Maisha ya Udalali: Kumzunguka dalali ni sawa?

Mkuu wewe muoga mno.
Yaani mjini hapa mtu anitishe kiasi hiko?
Halafu napendaga ligi za hivyo.
Unkinidindishia ndo nafanya kusudi.

Bora uje kistaarabu tukae mezani naweza walau kukupa hela ya serengeti 4.
Ila vitisho mhh
 

Asante amu.
dronedrake umejifunza kitu hapa?
 
Hiyo kitu ilinitokea siku ya kwenda kufanya malipo sikuenda pamoja na dalali Japo baadaye niliwapa ela
Changamoto ya udalali chain inakuwa ndefu.
MI nilimuagiza jamaa mmoja, na Yeye akamuuliza mtu mwingine,mtu mwingine naye akatuunganisha kwa watu wa eneo lile. Pesa ikatolewa kwa mtu wa kwanza kila dalali anadai ela, wakaishia kudhurumiana
 

Ukampa 10% yake yote ama kiasi?
 
Wale wabaya mno....[emoji23]
Kwa hela wanazopata bado wanaishi maisha ya kijinga.
Labda sababu ni hela za dhuluma.
Yaani mtu anauwezo wa kukunja laki 3 kwa siku kwa mtu mmoja au hata siku mbili.
Lakini bado na pesa za mwenye mazao anazitaka.
Atakuchengaaaaaa usipokaza imeisha hiyo.

Anachukua posho yake na mtaji wako [emoji28][emoji28]
 
Madalali watu wa ajabu sana, anaweza kuwa anasifia nyumba kumbe yeye mwenyewe hajawahi kuitembelea unafika unakuta analokwambia na jinsi mambo yalivyo tofauti. Anaweza kukwambia ina maji ya dawasa sijui luku yako unafika unakuta tofauti na yeye ukimuuliza anatoa macho kama panya kabanwa mlango
 
shida walio wengi wamekaa kumponda dalali wanasahau mada kuu ya mjadala.

swali ni je ni sawa kumzunguuka dalali???
na vipi kuna utaratibu wowote kisheria endapo ukinaunguuka dalali???

hachaneni na maswala ya kuita mara tapeli mara nini
Hakuna sheria inayowalinda madalali..
Kuna wadau wamesema ni sawa na wengine wanasema sio sawa mteja kumzunguka dalali..
Mimi naona inategemeana na mazingira ya huo udalali,, wata wanakataa kupigwa cha juu zaidi kutokana na janja janja za madalali zinazosababishwa na tamaa zao kubwa! Hata Mimi niliwahi kuvunja mikataba au makubaliano na madalali pindi tu ninapogundua naenda kuumizwa hivi hivi nikiona!
 
Mkuu wewe muoga mno.
Yaani mjini hapa mtu anitishe kiasi hiko?
Halafu napendaga ligi za hivyo.
Unkinidindishia ndo nafanya kusudi.

Bora uje kistaarabu tukae mezani naweza walau kukupa hela ya serengeti 4.
Ila vitisho mhh
Enzi hizo nilikua ndio nimeanza maisha mtaani natoka chuo. Kiringi cha madalali cha ule mtaa pia kilinitoa amani.
Nshawah kucheza lkn km wewe kuna nyumba niliinunua sehem, dalali kataja cha juu. Nkatengeneza urafk na mwenyewe tukashushana safi. Hii ilikua rahisi coz dalali anakaa mbali na nyumba ilipo.
Tena mwenye nyumba mitaa yetu ilikua karibu.
 
hakuna kitu sipendi duniani kama udalali mi huwa naona ni wizi,hata wale wanaokatisha ticket stend mawaona kama madalal tu nao wananikera balaa,basi moja,trip Moja nauli tofaut,KUMZUNGUKA DALALI NAONA IKO POA SANA
Niko hapa kwenye basi nmetulia baada ya kusevu 5000 nauli tofauti na abiria wengi,, sipendi ujinga Mimi naongea na mwenye Mali na sio hao wapambe
 
ulikuwa mwoga mno mzee afu nkuambie ktu mtu "mwenye uwezo wa kukudhuru huwa hana muda wa kutisha tisha kwa maneno yan"
 

Nilikuwa namsaidia rafiki yangu aliyehamia Dodoma kutafuta nyumba, Anakupeleka kwenye nyumba tofauti na unayoitarajia halafu anaanza kazi imesimama hii si unaona [emoji3] Ilifika muda niliwauliza kwa ukali “hivi ni sisi hatuna akili au ni ninyi hamna akili”?
 
Dunia ya ubepari haina msamiati usawa.
Madalali wengi wana tamaa mno,yani anataka apate cha juu kinacholingana n mmiliki.
Niliwahi kununua gari kwa kumzunguka,yani unakuta gari ya M8 anataka apate hapo M1
Kwny magari madalali ni wajinga tena mataahira kabisa.

Kuna dalali mmoja wa kule kupatana.com na hata humu JF yumo sana tu akiuza magari, alikua anauza nissan flan hivi kwa Mil 13.5,nikapambana sana nikampata mmiliki wa hio gari mwishowe akaiuza kwa mil 8.3 tu.

Kumuuliza mmiliki anasema dalali alimwambia huko mitandaoni anaiuza kwa mil.9 kumbe anaiuza mil 13.5m na amesababisha gari imekaa mwaka mzima bila kuuzika.
 
Madalali yani kweli inaweza fika muda ukahisi labd anakuona taahira kabisa. Yani ni wangese sana
 
Mama Debora kajibu vyema, wenye nyumba na dalali lao huwa moja. Na wao ndio hupanga bei mpaka za nyumba.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…