Maisha ya sasa Mwanaume na Mwanamke ni maadui wakubwa, tusitegemee tena ndoa kudumu

Umesahau hiyo rafiki yako alifariki
 
Shangaa unaacha lisaliti lakini mwingine anachukua, wanashidwana na mwingine anabeba. Sinaga swaga za ushenzi huo na sipendi bora niishi singo huku nikiwa tayari nina watoto
 
Mwaka wa 67 huu na umaskini wangu nadunda na Ndoa.
Acheni uhuni wajukuu zangu.

Kipindi ulichooa wewe si sawa na cha wakati huu,hivisasa me na ke ni kama ukoo wa panya kila mtu ana ndevu yani ubabe,jeuri,kiburi,visirani kila mtu ana maex msululu,hakuna jipya,hakuna wa kumtisha mwenzake.
 
Me naamini matatizo ya ndoa yalikuepo na yapo , kinachochangia kwa sasa kuonekana migogoro inaendelea ni mitandao ya kijamii kitu kidogo kinateka attention balaa Pia vijana wa sasa ni nyoro nyoro , mtu akiguswa kidogo anajiliza vibaya mno !! Wanaita kutendwa πŸ˜‚πŸ˜‚
Zamani mwanamke anajua kabisa baba akitimiza majukumu yake nyumbani kila kitu kimekaa mkao scandle nyingine za baba anajifanya hazioni ! Sijui michepuko anaishia tu kuhisi hisi !! Mzee nae ikitokea kamfuma mama wanafukuzana kiroho sasa wanaachana inakua aibu lakini haikamati attention kama sasa "kuchapiwa ilikua siri ya ndani"

Siku hizi vidada vinakaba mpaka penati hata likipita tako 64Gb ukigeuka ni kosa ! Madogo wa kiume wako bize kutaka kufit kwenye demand za msichana ! Wanaanza kutaka kumridhisha kila kitu atakachopenda ila apate attention ya mrembo !! Anayepaswa kutafuta attention kwa nguvu kwenye mahusiano ni dada , Mwanaume wewe unaitengeneza
Baada ya hapo ni maelewano sasa mwanaume na mwanamke wote wanatafuta attention. Lazima mfarakane
"Mwanaume tengeneza kukubalika , Mwanamke yeye atafute kukubalika"
 
Kweli kiongozi, kuna ushindani mkubwa sana, ushindani huu utamaliza watu
 
Kuhisi mwanamke ni adui kumesababisha kuona mwanaume mwenzako ni rafiki , mwisho urafiki umezaa ushoga , hili tatizo la ushoga kuna namna kila mtu ameshiriki uwepo wake kwa namna moja ama nyingne .
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…