Majina ya Kiafrika mbioni kutoweka

Majina ya Kiafrika mbioni kutoweka

Ndugu wanaJF,
Kufikia mwisho wa karne ya 21, majina kama Masawe, Otieno, Gwamaka, Kamugisha, Masanja n.k yatafutika nchini kwetu.

Imekuwa nadra mno kukuta mtanzania mwenye majina matatu, yote yenye asili ya kabila lake, au hata ya makabila ya hapa Tanzania au Afrika kwa ujumla.

Ubantu unaisha. Unailoti unaisha.

Watu wa pwani walishapotezwa kitambo. Wao wengi wao wana majina ya kiarabu tupu.
Wakina Mohammed Said. Hata Surname za kiafrika walishaacha.

Watu wa bara ndiyo walikuwa badobado, lakini nao sasa watoto wao ni wakina Brian McDonald, Humphrey Jr. Scott au Natasha-Rose Leonard.

Hata wazungu, wachina, wahindi na waarabu wanatushangaa sana.

Wao hawana huu ujinga.

Hakuna mzungu anaitwa Manka, hakuna muarabu anaitwa Mabula wala mchina anayeitwa Mahenge.

Ngugi wa Thiong'o huyaita haya majina colonial tags.
Yeye aliachana na colonial tag yake 'James' akabaki na Ngugi wa Thiong'o.

Je, waafrika tumeshindwa kuthamini majina ya tamaduni zetu na kuachana na majina ya kigeni?
Si ungeanza na Jina lako unalotumia wewe nalo ni la kikoloni.
 
Yan tabu kweli unakuta msukuma majina ya watoto wake ni Ian precious ivan sasa umkute akiwa anakosoa wazungu yan kama tumeshikiwa akili vile yan majitu yanapenda kila kitu cha wazungu huku yakijifanya kuwachukia
 
Acha ushamba maisha ya black Americans ni mazuri kuliko Yako usitake kudanganya watu hapa
Uzuri wa maisha ni swala la tafsiri kichwani tu. Mwenye ghorofa 50 anaona maisha ni mazuri. Lakini anayemudu kupanga chumba kimoja naye anaona maisha ni mazuri kwake, ili mradi hadaiwi halali njaa wala havunji sheria. Black American wanaokimbizana na askari wa kizungu kila siku wana uzuri gani wa maisha.
 
Ndugu wanaJF,

Kufikia mwisho wa karne ya 21, majina kama Masawe, Otieno, Gwamaka, Kamugisha, Masanja n.k yatafutika nchini kwetu.

Imekuwa nadra mno kukuta mtanzania mwenye majina matatu, yote yenye asili ya kabila lake, au hata ya makabila ya hapa Tanzania au Afrika kwa ujumla.

Ubantu unaisha. Unailoti unaisha.

Watu wa pwani walishapotezwa kitambo. Wao wengi wao wana majina ya kiarabu tupu. Wakina Mohammed Said. Hata Surname za kiafrika walishaacha.

Watu wa bara ndiyo walikuwa badobado, lakini nao sasa watoto wao ni wakina Brian McDonald, Humphrey Jr. Scott au Natasha-Rose Leonard.

Hata wazungu, Wachina, Wahindi na Waarabu wanatushangaa sana.

Wao hawana huu ujinga.

Hakuna mzungu anaitwa Manka, hakuna muarabu anaitwa Mabula wala mchina anayeitwa Mahenge.

Ngugi wa Thiong'o huyaita haya majina colonial tags.
Yeye aliachana na colonial tag yake 'James' akabaki na Ngugi wa Thiong'o.

Je, Waafrika tumeshindwa kuthamini majina ya tamaduni zetu na kuachana na majina ya kigeni?

Kule Karenga Iringa kuna kina Mwangimba. Cousins wake Mkwawa. Wote wamebadilika...kama sio James, basi Jamal etc.
Kutaja majina ya kizungu na kiarabu ina hadhi yake bwana 😂 😂 😂 😂 😂 😂
 
Uzuri wa maisha ni swala la tafsiri kichwani tu. Mwenye ghorofa 50 anaona maisha ni mazuri. Lakini anayemudu kupanga chumba kimoja naye anaona maisha ni mazuri kwake, ili mradi hadaiwi halali njaa wala havunji sheria. Black American wanaokimbizana na askari wa kizungu kila siku wana uzuri gani wa maisha.
We usiekimbizana na askari una unauzuri Gani wa maisha kuwazidi black Americans
 
Ubantu utaisha, lakini Unailoti hautaisha nakuambia, kuanzia lifestyle kama mavazi na hata Lugha

Kwa Mfano mimi naitwa

" LOBULU LASARUNYE LOPURUKWA LAIZER" kutoka Longonot'
Hongera Bwana Lobulu.
Mimi nimesoma na baadhi ya wamasai wenye majina ya kizungu kama Eddy na Isaya.
Ila pia wengi wao walikuwa na majina ya kimasai kama vile Saning'o na. Minyali Losipu.

Wamasai hawajavurugwa sana.
Hofu yangu ni hii spidi ya ukristo kuingia umasaini haitawaacha salama.
 
We usiekimbizana na askari una unauzuri Gani wa maisha kuwazidi black Americans
Amani yangu
Wewe ni nyani halali Yako kuita wanao hayo majina ya kibantu sababu wanao nao. Ni nyani
Sababu za majina yetu ya kibantu kuyafananisha na nyani ni nini ? Ukiitwa Sospeter, Macdonald na Donald unaongezeka akili, pesa na thamani sawa na mzungu au utabakia mweusi tu ?
 
We usiekimbizana na askari una unauzuri Gani wa maisha kuwazidi black Americans
Kwangu uzuri wa maisha ni jinsi nilivyojichagulia. Sioni black American au Bilgate au yeyote ananizidi kitu gani. Hoja yangu sio ya kujifariji bali ni uamuzi na mtazamo wa mtu, kwamba nakula nao, wanakula, nalala nao wanalala.
 
Kwangu uzuri wa maisha ni jinsi nilivyojichagulia. Sioni black American au Bilgate au yeyote ananizidi kitu gani. Hoja yangu sio ya kujifariji bali ni uamuzi na mtazamo wa mtu, kwamba nakula nao, wanakula, nalala nao wanalala.
Na wao hawaoni kama unawazidi Sasa sijui ni shobo au nini mpaka uwajadili watu ambao wanafurahia maisha Yao wakiwa America na wewe upo Kwa mtogole
 
Amani yangu

Sababu za majina yetu ya kibantu kuyafananisha na nyani ni nini ? Ukiitwa Sospeter, Macdonald na Donald unaongezeka akili, pesa na thamani sawa na mzungu au utabakia mweusi tu ?
Endelea kuita majina ya kibantu mzee kwani nani kakukataa tatizo unapotaka kumpangia watu nao wajiite hayo majina ya kibantu wakati duniani hujaja nao huoni kama huna akili
 
Musa pia alizaliwa na jina la kigeni ndugu mwandishi, una nini cha kufanya ili kuwakomboa watu wako kutoka misri?
 
Hongera Bwana Lobulu.
Mimi nimesoma na baadhi ya wamasai wenye majina ya kizungu kama Eddy na Isaya.
Ila pia wengi wao walikuwa na majina ya kimasai kama vile Saning'o na. Minyali Losipu.

Wamasai hawajavurugwa sana.
Hofu yangu ni hii spidi ya ukristo kuingia umasaini haitawaacha salama.
Kweli kabisa Mkuu
 
Endelea kuita majina ya kibantu mzee kwani nani kakukataa tatizo unapotaka kumpangia watu nao wajiite hayo majina ya kibantu wakati duniani hujaja nao huoni kama huna akili
Asiye na akili ni yule anayedharau asili yake wakati mzungu, anayekulaghai uache asili yake yeye haaachi asili yake. Anayejipendekeza kwa wazungu ana tatizo kubwa la kifikra.
 
Asiye na akili ni yule anayedharau asili yake wakati mzungu, anayekulaghai uache asili yake yeye haaachi asili yake. Anayejipendekeza kwa wazungu ana tatizo kubwa la kifikra.
Ndio maana nasema wewe akili huna ungekua unafata asili hata hiyo simu sio asili Yako imetengenezwa na mweupe mbona unaitumia
 
Hadhi ya jina wakati black hata kuoa tu, Mhindi au mwarabu huwezi.

Ukitaka wahindi nenda India. Utarudi nao kwa mafungu makubwa kama nyanya za masala soko la Mabibo. Waarabu, shida yao wanakata mkono kwanza. Ukirudia wanakata ile kitu.
Ila nenda Igunga, Nzega, Kahama, Shinyanga etc. Kule nako utarudisha timu mwenyewe nyuma. Kiufupi usiogope kitu
 
Back
Top Bottom