Pre GE2025 Majaliwa & Kinana washauri CCM itoe Fomu 1 ya Mgombea Urais 2025

Pre GE2025 Majaliwa & Kinana washauri CCM itoe Fomu 1 ya Mgombea Urais 2025

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

ChoiceVariable

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2017
Posts
66,537
Reaction score
75,687
Kwa Mujibu wa Kinana na Majaliwa mwaka 2025 CCM itatoa fomu Moja tuu ya mgombea Urais Kwa sababu ni utamaduni wa ccm mgombea Rais lazima aendelee kuwa mgombea Kwa awamu ya Pili.


My Take
Utaratibu wa fomu Moja alianzisha Mwendazake

=======
Mbunge wa Ruangwa (CCM), Kassim Majaliwa amesema maendeleo yanayofanyika jimboni humo chini ya utawala wa Rais Samia Suluhu Hassan yanawafanya kushawishi vikao vya juu ya chama hicho kutoa fomu moja tu ya Urais ndani ya chama katika Uchaguzi Mkuu 2025.

Majaliwa ambaye pia ni Waziri Mkuu wa Tanzania, amesema hayo leo Jumanne, Januari 2, 2025 kwenye Mkutano Mkuu Maalumu wa CCM wa Wilaya ya Ruangwa uliofanyika Uwanja wa Likangara.

“Na mimi sikosei, mbele ya wajumbe wenzangu hawa kusema kuwa mheshimiwa makamu mwenyekiti, vyovyote itakavyokuwa, tunaomba tushauri kule Kamati Kuu na Halmashauri Kuu tutoe fomu moja tu ya (Rais) Samia Suluhu Hassan mwaka 2025 kama mgombea pekee wa CCM.

Hoja hiyo, imeungwa mkono na Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Abdulrahman Kinana ambaye amesema: “Utamaduni tulionao, Rais anapokuwa kwenye awamu ya kwanza, huwa tunapenda aendelee kwenye awamu inayofuata, kweli sio kweli.” amesema Kinana akitoa mfano kwa kutaja marais waliotangulia kutumia utamaduni huo tangu awamu ya tatu chini ya Hayati Rais Benjamini Mkapa.

Soma zaidi katika tovuti ya Mwananchi
 
Hahahhaha safi sana, kuna watu humu walikua wanapiga kelele sijui the State imeanda mgombea, sijui Samia hawezi chukua fomu, sijui kuna wazee wameshauri jina la mgombea. Hii precedence aliifanya JPM 2020 kwa kufukuza wote waliotaka kugombea 2020 sasa wembe ule ule unatumika kwa sukuma gang wataotaka fomu 2025
 
Hahahhaha safi sana, kuna watu humu walikua wanapiga kelele sijui the State imeanda mgombea, sijui Samia hawezi chukua fomu, sijui kuna wazee wameshauri jina la mgombea. Hii precedence aliifanya JPM 2020 kwa kufukuza wote waliotaka kugombea 2020 sasa wembe ule ule unatumika kwa sukuma gang wataotaka fomu 2025
Rais ndio the State ,hizo zingine ni porojo za kufanya siku iende
 
Ndugu zangu Watanzania,

Nashukuru kuwa viongozi wetu wakubwa ngazi ya Taifa chamani na serikalini wameanza kutambua kiu ya mamilioni ya watanzania waliyo nayo ya vifuani pao ya kuhitaji utumishi wa Rais Samia kwa mhula wa pili.

Mh Kasimu Majaliwa ambaye ni waziri Mkuu wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania amemuomba makamu mwenyekiti wa CCM Taifa Mh Kinana kwenda kuwashawishi wajumbe wa kamati kuu na halmashauri kuu ya CCM Taifa kuchapisha Fomu moja tu ya Urais kwa ajili ya Rais Samia.

Jambo ambalo Mh kinana aliliunga mkono kwa kutambua kazi kubwa iliyofanywa na inayoendelea kufanywa na Mh Rais wetu mpendwa kipenzi cha watanzania mama samia suluhu Hasssan,akasema ni utamaduni wa CCM kumpa muhula wa pili kiongozi anayekuwa amemaliza muhula wake wa kwanza .akasema ameona kila mtu anayesimama kuzungumza anazungumza namna Mh Rais alivyofanya kazi kubwa katika Taifa letu.

Mimi mwashambwa nimewahi kuzungumza humu jukwaani kuwa wanaccm wanapaswa kukata kiu ya watanzania kwa kuwapa chaguo na hitaji lao Ambalo ni Rais Samia. CCM itawakatisha Sana tamaa , kuwavunja moyo na kuwabubujisha sana machozi Watanzania isipowapelekea Rais Samia kama mgombea wake.

Watanzania wanamhitaji Rais Samia.huyo ndio chaguo lako,.ndio chaguo la vijana,akina mama,wazee, bodaboda,waendesha bajaji,wakulima, wafanyabiashara,wanafunzi wa vyuo, watumishi wa umma.n.k.

CCM Haina budi kusikiliza sauti za watu zinazoendelea kupazwa zikimhitaji Rais samia muhula wa pili. Huyo ndiye ambaye atapewa kura za ndio kwa kishindo kitakachoitikisa Tanzania nzima. CCM tuleteeni Rais Samia kukata kiu yetu watanzania.CCM tuleteeni chaguo letu Rais Samia.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Nashukuru kuwa viongozi wetu wakubwa ngazi ya Taifa chamani na serikalini wameanza kutambua kiu ya mamilioni ya watanzania waliyo nayo ya vifuani pao ya kuhitaji utumishi wa Rais Samia kwa mhula wa pili.

Mh Kasimu Majaliwa ambaye ni waziri Mkuu wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania amemuomba makamu mwenyekiti wa CCM Taifa Mh Kinana kwenda kuwashawishi wajumbe wa kamati kuu na halmashauri kuu ya CCM Taifa kuchapisha Fomu moja tu ya Urais kwa ajili ya Rais Samia.

Jambo ambalo Mh kinana aliliunga mkono kwa kutambua kazi kubwa iliyofanywa na inayoendelea kufanywa na Mh Rais wetu mpendwa kipenzi cha watanzania mama samia suluhu Hasssan,akasema ni utamaduni wa CCM kumpa muhula wa pili kiongozi anayekuwa amemaliza muhula wake wa kwanza .akasema ameona kila mtu anayesimama kuzungumza anazungumza namna Mh Rais alivyofanya kazi kubwa katika Taifa letu.

Mimi mwashambwa nimewahi kuzungumza humu jukwaani kuwa wanaccm wanapaswa kukata kiu ya watanzania kwa kuwapa chaguo na hitaji lao Ambalo ni Rais Samia. CCM itawakatisha Sana tamaa , kuwavunja moyo na kuwabubujisha sana machozi Watanzania isipowapelekea Rais Samia kama mgombea wake.

Watanzania wanamhitaji Rais Samia.huyo ndio chaguo lako,.ndio chaguo la vijana,akina mama,wazee, bodaboda,waendesha bajaji,wakulima, wafanyabiashara,wanafunzi wa vyuo, watumishi wa umma.n.k.

CCM Haina budi kusikiliza sauti za watu zinazoendelea kupazwa zikimhitaji Rais samia muhula wa pili. Huyo ndiye ambaye atapewa kura za ndio kwa kishindo kitakachoitikisa Tanzania nzima. CCM tuleteeni Rais Samia kukata kiu yetu watanzania.CCM tuleteeni chaguo letu Rais Samia.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627.
Mods unganisha huu Uzi hapa Majaliwa & Kinana: Washauri CCM itoe Fomu 1 ya Mgombea Urais 2025.
 
Back
Top Bottom