Maisha yangu, ushuhuda wangu; Sijafika sijachoka usikate tamaa Mungu yupo.

Maisha yangu, ushuhuda wangu; Sijafika sijachoka usikate tamaa Mungu yupo.

Mkuu pole sana

Si uende hapo kariakoo kutana na wakinga wenzio waambie ukweli watakupa hata kibarua chchote huku ukiendelea kusoma mchezo

Usijaribu kurudi kwenu mwakavuta utaishia kunywa ulanzi tu
Hahahah dadaq, mwakauta not mwakavuta ( mwakavuta ni shule ). ( Mwakauta ni Kijiji ).

Kule asirudi mamaq ,, Kuna ulanzi kama nini ....hahah

N b ...pambana huko huko uliko ...c hatuna msaada aisee
 
Njia rahisi ya kuondokana na umasikini kwa mtu asiye na kipato.
Ardhi still bado ndio mtaji rahisi wa kutokea kimaisha.
Nje ya mji mapori tele yamejaa hata bure au kukodi unaweza pata safisha angalau si chini ya heka 10,panda mazao yasiyo na changamoto mfano kunde, alizeti, mtama, nk.
Chukua zao moja hili ni uhakika.
Baada ya kusafisha heka 10 au zaidi panda mmea wa nyonyo castro oil huu unavuna baada ya miezi 3 na utaendelea kuvuna kwa mda wa miaka 2.
Heka moja ya nyonyo utapata gunia 15 ukizikamua utapata lita 500 za mafuta, so heka 10 ni lita elf 5.
Jifunze kutengeneza sabuni za mche za mawingu
Lita moja ya mafuta utapata miche 2 mara lita elf 5 utapata miche elf 10.
Uza mche kwa sh 1500 mara elf 10 utapata milioni 15.
Jinsi ya kutengeneza mashine ya kukamua mbegu za mafuta tafuta bomba inchi nne tafuta Nondo mm 12 ikunje mfano wa spring ingiza ndani ya bomba mbele ya bomba ziba acha tundu dogo.Toboa toboa Bomba vitundu vidogo Ili mafuta yamwagike chini, weka mshikio wa kunyongea Ili ukamue mafuta.
Ukipata pesa kodi nyumba nenda viwandani kafunge bidhaa ambazo ni daily use kisha jaza kwenye nyumba uliyokodi kisha uwe tengeneza network na wauzaji wa dogo uwe unawasambazia bidhaa wanazoishiwa.
Kwa kufanya hivi ndani ya mwaka utakua mbali sana utaoa, utajenga, nk.

Mkuu kama unajua njia zote za kupita ili afanikiwe katika haya unayosema, mpe connection na pa kuanzia. Kwa hali aliyonayo pengine si tatizo la pesa au mawazo bali mtu wa kushika mkono katika hicho kidogo
 
Yaani una smartphone .....

Una laptop


Unaweza kununua bando ...

Harafu unasema maisha yamekuchapa...


Acha kudanganya watu mkuu ,Wewe ni miongoni mwa matajiri hapa Tanzania....

Hujakutana na watu waliopinda...
Hivi huwa mnajisikiaje kumtamkia mtu maneno ya kejeli anapotoa shida zake. Kesho ukisikia kajiua au kajidhuru utaweza kufuta haya maneno yako
 
Maisha ya sasa yamemnyoosha kila mtu, yaani yanapiga mpaka afya ya mwili inatetereka unajikuta unapoteza hadi radha ya kuishi,

Weka aibu pembeni rudi nyumbani, huko Dar utajikuta unakuwa mwizi,

Afadhali kuishi kwenu kwa amani kuliko kukaa huko mbona masela kibao tumerudisha mpira kwa kipa tunajipanga kujilipua tena,

Rudi nyumbani
I beg to differ. Never go back home. I insist, endelea kupambana. Mi mambo yaliniharibikiaga wakati nina familia ya watoto wawili. I lost all friends na hadi ndugu wengine walininanga... Wife hakua na kazi na tuliisha kwa neema ya Mungu tu huku familia yangu ikiwa ndo mfariji wangu pekee, watoto ndo walibaki marafiki zangu wa kunirudishia tabasamu na kusahau kwa muda ninayopitia. Imani yangu kwa Mungu ilisaidia sana na wife alisimama sana kwenye maombi. Nikahama chuga kwenda Dar kuhustle nikaacha familia kwa muda,huko ndo ikawa inapita siku mbili sijala chochote siku ya tatu ndo nakula..ukilala usiku unahisi huna hata nguvu kupump heart beats unaona zinapiga kwa slow motion. Mungu mwema hatimae mapito yakapita na haikua rahisi na haikua muda mfupi. Sembuse wewe single boy utashindwaje? Wenzio tumepitia hiyo hali tukiwa na familia...unapigwa mkwara na landlord hadi anaamua kujisahaulisha miez 8 hujalipa hata mia. Kikubwa muombe Mungu uzima tu...mengine atakubariki ni suala la muda tu. Nilishawahi pia comment kitambo sana kwenye ule uzi wa watu tuliowahi kufilisika.
Na nikuhakikishie kuna ninaowafaham walipitia changamoto zaidi hadi familia kusambaratika kabisa kila mtu na njia yake,wakakomaa hivyohivyo plus maumivu ya family kusambaratika na wakatoboa na ukikutana nao leo hutoamini waliyopitia
 
Mkuu kama unajua njia zote za kupita ili afanikiwe katika haya unayosema, mpe connection na pa kuanzia. Kwa hali aliyonayo pengine si tatizo la pesa au mawazo bali mtu wa kushika mkono katika hicho kidogo
Mafanikio yanaanza na mtu mwenyewe,pili mafanikio ni bahari hayana njia moja.
Tatu kwenye mitandao ndipo kuna majibu yote ya matatizo yote ya mwanadamu maana hadi sasa hakuna tatizo jipya duniani.Yote watu wameyashapitia na kuyatatua.
 
Mafanikio yanaanza na mtu mwenyewe,pili mafanikio ni bahari hayana njia moja.
Tatu kwenye mitandao ndipo kuna majibu yote ya matatizo yote ya mwanadamu maana hadi sasa hakuna tatizo jipya duniani.Yote watu wameyashapitia na kuyatatua.

Usiepuke wajibu wa kumsaidia mtu kama utaweza, mwisho wa siku hakuna aliyeweza kufanikiwa pasipo watu wa kumsaidia katika namna mbali mbali. Ukimsoma kijana kwenye kila mstari kaonesha nia na ari ya kufanya kazi ila kakwama. Anahitaji msaada wa karibu zaidi

Mungu amsaidie pengine kupitia humu atapata mtu sahihi inshaalaah
 
Hahahah dadaq, mwakauta not mwakavuta ( mwakavuta ni shule ). ( Mwakauta ni Kijiji ).

Kule asirudi mamaq ,, Kuna ulanzi kama nini ....hahah

N b ...pambana huko huko uliko ...c hatuna msaada aisee
Nakujua kule kama maji ya kunywa
 
Njia rahisi ya kuondokana na umasikini kwa mtu asiye na kipato.
Ardhi still bado ndio mtaji rahisi wa kutokea kimaisha.
Nje ya mji mapori tele yamejaa hata bure au kukodi unaweza pata safisha angalau si chini ya heka 10,panda mazao yasiyo na changamoto mfano kunde, alizeti, mtama, nk.
Chukua zao moja hili ni uhakika.
Baada ya kusafisha heka 10 au zaidi panda mmea wa nyonyo castro oil huu unavuna baada ya miezi 3 na utaendelea kuvuna kwa mda wa miaka 2.
Heka moja ya nyonyo utapata gunia 15 ukizikamua utapata lita 500 za mafuta, so heka 10 ni lita elf 5.
Jifunze kutengeneza sabuni za mche za mawingu
Lita moja ya mafuta utapata miche 2 mara lita elf 5 utapata miche elf 10.
Uza mche kwa sh 1500 mara elf 10 utapata milioni 15.
Jinsi ya kutengeneza mashine ya kukamua mbegu za mafuta tafuta bomba inchi nne tafuta Nondo mm 12 ikunje mfano wa spring ingiza ndani ya bomba mbele ya bomba ziba acha tundu dogo.Toboa toboa Bomba vitundu vidogo Ili mafuta yamwagike chini, weka mshikio wa kunyongea Ili ukamue mafuta.
Ukipata pesa kodi nyumba nenda viwandani kafunge bidhaa ambazo ni daily use kisha jaza kwenye nyumba uliyokodi kisha uwe tengeneza network na wauzaji wa dogo uwe unawasambazia bidhaa wanazoishiwa.
Kwa kufanya hivi ndani ya mwaka utakua mbali sana utaoa, utajenga, nk.
Samahani mkuu, umeandika au umeandikiwa na mtu hapa?
 
Mleta mada nilichokipenda kwako una spirit ya kazi,huchagui kazi,una Imani na Mungu pamoja na magumu unayopitia bado una muona Mungu Kama hajakusahau Ila bado upo kwenye foleni,unangojea zamu yako...Mungu akukumbuke akukutanishe na watu Sahihi hata kupitia hapa
 
Yaani una smartphone .....

Una laptop


Unaweza kununua bando ...

Harafu unasema maisha yamekuchapa...


Acha kudanganya watu mkuu ,Wewe ni miongoni mwa matajiri hapa Tanzania....

Hujakutana na watu waliopinda...
Ila atleast kafikisha msg, kwa hali yako utaelewa alichosema. Kupitia shida haina maana huna smartphone au laptop. Mambo yakigoma yamegoma.
Issue hapa . Ni mapambano yaendelee mpaka siku hela itapotosha.
Kuna jamaa yangu alikua na smartphone, laptop, cheni ya Gold na pete mbili, na account NMB elfu 30 tu, na ni dalali, anaishi kwao, kula kulala bure. Akipata kidogo anafanya jambo hata nyumbani kwao, maisha yake kama ya jamaa, kila bishara inaisha. Akipata hela kidogo inaisha kwenye matumizi. Akampa mwanamke mimba, kila dili akipiga la udalali ndipo na mwanamke anashida, anatuma hela yote. Muda wa kujifungua umefika madili yamenuna haelewi kitu. Issue haikua kuuza vitu. Ila alipambana, akafanikiwa kuweka kila kitu sawa. Mtoto alizaliwa kwenye neema, arobaini na ubatizo wa kutisha. Jamaa saiv anaishi kwake, gari yake, dada yule na watoto wa wawili wa kike. Na sasa ana cheni kubwa zaidi ya Gold. Na pete kaongeza design nne tofauti. True story.
ISSUE NI KUPAMBANA, HAKUNA KULIA. IPO SIKU.
 
Huwezi fanikiwa lolote bila kwanza kutengeneza ulimwengu wako wa kiroho.
Funga kwa mda wa siku 3 au zaidi.
Unaweza ukafunga kwa masaa 24 kwa kufungua na maji tu, tumia ndimu, maji ya chumvi hai kwa kuoga na kunywa, tumia mmea wa kivumbasi kwa kuogea na kunywa, huku ukifanya toba na kujipatanisha na Mola wako, huku ukinua ukitamka vitu vizuri vije kwako. Hapa kama kuna uchawi au negative energy ulitupiwa zitapotea zote. Ruhusu positive power/energy zije kwako kwa kuzivuta. Saidia masikini mfano ombaomba wape hata shilingi 100 au zaidi kulingana na uwezavyo.
Fanya zoezi la kushukuru ulivyo jaliwa na Mola mfano afya, uzima, nk.
Ndani ya mwezi mmoja utaanza kuona milango ikifunguka.
asante sana mkuu
 
Wengi awajui Siri kubwa ya kufanikiwa katika maisha ipo kwenye kutoa, hii Siri wanaijua weupe. Weusi ni masikini sababu awatoi.
Ukiona umekwama kwenye maisha toa. Kutoa ni ibada ni kitendo cha kuondoa uchafu kwenye mtaro umeziba Ili maji yapite safisha mtaro wako Ili upate maji.
Mafanikio yote ya mwanadamu uanzia kwenye ulimwengu wa roho kukwama means huna connection na positive energy Kati yako na positive energy kuna kizuizi kitoe hicho kizuizi kama ujaona mabaraka yakimwagika kwako huku KILA kitu kikienda. Pili changamoto ndio pesa yenyewe Katu ukipata changamoto usiache na kuanzisha kingine Pambana nazo jifunze kupitia changamoto ukizishinda tu mafanikio ni mteremko.
asante sana mkuu kwa ushauri, binafsi sijisifu lakini najitahidi kutoa kadri ya uwezo wangu sijawahi kuombwa msaada na mtu yeyote nikaacha kumsaidia kama nina uwezo, nitajitahidi sana kuongeza
 
Nusoma uzi huku nikila mchicha na muhogo wa kuchoma


Point kubwa
Unatkiwa kuhakikisha hufi kizembe
kweli mkuu mapambano yanaendelea najua wapo wenye changamoto kunizidi, ninaamini kuna mtu aliyekaribia kukata tamaa kwa kusoma huu uzi atasonga. tutatoboa mungu mwema.
 
I beg to differ. Never go back home. I insist, endelea kupambana. Mi mambo yaliniharibikiaga wakati nina familia ya watoto wawili. I lost all friends na hadi ndugu wengine walininanga... Wife hakua na kazi na tuliisha kwa neema ya Mungu tu huku familia yangu ikiwa ndo mfariji wangu pekee, watoto ndo walibaki marafiki zangu wa kunirudishia tabasamu na kusahau kwa muda ninayopitia. Imani yangu kwa Mungu ilisaidia sana na wife alisimama sana kwenye maombi. Nikahama chuga kwenda Dar kuhustle nikaacha familia kwa muda,huko ndo ikawa inapita siku mbili sijala chochote siku ya tatu ndo nakula..ukilala usiku unahisi huna hata nguvu kupump heart beats unaona zinapiga kwa slow motion. Mungu mwema hatimae mapito yakapita na haikua rahisi na haikua muda mfupi. Sembuse wewe single boy utashindwaje? Wenzio tumepitia hiyo hali tukiwa na familia...unapigwa mkwara na landlord hadi anaamua kujisahaulisha miez 8 hujalipa hata mia. Kikubwa muombe Mungu uzima tu...mengine atakubariki ni suala la muda tu. Nilishawahi pia comment kitambo sana kwenye ule uzi wa watu tuliowahi kufilisika.
Na nikuhakikishie kuna ninaowafaham walipitia changamoto zaidi hadi familia kusambaratika kabisa kila mtu na njia yake,wakakomaa hivyohivyo plus maumivu ya family kusambaratika na wakatoboa na ukikutana nao leo hutoamini waliyopitia
asante mkuu nilishaamua kutorudi nyumbani nakomaa hadi kieleweke as long as Mungu ananipa afya kila siku, ipo siku kila kitu kitakua sawa.
 
Yaani una smartphone .....

Una laptop


Unaweza kununua bando ...

Harafu unasema maisha yamekuchapa...


Acha kudanganya watu mkuu ,Wewe ni miongoni mwa matajiri hapa Tanzania....

Hujakutana na watu waliopinda...
hahaha! mkuu hii laptop yangu hata kwa laki moja hununui imechoka sio kitoto natumia kiswaswadu sio smartphone, angalau napunguza mawazo na kujifunza kupitia hii laptop nzee, Binafsi najiona napunguza mzigo mkubwa sana na kujifunza mengi ninapoingia JF nikipata nafasi. Pia inawezekana nina mtazamo mbaya mimi sio muumini wa kuuza vitu angalau nafarijika kuona vitu vichache nilivyo navyo. what if nikiuza vyote na matatizo yasiishe nitakua nimeongeza tatizo.
 
Ni kawaida kwa watu kutafuta hamasa kutoka kwa waliofanikiwa peke yao kwa sababu tunaamini ndio wanaijua njia sahihi ya mafanikio. Binafsi sijafanikiwa kiwango cha kutoa hamasa hiyo kwa wengine lakini nina Imani kuna mtu aliyekata tamaa kabisa atapata nguvu ya kupambana kwa kujua kuwa hayupo peke yake kwenye haya mapambano Mungu ataleta neema yake siku za mbele asilale, karibu jitahidi kusoma uzi wote.



Binafsi niliamini kuwa kila kitu kitakuwa sawa baada ya kumaliza chuo kwamba nitapata kazi na kila mazuri niliyotamani yatakuja hasa kuiheshimisha familia yangu lakini hali imekua tofauti kila kukicha afadhali ya jana, nimetembeza sana vyeti hadi kuomba kazi ikageuka kazi yenyewe ubaya haina mshahara.

Kila mpango niliojaribu kufanya iwe biashara au wazo lolote hakuna linapofanikiwa mpaka rafiki zangu wakaanza kuniita Utopianist (wakimaanisha mtu mwenye mawazo ya ujamaa ambayo hayatekelezeki). Kila ninachogusa hakiendi ilifika wakati nikashindwa kabisa kulipa koda mwenye nyumba akanitimua kisiasa nikahamia uswahilini napo hakuna chochote kilichofanikiwa.

Niliamua kuweka pembeni fahari ya kuwa nimesoma nikaingia site za ujenzi hakuna chochote pesa haionekani, nimetapeliwa mpaka sikumbuki namdai nani na nani na ilikuwa kiasi gani. Baada ya hapo nikageukia kwenye kufunga scaffold (mabomba ya chuma yanayofungwa kama jukwaa la kufanyia kazi hasa nje kwenye magorofa) nikazoea umbali mrefu kuning`inia kama nyani lakini napo sijafanikiwa chochote nimetapeliwa sana, hadi nikatamani niende kwa mganga niue kabisa (Nimetubu nina Imani Mungu wangu amenisamehe), Lakini wapi hakuna chochote hali imekua ngumu nikasamehe nimerudi kuwalamba miguu walionitapeli mara kibao angalau nipate chochote.

Nilipata kazi ya kufundisha shule za mitaani (education centers) nikaacha mwenyewe baada ya kuona hakuna ninachopata pesa yote ilikuwa inaishia kwenye nauli wakati mwingine hata pesa ya kula nilikosa kabisa plus kuamka saa kumi asubuhi na kulala saa sita kila siku (kwa sababu ya umbali na wingi wa kazi).

Wakati napambana angalau angalau maisha yaende msichana wangu akapata mimba na kutokana na hali yangu akataka kutoa nikamkatalia kabisa nikiamini Mungu ataniona angalau mtoto azaliwe nitamlea hata kama ni kwa shida sikutaka kuua, (hii imeleta ugomvi baina yetu nina miezi mitatu sijawahi hata kumuona nabembeleleza kama namtongoza sasa) bado hajatoa ninaomba Mungu amuondolee hiyo roho ya kuua.

Mambo hayakaa sawa kodi ya chumba ikaisha sina kitu mwenye nyumba akataka kunifukuza kweli nilichanganyikiwa kuna wakati natembea machozi yanatoka yenyewe najizuia kulia hadharani hapa ndipo kiu ya bangi na sigara ilipokuja juu angalau usiku niweze kulala na kuamka na nguvu (nashukuru Mungu amenisaidia nimeacha vyote), kitu pekee ninachoendelea kuamini ni kwamba Mungu hana ubaguzi kila mtu ana zamu yake, ya kwangu itafika nijitahidi niendelee kua hai.

Baada ya kukwama sana niliamua kujilipua na kwenda ferry kutafuta kazi za uvuvi nikiwa sijui chochote wala simjui yeyote nilichohitaji ni kupata pesa ya halali, ukweli hata kuogelea sijui na sijawahi kupanda chombo chochote cha majini Zaidi ya pantone. Mungu alisaidia nikapata nafasi nikakesha baharini siku mbili mfululizo (sikupata hata mia ya faida Zaidi ya samaki wadogo sita nilirudi nikala na ugali). Baada ya hapo nikakosa hata nauli ya kwenda ferry kufanya kazi nitaanza kwenda tena Mungu akijalia uzima.

Nakumbuka sikumwambia mtu yeyote kua naenda kuvua samaki nilichofanya nilichukua kitambulisho changu nikakifunga kwenye nguo ili lolote likitokea watu wanitambue baadae hofu ikazidi nikamwambia dada yangu kwa sharti la kutosema kwa yeyote Mungu ananitunza kila leo kesho itakua njema.

Wakuu siongopi kuna wakati zinakata hadi wiki mbili chakula changu ni ugali mboga ni uji wa chumvi mambo yakikaa sawa ni uji sukari angalau nikiwa site ndio nakula kawaida sitaki kila mtu ajue tabu yangu. Nashukuru Mungu ameweka tabasamu kwenye uso wangu kila wakati si rahisi kujua hadi nikwambie. Mama yangu amekua mgonjwa kwa kazi ngumu hadi alilazwa nilichoweza kusaidia ni kulia tu nilikosa hata mia ya kumtumia, anajikaza anatoka kufanya kazi Mungu mwema anamtunza siku moja apate nafsi ya kula jasho langu ndicho ninachoomba kila siku.

Kuna wakati nawaza kuhusu mwanangu aliyeko tumboni ambaye sijui kama mama yake atabadilisha mawazo au vipi maumivu yanazidi najihisi kuhumiwa sana moyoni nitakuwa baba gani iwapo hiyo mimba ikitolewa ninayeruhusu mwanangu afe kwa sababu nimeshindwa kumudu maisha lakini kesho itafika Mungu ataachilia neema naendelea kuomba tu (kufunga siwezi vidonda vya tumbo vitaniua). Nikiongeza madeni niliyoshindwa kulipa nazidi kuchoka, niuze laptop yangu iliyochoka ambayo sitapata hata laki moja na haitamaliza shida akili inagoma au niifanye mtaji wa biashara naogopa nayo itakufa kama nyingine zilizopita kikubwa uzima tu. Nikifikiria kurudi nyumbani mkoani hali ni ngumu nachanganyikiwa kabisa ni bora niwe mbali nisiione hiyo hali nilijiapiza kufa nikitafuta pesa ya halali siwezi kufanya hila.



Nimejaribu kufupisha wakuu samahani kwa post ndefu Mtafutaji mwenzangu usichoke jipe moyo kazana Mungu hajatutupa wakati wetu utafika usiwaze kutajirika kwa dhuluma afya ndiyo zawadi kubwa kuliko zote Mungu aliyotupa, omba pambana Mungu atasaidia hakuna utajiri wenye Amani kama hautoki kwa Mungu na kama huwezi kuutumia kusaidia ndugu na jamii inayokuzunguka. Kwenye Biblia (nimesahau ilipoandikwa) Yesu alimwambia mtume Petro kuwa kuna wakati shetani atampepeta kama ngano lakini amemuombea ili Imani yake isiyumbishwe atakapokuwa imara awaimarishe wengine.

Kuna siku Mungu atafungua malango ya mbingu mvua itatunyeshea jiitahidi usije ukasahau kuwasadia wahitaji ndio njia pekee ya kurudisha shukrani kwa Mungu.

Inuka songa mbele kesho hatuifahamu kazi yako ni kuamini kuwa Mungu anakuwazia mema siku zote hawezi kukuacha hajakusahau anakujua wewe ni wa kwake na atakupa kwa wakati wake kuwa na uvumilivu. Jitahidi sana kutunza Amani ya moyo wako.

View attachment 2147147
Ingia mafinga hapo kuna viwanda vya wachina kibao kwa siku buku 5...sasa sijui mke wako utamchukuaje....maaana ungekiwa alone atleast ungekuwa na 50ty...ungesonga
 
Ni kawaida kwa watu kutafuta hamasa kutoka kwa waliofanikiwa peke yao kwa sababu tunaamini ndio wanaijua njia sahihi ya mafanikio. Binafsi sijafanikiwa kiwango cha kutoa hamasa hiyo kwa wengine lakini nina Imani kuna mtu aliyekata tamaa kabisa atapata nguvu ya kupambana kwa kujua kuwa hayupo peke yake kwenye haya mapambano Mungu ataleta neema yake siku za mbele asilale, karibu jitahidi kusoma uzi wote.



Binafsi niliamini kuwa kila kitu kitakuwa sawa baada ya kumaliza chuo kwamba nitapata kazi na kila mazuri niliyotamani yatakuja hasa kuiheshimisha familia yangu lakini hali imekua tofauti kila kukicha afadhali ya jana, nimetembeza sana vyeti hadi kuomba kazi ikageuka kazi yenyewe ubaya haina mshahara.

Kila mpango niliojaribu kufanya iwe biashara au wazo lolote hakuna linapofanikiwa mpaka rafiki zangu wakaanza kuniita Utopianist (wakimaanisha mtu mwenye mawazo ya ujamaa ambayo hayatekelezeki). Kila ninachogusa hakiendi ilifika wakati nikashindwa kabisa kulipa koda mwenye nyumba akanitimua kisiasa nikahamia uswahilini napo hakuna chochote kilichofanikiwa.

Niliamua kuweka pembeni fahari ya kuwa nimesoma nikaingia site za ujenzi hakuna chochote pesa haionekani, nimetapeliwa mpaka sikumbuki namdai nani na nani na ilikuwa kiasi gani. Baada ya hapo nikageukia kwenye kufunga scaffold (mabomba ya chuma yanayofungwa kama jukwaa la kufanyia kazi hasa nje kwenye magorofa) nikazoea umbali mrefu kuning`inia kama nyani lakini napo sijafanikiwa chochote nimetapeliwa sana, hadi nikatamani niende kwa mganga niue kabisa (Nimetubu nina Imani Mungu wangu amenisamehe), Lakini wapi hakuna chochote hali imekua ngumu nikasamehe nimerudi kuwalamba miguu walionitapeli mara kibao angalau nipate chochote.

Nilipata kazi ya kufundisha shule za mitaani (education centers) nikaacha mwenyewe baada ya kuona hakuna ninachopata pesa yote ilikuwa inaishia kwenye nauli wakati mwingine hata pesa ya kula nilikosa kabisa plus kuamka saa kumi asubuhi na kulala saa sita kila siku (kwa sababu ya umbali na wingi wa kazi).

Wakati napambana angalau angalau maisha yaende msichana wangu akapata mimba na kutokana na hali yangu akataka kutoa nikamkatalia kabisa nikiamini Mungu ataniona angalau mtoto azaliwe nitamlea hata kama ni kwa shida sikutaka kuua, (hii imeleta ugomvi baina yetu nina miezi mitatu sijawahi hata kumuona nabembeleleza kama namtongoza sasa) bado hajatoa ninaomba Mungu amuondolee hiyo roho ya kuua.

Mambo hayakaa sawa kodi ya chumba ikaisha sina kitu mwenye nyumba akataka kunifukuza kweli nilichanganyikiwa kuna wakati natembea machozi yanatoka yenyewe najizuia kulia hadharani hapa ndipo kiu ya bangi na sigara ilipokuja juu angalau usiku niweze kulala na kuamka na nguvu (nashukuru Mungu amenisaidia nimeacha vyote), kitu pekee ninachoendelea kuamini ni kwamba Mungu hana ubaguzi kila mtu ana zamu yake, ya kwangu itafika nijitahidi niendelee kua hai.

Baada ya kukwama sana niliamua kujilipua na kwenda ferry kutafuta kazi za uvuvi nikiwa sijui chochote wala simjui yeyote nilichohitaji ni kupata pesa ya halali, ukweli hata kuogelea sijui na sijawahi kupanda chombo chochote cha majini Zaidi ya pantone. Mungu alisaidia nikapata nafasi nikakesha baharini siku mbili mfululizo (sikupata hata mia ya faida Zaidi ya samaki wadogo sita nilirudi nikala na ugali). Baada ya hapo nikakosa hata nauli ya kwenda ferry kufanya kazi nitaanza kwenda tena Mungu akijalia uzima.

Nakumbuka sikumwambia mtu yeyote kua naenda kuvua samaki nilichofanya nilichukua kitambulisho changu nikakifunga kwenye nguo ili lolote likitokea watu wanitambue baadae hofu ikazidi nikamwambia dada yangu kwa sharti la kutosema kwa yeyote Mungu ananitunza kila leo kesho itakua njema.

Wakuu siongopi kuna wakati zinakata hadi wiki mbili chakula changu ni ugali mboga ni uji wa chumvi mambo yakikaa sawa ni uji sukari angalau nikiwa site ndio nakula kawaida sitaki kila mtu ajue tabu yangu. Nashukuru Mungu ameweka tabasamu kwenye uso wangu kila wakati si rahisi kujua hadi nikwambie. Mama yangu amekua mgonjwa kwa kazi ngumu hadi alilazwa nilichoweza kusaidia ni kulia tu nilikosa hata mia ya kumtumia, anajikaza anatoka kufanya kazi Mungu mwema anamtunza siku moja apate nafsi ya kula jasho langu ndicho ninachoomba kila siku.

Kuna wakati nawaza kuhusu mwanangu aliyeko tumboni ambaye sijui kama mama yake atabadilisha mawazo au vipi maumivu yanazidi najihisi kuhumiwa sana moyoni nitakuwa baba gani iwapo hiyo mimba ikitolewa ninayeruhusu mwanangu afe kwa sababu nimeshindwa kumudu maisha lakini kesho itafika Mungu ataachilia neema naendelea kuomba tu (kufunga siwezi vidonda vya tumbo vitaniua). Nikiongeza madeni niliyoshindwa kulipa nazidi kuchoka, niuze laptop yangu iliyochoka ambayo sitapata hata laki moja na haitamaliza shida akili inagoma au niifanye mtaji wa biashara naogopa nayo itakufa kama nyingine zilizopita kikubwa uzima tu. Nikifikiria kurudi nyumbani mkoani hali ni ngumu nachanganyikiwa kabisa ni bora niwe mbali nisiione hiyo hali nilijiapiza kufa nikitafuta pesa ya halali siwezi kufanya hila.



Nimejaribu kufupisha wakuu samahani kwa post ndefu Mtafutaji mwenzangu usichoke jipe moyo kazana Mungu hajatutupa wakati wetu utafika usiwaze kutajirika kwa dhuluma afya ndiyo zawadi kubwa kuliko zote Mungu aliyotupa, omba pambana Mungu atasaidia hakuna utajiri wenye Amani kama hautoki kwa Mungu na kama huwezi kuutumia kusaidia ndugu na jamii inayokuzunguka. Kwenye Biblia (nimesahau ilipoandikwa) Yesu alimwambia mtume Petro kuwa kuna wakati shetani atampepeta kama ngano lakini amemuombea ili Imani yake isiyumbishwe atakapokuwa imara awaimarishe wengine.

Kuna siku Mungu atafungua malango ya mbingu mvua itatunyeshea jiitahidi usije ukasahau kuwasadia wahitaji ndio njia pekee ya kurudisha shukrani kwa Mungu.

Inuka songa mbele kesho hatuifahamu kazi yako ni kuamini kuwa Mungu anakuwazia mema siku zote hawezi kukuacha hajakusahau anakujua wewe ni wa kwake na atakupa kwa wakati wake kuwa na uvumilivu. Jitahidi sana kutunza Amani ya moyo wako.

View attachment 2147147
Nakuombea mwamba.
 
Back
Top Bottom