Majibu ya Ubalozi wa Marekani kwa BAWACHA baada ya kushinikiza Freeman Mbowe kuachiwa huru

Wito kautoa baada ya barua ya Bawacha? Kama anaandika kingereza kizuri ndiyo itasaidia ubalozi wa Marekani kumtoa Mbowe? Akili za Pro-Chadema bana.
Kwa hiyo wewe unaamini kabisa ndani ya dhamiri yako na MUNGU anakuona, yaani unaweza kusema Mbowe Ni Gaidi.
 
Kama mtu hajui maana ya kujipendekeza na kulamba makalio basi hiyo barua ya bawacha ndio text book example..Wamejinyenyekeza kwa beberu hadi huruma.
Mnapopeleka mabakuri kwa mabeberu mnafanyaje? Hamjipemdekezi na kulamba hayo uliyoyataja?
 
watafute nchi nyingine sasa waende ubalozi wao, marekani washawapiga chini.
Tatizo huwa wanakurupuka,walianza movie yao kwa pupa na dharau ,Rais aliwaambia wasubiri wakajiona vinara sasa wamepata hasara kote kote kwa kukurupuka.
 
TUKUMBUSHANE hivi lissu aliokoka kwa kukimbilia wapi vileee? pamoja na harakati za KAMANDA ZIRRO na vibaraka wake kutaka kumnyaka lakini mwishoe waliinua mikono. so usijisahaulishe dadangu
Kitaratibu ilikuwa malalamiko hayo yalikuwa yapelekwe UN, lakini si Marekani ambao ni taifa na wanakosa uhalali wa kuingilia moja kwa moja mambo ya nchi fulani, zaidi sana labda kuondoa misaada.

Pia wazungu wanatuchora sana na kujua akili zetu zimeishia wapi, sina hakika kama ni wazuri katika kuondoa matatizo ya namna hii katika nchi yoyote duniani kwa faida ya hyo nchi.

Swali; hv Uganda kuna demokrasia kuzidi Tanzania, vp uhusiano wake na Marekani. Tuamke, utatuzi sahihi wa matatizo yetu u mikononi mwetu watz, generally waafrika.

Jinsi barua ilivoandikwa juu ya utawala wa awamu ya tano mtu wa nje anaweza fikiri watz tulikuwa jehanamu, mi nasema ukikuza jambo lolote ama kwa chuki au malengo yako fulani, huja kudharauliwa hata kama ulikuwa na hoja za mantiki.

Marekani anajali maslahi yake, ukitishia maslahi yake mara moja unageuka dikteta hata kama sio.
 
Genta unadhani hawa jamaa hawajui basii...hiki chama kisahzoea sleeping with the enemy wakishirikiana na hao wanaharakati wa twitter..wanapangiwa cha kuandika baadae utasikia ubalozi unakuja na mashudu.....sijui maria sarungi..sijui kigogo hizi ni tarumbeta tu...mpigaji anajulikana article titled 'The Ford Foundation and the CIA', he writes, "The CIA uses philanthropic foundations as the most effective conduit to channel large sums of money to Agency projects without alerting the recipients to their source. From the early 1950s to the present the CIA's intrusion into the foundation field was and is huge. A US Congressional investigation in 1976 revealed that nearly 50% of the 700 grants in the field of international activities by the principal foundations were funded by the CIA (Who Paid the Piper? The CIA and the Cultural Cold War, Frances Stonor Saunders, Granta Books, 1999, pp. 134-135)."

 
Worldwide,wananchi wakionewa kimbilio la kwanza ni balozi za USA

Na sio balozi ingine yeyote

There is a reason for that!

Unakaa hapa unashangaa hili?
pushing for their imperialistics agendas...what else
 
Huku kwenye siasa tu ndio unaandika maandiko ya maana,kule kwenye soka sijui uwa kinakupata kitu gani aisee!
 
Wanakimbilia marekani coz wana demokrasia ya kweli ndio maana kila baada ya awamu mbili au moja chama tawala hubadilika!!Republican au Democratic wakati huku kwetu ccm ni MZIMU WA BABU LAZIMA ITAWALE MILELE IWE KWA JASHO NA DAMU HATA VIFO VYA RAIA LAZIMA ITAWALE!!!Hauoni tofauti hapo???!!!Hata kule kwenu RWANDA mambo ni haya haya kama ya ccm!!!
 
Nani alisema America hawana uwezo wa kuingilia serikali zetu!!!..(Iraq, Afghanistan, Sudan, Pakistan, Brazil, Libya etc)
 
human value ah ah mkibeba box hua mnafunga kabisa masikio How many people have been killed by US police since George Floyd?
 
Matukio wanayotafanya chadema ni kinyume kabisa na yalivyokuwa matarajio ya wengi. Yani ni chama ambacho hakina ushawishi tena.
inawezekanaje kwa chama kinachodai kuwa na wafuasi zaidi ya mil 6 kwenda kujigaragaza kwenye bustani za ubalozi wa marekani kuomba kusaidiwa.
Hiyo nguvu ya umma inafanya kazi gani sasa? au hata hiyo nguvu ya umma hakuna ni porojo tu.
 
Or Rwanda, pamoja na kumnanga sana Kagame ila ndiye kibaraka wao namba moja EA.
 
Thanks a lot for letting me know about this. Sincerely I never knew that CIA are having these Secret ( Shadow ) Projects world wide.

Now I can understand why most poor Countries especially in Africa despite having so many Natural Resources are facing Political Instabilities and Civil Wars.
 
Kwa hiyo umeona kabisaa kwamba hayo ni majibu ya ubalozi wa USA nchini Tanzania kwa BAWACHA? Yaani waandikiwe barua halafu waijibu barua hiyo kwenye TWITA..!!???
Kwa hiyo unaamini kuna majibu mengine ubalozi wa Marekani utayatoa yatasaidia Mbowe kutoka jela.
 
It has worked before!
 
Omba Mungu akunyime vyote ila asikunyime akili.

Kwa akili ya Chadema kuishtaki serikali kwa Marekani wanadhihirisha jinsi hiki Chama kilivyo NGO kama NGO zingine zinazofadhiliwa na USAID.

Takataka kabisa.
 
Kwa hiyo unaamini kuna majibu mengine ubalozi wa Marekani utayatoa yatasaidia Mbowe kutoka jela.
Naamini majibu yapo, yanaweza yasaidie au yasisaidie Mbowe kutoka huko aliko..!!! Lakini majibu hayo, kwa nchi kama Marekani, hayawezi kuwa kwenye TWITA wakati wameandikiwa barua official..!! Sijui kama unanielewa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…