Maisha ya ndoa yana changamoto nyingi sana.

Maisha ya ndoa yana changamoto nyingi sana.

FUSO

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2010
Posts
34,181
Reaction score
41,563
Kuna mshikaji wetu mmoja alimlaza mkewe ndani kwa makosa ya kijinga kijinga tu ya maisha ya ndoa... kesho yake tukaenda kumsalimia shemeji yetu tukamkuta pale nje kituoni so tukatoka naye tukaenda kupata supu jirani na kituo cha police.

Kwenye supu akatuambia sasa nawapa salaam, mpigieni simu mshikaji wenu mwambieni ya yeye leo ni zamu yake, tukacheka tukasema shemeji si yaishe tu haya mambo kifamilia, akagoma akasema na yeye lazima aje kunyea debe leo afu ndiyo tuangalie namna ya kuyamaliza.

Aisee kweli bana kabla hata hatujaondoka jamaa kafika na V8 lake, fasta bin vuu vua mkanda, kaa chini .. unapiga mkeo wewe bila makosa... mzee mzima akasonda ndani - sisi tukaendelea kupata ngano na shemeji yetu huku tukimsihi amtoe akagoma, tukakaa pale hadi saa 4 usiku ikashindikana kumtoa ikabidi tuondoke

Asubuhi yake tukafika pale ili tuone kama kesi itakwenda mahakamani, basi kuongea huku na huku yule afande akawaita wote akawaambia naona sasa kila mmoja karidhika - sasa nendenei mkayamalize nyumbani.

Jamaa akawasha V8 lake akasepa, huku shem na yeye akawasha BMW na yeye akasepa - sisi tukaona tuwaache kwanza then tuwatafute jioni tuone wamefikia wapi.

Basi ilipofika saa 11 jioni tukamcheki mshikaji akatuambia yupo sehemu tuende, tukafika pale tukawakuta yeye na mkewe wanapata Kmoto na moja moto moja baridi... asiee dunia hii.

mambo ya ndoa ni magumu sana.
 
Wale jamaa wa Centro wanaogopa V8 sio mchezo..
Hiyo chai kabisa Dingi V8 maza BMW hawawezi kufanya michezo ya kijinga namna hiyo
 
mkuu ni kweli, sema tu mambo ya ndoa huwa hayajiandiki mgongoni unapotembea ili watu wayasome, ni ya ajabu na ya aibu kubwa.
CHANZO CHA MUME KIMPIGA MKEWE NI KIPI? NA KWA NINI WAPEANE ZAMU YA KWENDA CENTRAL
 
CHANZO CHA MUME KIMPIGA MKEWE NI KIPI? NA KWA NINI WAPEANE ZAMU YA KWENDA CENTRAL
wivu wa kimapenzi, jamaa kamtuhumu mkewe kwamba ana jamaa dubai akienda kule kufunga mzigo wa biashara analiwa, ugomvi ukawa mkubwa demu akaakasirika kamwambia mumewe sawa hata nikigawa si ni yangu... mumewe akawambia sasa ngoja nikufundishe adabu kima wewe - ndiyo akafanya mpango alale ndani kwanza kutia adabu.
 
wivu wa kimapenzi, jamaa kamtuhumu mkewe kwamba ana jamaa dubai akienda kule kufunga mzigo wa biashara analiwa, ugomvi ukawa mkubwa demu akaakasirika kamwambia mumewe sawa hata nikigawa si ni yangu... mumewe akawambia sasa ngoja nikufundishe adabu kima wewe - ndiyo akafanya mpango alale ndani kwanza kutia adabu.
HAHAHA HII NDOA INA VITUKO
 
Wale jamaa wa Centro wanaogopa V8 sio mchezo..
Hiyo chai kabisa Dingi V8 maza BMW hawawezi kufanya michezo ya kijinga namna hiyo
Yaonesha mkewe alishawaeleza udhaifu wa mumewe na wakajua wambane wapi.Ila kama hii stori ni kweli nimecheka sana.Na yaonesha wanapendana hao.
 
Back
Top Bottom