Majibu ya CCM Mdahalo wa Odemba: Tunasikitishwa na jinsi alivyoupotosha umma, tumeshangazwa na machozi yake!

Makonda angeenda!!

Hivi ccm chama changu hao wanachama tunaowalipa mapesa ya mshahara kama hawana uwezo wa kukitetea chama kwenye midahalo tunawalipa wa nini!!?

Hadi hasira aiseh!!
Kuna mchungaji mmoja alikuwa anaitwa KATO anlikuwa anapenda kusema: "Ninachemka bila mfuniko" ni ndugu yako?
 
Ccm ni wahuni sana. Katibu wa chama anakimbia mdahalo!!!??? Aibu naona mimi.
 
Hata hivyo nchimbi anauwezo mdogo sana wa hoja ,alibebwa na baba yake ambaye alikuwa RPC ni kama nape na makamba yaani ccm ni ukoo wa panya
 
Je, unaweza kuthibitisha hilo? Au ni hisia zako chafu?
kesi ya ugaidi ya Lwakatare wakati inaunguruma ulikuwa bado hujazaliwa??? vipi kuhusu kutekwa kwa Dr ULIMBOKA????
 
kesi ya ugaidi ya Lwakatare wakati inaunguruma ulikuwa bado hujazaliwa??? vipi kuhusu kutekwa kwa Dr ULIMBOKA????
Nimekuuliza Uthibitisho unaniletea kesi ya Lwakatare.

Leta uthibitsho sitaki porojo.
 
Namsihi bwana Odemba aache kujiingiza kwenye siasa za maji taka. Chama Cha Mapinduzi siyo kikundi cha wahuni, Chama cha Mapinduzi ni Taasisi. Afuate utaratibu unaotakiwa.
CCM haijawahi kushiriki midhaho tangu walivyoumbuka kupitia wale wagombea wao wa ubunge, midahalo iloyokuwa ikiandaliwa na Tido Mhando alipokuwa mkurugenzi wa TBC. Kutokana na aibu ile iloyotokana na ukweli kuwa wagombea wengi wa CCM huwa ni watupu vichwani, CCM ilitoa maelekezo kwa watu wa CCM kutoshiriki midahalo.

Kama taarifa ya CCM ni ya kweli, na kwamba wahawaogopi midahalo, Nchimbi aseme mdahalo urudiwe lini, na yeye atashiriki.
 
Unamfahamu Faustin Ndugulile?
 
Bas wapange upya mdahalo,
This time CCM wapange ratiba wao ili mambo yasiwe mengi
Haya ndiyo maoni sahihi ya watu wenye akili na siyo yale ya wapiga porojo.

Nchimbi atamke tarehe ambayo yupo tayari kushiriki mdahalo. Lakini najua kamwe hawawezi kukubali. CCM inapenda kuwarubuni wasio na akili. Mahali popote wanapohisi wapo wenye akili, hawaendi. Zaidi watakachopanga ni kuwateka hao wanaowahofia.
 
Ningekuwa Mimi Emmanuel Nchimbi napambana mdahalo uwepo alafu siku hiyo nasubiri Odemba aniulize swali lolote na Mimi nitamuuliza eenhe kilichokuwa kinakuliza ni nini be mdogo mbele ya kamera
 
Unamfahamu Faustin Ndugulile?
Namfahamu sana. Huyu ni kati ya anomalies ndani ya CCM.

Ndugulile ana akili na ana weledi, ndiyo maana CCM hawakumtaka. Wakamwondoa kwenye uwaziri. Ni sawa na yule dada, binti yake Malecela. CCM huwa haitaki watu wenye uwezo wa akili. Wao hawataki kabisa watu wanaohoji. Wanawataka watu walio na uwezo tu wa kuitikia na kushangilia bila ya kujali kinachotendwa ni kizuri au cha kishetani. Anayehoji hugeuka kuwa adui yao.
 
Vipi kuhusu Dr Tulia Ackson. Rais wa Mabunge yote Duniani?
 
CCM walishaapa hawawezi kwenda kwenye midahalo.Ni mwiko.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…