Majina ya Kizungu na Kiarabu ambayo yamekuwa "Africanized" na kupata hadhi ya kuwa majina ya Kiafrika

Majina ya Kizungu na Kiarabu ambayo yamekuwa "Africanized" na kupata hadhi ya kuwa majina ya Kiafrika

LIKUD

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2012
Posts
18,037
Reaction score
33,681
Yapo majina ya kizungu na kiarabu ambayo yanatumiwa na kuhusudiwa sana na baadhi ya makabila ya kitanzania kiasi kwamba sasa yanaonekana kama ni majina ya makabila hayo.

Baadhi ya majina hayo ni pamoja na:

1. John: Wasukuma. Wasukuma wanalipenda sana hili jina. Ukikutana na mtanzania anaeitwa John basi most of the time atakuwa ni msukuma. Akina " John Msukuma" wapo wengi sana mitaani.

2. Erasto: Wachaga; Unaweza kudhani Erasto ni jina la kichaga kwa namna ambavyo wachaga wanalipenda jina hili.

3. Raphael: Wachaga: Uchagani kuna hadi "ukoo wa Raphael" if am not mistaken.

4. Bilal: Waha

5. Cyprian: Wajita

6. Wlibroad: Wambulu/ Wairaq.

7. Respicius na majina yote yanayoishia na " us ": Wahaya.

8. Feisal: Wapemba.

9. Anzuruni: Waha.

10: Rasul: Waha.

11. Fatuma: Waha.

12. Hamisi: Wasukuma (Hili jina wasukuma wanalitumia wote wakristo kwa waislamu)

13. Shabani: Wasukuma (wanalitumia wakristo kwa waislamu)

14. Veronika: Wasukuma.

15. Rahel (Not Rachel): Wasukuma.

16. Rhoda : Wasukuma.

17. Ruthu : Wasukuma.
18.
19.
20.

10000.
 
Abdalla/ Dulla usukumani wapo kibao tena wengine si waislam wala wakristu hata,au wakristu wengi tu wanaitwa hivyo pamoja na Selemani, Ibrahim/IBRA, Hamza usukumani yanatumika kama majina ya kilugha tu sijui walitoka wapi na hayo majina
 
Abdalla/ Dulla usukumani wapo kibao tena wengine si waislam wala wakristu hata,au wakristu wengi tu wanaitwa hivyo pamoja na Selemani, Ibrahim/IBRA, Hamza usukumani yanatumika kama majina ya kilugha tu sijui walitoka wapi na hayo majina
Kabisa bila kusahau na Ramadhani na Rajabu
 
Back
Top Bottom