Majambazi 13 wauawa Kibiti, wakutwa na Bunduki 8 pamoja na Pikipiki 2

Majambazi 13 wauawa Kibiti, wakutwa na Bunduki 8 pamoja na Pikipiki 2

Wakumbuke si bule watu hao kufanya ivyo? Waangalie pia upande wapi wa selikali ijitasimini waache kunyanya watu ili kuwepo na usalama wakutosha yangu ni hayo kamanda silo!!

Sent using Jamii Forums mobile app
Wewe inaonekana una kitu unakijua hapa na unaweza kuwa msaada kwa police, Nafurahi unajionea matunda ya huo utaahira mnaokaririshana huko mnapojazana ujinga na mtaendelea kula shaba mpaka kiama.
 
Criminal mind at work,sasa kama kila jambazi/gaidi ni mwendo wa risasi tu,tutapataje intelligence,kamateni mmoja,ahojiwe,ijurikane motive ya matendo wanayofanya nini,?
Je ni ugaidi tu,ni visasi tu,au kuna siasa ndani yake,jeshi inabidi lijipange,nimesikia baadhi ya waliouliwa,walikuwa na mafunzo ya kijeshi,sasa hapa ndio hatari zaidi,hawa wenye mafunzo wapo kibao mtaani,juzi nirikuwa wilaya ya misenyi mkoani Kagera,vijiji vya ndani kabisa,karibu na mpaka was UG,nikakuta,JWTZ,wanatoa mafunzo ya mgambo kwa vijana,kijijini hapo,kati ya vijana watano,unaokutana nao,watatu,wamepigilia kombati za mgambo,wanaishi kijeshi muda wote,kuanzia mavazi,mpaka staili ya kunyoa denge LA wazee,
Sasa hawa vijana,wakiamua kushika mitutu,polisi mtapona?jipangeni wakuu,kutwanga risasi tu,sio suluhisho,mnauwa 11,nyie mnapoteza vijana wenu 8,...no hatari
Hivi unadhani kama wasingekuwa na taarifa za kiitelijensia wangewapata hata hao 13. Naamini hawahitaji msaada wa hao watuhumiwa na ndio maana waliendelea kujibizana kwa risasi hata kuwapoteza. Watu wa intelijensia walishamaliza kazi yao siku nyingi, sasa hivi ni utekelezaji tu. Au ulitaka wawe wanapublish taarifa zao kwa media?
 
Hivi kwenye mapambano inakuwaje hata polisi wasiumi japo kidogo? Mi siamini kupata taarifa za upande mmoja, kwanini kila siku tunasikia vifo? Kwanini huyo aliye wapeleka naye hatukumsikia akikili kuwa haya yanayosemwa ni kweli? Mimi siamini kuchukua ripoti ya upande mmoja, hatuna jeshi la polisi, mnaua watu hovyo na mnajitokeza kujisifia!!! Kamateni waharifu na sio kuwauwa jamani. Mkumbuke hakuna kitu kibaya kumwaga damu ya mtu, damu ikisha mwagika haitatuacha salama. Ikidai haki nani atakuwa tayari kuisimamisha?

Sent using Jamii Forums mobile app
Na wakati mapolice wanauwawa hovyo ulisema hivi?
 
Mtuhumiwa wa tatu(3) huyu anakufa kwa kujeruhiwa kwa risasi alipokuwa ameambatana na polisi kwenda kuwaonyesha walipo wenzao.
Mtuhumiwa mlikuwa naye katika line moja. Yeye anapigwa risasi zaidi ya moja nyie mlio wengi hata mmoja hajajeruhiwa kwa risasi.
Ok. Mbinguni siri zote zitafichuliwa.
Kama ni kweli basi vizuri sana, haiwezekani watu wachache kwa hila zao watake Tanzania iendeshwe kama watakavyo.
 
Mkuu
Ndg zetu polisi wanafanyakazi zao katika mazingira magumu sana.
Ninamaanisha kuwa, wao si jeshi la vita. Lazima watamke maneno kulingana na mipaka na mazingira ya kazi zao kisheria.
Wanaruhusiwa kukamata tu na si kuua.
Wanatakiwa wafanye wawezavyo kukamata, kwa njia yoyote ile na kuhakikisha wanamkamata mhalifu wao akiwa hai, kuua kwao ni mwiko.
Eti kwao kuua ni hukumu itolewayo na mahakama kwa mhalifu aliyehukumiwa.
Nadhani ifike mahali kazi ya polisi isiwekewe siasa.
Polisi kuwekwa kisiasa hutukanishwa sana katika jamii kwa kuonekana waongo.
Polisi si waongo, ila mazingira ya sheria duni zilizopo huwabidi waongee uongo wa kulazimisha.
Mfano huo wa uongo ni hili la watuhumiwa 13 kujeruhiwa na kufa wakipelekwa hisipitali.
Jeshi lolote linapokuwa limeingia katika operesheni ya kivita, huwa hawakurupuki tu.
Hufanya maandalizi ya kina namna watakavyoendesha oparesheni hiyo.
Pamoja na mambo mbalimbali ya kiutawala, huunda Echeloni watakapopelekwa majeruhi na kutibiwa, lazima kuwe na madaktari bingwa wa kuweza kutibu wagonjwa na majeruhi wa pande zote mbili hukohuko kwenye uwanja wa mapambano kabla ya majeruhi hao kusafirishwa.
Lazima waelewe jinsi watakavyohifadhi maiti za wahanga pindi wanaposubiri kusafirisha.
Pia waelewe watakavyowahifadhi mateka wao kwa muda, kabla ya kuwasafirisha location ya jela iliyoteuliwa kuhifadhi aina hiyo ya wafungwa nk nk.
Tujiulize sasa, hivi mtu anaweza kupigwa risasi na kujeruhiwa Kibiti halafu ategemee kupata matibabu hosipitali ya Muhimbili bila kupata kwanza huduma ya kwanza kwa usafiri wa kusuasua na apone?
Ninajua lengo ni kuangamiza na kutokomeza, lakini kuua mateka wote kwa pamoja ni kupoteza fursa ya kupata habari za kina.
Ninajua pia ilivyo starehe adui yako aliyekusumbua kipindi kirefu kufia mikononi mwako ukishuhudia.
Lakini tunasahau kuwa kupata 'zawadi' ya kifo cha harakaharaka bila kukisotea pia ni starehe.
Kumuua mhalifu bila ya kumhangaisha ni kumstarehesha.
Wahalifu aina ya majambazi wa kibiti, ingawa wamekataa kuwapatia "cheo" cha magaidi, wanaoua watu kwa dhana za uonevu na bila hatia, hawastahili kupigwa risasi na kutunukiwa vifo vya starehe.
Walistahili wakamatwe wakiwa hai, waeleze kinagaubaga kwa kulazimishwa ama kwa hiari yao kuwa, ni kwanini wanawatenda ndugu zao Watanzania wasiokuwa na hatia?
Baadaye sasa baada ya kusoteshwa miaka kadhaa, ndiyo wangeliulizwa kila mtu aina ya kifo anachotaka auawe.
Aina yoyote ya kifo ambacho muuaji angelikichagua, angeuziwa kifo hicho na ndugu zake wangelikilipia.
Kwa mfano: kama muuaji angelichagua kuchinjwa, ama risasi ama kamba ya kitanzi, basi vifaa hivyo vya kumuulia vingegharamiwa na ndugu zake ama jamaa zake kwa kulazimishwa kuvinunua, kuepuka kutumia ovyo pesa za walipa kodi.
Hapo jamii ingelipata somo.
Lakini hili la kupigwa risasi za bure na kufa kifo cha starehe halikubaliki.
Mkuu umeongea vizuri sana lakini nadhani hwa jamaa ukiwatubza jela siasa, na mambo ya kidini yataingizwa.
 
Kwanini polisi wa Tz hawatoi picha za wahalifu waliouliwa? [emoji23][emoji23]
Wakisha kupa hiyo picha wewe itakusaidia nini? Unajua kuna vitu vingine hata ukivifikiria tu havina mantiki,

Kama una ndugu yako kapotea kapeleke taarifa police station.
 
Mtuhumiwa wa tatu(3) huyu anakufa kwa kujeruhiwa kwa risasi alipokuwa ameambatana na polisi kwenda kuwaonyesha walipo wenzao.
Mtuhumiwa mlikuwa naye katika line moja. Yeye anapigwa risasi zaidi ya moja nyie mlio wengi hata mmoja hajajeruhiwa kwa risasi.
Ok. Mbibguni siri zote zitafichuliwa.
mkuu hatari sana
 
Tumeomba mtusaidie njia za kukamata mtu anayekurushia risasi, hamtoi, bali mnatoa pvu tu humu. Unakamata vp watu wenye bunduki 8? Zabaf
ushahidi upo wapi wa kuthibitisha walikuwa wanawarushia risasi polisi?kitendo cha kuuwa watuhumiwa 13 sio cha wewe kukifurahia ,ni kitendo kinachoonyesha jeshi lako la polisi linazidi kuwa katiri na halina intelligence ya ti infiltrate mtandao huu wa ugaidi,polisi wanamafunzo waliyopewa ya kukabiliana na watumia silaha za moto,why hawakuita back up ili isaidie?,sasa umeua watu 13 ambao mimi na wewe hatuna hard evidence ya kuthibitisha ugaidi wao,na kwako ni furaha kubwa,we need a police watakao kuwa wanatekeleza kiapo cha kulinda raia,wanalazimika kutumia nguvu once maisha yao yanapokuwa hatarini na maisha ya raia wengine,waulize watuonyeshe picha za wahalifu waliouawa,kumbuka uvamizi wa msikiti pale Lindi recently je tumepewa taarifa rasmi kutoka polisi?
 
Mtuhumiwa wa tatu(3) huyu anakufa kwa kujeruhiwa kwa risasi alipokuwa ameambatana na polisi kwenda kuwaonyesha walipo wenzao.
Mtuhumiwa mlikuwa naye katika line moja. Yeye anapigwa risasi zaidi ya moja nyie mlio wengi hata mmoja hajajeruhiwa kwa risasi.
Ok. Mbibguni siri zote zitafichuliwa.
Police huwa wamevaa bulletproof na strong preventive gears pamoja na silaha za kujihami, jiulize huyo mtuhumiwa alikua equipped?

Mara nyingi mmoja wao akishaonesha wenzake nae huuwawa sababu kazi yake imeisha
 
Police huwa wamevaa bulletproof na strong preventive gears pamoja na silaha za kujihami, jiulize huyo mtuhumiwa alikua equipped?

Mara nyingi mmoja wao akishaonesha wenzake nae huuwawa sababu kazi yake imeisha
Umewahi pitia mafunzo yoyote ya kijeshi ndugu?
Polisi hawavai bullet proof.
 
Hii operation ya Kibiti niliwahi kusema wakimpeleka mafele watamaliza tatizo na kweli mtauona moto,mtu anasema waliouwawa in wa upande mmoja Je mbona wao walikuwa wanawaua wa upande mmoja awakulalamika? Ili kumaliza tatizo no yyte atakayekutwa na silaha au akagundulika in mfadhili wa hayo magenge dawa in kifo tuu maana tumechoka

Sent using Jamii Forums mobile app
Sare za kombati kuna mtu kakamatwa kwa kuwa nazo rukuki!!
 
Hell no. .that shouldn't be the way!
Washukiwa hawatakiwi kuuwawa hata kidogo.....

Kazi ya police ni ku enforce law and order na sio judgement......

Tukiwaachia police uhuru huo... Tumekwisha.

Hili ni kwa Usalama wetu sote, Hakuna Chama Wala Ushabiki kwenye mambo kama haya......
Swahiba mie nakuunga mkono kwenye hilo ila tatizo kubwa hawa washtakiwa wengi wakikamatwa wakiwa hai unakutana nao uraiani na wengine hujitamba mfano halisi mie kaka yangu alinyongwa na majambazi wakampora gari kwa bahati nzuri walimtupa kimara suka wakijua wameua lakini alizimia tu na kabla ya tukio alimtambua mmoja wa abiria wake ambae aliingia kwenye gari yake kama teksi ilipita miaka akamuona kariakoo mmoja wa mtu aliemfanyia tukio lile akakamatwa mpaka Central alivyoingia nae pale Central askari wote walikuwa wanamjua mtu yule dili zake ni wizi wa magari na akaachiwa ilhali kaka yangu hadi leo anazo alama za mnyororo shingoni hadi leo kwa hiyo bora wapotezwe tu wapungue.
 
Hiki ni kiinimacho tu. Wanauhadaa uma jeshi lionekane linafanya kazi inayostahili. Kazi ya polisi sio kuua, na ikitokea wameua haitakiwi kudanganya walijeruhiwa wakafa baadae. Si rahisi kujeruhi watu 13 na wote 13 wakafa ndani ya saa chache.
Habari zingine wanatangaza lakini hazistahili kutangaziwa umma. Ni habari za intelijensia ya jeshi na zinabaki jeshini. Ni maadili gani ya kazi ya jeshi unatangaza hadi sehemu silaha ilipoibiwa na ilipotumika katika uhalifu? Ni sawa kwa jeshi kuhitimisha kuwa waliouawa walikuwa majambazi na/au wahalifu? Hii ni kazi ya mahakama, hata kama polisi inahisi hivyo hao wanabaki kuwa watuhumiwa tu. Ni mahakama pekee ndiyo ingehitimisha kuwa hawa jamaa ni wahalifu.
Jeshi la polisi linahadaa sana umma kwa kuuaminisha watu fulani ni wahalifu. Tena mbaya zaidi linataja na majina ya wengine ambao hawajakamatwa! Ni intelijensia ya wapi hii?
Ni wakati muafaka kitengo cha intelijensia cha jeshi la polisi kiangaliwe upya. Inawezekana hawatambui miiko ya kazi yao au kuna watu wanaingilia kazi isiyo yao, kazi inayotakiwa kufanywa na kitengo cha intelijensia cha jeshi.
kwa mtindo huu ni rahisi sana kwa siri za jeshi kuvuja, na ni moja ya sabau ya kukomaa kwa uhalifu nchini.
Unachokiandika hapa nasoma kitu kingine ndani yako
Ni wazi pia kuwa hii taarifa si nzuri kwako

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom