Maisha yangu ya ndoa ni tofauti na nilivyoyatarajia

Maisha yangu ya ndoa ni tofauti na nilivyoyatarajia

Hao viumbe wakitaka hela wanajua ipo tu na kama haipo ni kama watoto utatupiwa lawama zote zilizo chini ya jua
Hao viumbe itoshe tu kusema HATA UNGEMPA NINI; HAWATOSHEKI.
Kwa wale walio ndani ya ndoa watatoa uzoefu wao hapa. Mwanamke kabla ya ndoa utamwona anajiremba, msafi, lugha nzuri na ya sauti ya chini, hakasiriki hovyo i.e. muda wote anapendeza; anamvuto. Mkifunga ndoa tu baada ya ndoa e.g. mwezi mmoja hata pengine mwezi haupiti..utaona: Sauti kubwa, mahitaji na matumizi ya kijinga-jinga e.g. hichi silagi mie, naumwa hapa au pale, naenda kusalimia fulani, nimejiunga vikoba na leo kuna kikao, umeme & maji wanataka malipo yao n.k. Ukimshauri labda aibue na aanzishe kamradi fulani amazing atakuuliza mradi gani?? utasikia unanidharau n.k. ww ni mbishi sana etc. Kwa mantiki hiyo; ndoa ni mapambano na ni mtihani endelevu wa kudumu.
Na cha kushangaza zaidi ni kwamba unatunukiwa cheti hata kabla ya kumaliza kozi.
 
Unapata pressure na msongo wa mawazo kwa ajili ya nini?

Binafsi naona kama unafake life mkuu. Ishi uhalisia wako na mkae chini na mkeo muelekezane muishi lwa kulingana na kipato chenu. Kwa umri wangu wa kuishi ndoani kwa miaka 25 sasa nimejifunza mwanaume ndiye anayeamua ndoa na nyumba yake iwaje.
Kumbe hata nzi akitulia anaweza tengeneza asali ? Leo umetema madini sana mkuu , kongole kwako.
 
Hukuchagua vizuri
Wewe unaishi maisha ya ndoa au umeshaishi na mwanamke/mwanaume kinyumba zaidi ya miezi 6? (Sio wale unaoa jioni asbh. mnaachana hapana. Hiyo sio ndoa).
Hakuna hata mtu mmoja hapa duniani anayeishi maisha ya ndoa atakuambia alichagua vizuri. Kila ndoa ina KASORO zake na CHANGAMOTO zake..
 
Wewe unaishi maisha ya ndoa au umeshaishi na mwanamke/mwanaume kinyumba zaidi ya miezi 6? (Sio wale unaoa jioni asbh. mnaachana hapana. Hiyo sio ndoa).
Hakuna hata mtu mmoja hapa duniani anayeishi maisha ya ndoa atakuambia alichagua vizuri. Kila ndoa ina KASORO zake na CHANGAMOTO zake..
Basi umeangukia pua
 
Umeandik kwa uchache lakn umemanisha Ndoa kwa upana wake na kwa mtazamo wake katika karne hii tunayoishi ,

Hayo tunaptia mengi , mi najiapang kuhamia mkoani , nitahudumia familia nkiwa mbali maan ukiwa karbu shda ukiw mbali shida ila nmeona ukiw mbali bora utarud utavyojisikia na utaondok utapo choka
 
Kabla ya kuoa, nilidhani ndoa ni chanzo cha furaha na baraka. Nilitarajia amani na utulivu, lakini ukweli umekuwa tofauti kabisa. Nimegundua kwamba changamoto za ndoa zinaweza kukuletea presha kubwa, hasa unapokuwa na kipato cha chini.

Kipato kidogo kimekuwa chanzo cha migogoro isiyoisha. Mahitaji ya nyumbani ni mengi, na mara nyingi mapato hayatoshi. Matokeo yake ni msongo wa mawazo, mabishano, na lawama zisizo na kikomo. Nilipokuwa peke yangu, nilikuwa na uwezo wa kujipanga na kufurahia maisha kwa kipato kidogo. Lakini sasa, inaonekana kama haitoshi hata kwa mahitaji ya msingi

Zaidi ya hayo, nilitarajia mke kuja na upendo, ushirikiano, na msaada. Badala yake, nimejikuta kwenye presha ya kukidhi matarajio ambayo ni vigumu kuyafikia kutokana na hali ya uchumi. Wanawake wengi wanatarajia waume zao wawape kila kitu bila kujali hali halisi ya kipato. Hili limeongeza msongo wa mawazo na kunifanya nipoteze amani ya moyo na hata afya yangu imeanza kudorora.

Kabla ya ndoa, nilikuwa na uzito wa kilo 68 na presha yangu ilikuwa 120/80. Sasa, uzito umeshuka hadi kilo 59 na presha imepanda hadi 130/81. Hii yote ni kutokana na presha ya maisha ya ndoa na kutokuwa na amani ya akili.

Nimejifunza kuwa kuoa kwa kutegemea kwamba mwanamke ataleta baraka au neema ni kujidanganya. Badala ya baraka, nimekutana na changamoto na presha zisizo na mwisho. Ni wazi kwamba bila kipato cha kutosha na ushirikiano wa kweli katika ndoa, maisha yanakuwa magumu sana.

Ndoa inahitaji zaidi ya upendo; inahitaji uvumilivu, ushirikiano, na uelewa wa hali halisi ya maisha. Bila haya, ni rahisi kugeuka kuwa chanzo cha laana badala ya baraka.
Ndoa inahitaji pia mwanamke amheshimu mumewe
 
Umeandik kwa uchache lakn umemanisha Ndoa kwa upana wake na kwa mtazamo wake katika karne hii tunayoishi ,

Hayo tunaptia mengi , mi najiapang kuhamia mkoani , nitahudumia familia nkiwa mbali maan ukiwa karbu shda ukiw mbali shida ila nmeona ukiw mbali bora utarud utavyojisikia na utaondok utapo choka
Mkuu; Hauogapi kwamba utakuwa umejisogeza karibu zaidi na upande wa lile kundi la Kataa ndoa?
 
Sawa. Basi, kama yupo aliyefanya vizuri kwenye hilo, wewe utakuwa ni wa kwanza na ni wa kutolea mfano. Otherwise ur a unique person or unmarried dude.
Duniani pair zipo tafuta pair yako utaipata
 
I bet mke wako anavaaa mawigi mda wote, ana shepu na tako, anatumia mkorogo alaf ni much know. Pole sana
 
Kabla ya kuoa, nilidhani ndoa ni chanzo cha furaha na baraka. Nilitarajia amani na utulivu, lakini ukweli umekuwa tofauti kabisa. Nimegundua kwamba changamoto za ndoa zinaweza kukuletea presha kubwa, hasa unapokuwa na kipato cha chini.

Kipato kidogo kimekuwa chanzo cha migogoro isiyoisha. Mahitaji ya nyumbani ni mengi, na mara nyingi mapato hayatoshi. Matokeo yake ni msongo wa mawazo, mabishano, na lawama zisizo na kikomo. Nilipokuwa peke yangu, nilikuwa na uwezo wa kujipanga na kufurahia maisha kwa kipato kidogo. Lakini sasa, inaonekana kama haitoshi hata kwa mahitaji ya msingi

Zaidi ya hayo, nilitarajia mke kuja na upendo, ushirikiano, na msaada. Badala yake, nimejikuta kwenye presha ya kukidhi matarajio ambayo ni vigumu kuyafikia kutokana na hali ya uchumi. Wanawake wengi wanatarajia waume zao wawape kila kitu bila kujali hali halisi ya kipato. Hili limeongeza msongo wa mawazo na kunifanya nipoteze amani ya moyo na hata afya yangu imeanza kudorora.

Kabla ya ndoa, nilikuwa na uzito wa kilo 68 na presha yangu ilikuwa 120/80. Sasa, uzito umeshuka hadi kilo 59 na presha imepanda hadi 130/81. Hii yote ni kutokana na presha ya maisha ya ndoa na kutokuwa na amani ya akili.

Nimejifunza kuwa kuoa kwa kutegemea kwamba mwanamke ataleta baraka au neema ni kujidanganya. Badala ya baraka, nimekutana na changamoto na presha zisizo na mwisho. Ni wazi kwamba bila kipato cha kutosha na ushirikiano wa kweli katika ndoa, maisha yanakuwa magumu sana.

Ndoa inahitaji zaidi ya upendo; inahitaji uvumilivu, ushirikiano, na uelewa wa hali halisi ya maisha. Bila haya, ni rahisi kugeuka kuwa chanzo cha laana badala ya baraka.
Ishi nao kwa akili.
Bado Kuna wanawaqke wema na wacha Mungu.
 
Shida ni kwamba vigezo vya msingi katika kuoa tunaviepuka tunafuata chura la mwanamke. Matokeo yake ndio tunaoa wanawake hawana akili hata ya kujiongoza wao wenyewe achilia mbali kuongoza watoto.
Hapa ndipo penye tatizo,vijana hawazingatii kuoa kwa kuangalia mwanamke ana siha gani wanachoangalia wao amebinuka vipi na akikatiza nae mitaani watu macho yanawatoka?
 
Back
Top Bottom