Maisha ya Osama kabla hajakamatwa yafichuliwa

Maisha ya Osama kabla hajakamatwa yafichuliwa

Mie nauliza
1 ni speech gani ya Osama aliyokubali kwa matamshi yake kuwa anahusika na 9/11.
2 Bush alitangaza zawadi nono kwa atakaye toa taarifa/kumkamata Osama dead o alive.
Iweje ipangwe mission ya kumuua na kumzikia baharini eti wamefuata sheria za kislam,muislam gani aliezikwa au kazika baharini?
Zaidi ya firauni aliekufa majini na akarudishwa ufukweni kwa uwezo wa mwenyezi mungu ili awe fundisho kwa bin adam.
Naombeni majibu?
 
Marekani ana mikwala,uwongo na fitna nyingi kwenye siasa yake kwa maslahi yake na shoga zake.
Pamoja na kufa kwa Osama marekani hana ushindi Afgan wala Iraq na leo tunaskia Mali,Somalia,Nigeria.
Mbona hawaishi kama sio fitna?
 
Vile vile katika ripoti hiyo ya commission inamtaja afisa mmoja wa shirika la kijasusi la Pakistani (ISI) kuwa kuna uwezekano alihusika katika njama za marekani kumkamata Osama kwa kuwa wiki moja kabla ya tukio la kumkamata Osama, aliwatuma watu kukata miti mikubwa iliyokuwa inazunguka ile nyumba Abbottabad ikiwa ni maandalizi ya helicopter kutua. Vile vile baada ya tukio la kukamatwa Osama aliuza vitu vyake na kuondoka Pakistani. Tofauti kati ya mashirika ya intelligence ya huku kwetu na nchi zilizoendelea ni kuwa wenzetu mashirika yao yanafanya mission zenye maslahi kwa taifa siyo kwa chama tawala. Ndio maana mission ikishakamilika wanatoa taarifa yote in detail kasoro baadhi tu ya tactics ambazo wanaona wataendelea kuzitumia kwenye mission nyingine. Huku kwetu mission zilizojaa TISS ni zile za kukandamiza Upinzani kama kumuua Kombe, kuua viongozi wa upinzani, kuwarushia mabomu Chadema n.k hizi mission hauwezi kuja kujua ukweli mpaka mmoja wao awageuke aropoke. Wenzetu mission zao zinakuwa high classified, lakini ikishakamilika tu wana-disclose kila kitu. Kwa mfano mission ya kumkamata Khaleed Sheikh Mohamed (KSM) the ring leader and mastermind wa 9/11 na akina Ramzi Yousef inajulikana ilifanywaje. Walifuatilia trail ya hela zote zilizokuwa wired kwenye account ya Mohamed Attar (kiongozi wa magaidi waliobamiza ndege WTC) Walianzia Dortimund Ujerumani ambakao Mohammed Attar alikuwa anasoma master of Science in Urban Planning katika chuo kikuu cha Dortimund. Walifuatilia trail ya ufadhili wa hela, msikiti aliokuwa anaswali hadi wakajua cell yao ilikuwa na kina nani, safari zake Pakistani na watu aliokuwa anakutana nao. Mohamed Attar ndio alikuwa ana-distribute hela kwa wale wengine za kusomea u-pilot wa ndege marekani. lakini hadi wanasomea upilot walikuwa hawajui mission yao itakuwaje. aliekuwa anajua mission ni KSM na Mohamed Attar. Kuna gaidi mmoja ambaye alikuwa yupo kwenye kikosi cha kwanza lakini alinyimwa viza ya kuingia marekani ndio alimtaja KSM kuwa ndie aliekuwa anawafadhili. Tofauti na kina Osama, KSM alikuwa anaishi maisha ya kifahari, anaingia kwenye club za usiku, anatumia vileo, anatumia simu, anachukua machangu, hakuwa anaishai maisha ya kiislamu. Kosa la kwanza na kubwa ambalo KSM na Ramzi walilifanya ni kumualika mwandishi wa habari wa Al-jazeera kwenda kuwahoji Pakistani. Ikieleweka kuwa kabla ya 9/11, Osama alikuwa anajulikana lakini hakuwa maarufu sana, hivyo kulikuwa na struggle kati ya magaidi kila mtu akitaka kupata umaarufu kuwa yeye ndio gaidi zaidi. Hiki ndicho kiliwasukuma KSM na Ramzi kumualika yule mtangazaji wa Al-jazeera kwenda kuwahoji. Yule mtangazaji alienda Islamabad akafungwa kitambaa usoni akazungushwa kwenye gari kuanzia asubuhi hadi jioni ili asijue muelekeo, mwishowe akashushwa kwenye gari wakamuingiza kwenye nyumba ambayo ina bunker alipofunguliwa kitambaa akakutana uso kwa uso na KSM akiwa na Ramzi Yousef. Pale KSM aka-declare jihad against American na ku-confess yeye ndiye aliyepanga na ku-finance mission nzima ya kubamiza ndege WTC. Yule mtangazaji wa Al-jazeera alipomaliza kuwahoji akaomba aondoke na Video footage wakamkatalia ila wakamruhusu achukue Audio record, hilo ndilo lilikuwa kosa kubwa sana maana ile audio iliporushwa tu Al-Jazeera, CIA wakaenda kuichukua Al-Jazeera wakatenganisha voice print za kila mtu alieongea kwenye ule mkutano wakaingiza kwenye mashine yao inayo-identify voice print ya kila mtu kama finger print. Hapo ndio ukawa mwanzo wa Drone attack Pakistani. Mtu akiongea kwenye simu kabla hajakata simu anashangaa bomu limeshatua. Kuna tukio moja walikuwa wamewasiliana wahudhurie harusi na Ayman Al Zawahil atakuwepo, machale yakawacheza Zawahili hakwenda, ile harusi ilibutuliwa na drone walikufa watu ukoo mzima. Baada ya kukamatwa Ramzi, KSM alistuka kuwa anafuatiliwa kwenye simu hivyo alikuwa hatumii simu yake, anaomba watu atumie simu zao ndio maana zoezi la kumkamata KSM lilishindikana zaidi ya mara 20, wakimtrace sehemu wakienda hawamkuti, alikuwa halali sehemu moja mara mbili mfululizo, Mpaka walipoamua kumtengenezea ramani kwa kutumia simu anazotumia, waka-identify sehemu 14 ambazo kuna uwezekano mkubwa wa kumkuta. Hizo sehemu zote zikafanyiwa kitu kinaitwa "synchronized ambush", yaani vikatengenezwa vikosi 14 vya askari wa Pakistani vikishirikisha maafisa wa CIA katika kila kikosi ambavyo vita-ambush sehemu zote 14 kwa muda mmoja, hapo ndipo walipomkamata KSM lakini walichoshangaa ni kuwa kwenye location moja katika zile 14 walikuta kiwanja hakina nyumba. walipofuatilia waya wa simu unaotumika kwa ID ya kiwanja hicho uko kwenye nyumba ipi ndipo ofisa wa ISI mtaalamu wa IT akai-trace nyumba inayotumia ID ya kile kiwanja humo ndipo walipomfurumusha na kumpiga risasi Abu Zubeida ambaye alipelekwa kutibiwa ujerumani akapona na kutoa siri kibao.

Ahsante kaka
 
Mie nauliza
1 ni speech gani ya Osama aliyokubali kwa matamshi yake kuwa anahusika na 9/11.
2 Bush alitangaza zawadi nono kwa atakaye toa taarifa/kumkamata Osama dead o alive.
Iweje ipangwe mission ya kumuua na kumzikia baharini eti wamefuata sheria za kislam,muislam gani aliezikwa au kazika baharini?
Zaidi ya firauni aliekufa majini na akarudishwa ufukweni kwa uwezo wa mwenyezi mungu ili awe fundisho kwa bin adam.
Naombeni majibu?
nafikiri katika mashambulizi ya WTC Al Qaeda walihusika na kiongozi wao kwa kipindi hicho alikuwa Osama bin Laden kwa hiyo moja kwa moja Osama alihusika...

hata milipuko ya balozi za Marekani huku Tanzania na Kenya mwaka 1998 Mtandao wa Al Qaeda ulihusika...

kwa hiyo Osama moja kwa moja alikuwa anahusika na Mashambulizi mbali mbali na mtandao wake wa Al Qaeda...

Vinginevyo ulete uthibitisho kwamba alikuwa hausiki ulete na uthibitisho akikana kwamba hausiki au akisema yeye hausiki wanamsingizia tu...
 
Marekani ana mikwala,uwongo na fitna nyingi kwenye siasa yake kwa maslahi yake na shoga zake.
Pamoja na kufa kwa Osama marekani hana ushindi Afgan wala Iraq na leo tunaskia Mali,Somalia,Nigeria.
Mbona hawaishi kama sio fitna?
Sidhani kama Marekani ana mikwara kama unavyosema jamaa wapo makini na mambo yao...

kama unavyosema huko Nigeria kuna kikundi cha Boko haram lakini wenyewe wanapambana na wanigeria wenzao! vivyo hivyo kwa Al Shaabab ya Somalia pamoja na wale jamaa wa Mali lakini kule Mali naona Wafaransa wapo kule...
 
Last edited by a moderator:
mkuu FUHRER nipo nakusoma vizuri sana kama ulivyosema nipo kwa makini nafuatilia hizo mambo utakazokuwa unaweka...

Tupo pamoja sana, inabidi tuweze kujifunza kwa hizo Intelligence zilizofanikiwa za wenzetu wa dunia ya kwanza huko...

Inabidi TISS yetu iweze kujitofautisha na green guard ya CCM iweze kuwa makini sio kwa ajili ya kutumikia chama ila iwe kwa ajili ya taifa zima...

na kina Ramadhani Ighondu wajifunze zaidi waachane na mbinu za kung'oa watu kucha pamoja na meno bila ya ganzi...

kwa ajili ya kulinda maslahi ya chama tu, ni somo zuri kwa kina Jack Zoka na wenzake, TISS isitumike kwa kuiba kura za wapinzani bali iwe kwa maslahi ya Taifa kwa ujumla

Pamoja sana...
 
Last edited by a moderator:
kweli penye nia pana njia, huu ufafanuzi umesaidia sana.

kuna novel nyingi kumhusu osama ziliandikwa haraka sana baada ya osama kuuliwa ili kuchuma pesa,huyo jamaa huyo jamaa ufafanuzi wake unaweza kuwa ameutoa kwenye finction novel.licha ya kutoweka link pia hataki kutuambia huyo mwana wa mfalume ni nani aliekua akimfinance bin laden,na alikufa lini ili tufanye search,na uzuri watoto wa marehemu king saud bin abdila aziz wanajulikana na mmojawapo ndo king abdullah wa saud.
 
elungata upo sahihi kabisa mkuu.jamaa is a good narrator na ninamfatilia vizuri sana.lakini haweki source au majina ya vitabu anavyosoma/alivyosoma ili mwisho wa siku nasi tuvitafute.hala hala asije tu akaja na porojo za "i get all these info from an inside CIA and ISI source or intelligence agencies/zile mambo za chanzo ni mimi mwenyewe".wenye hekima hapa jf watamdharau.
 
wakuu Elungata pamoja na kadoda11 leteni vitu kama mnavyo ili tuweze kuchambua tuone tupate ulinganifu...

Msiishie kuponda tu kuhusiana na source shusheni mambo wakuu...

Hata katika school of thought huwa zipo nyingi, au katika model huwa zipo mbali mbali mtu anapinga halafu anakuja na ya kwake inaweza kukubalika au isikubalike...

Sasa na nyie mngeshusha vitu sio mnasubiri mtu achemke halafu mpinge bila ya kuleta mbadala...

Kama vitabu au source zina fiction mngeleta mkasema hizi source hazina fiction, au mngesema hizo source unavyotoa hivyo vitu ina fiction maana imeandikwa hivyo...

Ndio maana kuna theory kama za Helicentric na Geocentric... Tuigeni kutoka huko kwa muktadha kama huu...
 
Last edited by a moderator:
Hivi hakuna hata dizain ya movie........nipo very interested kufuatilia........more news plz......
Preta there is this book "No Easy Day" an account by one of the Navy Seal - UBL Mission. Story yake matches to what FUHRER is putting forth...
Kwa mfano from chpt 10 anasimulia....

Walt and Charlie came in next. They both had big grins on their faces.
"You called it," I said to Charlie. "How did they find him?"​
"One of his couriers," Charlie said. "He has two guys working for him."

Al-Kuwait
The CIA learned of Ahmed al-Kuwaiti after the interrogation of a man named Mohammed al-Qahtani, a Saudi citizen and the alleged twentieth hijacker on September 11, 2001.
Immigration agents barred him from entering the United States in August 2001 because they thought he was trying to immigrate illegally to the United States.​

Al-Qahtani eventually told them that Khalid Sheikh Mohammed, the planner of the September 11 attacks, sent him to the United States. He also admitted to meeting Bin Laden and receiving terrorist training, and identified a man named Ahmed al-Kuwaiti as one of Bin Laden's couriers and right-hand men. Khalid Sheikh Mohammed, who was by this time in American custody as well, also acknowledged he knew al-Kuwaiti,

The agency started to track Ahmed al-Kuwaiti in Pakistan, hoping he would lead them to his brother and then to Bin Laden.Then, during an intercepted call to his family in 2010, one of his family members asked him what he was doing for work. For the most part, al-Kuwaiti had been savvy and kept his employer secret. So, when the family member asked what he was doing for work, al-Kuwaiti said he was "doing what he used to do."That subtle answer connected some dots and provided a good starting point for this operation. It was all circumstantial evidence, but it was all we had to go on.The CIA started to track Ahmed al-Kuwaiti, watching his patterns. They noticed he drove a white truck with a picture of a rhino on the spare-tire cover. The CIA eventually tracked the truck back to the compound in Abbottabad, which now sat in model-form in front of me.​


Kipo on pdf naweza kipandisha hapa kwa watakaopenda kusoma​
 
wakuu Elungata pamoja na kadoda11 leteni vitu kama mnavyo ili tuweze kuchambua tuone tupate ulinganifu...

Msiishie kuponda tu kuhusiana na source shusheni mambo wakuu...

Hata katika school of thought huwa zipo nyingi, au katika model huwa zipo mbali mbali mtu anapinga halafu anakuja na ya kwake inaweza kukubalika au isikubalike...

Sasa na nyie mngeshusha vitu sio mnasubiri mtu achemke halafu mpinge bila ya kuleta mbadala...

Kama vitabu au source zina fiction mngeleta mkasema hizi source hazina fiction, au mngesema hizo source unavyotoa hivyo vitu ina fiction maana imeandikwa hivyo...

Ndio maana kuna theory kama za Helicentric na Geocentric... Tuigeni kutoka huko kwa muktadha kama huu...
Mkuu wa chuo jaribu kupitisha macho kwa hii kitu...huwezi acha kusoma mwanzo mwisho...Utakuta kuna dada wa CIA kwa 10yrs yeye kazi yake ilkuwa kuchambua intel za OSAMA tu
 

Attachments

Last edited by a moderator:
osama walimkamata kwa shida katika report ya CIA ambayo siri zake zilivuja ni kwamba osama alikuwa na connection ya zaidi ya watu 20 ili uweze kufika au kitu kiweze kumfikia na pale tu walipombana yule bwana wa gereza la guantanamo na kuwaambia msihangaike na osama anzeni na network ya kutoka kwa fulani mwishowe mtampata , na mpaka leo ndiyo maana wamerakani wanahisi lile gereza lina mchango mkubwa katika kufanikisha maswala ya kiugaidi

Sasa una ushauri gani kwa wale ambao hadi Leo wanasema Osama hajakamatwa wala kufa na he's still alive and on the run
 
Sasa una ushauri gani kwa wale ambao hadi Leo wanasema Osama hajakamatwa wala kufa na he's still alive and on the run

huo uwezekano upo kuwa wala hata hajauawa na kuna uwezekano alikua anafanya yote kwa niaba ya marekani,ndo maana baada ya tukio la sptember 11,anga la marekani lilifungwa kwa ndege za kiraia kwa zaidi ya wiki tatu hakukuwa na ruksa ya ndege ya abiria kuingia au kutoka marekani,lakini serikali ya marekani iliruhusu saudi arabia itume ndege zake kuja kuwachukua raia wa saudi arabia wakiwemo family ya bin laden na kuwarudisha saud.
Kwanini ndege ya saudia peke yake iliruhusiwa kutua marekani na kuondoka na raia wake wakati kwanza ilijulikana wazi kwamba kati ya wateka ndege 19 waliofanya tukio la september11, 15 walikua raia wa saudi arabia.
Just google..saudi arabia citizen removed from US after 9/11.
 
wakuu Elungata pamoja na kadoda11 leteni vitu kama mnavyo ili tuweze kuchambua tuone tupate ulinganifu...

Msiishie kuponda tu kuhusiana na source shusheni mambo wakuu...

Hata katika school of thought huwa zipo nyingi, au katika model huwa zipo mbali mbali mtu anapinga halafu anakuja na ya kwake inaweza kukubalika au isikubalike...

Sasa na nyie mngeshusha vitu sio mnasubiri mtu achemke halafu mpinge bila ya kuleta mbadala...

Kama vitabu au source zina fiction mngeleta mkasema hizi source hazina fiction, au mngesema hizo source unavyotoa hivyo vitu ina fiction maana imeandikwa hivyo...

Ndio maana kuna theory kama za Helicentric na Geocentric... Tuigeni kutoka huko kwa muktadha kama huu...

madam thread haiondoki nitaleta after i do datamining.afterall thread nimeiona kwa ghafla..jamaa nimemchallenge sababu alikua haweki source,ina maana angeweka source tungeweza kufuata ili kupata uhakika wa anachokisema
 
Last edited by a moderator:
Preta there is this book "No Easy Day" an account by one of the Navy Seal - UBL Mission. Story yake matches to what FUHRER is putting forth...
Kwa mfano from chpt 10 anasimulia....



Al-Kuwait






Kipo on pdf naweza kipandisha hapa kwa watakaopenda kusoma​

navy seal wengi tu waliandika baada ya tukio la abbotabad akiwemo yule anaedai ndo alimtwanga risasi bin laden,lakini ujue kuwa Navy seal ni watu ambao walipewa mission wakaonyeshwa target wakaenda kufanya walichotumwa..intelligence na process zote zilizofanywa hadi wakapin point alipojificha binladen hawezi akawa nazo huyo navy seal,wao walipewa jukumu la kwenda kumkamata binladen baada ya intelligence kuwa wamefanya kazi zao.kwahiyo hicho kitabu hakiwezi kuwa reliable source.
 
sasa hivi naona hali imetulia baada ya huyu jamaa kuuawa, kuna jamaa mmoja ndio sasa hivi amechukua nafasi ya Osama anaitwa Zawahir lakini hakuna kitu...

Al Qaeda kwa sasa hawafanyi milipuko ya kijinga kijinga

hapo ndipo ninapowakubali CIA wanapiga shughuli zao bila hata intelligence ya Pakistan kushtuka...

CIA hawa ndio wanajua kazi sio kama TISS ya Tanzania ni ya kijinga sana...

wenyewe wanachojua ni kung'oa watu kucha na meno badala ya kulinda raia...

Bomu limelipuka Arusha lakini hadi leo hii ni ubabaishaji mtupu yaani hawa TISS hakuna kitu...

CIA hawa jamaa ni noma...

hii summary yako bado sijakubaliana na ww, kwa kutaka kufananisha TISS na CIA kuna bonde kubwa sana kati yetu kuanzia utaratibu wa utendaji mpaka zana za utendaji kazi.

Jaribu kufuatilia matatizo yanayowakumba CIA japo upate mwanga kidogo ingawa inaweza kua ngumu kupata taarifa hasa ukizingatia wanahusika na kuchuja taarifa za mfumo wa digital kama za humu kwny Internet. Hivyo wanaweza pandikiza taarifa yeyote ambayo watataka wewe uisome na kuamini.

Labda katiba mpya inaweza kuleta mabadiliko katika utendaji wa TISS ila uelewa wangu mdogo hawa jamaa zetu wanafanya kazi katika mazingira magumu na ya utata wa kuhatarisha hata maisha yao japo ni siri wanayoitunza baada ya kiapo kikali.
 
Asante Fuhrer. Na pia movie iliyotengenezwa kutoka kwenye hayo maelezo ni 'ZERO DARK THIRTY'
Ni movie nzuri kuiangalia...
 
madam thread haiondoki nitaleta after i do datamining.afterall thread nimeiona kwa ghafla..jamaa nimemchallenge sababu alikua haweki source,ina maana angeweka source tungeweza kufuata ili kupata uhakika wa anachokisema

navy seal wengi tu waliandika baada ya tukio la abbotabad akiwemo yule anaedai ndo alimtwanga risasi bin laden,lakini ujue kuwa Navy seal ni watu ambao walipewa mission wakaonyeshwa target wakaenda kufanya walichotumwa..intelligence na process zote zilizofanywa hadi wakapin point alipojificha binladen hawezi akawa nazo huyo navy seal,wao walipewa jukumu la kwenda kumkamata binladen baada ya intelligence kuwa wamefanya kazi zao.kwahiyo hicho kitabu hakiwezi kuwa reliable source.
Elungata naona na wewe unazunguka palepale...unaomba uwekewe source yet wewe hufanyi hivyo..

Umesoma vitabu vingapi vya navy seals walokwenda kwenye hii mission....they were 23 na mbwa wa 24. Ni wangapi kati yao wameandika vitabu...tuwekee hapa pls!!!

Ila kama ulisoma "No Easy Day" kisha usome hii ripoti ya Commission then add a little of your intelligence (Knowledge) utajua the book has an "on hands experience" on this mission.
 
Back
Top Bottom