafiri na kufika Singida. Nikaoneshwa nyumba ya kuishi. Ilikuwa na kila kitu. Muda wote huo nilikuwa na mawazo sana. Sikuwa sawa. Niliwaza ni kwanini Upendo afanye vile. Niliingia chumbani kwenye ile nyumba. Nikatoka nikaingia jikoni. Nikaona kisu kikiwa kwenye beseni. Kipya kabisa. Akili ilinitima kwamba nilipaswa kumumaliza Charles. Nilikibeba kisu nikaelekea sebuleni alipokuwa amekaa Upendo na Charles. Nilitetemeka nikaangusha kile kisu.

Wakati huo, nilikuwa sijamueleza Charles chochote kuhusu alichokifanya kwa Upendo. Baada ya tukio lile, Upendo alilia sana. Akainama akanishika miguu na kuniomba msamaha. Niliongea na Charles kwa uchungu sana na kuamua kusitisha urafiki wetu tangu siku ile. Charles aliondoka kurudi Dodoma.

Itaendelea,,,
Ok
 
Back
Top Bottom