binti kiziwi
JF-Expert Member
- Aug 4, 2014
- 11,201
- 28,642
Dada kuna sheria mpya inaandaliwa, muda wowote muswada wake utapelekwa bungeni kusomwa,...itawalazimisha madalali kusajiliwa kwa level ya mtaa/kata/wilaya/mkoa na taifa. Na pia watatakiwa wawe na taaluma husika kutoka vyuo vinavyotambulika.
Ubabaishaji ulizidi na serikali inakosa mapato huku wananchi wakiumia.
Hio ndio inatakiwa yani, hawa madalali wanahisigi hela ni nyepesi sana. Yani nikupe laki 2 kwa kunionesha nyumba tu! Na labda usinikutanishe na mwenye nyumba maana nikikutana nae tu umeisha!Sijajua ni uoga, Udaslamu au ni unini unaopelekea watu kuwahanya madalali kiasi hicho, imagine mwenye nyumba pia anamuogopa dalali! Au ni ule ubabe mbuzi wa mitaani kwamba anaweza kukuvamia akakupiga?!
Okay, mi nyumba ninayoishi inajulikana kwa mtaa huu mzima kuwa Landlady hataki madalali, hata wakileta mteja wanampa mteja namba ampigie mwenyewe mwenye nyumba halafu wanakaa pembeni wanakusikiliza makubaliano yenu.
Nilienda na dalali mmoja bahati nzuri ilikuwa jumapili, tukafika tukakuta mafundi wanamalizia vitu vidogo vidogo nje ikiwemo na kufitisha geti, tukaomba namba mafundi wakatupa, nikampigia akanambia naomba dakika 10 natokea nyumbani kwangu nakuja. Dalali akanambia usimwambie mi ni dalali mwambie tu ni rafiki yako nikamuuliza why akasema tunasikia hatakagi madalali (bila ye kujua nikashangilia kiroho roho). Yule mama akaja nikaongea nae tukakubaliana ilikuwa katikati ya mwezi nikamwambia basi nadeposit now kwa mpesa 500k ili nihold nyumba maana watu wengi walikuwa wanatafuta nyumba, halafu mwisho wa mwezi nadeposit 1M iliyobaki then nahamia tukawa tumemalizana na mwenye nyumba kimtindo huo tukaachana. Dalali bila kujua amejiloga mwenyewe akaanza Bosi nyumba umeshachukua sasa chetu vipi, nikamwambia nina laki hapa niwape 50k tuachane maana 250k siwezi wapa mnaona nyumba yenyewe nalipa kwa installment sina hela, wakaanza ohh tuko wengi hiyo hailipi na blah blah, nikajiuliza kichwani wapo wengi? Na pale amenipeleka mmoja? Na amenipeleka kunionesha tu! Nikamwambia chukua tu hii 50k sababu nimekutoa kwa kazi zako kiheshima tu kiroho safi akaendeleza malalamiko, nikaichomoa nikampa nikapanda bajaji huyooo. Sasa mwisho wa mwezi wakawa wananivizia waone ninavohamia wanidai, nilimjibu tu kiufupi hiyo hela sina labda nikipata ntakwambia. Hadi leo hii ndio nitolee.
Huwa namuuliza mwenye nyumba wanasema kuna siku utakosa wateja, ananijibu kazini kwangu kila mwaka inaingia intake mpya nianze kukimbizana na madalali mimi? Hata nikikosa nitatumia connections zangu kupata wateja, Mama mmoja mstaarabu sana na msomi pia.
Saingine wanakupeleka kwenye nyumba ambazo hazikaliki unakuta ushampa hela na kodi umelipa usiku hulali! ila watasema nyumba nzuri haina shida 🤣🤣🤣Hapo ni sawa, bora umlipe kihalali kuliko kumlipa mtu ambaye kwanza kazi aliyofanya hailingani na malipo anayodai na halipi kodi popote. Binafsi siwezi mlipa dalali pesa ya mwezi mmoja, mpaka walete hiyo sheria.
Na hata hio ya kulipa mwezi mmoja kiutaratibu anatakiwa alipe mwenye nyumba. Amuachie dalali mwezi mmoja katika ile 6!Kesi ya kuzungukwa hiyo ni kati yake na Mmiliki sio mimi Mteja, kama Mmiliki kakubali biashara bila Dalali wake basi wamalizane wao kwa wao.
Hahaaaaa, wale jamaa wanakera sanaaaa...wale wakatisha tiketi ndo kiboko sasa yaan ukiwa na safar afu hujui nauli ya unakoenda ahahahaa watakupiga ushangae
juzi naenda mwanza nkapanda basi moja na mdada mmoja anashukia dodoma. nauli wamemkatia elfu 40 wakat mie wa mwanza nmelipa 35 daah nlisikitka sana. mm siez kulipa nauli mpaka nipeleleze je nauli ya nnako3nda ni sh ngapi?? yaan pale kwny bus naenda nkiwa na nauli yangu kichwan.
jerrybanks nimemuita kabisa.Hahah hapana ni jamaa mmoja hivi hua ana story za uongo uongo kwa sana tu.
Hahah daah naona unataka vita vya 3 vya dunia mkuu.jerrybanks nimemuita kabisa.
Usijali.Hahah daah naona unataka vita vya 3 vya dunia mkuu.
Hahah wanakaribishwa.Usijali.
Ngoja waje tupambane nao [emoji23][emoji23][emoji23]
Na imagne vyenye ulivokuwa unaongea kwan ukali, nmebaki kucheka had mbavu znauma mweeeeeeh.Nilikuwa namsaidia rafiki yangu aliyehamia Dodoma kutafuta nyumba, Anakupeleka kwenye nyumba tofauti na unayoitarajia halafu anaanza kazi imesimama hii si unaona [emoji3] Ilifika muda niliwauliza kwa ukali “hivi ni sisi hatuna akili au ni ninyi hamna akili”?
Dalali ni kazi Kama kazi zingine hata Mino Raiola ni dalali was CR7 ila tu kwa sababu tunatumia neno agent ndio maana anaheshimika.Habarini wakuu poleni na majukumu. Ttwende kwenye mada.
1. Unatafuta chumba/kiwanja, ukaingia Jamiiforums ukaona tangazo la dalali na ametaja eneo na bei.
Sasa kuepuka kumlipa ile 10%
Kwakuwa unafahamu lile eneo wewe unaenda unaulizia mwenyewe na ukalipa direct kwa mwenye mali.
Je, hiyo ni sawa?
2. Unatafuta chumba cha kupanga ukampata dalali ana chumba kizuri tu na ukakipenda. Bwana dalali akakupeleka kukiona hicho chumba ila mteja ukadai hujakipenda, ukampa elfu 10 yake ya kukuzungusha.
Baada ya muda ukarudi ukaongea na mwenye nyumba direct ukamlipa kodi yake. Hapa ukawa umeruka kumpa dalali kodi ya mwezi mmoja.
Swali kwa wadau (dalali na wateja)
1. Je, ni sawa mteja kumzunguka kutumia mbinu hizo?
2. Je, huyu dalali akigundua kuwa umemzunguka atakufanya nini, kuna sheria au taratibu zozote?
Wadau (dalali na mteja) waliowahi kufanya hivi.
Share na sisi tafadhilini.