Maisha ya Osama kabla hajakamatwa yafichuliwa

Maisha ya Osama kabla hajakamatwa yafichuliwa

Acha uwongo, mbona report ya mission yake ilishawekwa wazi tokea alipouwawa kaisome acha stori za vijiweni. Taarifa za Osama zilitolewa na detainee watatu wa alqueda waliopo Guantanamo. wa kwanza ni Mastermind wa 9/11 Khaleed Sheikh Mohamed (KSM), huyu ndie alimtaja Courier wa Osama ajulikanaye kwa jina la Al Kuwait ambaye ndiye anaebeba maelekezo na mawasiliano yote kutoka kwa osama na kupeleka kwa foot soldiers, Wa pili kumtaja Al Kuwait ni Abu Zubeida, Huyu Abu zubeida pamoja na Ramzi Yousef ndio waliolipua WTC kabla ya 9/11. Abu zubeida kwanza aliteswa na CIA kwa kutumia Enhanced Interogation techniques kama water borne akagoma kutoa information yoyote, mpaka CIA wakamtishia kumkabidhi kwa intelligence ya Saudi Arabia wakiamini ataogopa maana Saudi Arabia wanajulikana kwa kutesa, wakashangaa anawaambia wampeleke Saudi. Hapo ndio CIA wakacheza trick wakampakiza kwenye ndege na kuzunguka naye muda mrefu angani wakijifanya wanampeleka Saudi Arabia mwisho wakatua naye sehemu hukohuko marekani wakawachukua maofisa wa CIA waarabu wakiwa na nguo za jeshi la Saudi Arabia wakaanza kumuuliza maswali hapo ndio akamtaja Al Kuwait, halafu akawataja wafadhili wa Osama akiwepo Mtoto wa mfalme wa Saudi, Generali wa Jeshi la Saudi na maofisa wengine wawili wa serikali ya Saudi na akawapa namba ya motto wa mfalme wampigie ili awaamrishe wamwachie. watu wote waliotajwa na Abu zubeida CIA waliwaua kuanzia mtoto wa mfalme alikutwa amekufa akiwa vacation, yule General wa jeshi alikutwa amekufa jangwani kwa kiu na kukosa maji na wale maofisa wote. Huo ndio ukawa mwanzo wa Osama kukosa hela (financial suffocation). wakaanza kumfuatilia Al Kuwait Pakistani wakamtrace akitokea sokoni hadi nyumba aliyokuwa akienda Abbottabad. Osama aliishiwa hela mpaka wake zake walikuwa wanaenda kwa sonara wanauza mikufu na herein zao ili wapate hela ya kula. Ndio CIA wakamkodia nyumba karibu na nyumba ya Osama Afisa wake aliyekuwa anafanya kazi katika Shirika la Save the Children ambalo lilikuwa linafanya kampeni ya kinga ya magonjwa ya watoto. Na sio kwamba eti marekani walikuwa wanachukua DNA za watoto na ku-match na za Osama huo ni uwongo kwa sababu kinga iliyokuwa inaratibiwa na Save the Children ilikuwa ni ya Matone sasa kuwapa watoto matone uta-extract vipi DNA. Aliyebaki sasa ni second in command wa alqaeda daktari wa Misri Ayman Al Zawahil ambaye naye inaaminika amejificha kwenye mpaka wa Afg na Pak.
kweli penye nia pana njia, huu ufafanuzi umesaidia sana.
 
Mi nasikiliza tu maana hapa naona watu wa TISS aka GREEN GUARD wanatoa data zao
 
Wote mnajidanganya ingia kwenye osamaciawaxkill.newz upate update vzr .
 
Wote mnatuletea hadithi za Abunuwasi. Hii ngoma bado ipo classified. Hizo stori mnazoleta link hapa niza vijiweni tu
 
Hivi hakuna hata dizain ya movie........nipo very interested kufuatilia........more news plz......
 
Hivi hakuna hata dizain ya movie........nipo very interested kufuatilia........more news plz......
kuna moja inaitwa Osama's fall kama sijakosea... inaonyesha jinsi wale seal team 6 walivyopanga mission mpaka kwenda kumshoot Osama kule Abottabad Pakistan alipokuwa anaishi...

yaani wanaonyesha mission yote hadi kina Obama walivyokuwa wanafuatilia...

yaani jamaa wako vizuri sana...
 
Acha uwongo, mbona report ya mission yake ilishawekwa wazi tokea alipouwawa kaisome acha stori za vijiweni. Taarifa za Osama zilitolewa na detainee watatu wa alqueda waliopo Guantanamo. wa kwanza ni Mastermind wa 9/11 Khaleed Sheikh Mohamed (KSM), huyu ndie alimtaja Courier wa Osama ajulikanaye kwa jina la Al Kuwait ambaye ndiye anaebeba maelekezo na mawasiliano yote kutoka kwa osama na kupeleka kwa foot soldiers, Wa pili kumtaja Al Kuwait ni Abu Zubeida, Huyu Abu zubeida pamoja na Ramzi Yousef ndio waliolipua WTC kabla ya 9/11. Abu zubeida kwanza aliteswa na CIA kwa kutumia Enhanced Interogation techniques kama water borne akagoma kutoa information yoyote, mpaka CIA wakamtishia kumkabidhi kwa intelligence ya Saudi Arabia wakiamini ataogopa maana Saudi Arabia wanajulikana kwa kutesa, wakashangaa anawaambia wampeleke Saudi. Hapo ndio CIA wakacheza trick wakampakiza kwenye ndege na kuzunguka naye muda mrefu angani wakijifanya wanampeleka Saudi Arabia mwisho wakatua naye sehemu hukohuko marekani wakawachukua maofisa wa CIA waarabu wakiwa na nguo za jeshi la Saudi Arabia wakaanza kumuuliza maswali hapo ndio akamtaja Al Kuwait, halafu akawataja wafadhili wa Osama akiwepo Mtoto wa mfalme wa Saudi, Generali wa Jeshi la Saudi na maofisa wengine wawili wa serikali ya Saudi na akawapa namba ya motto wa mfalme wampigie ili awaamrishe wamwachie. watu wote waliotajwa na Abu zubeida CIA waliwaua kuanzia mtoto wa mfalme alikutwa amekufa akiwa vacation, yule General wa jeshi alikutwa amekufa jangwani kwa kiu na kukosa maji na wale maofisa wote. Huo ndio ukawa mwanzo wa Osama kukosa hela (financial suffocation). wakaanza kumfuatilia Al Kuwait Pakistani wakamtrace akitokea sokoni hadi nyumba aliyokuwa akienda Abbottabad. Osama aliishiwa hela mpaka wake zake walikuwa wanaenda kwa sonara wanauza mikufu na herein zao ili wapate hela ya kula. Ndio CIA wakamkodia nyumba karibu na nyumba ya Osama Afisa wake aliyekuwa anafanya kazi katika Shirika la Save the Children ambalo lilikuwa linafanya kampeni ya kinga ya magonjwa ya watoto. Na sio kwamba eti marekani walikuwa wanachukua DNA za watoto na ku-match na za Osama huo ni uwongo kwa sababu kinga iliyokuwa inaratibiwa na Save the Children ilikuwa ni ya Matone sasa kuwapa watoto matone uta-extract vipi DNA. Aliyebaki sasa ni second in command wa alqaeda daktari wa Misri Ayman Al Zawahil ambaye naye inaaminika amejificha kwenye mpaka wa Afg na Pak.

thanks mkuu for a detailed explanation/narration
 
Vile vile katika ripoti hiyo ya commission inamtaja afisa mmoja wa shirika la kijasusi la Pakistani (ISI) kuwa kuna uwezekano alihusika katika njama za marekani kumkamata Osama kwa kuwa wiki moja kabla ya tukio la kumkamata Osama, aliwatuma watu kukata miti mikubwa iliyokuwa inazunguka ile nyumba Abbottabad ikiwa ni maandalizi ya helicopter kutua. Vile vile baada ya tukio la kukamatwa Osama aliuza vitu vyake na kuondoka Pakistani. Tofauti kati ya mashirika ya intelligence ya huku kwetu na nchi zilizoendelea ni kuwa wenzetu mashirika yao yanafanya mission zenye maslahi kwa taifa siyo kwa chama tawala. Ndio maana mission ikishakamilika wanatoa taarifa yote in detail kasoro baadhi tu ya tactics ambazo wanaona wataendelea kuzitumia kwenye mission nyingine. Huku kwetu mission zilizojaa TISS ni zile za kukandamiza Upinzani kama kumuua Kombe, kuua viongozi wa upinzani, kuwarushia mabomu Chadema n.k hizi mission hauwezi kuja kujua ukweli mpaka mmoja wao awageuke aropoke. Wenzetu mission zao zinakuwa high classified, lakini ikishakamilika tu wana-disclose kila kitu. Kwa mfano mission ya kumkamata Khaleed Sheikh Mohamed (KSM) the ring leader and mastermind wa 9/11 na akina Ramzi Yousef inajulikana ilifanywaje. Walifuatilia trail ya hela zote zilizokuwa wired kwenye account ya Mohamed Attar (kiongozi wa magaidi waliobamiza ndege WTC) Walianzia Dortimund Ujerumani ambakao Mohammed Attar alikuwa anasoma master of Science in Urban Planning katika chuo kikuu cha Dortimund. Walifuatilia trail ya ufadhili wa hela, msikiti aliokuwa anaswali hadi wakajua cell yao ilikuwa na kina nani, safari zake Pakistani na watu aliokuwa anakutana nao. Mohamed Attar ndio alikuwa ana-distribute hela kwa wale wengine za kusomea u-pilot wa ndege marekani. lakini hadi wanasomea upilot walikuwa hawajui mission yao itakuwaje. aliekuwa anajua mission ni KSM na Mohamed Attar. Kuna gaidi mmoja ambaye alikuwa yupo kwenye kikosi cha kwanza lakini alinyimwa viza ya kuingia marekani ndio alimtaja KSM kuwa ndie aliekuwa anawafadhili. Tofauti na kina Osama, KSM alikuwa anaishi maisha ya kifahari, anaingia kwenye club za usiku, anatumia vileo, anatumia simu, anachukua machangu, hakuwa anaishai maisha ya kiislamu. Kosa la kwanza na kubwa ambalo KSM na Ramzi walilifanya ni kumualika mwandishi wa habari wa Al-jazeera kwenda kuwahoji Pakistani. Ikieleweka kuwa kabla ya 9/11, Osama alikuwa anajulikana lakini hakuwa maarufu sana, hivyo kulikuwa na struggle kati ya magaidi kila mtu akitaka kupata umaarufu kuwa yeye ndio gaidi zaidi. Hiki ndicho kiliwasukuma KSM na Ramzi kumualika yule mtangazaji wa Al-jazeera kwenda kuwahoji. Yule mtangazaji alienda Islamabad akafungwa kitambaa usoni akazungushwa kwenye gari kuanzia asubuhi hadi jioni ili asijue muelekeo, mwishowe akashushwa kwenye gari wakamuingiza kwenye nyumba ambayo ina bunker alipofunguliwa kitambaa akakutana uso kwa uso na KSM akiwa na Ramzi Yousef. Pale KSM aka-declare jihad against American na ku-confess yeye ndiye aliyepanga na ku-finance mission nzima ya kubamiza ndege WTC. Yule mtangazaji wa Al-jazeera alipomaliza kuwahoji akaomba aondoke na Video footage wakamkatalia ila wakamruhusu achukue Audio record, hilo ndilo lilikuwa kosa kubwa sana maana ile audio iliporushwa tu Al-Jazeera, CIA wakaenda kuichukua Al-Jazeera wakatenganisha voice print za kila mtu alieongea kwenye ule mkutano wakaingiza kwenye mashine yao inayo-identify voice print ya kila mtu kama finger print. Hapo ndio ukawa mwanzo wa Drone attack Pakistani. Mtu akiongea kwenye simu kabla hajakata simu anashangaa bomu limeshatua. Kuna tukio moja walikuwa wamewasiliana wahudhurie harusi na Ayman Al Zawahil atakuwepo, machale yakawacheza Zawahili hakwenda, ile harusi ilibutuliwa na drone walikufa watu ukoo mzima. Baada ya kukamatwa Ramzi, KSM alistuka kuwa anafuatiliwa kwenye simu hivyo alikuwa hatumii simu yake, anaomba watu atumie simu zao ndio maana zoezi la kumkamata KSM lilishindikana zaidi ya mara 20, wakimtrace sehemu wakienda hawamkuti, alikuwa halali sehemu moja mara mbili mfululizo, Mpaka walipoamua kumtengenezea ramani kwa kutumia simu anazotumia, waka-identify sehemu 14 ambazo kuna uwezekano mkubwa wa kumkuta. Hizo sehemu zote zikafanyiwa kitu kinaitwa "synchronized ambush", yaani vikatengenezwa vikosi 14 vya askari wa Pakistani vikishirikisha maafisa wa CIA katika kila kikosi ambavyo vita-ambush sehemu zote 14 kwa muda mmoja, hapo ndipo walipomkamata KSM lakini walichoshangaa ni kuwa kwenye location moja katika zile 14 walikuta kiwanja hakina nyumba. walipofuatilia waya wa simu unaotumika kwa ID ya kiwanja hicho uko kwenye nyumba ipi ndipo ofisa wa ISI mtaalamu wa IT akai-trace nyumba inayotumia ID ya kile kiwanja humo ndipo walipomfurumusha na kumpiga risasi Abu Zubeida ambaye alipelekwa kutibiwa ujerumani akapona na kutoa siri kibao.
 
Very interesting. Mkuu FUHRER kama kuna ulichokisahau kiongezee maana umeidadavua vizuri sana hii ishu. Much respect
 
Very interesting. Mkuu FUHRER kama kuna ulichokisahau kiongezee maana umeidadavua vizuri sana hii ishu. Much respect

Unamwagiwa umbea unashangilia tu. Habari za alkaeda ni puzzle na wengi wanatengeneza tu. Kama alivyotengeneza Obama kumuua Osama aliyekufa more than 2 year ago.
 
Mkuu FUHRER huwezi cheza movie na bongo movie?
 
Last edited by a moderator:
mkuu FUHRER hakika umechambua vizuri sana, tungependa uendelee kutupa mambo...

safi sana...
 
Last edited by a moderator:
FUHRER,

kuna uzi mmoja watu walibishana humu kitambo kwamba ISI ni bora kuliko c.i.a,mossad,kgb n.k

kwa hili achilia mbali mengi tusiyoyajua hawa wapakistan ni corrupt,double agent na kutakua na mule wengi kwa ajili ya operation za kivita afghanistan na za kiuchumi dhidi ya india-BRICKS
 
Wakuu nitaendelea kuwapa simulizi hizi za mission za CIA, MOSSAD na KGB maana wenzetu wanaziweka wazi hawana cha kuficha kama bongo. Ile mission ya kumkamata Osama ni kali lakini kwa watu wanaojua mission zilizofanyika hapa duniani, hakuna mission kali kuizidi ile ya Entebbe iliyofanywa na MOSSAD, hata hii ya Osama ilichukua items nyingi kwenye mission ya Entebbe. Ukitaka kujua ile ya Entebbe ni kali kuliko ya Osama linganisha technologia zilizotumika, hii ya Osama walitumia chopa za shinoku zenye technology ya stealth inayoweza kukwepa rada wakati ya Entebbe hakukuwa na technology hiyo. Ndege zilizohusika kwenye mission ya Osama ziliruka kutoka kwenye military base ya marekani iliyopo Jalalabad Afg ambayo ipo ka 20 km kutoka kwenye mpaka na Pak wakati Ndege zilizohusika kwenye mission ya Entebbe ziliruka kutoka Tel Aviv kupita nchi mbili ambazo ni hostile Egypt na Sudan 5,000km kuja Entebbe. Operation ya Osama kulikuwepo na maofisa wa CIA waliokuwa kwenye ofisi ya ubalozi ambao walielekea Abbottabad mapema kwaajili ya ku-monitor situation na kuna maofisa wa ISI ambao walikuwa kwenye jeshi la Pakistani ambao walikuwa wanatoa taarifa kwa maofisa wa CIA kila kinachoendelea kuhusiana na response ya jeshi la Pakistani. Siku nikipata nafasi nitawasimulia ile operation ya Entebbe ilivyopangwa na failures na success zake. kama ilivyokuwa ya Osama zilipangwa plana 4 za kuifanya ile mission ya Osama na zote zilifanyiwa mazoezi ndio maana ile helicopter ilivyokosa thrust na kudondoka walibadili plan kutoka Plan A kwenda plan C, sasa siku nikipata nafasi nitawaeleza Plani A ilikuwa ikoje, plan b,c na d. Na kwa nini ile helicopter ilivyodondoka walibadili plan kutoa A kwenda C, kwa nini hawakuenda plan B.
 
Vile vile katika ripoti hiyo ya commission inamtaja afisa mmoja wa shirika la kijasusi la Pakistani (ISI) kuwa kuna uwezekano alihusika katika njama za marekani kumkamata Osama kwa kuwa wiki moja kabla ya tukio la kumkamata Osama, aliwatuma watu kukata miti mikubwa iliyokuwa inazunguka ile nyumba Abbottabad ikiwa ni maandalizi ya helicopter kutua. Vile vile baada ya tukio la kukamatwa Osama aliuza vitu vyake na kuondoka Pakistani. Tofauti kati ya mashirika ya intelligence ya huku kwetu na nchi zilizoendelea ni kuwa wenzetu mashirika yao yanafanya mission zenye maslahi kwa taifa siyo kwa chama tawala. Ndio maana mission ikishakamilika wanatoa taarifa yote in detail kasoro baadhi tu ya tactics ambazo wanaona wataendelea kuzitumia kwenye mission nyingine. Huku kwetu mission zilizojaa TISS ni zile za kukandamiza Upinzani kama kumuua Kombe, kuua viongozi wa upinzani, kuwarushia mabomu Chadema n.k hizi mission hauwezi kuja kujua ukweli mpaka mmoja wao awageuke aropoke. Wenzetu mission zao zinakuwa high classified, lakini ikishakamilika tu wana-disclose kila kitu. Kwa mfano mission ya kumkamata Khaleed Sheikh Mohamed (KSM) the ring leader and mastermind wa 9/11 na akina Ramzi Yousef inajulikana ilifanywaje. Walifuatilia trail ya hela zote zilizokuwa wired kwenye account ya Mohamed Attar (kiongozi wa magaidi waliobamiza ndege WTC) Walianzia Dortimund Ujerumani ambakao Mohammed Attar alikuwa anasoma master of Science in Urban Planning katika chuo kikuu cha Dortimund. Walifuatilia trail ya ufadhili wa hela, msikiti aliokuwa anaswali hadi wakajua cell yao ilikuwa na kina nani, safari zake Pakistani na watu aliokuwa anakutana nao. Mohamed Attar ndio alikuwa ana-distribute hela kwa wale wengine za kusomea u-pilot wa ndege marekani. lakini hadi wanasomea upilot walikuwa hawajui mission yao itakuwaje. aliekuwa anajua mission ni KSM na Mohamed Attar. Kuna gaidi mmoja ambaye alikuwa yupo kwenye kikosi cha kwanza lakini alinyimwa viza ya kuingia marekani ndio alimtaja KSM kuwa ndie aliekuwa anawafadhili. Tofauti na kina Osama, KSM alikuwa anaishi maisha ya kifahari, anaingia kwenye club za usiku, anatumia vileo, anatumia simu, anachukua machangu, hakuwa anaishai maisha ya kiislamu. Kosa la kwanza na kubwa ambalo KSM na Ramzi walilifanya ni kumualika mwandishi wa habari wa Al-jazeera kwenda kuwahoji Pakistani. Ikieleweka kuwa kabla ya 9/11, Osama alikuwa anajulikana lakini hakuwa maarufu sana, hivyo kulikuwa na struggle kati ya magaidi kila mtu akitaka kupata umaarufu kuwa yeye ndio gaidi zaidi. Hiki ndicho kiliwasukuma KSM na Ramzi kumualika yule mtangazaji wa Al-jazeera kwenda kuwahoji. Yule mtangazaji alienda Islamabad akafungwa kitambaa usoni akazungushwa kwenye gari kuanzia asubuhi hadi jioni ili asijue muelekeo, mwishowe akashushwa kwenye gari wakamuingiza kwenye nyumba ambayo ina bunker alipofunguliwa kitambaa akakutana uso kwa uso na KSM akiwa na Ramzi Yousef. Pale KSM aka-declare jihad against American na ku-confess yeye ndiye aliyepanga na ku-finance mission nzima ya kubamiza ndege WTC. Yule mtangazaji wa Al-jazeera alipomaliza kuwahoji akaomba aondoke na Video footage wakamkatalia ila wakamruhusu achukue Audio record, hilo ndilo lilikuwa kosa kubwa sana maana ile audio iliporushwa tu Al-Jazeera, CIA wakaenda kuichukua Al-Jazeera wakatenganisha voice print za kila mtu alieongea kwenye ule mkutano wakaingiza kwenye mashine yao inayo-identify voice print ya kila mtu kama finger print. Hapo ndio ukawa mwanzo wa Drone attack Pakistani. Mtu akiongea kwenye simu kabla hajakata simu anashangaa bomu limeshatua. Kuna tukio moja walikuwa wamewasiliana wahudhurie harusi na Ayman Al Zawahil atakuwepo, machale yakawacheza Zawahili hakwenda, ile harusi ilibutuliwa na drone walikufa watu ukoo mzima. Baada ya kukamatwa Ramzi, KSM alistuka kuwa anafuatiliwa kwenye simu hivyo alikuwa hatumii simu yake, anaomba watu atumie simu zao ndio maana zoezi la kumkamata KSM lilishindikana zaidi ya mara 20, wakimtrace sehemu wakienda hawamkuti, alikuwa halali sehemu moja mara mbili mfululizo, Mpaka walipoamua kumtengenezea ramani kwa kutumia simu anazotumia, waka-identify sehemu 14 ambazo kuna uwezekano mkubwa wa kumkuta. Hizo sehemu zote zikafanyiwa kitu kinaitwa "synchronized ambush", yaani vikatengenezwa vikosi 14 vya askari wa Pakistani vikishirikisha maafisa wa CIA katika kila kikosi ambavyo vita-ambush sehemu zote 14 kwa muda mmoja, hapo ndipo walipomkamata KSM lakini walichoshangaa ni kuwa kwenye location moja katika zile 14 walikuta kiwanja hakina nyumba. walipofuatilia waya wa simu unaotumika kwa ID ya kiwanja hicho uko kwenye nyumba ipi ndipo ofisa wa ISI mtaalamu wa IT akai-trace nyumba inayotumia ID ya kile kiwanja humo ndipo walipomfurumusha na kumpiga risasi Abu Zubeida ambaye alipelekwa kutibiwa ujerumani akapona na kutoa siri kibao.

salute mkuu,napenda sana hizi habari za masuala ya kijasusi,ease add some more.
 
Unamwagiwa umbea unashangilia tu. Habari za alkaeda ni puzzle na wengi wanatengeneza tu. Kama alivyotengeneza Obama kumuua Osama aliyekufa more than 2 year ago.

Nampa sifa coz he explained it in details nawe ingekuwa vizuri kama ungepinga kwa hoja na kututhibitishia huyo Osama unayeemjua aliyekufa miaka miwili iliyopita. Karibu
 
Back
Top Bottom