Maji ni huduma ambayo Serikali inafeli vibaya mno, uhaba na mgao karibu kila mkoa japo mabilioni yanatumika. Rais Samia anashindwa wapi?

Maji ni huduma ambayo Serikali inafeli vibaya mno, uhaba na mgao karibu kila mkoa japo mabilioni yanatumika. Rais Samia anashindwa wapi?

Nipo chanika hapa huu mwezi sasa maji hayatoki ,dawasa bora mngetuacha na maisha yetu tulishayazoea mmeleta mimaji yenu maji yamekuwa ya shida kuliko mwanzo..
 
Mimi niko Njombe mjini hii ni wiki 2 hakuna maji tunatumia ya mtoni ambayo sio salama kabisa
 
Sawa tuchukulie mfano hiyo Rusumo HEP station ambayo ni run-of-the-river maji ya mto Kagera yakauke je, hiyo hiyo Rusumo hydropower station wataweza kuzalisha umeme?
Mkuu unapendekeza tuache kutumia maji ili tuwe na maji ya kutosha kuzalisha umeme? Umeme una source mbadala lakini sio maji.
 
Mimi niko Njombe mjini hii ni wiki 2 hakuna maji tunatumia ya mtoni ambayo sio salama kabisa
Njombe ni green country! Mnakosaje maji huko? Na watu wa Singida watasemaje? Hawa viongozi hawako serious.
 
Njombe ni green country! Mnakosaje maji huko? Na watu wa Singida watasemaje? Hawa viongozi hawako serious.
Kwa kweli inashangaza sana na hapo ni mjini Mkuu sio pembeni ya mjini hapana ni mjini kabisa hakuna maji wiki ya 2 sasa sasa sijui wale wa nje mji hali ikoje
 
Nimelipia huduma ya kuunganishiwa maji huu mwezi wa 3 bila bila,ukifuatilia unaambiwa vifaa havijafika...sasa kama Dar inachukua 3months kuunganishiwa maji,je huko Wilaya ya Tanganyika hali ikoje?
 
Ni aibu kubwa kwa raifa lilo na mito, maziwa na bahari kuwa na mgao wa maji.
 
Mbezi Makabe, Msakuzi,Msumi, Mpiji mpaka leo hakujawahi kuwa na maji ya Dawasco.
Umeme umefika kabla ya 2010, maji kuna watu wanauza na magari ndio wanawahonga DAWASCO wasilete maji maeneo hayo ili biashara yao iwe nzuri.
 
Nilitegemea kwamba serikali inayosema inapigana na kupambana sana kuhudumia watu wake ingefanikiwa sana katika suala la kutoa maji kwa watu wake. Lakini inasikitisha sana kwamba hadi leo Tanzania inafeli sana katika kutoa huduma hii kwa wananchi. Na kinachosikitisha hata zaidi ni kwamba hii ni huduma muhimu sana hasa kwa wananwake na watoto, na ina athari katika mambo mengi.

Huduma mbovu za maji zina athari nyingi sana, kwa mfano;
  • Wanawake wanapoteze muda mwingi katika kufuata maji
  • Matatizo ya kijamii kama kubaka watoto na wanawake wanapokuwa wakifuata maji
  • Hatari za afya za wananchi kutokana na kutokunywa maji safi na kutokuwa na usafi wa mwili
  • Ugomvi katika familia na jamii kutokana na uhaba wa maji
Matarajio yangu yalikuwa kwamba kuwa na raisi mwanamke kungekuwa ni chachu ya tatizo hili kukomeshwa nchini, lakini hali bado ni mbaya leo kama ilivyokuwa jana. Tunachoona ni matumizi makubwa ya fedha kwenye miradi ya maji bila kuona matukio ya miradi huo. Ufisadi umezidi mno kwenye miradi ya maji na hatusikii watu kuchukuliwa hatua.

Jambo la aibu hata zaidi ni kwamba hata sehemu zenye rasilimali ya maji kubwa sana zinakuwa na matatizo ya maji. Mikoa kama Mbeya, KIlimanjaro, Iringa, Morogoro, nk, yenye mito na vyanzo vya maji tele kwa nini iwe na matatizo ya maji?

Kichekesho kwa mfano, ni mwanzoni mwa mwaka huu nilitembelea mji wa Tukuyu huko Mbeya, na kukuta kuna uhaba mkubwa wa maji, ambapo sehemu za mji huu zina mgawo wa maji wa siku mbili au tatu kwa wiki. Niliuliza viongozi wa mji, chanzo cha maji katika mji huu ni wapi? Nikaambiwa ni pembezoni mwa Mlima Rungwe. Nikasema ikiwa chanzo ni huko mlimani, ina maana mnaweza kugawa maji kwa kutumia gravity tu, na kinachihitajika ni mambomba na matenki makubwa labda matatu tu. Sasa kwa nini mji una shida ya maji muda wote huu ikiwa gharama za kusambaza maji ya gravity ni za nchini kiasi hiki? Hakuna aliyenipa jibu la kitaalamu zaidi ya majibu ya kitoto ya kisiasa.

Nina uhakika mikoa kama KIlimanjaro, Arusha, ziko katika mazingira kama haya ya kupata maji kwa gravity lakini hakuna chochote kinachoendelea.

Mama Samia, watu wako wanashindwa wapi katika hili? Huenda ni jambo linahitaji liangaliwe upya na sio kutumia njia za zamani ambazo zimefeli kwa muda mrefu sana. Tunaweza kuelewa matatizo ya umeme na kuyavumilia, lakini sio maji. Ikibidi dedicate tozo za mwaka mzima ziende kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za maji. Kama raisi wa kwanza Tanzania mwananke, ukimaliza muda wako bila kuhakikisha access ya maji nchini ni 100% nitakushangaa sana. Utakuwa umewaangusha na hata kuwasaliti mno wanawake wenzio.

Reference: Mgawo wa maji watikisa mijini, vijijini
Wakati wabunge wa upinzani wakiongozwa na Mh Myika kuishauri Serikali kujenga bwawa la Kidunda Ruvu mkoani Pwani, waldhihakiwa sana na wabunge wa CCM.
Leo maji shida Dar kila mtu anahangaika.
Huku Mbezi Beach garden zimenyauka maji ya kumwagilia hakuna
Sasa maji yanatoka mara tatu kwa wiki, sasa tunaona hadi maboza ya maji kwa ajili ya matumizi ya ndani,
 
Nilitegemea kwamba serikali inayosema inapigana na kupambana sana kuhudumia watu wake ingefanikiwa sana katika suala la kutoa maji kwa watu wake. Lakini inasikitisha sana kwamba hadi leo Tanzania inafeli sana katika kutoa huduma hii kwa wananchi. Na kinachosikitisha hata zaidi ni kwamba hii ni huduma muhimu sana hasa kwa wananwake na watoto, na ina athari katika mambo mengi.

Huduma mbovu za maji zina athari nyingi sana, kwa mfano;
  • Wanawake wanapoteze muda mwingi katika kufuata maji
  • Matatizo ya kijamii kama kubaka watoto na wanawake wanapokuwa wakifuata maji
  • Hatari za afya za wananchi kutokana na kutokunywa maji safi na kutokuwa na usafi wa mwili
  • Ugomvi katika familia na jamii kutokana na uhaba wa maji
Matarajio yangu yalikuwa kwamba kuwa na raisi mwanamke kungekuwa ni chachu ya tatizo hili kukomeshwa nchini, lakini hali bado ni mbaya leo kama ilivyokuwa jana. Tunachoona ni matumizi makubwa ya fedha kwenye miradi ya maji bila kuona matukio ya miradi huo. Ufisadi umezidi mno kwenye miradi ya maji na hatusikii watu kuchukuliwa hatua.

Jambo la aibu hata zaidi ni kwamba hata sehemu zenye rasilimali ya maji kubwa sana zinakuwa na matatizo ya maji. Mikoa kama Mbeya, KIlimanjaro, Iringa, Morogoro, nk, yenye mito na vyanzo vya maji tele kwa nini iwe na matatizo ya maji?

Kichekesho kwa mfano, ni mwanzoni mwa mwaka huu nilitembelea mji wa Tukuyu huko Mbeya, na kukuta kuna uhaba mkubwa wa maji, ambapo sehemu za mji huu zina mgawo wa maji wa siku mbili au tatu kwa wiki. Niliuliza viongozi wa mji, chanzo cha maji katika mji huu ni wapi? Nikaambiwa ni pembezoni mwa Mlima Rungwe. Nikasema ikiwa chanzo ni huko mlimani, ina maana mnaweza kugawa maji kwa kutumia gravity tu, na kinachihitajika ni mambomba na matenki makubwa labda matatu tu. Sasa kwa nini mji una shida ya maji muda wote huu ikiwa gharama za kusambaza maji ya gravity ni za nchini kiasi hiki? Hakuna aliyenipa jibu la kitaalamu zaidi ya majibu ya kitoto ya kisiasa.

Nina uhakika mikoa kama KIlimanjaro, Arusha, ziko katika mazingira kama haya ya kupata maji kwa gravity lakini hakuna chochote kinachoendelea.

Mama Samia, watu wako wanashindwa wapi katika hili? Huenda ni jambo linahitaji liangaliwe upya na sio kutumia njia za zamani ambazo zimefeli kwa muda mrefu sana. Tunaweza kuelewa matatizo ya umeme na kuyavumilia, lakini sio maji. Ikibidi dedicate tozo za mwaka mzima ziende kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za maji. Kama raisi wa kwanza Tanzania mwananke, ukimaliza muda wako bila kuhakikisha access ya maji nchini ni 100% nitakushangaa sana. Utakuwa umewaangusha na hata kuwasaliti mno wanawake wenzio.

Reference: Mgawo wa maji watikisa mijini, vijijini
Aisee maji hata uku kwetu yanasumbua sana.
 
Nimelipia huduma ya kuunganishiwa maji huu mwezi wa 3 bila bila,ukifuatilia unaambiwa vifaa havijafika...sasa kama Dar inachukua 3months kuunganishiwa maji,je huko Wilaya ya Tanganyika hali ikoje?
Mkuu hivi bado unaletewa vifaa vya kuunganisha maji? Sie tuliacha siku nyingi tunanunua wenyewe. Vile vifaa vingi vya maji kwenye maduka ya vifaa vya ujenzi sio kwa ajili ya idara za maji za serikali, ni kwa ajili ya watu binafsi kujinunuia! Serikali kununua ilikuwa enzi za Nyerere
 
Mkuu hivi bado unaletewa vifaa vya kuunganisha maji? Sie tuliacha siku nyingi tunanunua wenyewe. Vile vifaa vingi vya maji kwenye maduka ya vifaa vya ujenzi sio kwa ajili ya idara za maji za serikali, ni kwa ajili ya watu binafsi kujinunuia! Serikali kununua ilikuwa enzi za Nyerere
Wale mabwana wakubwa hata connector tu ya 2500 hawanaga kwenye stoo zao. Daaah! Hapo ndo huwa nachokaga
 
Nilitegemea kwamba serikali inayosema inapigana na kupambana sana kuhudumia watu wake ingefanikiwa sana katika suala la kutoa maji kwa watu wake. Lakini inasikitisha sana kwamba hadi leo Tanzania inafeli sana katika kutoa huduma hii kwa wananchi. Na kinachosikitisha hata zaidi ni kwamba hii ni huduma muhimu sana hasa kwa wananwake na watoto, na ina athari katika mambo mengi.

Huduma mbovu za maji zina athari nyingi sana, kwa mfano;
  • Wanawake wanapoteze muda mwingi katika kufuata maji
  • Matatizo ya kijamii kama kubaka watoto na wanawake wanapokuwa wakifuata maji
  • Hatari za afya za wananchi kutokana na kutokunywa maji safi na kutokuwa na usafi wa mwili
  • Ugomvi katika familia na jamii kutokana na uhaba wa maji
Matarajio yangu yalikuwa kwamba kuwa na raisi mwanamke kungekuwa ni chachu ya tatizo hili kukomeshwa nchini, lakini hali bado ni mbaya leo kama ilivyokuwa jana. Tunachoona ni matumizi makubwa ya fedha kwenye miradi ya maji bila kuona matukio ya miradi huo. Ufisadi umezidi mno kwenye miradi ya maji na hatusikii watu kuchukuliwa hatua.

Jambo la aibu hata zaidi ni kwamba hata sehemu zenye rasilimali ya maji kubwa sana zinakuwa na matatizo ya maji. Mikoa kama Mbeya, KIlimanjaro, Iringa, Morogoro, nk, yenye mito na vyanzo vya maji tele kwa nini iwe na matatizo ya maji?

Kichekesho kwa mfano, ni mwanzoni mwa mwaka huu nilitembelea mji wa Tukuyu huko Mbeya, na kukuta kuna uhaba mkubwa wa maji, ambapo sehemu za mji huu zina mgawo wa maji wa siku mbili au tatu kwa wiki. Niliuliza viongozi wa mji, chanzo cha maji katika mji huu ni wapi? Nikaambiwa ni pembezoni mwa Mlima Rungwe. Nikasema ikiwa chanzo ni huko mlimani, ina maana mnaweza kugawa maji kwa kutumia gravity tu, na kinachihitajika ni mambomba na matenki makubwa labda matatu tu. Sasa kwa nini mji una shida ya maji muda wote huu ikiwa gharama za kusambaza maji ya gravity ni za nchini kiasi hiki? Hakuna aliyenipa jibu la kitaalamu zaidi ya majibu ya kitoto ya kisiasa.

Nina uhakika mikoa kama KIlimanjaro, Arusha, ziko katika mazingira kama haya ya kupata maji kwa gravity lakini hakuna chochote kinachoendelea.

Mama Samia, watu wako wanashindwa wapi katika hili? Huenda ni jambo linahitaji liangaliwe upya na sio kutumia njia za zamani ambazo zimefeli kwa muda mrefu sana. Tunaweza kuelewa matatizo ya umeme na kuyavumilia, lakini sio maji. Ikibidi dedicate tozo za mwaka mzima ziende kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora za maji. Kama raisi wa kwanza Tanzania mwananke, ukimaliza muda wako bila kuhakikisha access ya maji nchini ni 100% nitakushangaa sana. Utakuwa umewaangusha na hata kuwasaliti mno wanawake wenzio.

Reference: Mgawo wa maji watikisa mijini, vijijini
Kwa ujumla Serikali inafanya kazi nzuri sana hata hivyo kwa mtazamo wangu wanavyotumia Nguvu kubwa kusambaza maji; Wangetumia pia angalau robo ya hiyo Nguvu Kuhuisha vyanzo vya maji.

Sasa hivi vyazo vya maji (chemchem)vingi vimevamiwa na kuharibiwa kwa asilia kama 85% hivi; hivyo pamoja na kazi nzuri ya Serikali ya kusambaza maji mfano kwa 80% huku nyuma utakuta kama asilia 40% ya vyanzo vimeharibika maana yake imesambaza kwa 40%. Tukiendelea na huu utaratibu maji hayatakaa yatoshe badala yake tunakuwa tunapoteza Bilions bure!

Long-term plan:
1. Kila wilaya, Tarafa, Kata, Kijiji, Kitongoji kitambue maeneo yao yaliyokuwa na vyanzo vya maji ( Chemchem) Yaboreshwe kwa kuotesha miti inayo support maji nk yawekewe mipaka... Kwa gharama za Wilaya na husika na sio kuchukulia mchezo mchezo. Taasisi yetu ya SUA inaweza kutupatia miti stahiki
Mfano: Mimi nilipo zaliwa najua Chemchem zote tulizokuwa tunachota maji na naamini kabisa tukizipanda miti stahiki na kuzuia shughuli zote za binadamu; ndani ya miaka 10 tutakuwa na maji yakutosha

2. Walioekeza kwenye vyanzo rasmi vya maji (Chemchem) wapewe Viwanja mbadala bure na pengine findia kiasi ili watoke na pawekwe mipaka raski (hapa nasema chemchem sisemei mito)

3. Hawa wataalam wetu waweze kutofautisha mto na Chemchem/Chanzo cha maji. Unaweza kusikia wapo huko wilayani wanakimbizana na watu wanaolima karibu na mto huku Chanzo cha maji/chemchem inakauka wala hawaipi uzito. Yaani sisi watu weusi sijui nani katuroga....

4. Suala la kulinda Vyanzo vya maji (Chemchem) lisiachiwe idara ya maji pekee; namaanisha, Baada ya kuvitambua na kuviwekea mipaka/Utaratibu, migambo wanaweza kutusaidia kuvilinda
Pengine Bunge lipitishe Sheria maalum inayotekelezeka (Inayowahusu watu wa kawaida na matajiri

5. Maji yabakie huduma kwa mtu anayotumia kwa matumizi yake na sio BIashara

Inauma sana kuona watu wanajenga/ wanafanya miradi kibao kwenye vyanzo vya maji (Chemchem) WAZI WAZI tena kwa gharama kubwa ya kukausha maji na hakuna mtu anayechukua hatua!!!
 
Mkuu, Tanzania kuna miji mingapi ya Wamasai na Wahdzabe? Hicho ndio kisingizio? Kwanza tangu Wamasai wahamia Vigwaza njia ya Morogoro sijaona kama wamehama, miaka zaidi ya ishirini sasa
inasikitisha sana kuona mtu anamtazamo wa kizamani kama huo na cha kushangaza utakuta yupo RUWASA,mfano mzuri ni mradi wa maji wa ruwasa kijiji cha lopolun na lemishiri kata ya oloirien wilaya ya ngorongoro mradi umezinduliwa na mwenge lakini yamebaki mapambo tu hakuna usambazaji wa maji kwa wananchi.
 
Back
Top Bottom