Majambazi 13 wauawa Kibiti, wakutwa na Bunduki 8 pamoja na Pikipiki 2

Majambazi 13 wauawa Kibiti, wakutwa na Bunduki 8 pamoja na Pikipiki 2

Mkuu umeiweka vibaya hoja yako, hawakuuwawa badi kulikuwa na majibizano ya risasi kati ya polisi na hao jamaa in the process ndipo wakufa ni criminal action.
Kuuwawa kwa maana uliyomaanisha ni kwamba walikamatwa, badala ya kuwafikisha kwenye usalawa kaliuliwa, kitu ambacho si sahihi.
Naomba majeruhi japo mmoja tu upande wa pili kama yupo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hell no. .that shouldn't be the way!
Washukiwa hawatakiwi kuuwawa hata kidogo.....

Kazi ya police ni ku enforce law and order na sio judgement......

Tukiwaachia police uhuru huo... Tumekwisha.

Hili ni kwa Usalama wetu sote, Hakuna Chama Wala Ushabiki kwenye mambo kama haya......
Kama hao majambazi wamekufa kwenye mapambano nadhani ni sawa, maana vita ni vita, pande zote mbili zinazopigana zinatumia risasi ambapo yeyote itakayempata awe polisi au jambazi kuna uwezekano huo wa kufa. Na ni sahihi kuwa anayekufa hapo ni jambazi na siyo polisi wetu, maana polisi wetu wana mafunzo ya kazi hiyo na wana wajibu wa kuonyesha uwezo wao. Lakini lipo jambo linalonitatiza sana. Inakuwaje hata yule mtuhumiwa waliyemkamata kabla ya mapambano akiwa hana silaha, tena akiwa alishajeruhiwa siku nyingi, naye ameingia katika mkumbo huo wa waliouawa? Mtuhumiwa aliyeko mikononi mwa polisi tayari amewezaje kurudi upande wa majambazi katika mpambano hadi naye akaishia kuuawa? Hapo kuna walakini, na hii inaweza kusababisha tukafikiri kuwa hapakuwako mapambano tunayoambiwa, labda walikamatwa wazima katika 'chimbo' lao hilo, na polisi wakaamua kumaliziapo hasira zao na visasi vya kuuawa wenzao.
 
Alafu wakienda kuwaonyesha walipo wenzao polisi wanawaua na hao watoataarifa! Hiyo imekaaje?!

Kwanini mara zote polisi wakienda na mtoa taarifa/shahidi ambaye wanamshikilia tayari kuwaonyesha walipo wengine, wakifika naye huko porini wanamuua?! Kwanini?!
Anakuwa ameshamaliza kazi yake, so naye shaba tu. Atapatikana mpya kwenye majibizano mapya kama naye alivyopatikana katika majibizano yaliyotangulia.
 
Kama hao majambazi wamekufa kwenye mapambano nadhani ni sawa, maana vita ni vita, pande zote mbili zinazopigana zinatumia risasi ambapo yeyote itakayempata awe polisi au jambazi kuna uwezekano huo wa kufa. Na ni sahihi kuwa anayekufa hapo ni jambazi na siyo polisi wetu, maana polisi wetu wana mafunzo ya kazi hiyo na wana wajibu wa kuonyesha uwezo wao. Lakini lipo jambo linalonitatiza sana. Inakuwaje hata yule mtuhumiwa waliyemkamata kabla ya mapambano akiwa hana silaha, tena akiwa alishajeruhiwa siku nyingi, naye ameingia katika mkumbo huo wa waliouawa? Mtuhumiwa aliyeko mikononi mwa polisi tayari amewezaje kurudi upande wa majambazi katika mpambano hadi naye akaishia kuuawa? Hapo kuna walakini, na hii inaweza kusababisha tukafikiri kuwa hapakuwako mapambano tunayoambiwa, labda walikamatwa wazima katika 'chimbo' lao hilo, na polisi wakaamua kumaliziapo hasira zao na visasi vya kuuawa wenzao.
Ndugu, kesi nyingine ni bora kupoteza tu ushahidi. Hawa watu ukiwapeleka kizimbani watatoka tu halafu watakuja kusumbua tena uraiani, tena kwa kulipiza visasi kwa watoa taarifa (informants). Acha dola ifanye kazi yake. Vitu vingine ni vya ndani sana kiusalama, hatuwezi kupewa kila taarifa, tupende tusipende
 
Hongera Jeshi la Polisi, tuna imani kubwa na nyinyi.

Raia asiye na hatia, anavamiwa usiku na watu wenye silaha, anatolewa nje na kuchinjwa kama kuku, au anapigwa risasi hadi kifo, ukatili huu hauvumiliki kamwe.

Watu hao hawastahili kitu chochote, nasema tena hawastahili jambo lolote zaidi ya kuuwawa popote wanapoonekana.

Hao sio binadamu, na hawatakuwa binadamu kamwe, na hawatakiwi kushughurikiwa kama binadamu.

Wanaiga tabia za kigaidi, au ni magaidi kabisa.

Msiwatetee wala kuwachekea hao, ni makatili kupita kiasi, na kamwe hawaachi vitendo vyao viovu.

Chonde chonde jeshi la Polisi, mkishajirithisha kuwa ni wao, wapigeni risasi maramoja popote mnapowaona.

Asante jeshi la Polisi

Asante Kamanda Simon Siro

Mapambano ndo kwanza yameanza.
Wako wengi bado wazima.
Hawastahili kuwa hai.
 
Sema nao hata hawaelewekagii silaaa za staki shari siwalisema walizikama zote zikiwa zimefukiwa? Na jee wale majambazi waliokuwa wanauwawaa wanatwambia niwale waliouwa askar walikuwa hajaisha au ni wapya?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yan tunavyopenda makamera na malikes tuwauwe tusiwaonyeshee? Wale wamwanza waliuwawa tukaonyeshwa silaha zao na miili ilivyo zagaaa . huku kibiti huwa ni saund kila siku na upo uwezekano ni matukio yakutengenezaa ili waonekane wanafanya kazi kama kawaida yao. Kutaja majina sio shida inawezekana ni watu wanawatafuta wameshindwa kuwapata wanatumia gia hiyo ukijichanganya kwenda kumwangalia ndugu yako umeishaa wewe ndo ukamuonyeshe unae mtafuta. Toka matukio yameanza majambazi wanavamia na bunduki za mabomu ya machozi toka lini? Hiiii michezo yakimama sanaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanapeleka watu kule na kuwapiga risasi na kuwawekea bunduki na silaha halafu wanajitekenya kuwa tumeua majambazi kibiti. Ndio tatizo la afrima uongo mwingi kwa kuogopa kufukuzwa kazi. Kwani unafukuzwa kazi pasipo hata kuchunguza kosa. Hakuna majambazi ambao tunaambiwa ni waliobobea na wamepata mafunzo nje leo hii wakae pmj. Watu wanapelekwa kibiti wanauwawa then polisi wanasingizia majambazi wa kibiti. Tusubiri muda utasema ndio polisi tanzania

Kwa nini wasikupeleke kukupiga risasi wewe mchonga ngenga?
 
Picha ni kitu muhimu sana usijifanye huelewi labda tukiona picha tunaweza kuwatambua na kujua marafiki zao wengine tukatoa msaada kwenye vyombo vya ulinzi kwani hizo picha za bunduki na mabomu zinatudaidia nini
Nenda mortuary
 
Afu Naona Humu Watu Wapimwe Akili Zao Kwanza
Yaani Jambazi Anafyatua Risasi Na bado Unashinikiza Polisi Wangewanasa wakiwa hai.
Naona Kupimwa Mikojo Watu Kumefika sasa😀😀😀😀😀😀😀
 
Afu Naona Humu Watu Wapimwe Akili Zao Kwanza
Yaani Jambazi Anafyatua Risasi Na bado Unashinikiza Polisi Wangewanasa wakiwa hai.
Naona Kupimwa Mikojo Watu Kumefika sasa😀😀😀😀😀😀😀

Risasi za majambazi za MCHANGA au maanake hata POLISI aliyejeruhiwa hakuna
 
Watu 13 wanaodaiwa kuwa wahalifu wameuawa na Askari wa Jeshi la Polisi. Watu hao wamekutwa na Bunduki nane, Pikipiki mbili pamoja na Begi moja la nguo.

Tukio hilo limetokea katika maeneo ya Tangibovu Kijiji cha Milaweni, huko Kibiti Mkoani Pwani.
View attachment 562464 View attachment 562465
View attachment 562467
View attachment 562466
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro akipata maelezo kutoka kwa Mkuu wa Operesheni Maalumu za Jeshi la Polisi, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Liberatus Sabas kuhusiana na tukio la kuuawa wahalifu 13 katika majibizano ya risasi baina ya Polisi na wahalifu hao katika eneo la Tangibovu, Kijiji cha Miwaleni Kata ya Mchukwi, Tarafaya Kibiti.Chini ni silaha 8 aina ya SMG pamoja na vifaa vingine zilizopatikana katika majibizano hayo.
Chanzo: Jeshi la Polisi Tanzania(Ukurasa wa Twitter)
--------------

UPDATES..

Orodha ya Majina ya wahalifu 7 kati ya 13 waliouawa leo na Jeshi la Polisi eneo la Tangibovu ktk Wilaya ya Kibiti mkoani Pwani
1be4dcb1030cefec4c7b5919ad64b788.jpg

Tarehe 09.08.2017 majira ya saa 21:00 Hrs (saa tatu usiku) katika mapori ya kijiji cha Rungungu mtuhumiwa akiambatana na Askari Polisi alikwenda kuonyesha Ngome ya watuhumiwa wenzake aliokuwa anashirikiana nao kufanya uhalifu.

Baada ya kukaribia eneo la tukio ulitokea upinzani mkali wa majibizano ya risasi jambo lililopelekea hata Abdallah Abdallah Mbindimbi @Abajani kujeruhiwa na risasi sehemu mbalimbali za mwili wake.

Kufuatia majibizano hayo, Askari Polisi walifanikiwa kuwajeruhi wahalifu 12 (kumi na mbili. Jitihada zilifanyika kuwapeleka Hospitali majeruhi wote 13 (kumi na tatu) ingawa baadae walifariki dunia kwa nyakati tofauti wakipelekwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kutokana na kuvuja damu nyingi zilizosababishwa na majereha ya risasi sehemu mbalimbali za miili yao. Miili ya marehemu imehifadhiwa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Jijini Dar es salaam.

Ndugu Wanahabari
Watuhumiwa 7 (Saba) kati ya 13 (kumi na tatu) waliopoteza maisha kutokana na majibizano ya risasi wametambuliwa kuwa ni:

1. Hassani Ali Njame
2. Abdallah Abdallah Mbindimbi @ Abajani
3. Saidi Abdallah Kilindo
4. Abdulshakuru Mohamed Ubuguyu
5. Issa Mohamed Mseketu mtawa
6. Rajabu Thomas roja
7. Mohamed Ally Kadude @Upolo
Miili 6 (sita) iliyobaki haikuweza kutambulika mara moja hivyo utambuzi utaendelea huko ilikohifadhiwa Hospitalini DSM.

Ndugu Wanahabari
Vielelezo mbalimbali vilipatikana katika eneo la tukio, kama ifuatavyo:
S/N
KIELELEZO
UTAMBUZI
SILAHA, RISASI NA MABOMU
1.
SMG = 5
Mali ya Jeshi la Polisi tukio la kupora Silaha Askari huko Mtengeni – Jaribu Mpakani

2.
Anti Riot Gun 38mm = 2
Mali ya Jeshi la Polisi tukio la kupora Silaha Askari huko Mtengeni – Jaribu Mpakani

3.
SAR = 1
Mali ya Jeshi la Polisi tukio la kupora Silaha Askari Polisi huko Stakishari Jijini Dar es Salaam

4.
MAGAZINI = 2
Mali ya Jeshi la Polisi tukio la kupora Silaha Askari huko Mtengeni – Jaribu Mpakani

5.
Risasi za SMG 158
Mali ya Jeshi la Polisi tukio la kupora Silaha Askari huko Mtengeni – Jaribu Mpakani

6.
Bomu la kurusha kwa mkono = 1
Uchunguzi dhidi ya Bomu hilo unaendelea

7.
Mabomu ya kutuliza ghasia = 4
Mali ya Jeshi la Polisi tukio la kupora Silaha Askari huko Mtengeni – Jaribu Mpakani

VIELELEZO VINGINE

8.
Pikipiki = 2
Pikipiki hizi zilitumika kuwasafirisha wahalifu hawa kwenye utekelezaji wa matukio ya uhalifu maeneo mbalimbali

9.
Vitenge na Nguo mbalimbali
Vitenge na nguo mbalimbali viliporwa baada ya kufanya tukio la kumuua Diwani wa Zamani wa Kibwiwi

10.
Begi = 1
Liliporwa baada ya kumuua Mtendaji wa Kijiji cha Mangwe

Ndugu Wanahabari
Kwa mujibu wa taarifa za utambuzi wa vielelezo vilivyopatikana eneo la tukio na utambuzi wa baadhi ya miili ya watuhumiwa waliofariki inaonyesha kuwa walishiriki matukio ya uhalifu maeneo mbalimbali kama ifuatavyo:
1. Kuua OC CID na Watumishi 2 (Wawili) wa Idara ya Maliasili katika tukio la Jaribu Mpakani – Wilaya Kibiti
2. Kuua Askari Polisi 8 (Nane) katika tukio la Mkengeni – Wilayani Kibiti
3. Kuua Trafiki 2 (Wawili) katika tukio la Bungu “B” – Wilaya ya Kibiti
4. Kumuua Diwani wa Zamani CCM katika tukio la Kibwibwi – Wilaya ya Kibiti
5. Kuua Afisa Mtendaji, Mwenyekiti wa Mtaa na Mkulima katika tukio la Kijiji cha Mangwi – Wilaya ya Kibiti

Ndugu Wanahabari
Wito wangu kwa Wananchi ni kuhusu mambo muhimu yafuatayo:

a. Wananchi wote nchini kuondoa hofu ya kwamba eneo hili si salama. Nawaomba wananchi waendelee kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi na kwa kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha nawaomba wananchi kutoa taarifa mara moja kwa Jeshi la Polisi wanapohisi kuna jambo lolote wanalolitilia mashaka.

b. Natoa wito kwa wananchi wa mkoa wa Pwani, hususani maeneo ya Mkuranga, Kibiti na Ikwiriri, kuendelea na shughuli zao mbalimbali za kujiletea maendeleo. Nawasihi kwa dhati kabisa waendelee kutupatia taarifa zitakazosaidia kumaliza kabisa uhalifu kwenye eneo hili. Nitumie fursa hii kuwashukuru sana wananchi wa maeneo ya Mkuranga, Kibiti na Ikwiriri kwa ushirikiano mnaotupatia ambao umesaidia sana kuwadhibiti wahalifu.

c. Mamlaka za Hospitali, Zahanati, Vituo vya Afya, Maabara za Afya ya Binadamu na Maduka ya Kuuza Dawa za kutibu Binadamu zijiepushe na utaratibu wa kutoa matibabu kienyeji au kificho kwa watu waliojeruhiwa bila kufuata taratibu za kisheria ikiwemo kupata taarifa ya Polisi “kupitia Fomu maalum ya kuruhusu matibabu (maarufu kama PF. 3)”. Wahalifu wakijeruhiwa ni lazima watafute matibabu.

Kwa hiyo idara hizi ni muhimu sana kutoa ushirikiano ili kutuwezesha kuwakamata watuhumiwa maana baadhi yao wamekutwa na majeraha sehemu mbalimbali za miili yao na walikuwa wanaendelea kujitibia kwa kificho kwa kutumia dawa za hospitali.

Natoa wito kwa Mamlaka hizo kutoa taarifa mara moja kwa Jeshi la Polisi wanapoona ama kumbaini mtu ambaye ataonekana kuwa na majeraha na anatafuta tiba bila ya kufuata taratibu.

Ndugu Wanahabari
Napenda kuujulisha Umma kwamba wapo baadhi ya Watuhumiwa, Wafadhili na Washirika wa Uhalifu na Wahalifu wa ujambazi maeneo haya ambao bado hawajakamatwa. Jambo la kufurahisha ni kwamba taarifa zao zipo kwa Jeshi la Polisi nchini na zinaendelea kufanyiwa kazi ili waweze kukamatwa na kufikishwa kwenye mkono wa Sheria mara moja.

Natoa wito kwa wananchi ambao wanawafahamu watuhumiwa wafuatao kutoa taarifa katika kituo chochote cha Polisi ili waweze kukamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria.

Picha za watuhumiwa hao zitasambazwa kote nchini ili iwe rahisi kuwabaini. Majina ya watuhumiwa hao ni:
i.Anafi Rashid Kapelo @ Abuu Mariam
ii. Hassan Haruna Kyakalewa @ Abuu Salma @ Shujaa @ Dokta
iii. Haji Ulatule
iv. Shekhe Hassan Nasri Mzuzuri
v. Rashid Mtutula

Ndugu Wanahabari
Nimalizie kwa kusema kwamba uhalifu kwenye eneo hili ni suala la muda mfupi. Na tunaendelea vizuri sana. Hali ya usalama imeimarika sana eneo hili. Nazidi kutoa wito kwa wananchi kuendelea kuliunga mkono Jeshi la Polisi ili kufikia malengo yake ya kuzuia, kubambana na kutanzua uhalifu nchini.



Imetolewa na;

Simon Nyakoro Sirro
Inspekta Jenerali wa Polisi
IKWIRIRI
10.08.2017
Hapa ninachoshangaa ni kwamba wakti askari walipouliwa walionyesha miili yao. Hasa hawa 13 mbona hatuonyeshwi? Halafu tunaonyeshwa tu vifaa? Mkubali mkatae Jeshi letu la polisi lina ombwe na usanii mwingi sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wahub
Watu 13 wanaodaiwa kuwa wahalifu wameuawa na Askari wa Jeshi la Polisi. Watu hao wamekutwa na Bunduki nane, Pikipiki mbili pamoja na Begi moja la nguo.

Tukio hilo limetokea katika maeneo ya Tangibovu Kijiji cha Milaweni, huko Kibiti Mkoani Pwani.
View attachment 562464 View attachment 562465
View attachment 562467
View attachment 562466
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro akipata maelezo kutoka kwa Mkuu wa Operesheni Maalumu za Jeshi la Polisi, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Liberatus Sabas kuhusiana na tukio la kuuawa wahalifu 13 katika majibizano ya risasi baina ya Polisi na wahalifu hao katika eneo la Tangibovu, Kijiji cha Miwaleni Kata ya Mchukwi, Tarafaya Kibiti.Chini ni silaha 8 aina ya SMG pamoja na vifaa vingine zilizopatikana katika majibizano hayo.
Chanzo: Jeshi la Polisi Tanzania(Ukurasa wa Twitter)
--------------

UPDATES..

Orodha ya Majina ya wahalifu 7 kati ya 13 waliouawa leo na Jeshi la Polisi eneo la Tangibovu ktk Wilaya ya Kibiti mkoani Pwani
1be4dcb1030cefec4c7b5919ad64b788.jpg

Tarehe 09.08.2017 majira ya saa 21:00 Hrs (saa tatu usiku) katika mapori ya kijiji cha Rungungu mtuhumiwa akiambatana na Askari Polisi alikwenda kuonyesha Ngome ya watuhumiwa wenzake aliokuwa anashirikiana nao kufanya uhalifu.

Baada ya kukaribia eneo la tukio ulitokea upinzani mkali wa majibizano ya risasi jambo lililopelekea hata Abdallah Abdallah Mbindimbi @Abajani kujeruhiwa na risasi sehemu mbalimbali za mwili wake.

Kufuatia majibizano hayo, Askari Polisi walifanikiwa kuwajeruhi wahalifu 12 (kumi na mbili. Jitihada zilifanyika kuwapeleka Hospitali majeruhi wote 13 (kumi na tatu) ingawa baadae walifariki dunia kwa nyakati tofauti wakipelekwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kutokana na kuvuja damu nyingi zilizosababishwa na majereha ya risasi sehemu mbalimbali za miili yao. Miili ya marehemu imehifadhiwa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Jijini Dar es salaam.

Ndugu Wanahabari
Watuhumiwa 7 (Saba) kati ya 13 (kumi na tatu) waliopoteza maisha kutokana na majibizano ya risasi wametambuliwa kuwa ni:

1. Hassani Ali Njame
2. Abdallah Abdallah Mbindimbi @ Abajani
3. Saidi Abdallah Kilindo
4. Abdulshakuru Mohamed Ubuguyu
5. Issa Mohamed Mseketu mtawa
6. Rajabu Thomas roja
7. Mohamed Ally Kadude @Upolo
Miili 6 (sita) iliyobaki haikuweza kutambulika mara moja hivyo utambuzi utaendelea huko ilikohifadhiwa Hospitalini DSM.

Ndugu Wanahabari
Vielelezo mbalimbali vilipatikana katika eneo la tukio, kama ifuatavyo:
S/N
KIELELEZO
UTAMBUZI
SILAHA, RISASI NA MABOMU
1.
SMG = 5
Mali ya Jeshi la Polisi tukio la kupora Silaha Askari huko Mtengeni – Jaribu Mpakani

2.
Anti Riot Gun 38mm = 2
Mali ya Jeshi la Polisi tukio la kupora Silaha Askari huko Mtengeni – Jaribu Mpakani

3.
SAR = 1
Mali ya Jeshi la Polisi tukio la kupora Silaha Askari Polisi huko Stakishari Jijini Dar es Salaam

4.
MAGAZINI = 2
Mali ya Jeshi la Polisi tukio la kupora Silaha Askari huko Mtengeni – Jaribu Mpakani

5.
Risasi za SMG 158
Mali ya Jeshi la Polisi tukio la kupora Silaha Askari huko Mtengeni – Jaribu Mpakani

6.
Bomu la kurusha kwa mkono = 1
Uchunguzi dhidi ya Bomu hilo unaendelea

7.
Mabomu ya kutuliza ghasia = 4
Mali ya Jeshi la Polisi tukio la kupora Silaha Askari huko Mtengeni – Jaribu Mpakani

VIELELEZO VINGINE

8.
Pikipiki = 2
Pikipiki hizi zilitumika kuwasafirisha wahalifu hawa kwenye utekelezaji wa matukio ya uhalifu maeneo mbalimbali

9.
Vitenge na Nguo mbalimbali
Vitenge na nguo mbalimbali viliporwa baada ya kufanya tukio la kumuua Diwani wa Zamani wa Kibwiwi

10.
Begi = 1
Liliporwa baada ya kumuua Mtendaji wa Kijiji cha Mangwe

Ndugu Wanahabari
Kwa mujibu wa taarifa za utambuzi wa vielelezo vilivyopatikana eneo la tukio na utambuzi wa baadhi ya miili ya watuhumiwa waliofariki inaonyesha kuwa walishiriki matukio ya uhalifu maeneo mbalimbali kama ifuatavyo:
1. Kuua OC CID na Watumishi 2 (Wawili) wa Idara ya Maliasili katika tukio la Jaribu Mpakani – Wilaya Kibiti
2. Kuua Askari Polisi 8 (Nane) katika tukio la Mkengeni – Wilayani Kibiti
3. Kuua Trafiki 2 (Wawili) katika tukio la Bungu “B” – Wilaya ya Kibiti
4. Kumuua Diwani wa Zamani CCM katika tukio la Kibwibwi – Wilaya ya Kibiti
5. Kuua Afisa Mtendaji, Mwenyekiti wa Mtaa na Mkulima katika tukio la Kijiji cha Mangwi – Wilaya ya Kibiti

Ndugu Wanahabari
Wito wangu kwa Wananchi ni kuhusu mambo muhimu yafuatayo:

a. Wananchi wote nchini kuondoa hofu ya kwamba eneo hili si salama. Nawaomba wananchi waendelee kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi na kwa kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu. Aidha nawaomba wananchi kutoa taarifa mara moja kwa Jeshi la Polisi wanapohisi kuna jambo lolote wanalolitilia mashaka.

b. Natoa wito kwa wananchi wa mkoa wa Pwani, hususani maeneo ya Mkuranga, Kibiti na Ikwiriri, kuendelea na shughuli zao mbalimbali za kujiletea maendeleo. Nawasihi kwa dhati kabisa waendelee kutupatia taarifa zitakazosaidia kumaliza kabisa uhalifu kwenye eneo hili. Nitumie fursa hii kuwashukuru sana wananchi wa maeneo ya Mkuranga, Kibiti na Ikwiriri kwa ushirikiano mnaotupatia ambao umesaidia sana kuwadhibiti wahalifu.

c. Mamlaka za Hospitali, Zahanati, Vituo vya Afya, Maabara za Afya ya Binadamu na Maduka ya Kuuza Dawa za kutibu Binadamu zijiepushe na utaratibu wa kutoa matibabu kienyeji au kificho kwa watu waliojeruhiwa bila kufuata taratibu za kisheria ikiwemo kupata taarifa ya Polisi “kupitia Fomu maalum ya kuruhusu matibabu (maarufu kama PF. 3)”. Wahalifu wakijeruhiwa ni lazima watafute matibabu.

Kwa hiyo idara hizi ni muhimu sana kutoa ushirikiano ili kutuwezesha kuwakamata watuhumiwa maana baadhi yao wamekutwa na majeraha sehemu mbalimbali za miili yao na walikuwa wanaendelea kujitibia kwa kificho kwa kutumia dawa za hospitali.

Natoa wito kwa Mamlaka hizo kutoa taarifa mara moja kwa Jeshi la Polisi wanapoona ama kumbaini mtu ambaye ataonekana kuwa na majeraha na anatafuta tiba bila ya kufuata taratibu.

Ndugu Wanahabari
Napenda kuujulisha Umma kwamba wapo baadhi ya Watuhumiwa, Wafadhili na Washirika wa Uhalifu na Wahalifu wa ujambazi maeneo haya ambao bado hawajakamatwa. Jambo la kufurahisha ni kwamba taarifa zao zipo kwa Jeshi la Polisi nchini na zinaendelea kufanyiwa kazi ili waweze kukamatwa na kufikishwa kwenye mkono wa Sheria mara moja.

Natoa wito kwa wananchi ambao wanawafahamu watuhumiwa wafuatao kutoa taarifa katika kituo chochote cha Polisi ili waweze kukamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria.

Picha za watuhumiwa hao zitasambazwa kote nchini ili iwe rahisi kuwabaini. Majina ya watuhumiwa hao ni:
i.Anafi Rashid Kapelo @ Abuu Mariam
ii. Hassan Haruna Kyakalewa @ Abuu Salma @ Shujaa @ Dokta
iii. Haji Ulatule
iv. Shekhe Hassan Nasri Mzuzuri
v. Rashid Mtutula

Ndugu Wanahabari
Nimalizie kwa kusema kwamba uhalifu kwenye eneo hili ni suala la muda mfupi. Na tunaendelea vizuri sana. Hali ya usalama imeimarika sana eneo hili. Nazidi kutoa wito kwa wananchi kuendelea kuliunga mkono Jeshi la Polisi ili kufikia malengo yake ya kuzuia, kubambana na kutanzua uhalifu nchini.



Imetolewa na;

Simon Nyakoro Sirro
Inspekta Jenerali wa Polisi
IKWIRIRI
10.08.2017

Wahuni tu hawa hakuna lolote wanaigiza ili ionekane wanafanya kazi waonyeshe miili yao kama siyo uongo huo.
 
nimeona erythrocyte amecomment vizuri, lakini ni ukweli usiopingika kwamba, kuna wana chadema wengi hawajafurahia kabisa hii taarifa ya kazi nzuri ya jeshi la polisi ktk kukomesha uharifu nchini.
ni wakati sasa wa kujitafakari kama upo kwenye chama sahihi cha siasa ama la!

Mkuu hili igizo haliuzi kabisa. Wewe ingiza itikadi za kitoto za kuchafua jina la cdm ukidhani watu ni wajinga wa hivyo. Maiti 13 wala zisionekane zikipelekwa hospitali? Anyway hiyo sio lazima, maiti 7 zimetambulika na wenyewe wameenda kuzichukua hata wachukua maiti hapo mortuary wasionekane? Kama kukamata hao majambazi imeshindikana tafuteni mbinu nyingine sio hii ya kuona watu watoto na kuchafua majina ya vyama vya vingine kwa mambo ya kipuuzi.
 
Bunduki umetuonesha mbona hatukwenda CENTRAL POLICE STATION.
Mortuary ntaenda 2020 kuiangalia CCM
Pumba nyingine pelekeni huko DODOMA.....
Kwa akili yako ulishaona maiti inaoneshwa kwenye TV na police?
 
Back
Top Bottom