Majibu ya Rais Samia Suluhu hata Kama yangekuwa uongo lakini Yanaridhisha

Majibu ya Rais Samia Suluhu hata Kama yangekuwa uongo lakini Yanaridhisha

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
Assalamu Aleykum

Nimemsikia Mhe. Rais, Mama Samia Suluhu akiwa anahojiwa na Mwandishi, Salimu Kikeke. Kwa kweli Maswali yamejibiwa vizuri Sana.
Nafahamu Siasa zilivyo, nafahamu mambo ya kiutawala Kwa kiasi kidogo, Kwa majibu ya Rais Samia ni wazi amejibu kwa kiwango cha juu mno.

Ingawaje amejibu kirahisi sana karibu maswali yote lakini majibu yake yalikuwa yanafungua majibu ya baadhi ya maswali ambayo angeulizwa Mbele.

Hata Kama Samia atakandiwa na mahasimu wake kuwa amejibu Kama mjinga, au ameongea uongo, au vyovyote watakavyo mwambia lakini ukweli ni kuwa amejibu Kwa kiwango kizuri cha juu kabisa. Kama ni uongo basi ni ule uongo unaoridhisha kabisa.

SSH moja ya majibu yake, hasa kwenye mikutano ya Kisiasa ameniongezea Jambo jipya ambalo nikiri kuwa sikuwa nalifahamu.
Jambo Hilo ni kuhusu Katiba ya Vyama vya Kisiasa ambapo ndani yake kuna vipengele vinavyoelezea idadi ya vikao na mikutano Kwa mwaka ambayo Chama kitapaswa kikae.

Mikutano hii Kwa vile IPO kikatiba(ya kila chama kulingana na Chama) ikiitishwa haina haja ya kuomba kibali Kwa polisi.
Hii Kwa kweli sikuwa nafahamu.

Kwa maelezo yake Kama nitakuwa nimekuelewa Sawia, alikuwa anamjibu Kikeke kuwa, Mikutano au vikao vya kichama inaruhusiwa ikiwa vimeorodheshwa ndani ya Katiba. Na Kama havijaorodheshwa basi sharti kuwepo na Kibali kutoka Polisi.

Kwa mujibu wa maelezo ya SSH anajaribu Kueleza kuwa baadhi ya Vyama vya Upinzani hutaka kufanya mikutano hovyo hovyo hata Kama vikao/mikutano hiyo haipo kikatiba(Katiba ya chama husika) na pia hawajaomba Kibali polisi.

Nikiri kuwa sikujua Jambo Hilo. Na niliona Wapinzani wanaonewa lakini Kama ni hivyo basi nilikuwa sipo Sahihi.

Lakini Kama SSH anadanganya basi Wanasheria mtanieleza kuhusiana na hoja hiyo aliyoisema Mhe. Rais.

Kuhusiana na Kesi ya Mbowe, siwezi elezea lolote isipokuwa naiachia Mahakama, ingawaje maswali ninaweza kuwa nayo, mathalan, iweje Mbowe akamatwe kipindi hiki akidai Katiba mpya na sio kipindi cha nyuma?

Ingawaje SSH ameeleza kana kwamba Tayari kulikuwepo na mchakato wa kesi hiyo na ndio maana Mbowe amejiingiza katika kudai Katiba mpya kujikinga na mshale wa kesi hiyo.

Yote tisa, mwisho ni majibu ya Mhe. Rais ni mepesi Sana lakini Yanaridhisha mno kiasi kwamba hata muulizaji anajikuta maswali mengine aliyonayo kichwani yanayeyuka.

Muhimu:. Tunataka Katiba Mpya Kwa kizazi kipya.
Ishu ya Katiba si suala la kiongozi kuamua liendelee ama liendelee. Ni takwa la kizazi kipya.

Taikon wa Fasihi
Turiani, Mvomero
 
Tatizo mnalazimisha watanzania wote waende na hii ajenda ya katiba mpya ukweli ni kwamba ... muda bado wa kuwa na katiba mpya ukifika hakutakua na haja ya kutumia nguvu nyingi.

Kuna matatizo kweli ambayo wanaweza wakayajadili na wakatengeneza ground-base kutaka kuaminisha watz kua kila tatizo ni kwasababu ya katiba mbovu hata kama ni kweli it will take time mpka tuelewe anzeni na ambayo yanamgusa kila mtu moja kwa moja
 
Tatizo mnalazimisha watanzania wote waende na hii ajenda ya katiba mpya ukweli ni kwamba ... muda bado wakua na katiba mpya ukifika hakutakua na haja ya kutumia nguvu nyingi. kuna matatizo kweli ambayo wanaweza wakayajadili na wakatengeneza ground-base kutaka kuaminisha watz kua kila tatizo ni kwasababu ya katiba mbovu hata kama ni kweli it will take time mpka tuelewe ...anzeni na ambayo yanamgusa kila mtu moja kwa moja
Hujui Katiba inagusa mtu mmoja mmoja?
 
Tatizo mnalazimisha watanzania wote waende na hii ajenda ya katiba mpya ukweli ni kwamba ... muda bado wakua na katiba mpya ukifika hakutakua na haja ya kutumia nguvu nyingi...
Naungana nawe keama wanaodai Katiba mpya waanze na yanayowagusa watu wengi.

Madai ya Katiba mpya ni dhana potofu ya wanasiasa, wenye uchu wa madaraka, kwa kuamini kuwa itawapa uwanja mpana wa kuingia madarakani.

Kwenye Katiba iliyopo sijaona kifungu kinachominya Demokrasia, Haki na Uhuru nchini. Kama kipo naomba wadai Katiba mpya wakitaje
 
Wote wanaomsifia Samia ni Kwa sababu ya udini and nothing else , wanajaribu kumkingia kifua agombee tena 2025 japo indicator zinaonyesha worst to come!!! Kama nilimpinga Jiwe , sina cha kumsifia SSH madam Yale ya Maghufuli anayaendeleza Kwa udhabiti zaid
 
Wote wanaomsifia Samia ni Kwa sababu ya udini and nothing else , wanajaribu kumkingia kifua agombee tena 2025 japo indicator zinaonyesha worst to come!!! Kama nilimpinga Jiwe , sina cha kumsifia SSH madam Yale ya Maghufuli anayaendeleza Kwa udhabiti zaid


Nilimpinga Jiwe
Kwa Samia bado namvutia Kasi,
Mpaka sasa hivi bado yupo 50/50
 
Wote wanaomsifia Samia ni Kwa sababu ya udini and nothing else , wanajaribu kumkingia kifua agombee tena 2025 japo indicator zinaonyesha worst to come!!! Kama nilimpinga Jiwe , sina cha kumsifia SSH madam Yale ya Maghufuli anayaendeleza Kwa udhabiti zaid
Mpaka sasa hivi watanzania bado hamjui mnataka nini.

Wakati huu watu wanamsifia magufuli ambae walimpinga sana,lakini sasa hivi watu wanamsifia kwa misimamo yake hasa kuhusu chanjo.

Tehehehhe ndio maana simsikilizi mpuuzi yeyote anaejaribu kuniaminisha na kunilisha mabaya dhidi ya raisi yeyote yule.

Msimamo huu ninao tokea enzi na enzi na ndio maana hata wakati wa magufuli ambao wapumbavu waliendelea kulaani mimi nilibaki na msimamo wangu huu huu.

Na nilikuwa tayari kujenga hoja dhidi ya wale wanaoponda serikali ns raisi mwenyewe.

Kuwa na msimamo huu haimaanishi kwamba tunaamini raisi hakosei laa hasha tunaamini anakosea.

Lakini pia kuamini kuwa raisi anakosea haimaanishi kuwa raisi hafai.
 
Naungana nawe keama wanaodai Katiba mpya waanze na yanayowagusa watu wengi.

Madai ya Katiba mpya ni dhana potofu ya wanasiasa, wenye uchu wa madaraka, kwa kuamini kuwa itawapa uwanja mpana wa kuingia madarakani.

Kwenye Katiba iliyopo sijaona kifungu kinachominya Demokrasia, Haki na Uhuru nchini. Kama kipo naomba wadai Katiba mpya wakitaje
Wewe hupaswi hata kujibiwa maana inaonekana una Nia mbaya
 
Rais amezungumza vizuri kweli tena kwa uwazi ulio uwazi kwamba sauli hili sio la leo lilikuwepo na bw yule yule alikuwa analifahamu fika na baadhi ya wahusika wa jambo hili walikuwepo rumamnde kwa muda mrefu tu kabla bwana yule hajakamatwa isipokuwa bw yule ni intelegent wa kutisha sana ana akili nyingi sana akaona atafanyaje suala hile alipe mlangpo au mwonekano mwingine wa ki umma zaidi akaingilia kwa kasi ya katiba mpya bahati mbaya kondoo wake hawajui haya au intelegency aliyonayo kiongozi wao katika kuwatumia vyema koondoo wake, ''Rais amesaema mahakama itatupa majawabu sahihi baada ya mahakimu na wanasheria wa pande zote mbili kukabiliana kwa kina na kuja na jawabu moja tuvute subraaaaa''
 
Tatizo mnalazimisha watanzania wote waende na hii ajenda ya katiba mpya ukweli ni kwamba ... muda bado wa kuwa na katiba mpya ukifika hakutakua na haja ya kutumia nguvu nyingi... kuna matatizo kweli ambayo wanaweza wakayajadili na wakatengeneza ground-base kutaka kuaminisha watz kua kila tatizo ni kwasababu ya katiba mbovu hata kama ni kweli it will take time mpka tuelewe ...anzeni na ambayo yanamgusa kila mtu moja kwa moja

Tatizo la tozo linamgusa kila mtu, mbona halirekebishwi?
 
Rais amezungumza vizuri kweli tena kwa uwazi ulio uwazi kwamba sauli hili sio la leo lilikuwepo na bw yule yule alikuwa analifahamu fika na baadhi ya wahusika wa jambo hili walikuwepo rumamnde kwa muda mrefu tu kabla bwana yule hajakamatwa isipokuwa bw yule ni intelegent wa kutisha sana ana akili nyingi sana akaona atafanyaje suala hile alipe mlangpo au mwonekano mwingine wa ki umma zaidi akaingilia kwa kasi ya katiba mpya bahati mbaya kondoo wake hawajui haya au intelegency aliyonayo kiongozi wao katika kuwatumia vyema koondoo wake, ''Rais amesaema mahakama itatupa majawabu sahihi baada ya mahakimu na wanasheria wa pande zote mbili kukabiliana kwa kina na kuja na jawabu moja tuvute subra''

Samahani mzee, naona hujavaa miwani yako ya kusomea, hivyo hujaweka nukta wala koma. Mtafute mjukuu wako akusaidie kuhariri huu uhuni ulioandika hapa.
 
Naungana nawe keama wanaodai Katiba mpya waanze na yanayowagusa watu wengi.

Madai ya Katiba mpya ni dhana potofu ya wanasiasa, wenye uchu wa madaraka, kwa kuamini kuwa itawapa uwanja mpana wa kuingia madarakani.

Kwenye Katiba iliyopo sijaona kifungu kinachominya Demokrasia, Haki na Uhuru nchini. Kama kipo naomba wadai Katiba mpya wakitaje

Rais kuchagua viongozi wa tume ya uchaguzi wakati hatuna marais waadilifu. Matokeo yake tume ya uchaguzi inafanya atakavyo rais. Na udhaifu huu tumeushuhudia kwa macho yetu.
 
Wanaouliza kwa nini Mbowe amekamatwa sasa na si vinginevyo wanasahau kuwa Mbowe, Lema, Meya wa zamani Ubungo Boniface walikamatwa mara baada ya matokeo ya uchaguzi mkuu kutangazwa na kabla Rais hajaapishwa kwa kuchochea maandamano yasiyo na kikomo kupinga matokeo. Mambosasa alihojiwa na vituo vya ITV na TBC na kutoa madai hayo hayo ya ugaidi.
 
Samahani mzee, naona hujavaa miwani yako ya kusomea, hivyo hujaweka nukta wala koma. Mtafute mjukuu wako akusaidie kuhariri huu uhuni ulioandika hapa.
Ukweli halisi unathubutu kuuita uhuni, chadomo jifunzeni kuelewa mambo kwa kina dhana ya ukaidi na ubishi na kujifanya kujua sana kana kwamba mna akili nyingi sana mnajidanganya sana wajukuu zangu tunakuangalieni tu kwa macho yetu manne nyinyi vijana wa Djs na kazi ya Dj ni moja tu kupigisha disco kule mlio wengi mnakata tu mauno.
 
Wanaouliza kwa nini Mbowe amekamatwa sasa na si vinginevyo wanasahau kuwa Mbowe, Lema, Meya wa zamani Ubungo Boniface walikamatwa mara baada ya matokeo ya uchaguzi mkuu kutangazwa na kabla Rais hajaapishwa kwa kuchochea maandamano yasiyo na kikomo kupinga matokeo. Mambosasa alihojiwa na vituo vya ITV na TBC na kutoa madai hayo hayo ya ugaidi.

Rais akikosea au akivunja sheria ni sheria ipi inamuwajibisha??
 
Kama yote haya ulikuwa hujui na ulikuwa unatokwa povu kwamba ccm ni madikteta basi wewe ni mpumbavu!

Na siyo pekeako chadema wote mko hivyo huwa mnatokwa na mipovu kwa vitu msivyovijua!

Jinga kabisa.
 
Back
Top Bottom