Maisha yangu baada ya miaka 37!

Maisha yangu baada ya miaka 37!

Habari.
Nina miaka 37. Sifurahii maisha katika umri huu. Kama Kuna mtu anaweza kutoa ushauri wa kunikomboa asisite...Mshana Jr etc. Mtiririko wa matukio ni kama ufuatavyo.

1. Ninafanya kazi serikalini mshahara take home ni 1.3m. hapo Nina mkopo wa miaka 5 NMB.

2. Kazi nimeanza tangu 2012. Hivyo Nina miaka 9+ kazini.

3. Naishi Dar es Salaam.

4. Nina mke na watoto wanne. Mtoto wa nne bado ni kichanga.

5. Tangu nianze kazi sijui pesa zangu zinapoenda. Sina kiwanja Sina akiba. Bado nimepanga Kodi laki tatu kwa mwezi.

6. Mahusiano yangu na wife sio mazuri sana kwa sababu ya ugumu wa maisha. Lakini bado tunasonga.

7. Wife Hana kazi Hana biashara.

8. Nakunywa pombe mara kwa mara.

9. Siendi kanisani kabisa ila kwa matukio maalum mfano ndoa, ubatizo wa mtoto, etc

10. Sina gari. Nilioanza nao kazi Wana nyumba kubwa na magari mawili. Moja la wife....

Nahisi Nina mkosi nifanye nini? Yapo mengi kuonesha hasara ninayoihisi. Kazini napata marupurupu ya hapa na pale. Ila najiona sitoboi. Wadogo zangu wenye mshahara wa laki Tano wametoboa mi nipo nipo tu mpka mama yangu amekata tamaa. Faraja yangu iliyobaki ni Binti zangu ambao hawaelewi chochote kwenye hii Dunia ya vita.
Nenda Instagram kamtafute joelnanauka anafundisha sana namna ya watu kujikomboa kiuchumi...na wengi kupitia mafundisho yake wamejikomboa na madeni pia wamesimama kiuchumi hata kama awali walianguka.....Mimi binafsi tumejiari na tunapata pesa kidogo tu lakini life linasonga..yaani haya maisha ni kuwa na nidhamu ya pesa...ukiwa huna mipango ya kuitumia pesa basi pesa yenyewe ndiyo itakupangia matumizi kwa sababu wewe huipangii matumizi...

Ushauri wa awali ni huu...fungua account, ukipata hata kidogo tupia huko...jipe muda..utakuta umenunua kiwanja na hata kujenga....jiwekee malengo lazima utayatimiza tu...lakini usiache kusali na pia acha pombe na kufuja pesa....

Nidhamu ya pesa ni muhimu.
 
Pole sana mkuu ila njia yako haina tofauti sana na yangu. Ili nikushauri naanza kujielezea mm kwanza.

Nimeanza kaz X 2018 kwa mshahara wa 1.8m haina makato na ikafika had 5.4m

Mshahara wote huo nilikua naona hautoshi kuanza maisha.

Siku moja nilienda mkoani nikaona walimu wa shule za msingi wana nyumba na pikpk wakati huo mm sina hata baiskel (hii kitu iliniuma sana)

Nikaamua kufanya maamuzi magumu nikanunua gari japo nilikua sina uhitaji wa gari ila nilitaka linichangamshe akili kidgo

Baada ya hapo nikaingia kwenye viwanja japo sina uhitaji wa kujenga pia.

Nikaamua kujiingiza kwenye majukumu yatakayonifanya niache kutumia hela vibaya (hapa nilifanikiwa sana, asikwambie mtu kumsaidia mtu especially ndugu na akasema asante hiyo kitu inaleta baraka sana).

Mwisho nikajikuta siipendi pombe kwasababu ya majukumu niliyojiwekea.

Narudi kwako sasa, unaonekana humuamini mkeo na wewe ni aina ya watu wa changu ni changu mtu asinipangie namna ya kutumia hela yangu.

Tenga pesa ya kumuachia mkeo yaani usiwe na shida ya chakula hapo nyumbani halafu inayobaki anza kununua assets (najua unaogopa atarithi mkeo kwa njia ya kitonga ila fanya hivyo kwaajili ya wanao)

Kuacha pombe ni ngumu sana ni sawa na kuanzisha kikundi cha waasi wakati hauna jeshi la kutosha.

Punguza marafiki hata ukienda bar nenda na hela inayokutosha ww tu usiweke mambo ya emergency kwenye pombe, pombe italamba emergency yote.
Asante sana. Yaani pamoja na kupokea pesa kila mwisho wa mwezi suala la mahitaji ya nyumbani limekua topic. Lazima nidhibiti hali hii
 
Kwanza kanisani huendi unadhulumu Hela za zaka na michango kede unaenda kulewea🤣, na bado unalalama kuwa Hela huoni. Aisee tunaenda kanisani maisha magumu na bado Kuna sadaka, zaka, harambee, shukrani, na michango ya wahitaji ambayo hulipi. .

1. Kwanza kabisa acha kumdhulumu padri unataka akale wapi?
2 Pili jitahidi kupunguza gharama angalia matumizi yasiyo ya lazima, achana nayo
3. Mtafutie mama watoto wako Kaz ambayo anaweza Fanya hata akiwa nyumbani hata kuuza viungo vya chai na pilau
4. Fanya uzazi wa mpango ikiwezekama usipate mtoto mwingine kwa sasa. Fanya Vasectomy ( fungal mirija ya pumbu usitoe mbegu)
5. Jenga amani na furaha sana na mkeo achana na watu wa dunia. Huyo anakuvumilia mengi hujui tu. .

Mwisho kabisa hata mie Niko kwenye ndoa aisee ndoa tamu ukipuuzia mambo. Ukiwaza Kila Jambo utaumwa mda mwingine tunaweza chemsha mahindi Huku tunapigana denda siku inaisha😊

Kumbuka miaka mia toka sasa utakuwa umekufa utaona Kuna mambo hayana msingi. Acha kulewea na marafiki Kaa karibu na mkeo. .
Aise asante! Ila mirija sifungi
 
Tatizo lako lipo hapa

ID yako ni Kufa Kuzikana, kwa nini umechagua ili neno . Wakati Mwingine majina yanabeba siri katika maisha yetu.

Unahitaji Ukombozi wa kufunguliwa so tafuta Mchungaji wa kweli upate kufunguliwa. Inawezekana umeunganishwa unachokipanga kinajulikana wanakuja kuharibu mipango yako.
Labda. Hii ID niliiandika tu baada ya kusoma riwaya moja iliyoandikwa na mwandishi wa KENYA inaitwa KUFA KUZIKANA. Ni riwaya tamu sana hivyo kwa ajili ya mapenzi nikatumi hilo jina.
 
Nenda Instagram kamtafute joelnanauka anafundisha sana namna ya watu kujikomboa kiuchumi...na wengi kupitia mafundisho yake wamejikomboa na madeni pia wamesimama kiuchumi hata kama awali walianguka.....Mimi binafsi tumejiari na tunapata pesa kidogo tu lakini life linasonga..yaani haya maisha ni kuwa na nidhamu ya pesa...ukiwa huna mipango ya kuitumia pesa basi pesa yenyewe ndiyo itakupangia matumizi kwa sababu wewe huipangii matumizi...

Ushauri wa awali ni huu...fungua account, ukipata hata kidogo tupia huko...jipe muda..utakuta umenunua kiwanja na hata kujenga....jiwekee malengo lazima utayatimiza tu...lakini usiache kusali na pia acha pombe na kufuja pesa....

Nidhamu ya pesa ni muhimu.
Nita
Nenda Instagram kamtafute joelnanauka anafundisha sana namna ya watu kujikomboa kiuchumi...na wengi kupitia mafundisho yake wamejikomboa na madeni pia wamesimama kiuchumi hata kama awali walianguka.....Mimi binafsi tumejiari na tunapata pesa kidogo tu lakini life linasonga..yaani haya maisha ni kuwa na nidhamu ya pesa...ukiwa huna mipango ya kuitumia pesa basi pesa yenyewe ndiyo itakupangia matumizi kwa sababu wewe huipangii matumizi...

Ushauri wa awali ni huu...fungua account, ukipata hata kidogo tupia huko...jipe muda..utakuta umenunua kiwanja na hata kujenga....jiwekee malengo lazima utayatimiza tu...lakini usiache kusali na pia acha pombe na kufuja pesa....

Nidhamu ya pesa ni muhimu.
Nitafuatilia hiyo account ya IG. Asante kwa ushauri
 
Tangu nianze kazi sijui pesa zangu zinapoenda. Sina kiwanja Sina akiba. Bado nimepanga Kodi laki tatu kwa mwezi.
Kosa lilianzia hapa.
Na sio wewe tu wapo vijana wengi.

Ishi nyumba ya kawaida huku ukijiandaa kujenga yako.

Usijali marafiki zako wanasemaje.
Jifunze kwa wahindi wanarundikana familia na ukoo mzima kwenye magofu huku wakitengeneza mitaji ya biashara inayowapa uyajiri baadae
 
Pombe haikufanyi usifanye maendeleo, pombe ni starehe kama starehe nyingine starehe zipo nyingi sana na hakuna tatizo kwa binadamu kufanya starehe baada ya kazi is nature hata Mwenyezi Mungu alifanya siku ya jpili,. Ipo sababu nyingine kaa chini tafakari Hilo.
Tazizo hizo starehe unazifanya kwa nidhamu???

Ninaye rafiki yangu akinywa akifika chupa ya tano anatoa simu yake kuita washkaji zake hovyo kuna siku aliita watu tisa (9 people just imagine wanakunywa na kula kwa hela zake) sikuweza kuvumilia nikaaga nikaondoka na toka siku hiyo kampan yake sikuitamani tena.

Na mpaka sasa na yeye anaishi kwenye nyumba ya kupanga Tegeta huku mwanae aged 5½ kampeleka shule ada 2.5 mill na baadhi ya anaowanunulia pombe wanaishi kwenye nyumba zao,starehe bila nidhamu ni laana mleta mada shida ipo hapo kwenye pombe hakuna kingine.
 
Na mpaka sasa na yeye anaishi kwenye nyumba ya kupanga Tegeta huku mwanae aged 5½ kampeleka shule ada 2.5 mill na baadhi ya anaowanunulia pombe wanaishi kwenye nyumba zao,starehe bila nidhamu ni laana mleta mada shida ipo hapo kwenye pombe hakuna kingine.
Pombe kama huna hela ya Walamba asali umekwisha.

Watu wana mbinu nyingi ya kupata pesa. Ukiwa wewe ni mvuja jasho starehe ya pombe unatakiwa ujicontrol kweli kweli.

Pesa za michongo ndizo watu wananywea pombe na starehe sio hizi za kulala njaa
 
Na mpaka sasa na yeye anaishi kwenye nyumba ya kupanga Tegeta huku mwanae aged 5½ kampeleka shule ada 2.5 mill na baadhi ya anaowanunulia pombe wanaishi kwenye nyumba zao,starehe bila nidhamu ni laana mleta mada shida ipo hapo kwenye pombe hakuna kingine.
Kosa lingine watu wengi wanafanya ni kujikakamua kusomesha watoto kwenye shule za gharama wakidhani ni sifa.

Kama huna uwezo peleka mtoto kwenye shuke unayomuda ili upate salio la kuendeleza gurudumu.

Huku makazini tunafanya kazi na watu full stress. Ukiuliza eti anasomesha mtoto mwenyewe nursery
 
Back
Top Bottom