Majina ya Madhehebu Kuendana na Asili/Waasisi Wake

Majina ya Madhehebu Kuendana na Asili/Waasisi Wake

Mkuu ni uelekeo wa kifo cha dini za kizungu,na kuibuka upya kwa nguvu kwa kitu kinachoitwa ushirikina na imani za mizimu.

Mkuu, Ukisoma habari utakuta makanisa makubwa sana hasa Nigeria na Marekani. Haya, yanaitwa Megachurches kwa sababu ni makubwa na ni matajiri sana. Tofauti na makanisa madogo ya mitaani.

Pia yapo makanisa ya Korea ya Kusini tangu miaka ya 50, yanayoendeshwa na familia ya Sun Myung Moon, na waumini wao wanaitwa Moonies. Wanajulikana pia kama Kanisa la Muungano. Hawa huwa wanaozesha kwa mpigo watu 100 na zaidi na wana biashara nyingi sana.

Watu wengi hawajui kuwa Korea ya Kusini kuna Wakristo wengi. Nilipoenda Busan, nikaona makanisa mengi sana.

Sidhani dini za "kizungu" zitakufa ila utamaduni na dini huwa zinaenda pamoja.

Kwa mfano, nchi ya Kikatoliki kama Ufilipino, wana sherehe zao za kukimbiza sanamu za watakatifu wao mitaani lakini hukuti hizi sherehe Tanzania.
 
Mkuu, Ukisoma habari utakuta makanisa makubwa sana hasa Nigeria na Marekani. Haya, yanaitwa Megachurches kwa sababu ni makubwa na ni matajiri sana. Tofauti na makanisa madogo ya mitaani.

Pia yapo makanisa ya Korea ya Kusini tangu miaka ya 50, yanayoendeshwa na familia ya Sun Myung Moon, na waumini wengi wanaitwa Moonies. Wanajulikana pia kama Kanisa la Muungano. Hawa huwa wanaozesha kwa mpigo watu 100 na zaidi na wana biashara nyingi sana.

Watu wengi hawajui kuwa Wakorea wa Kusini kuna Wakristo wengi. Nilipoenda Busan, nikaona makanisa mengi sana.

Sidhani dini za "kizungu" zitakufa ila utamaduni na dini huwa zinaenda pamoja.

Kwa mfano, nchi ya Kikatoliki kama Ufilipino, wana sherehe zao za kukimbiza sanamu za watakatifu wao lakini hukuti hizi sherehe Tanzania.
Dah asante kwa elimu mkuu
 
Ikiwakuta wasioweza kufanya maamuzi yao binafisi wanaama makanisa kila siku
 
Mbona Umesahahu na Muslim wale Muhamadiya Jina asili na Mtume Wao..

Wahabism

Sunni

Shia

Takfiri

Ansal Sunni

Bohora

Ritz

Hata kahtaan naye anawafuasi wake humu... japo yeye mwenyewe hajujui kama Sunni au Shia
hao jamaa hawaguswagi mkuu
 
hao jamaa hawaguswagi mkuu
Duh Mbona mimi ndio Kiboko yao acha uoga mkuu... Wanatulia kama Maji Mtungini.... Wakikuzidia Niite Kaka yako hata wawe billion Moja na zaidi niite nawatuliza wote
 
hoja safi sana lakini najiuliza kuhusu ufufuo na uzima, mapambazuko , ngurumo ya upako, mlima wa horeb , marafiki wa yesu, mashahidi wa yehova , hawa wote msingi wa majina haya wameyatoa kwenye biblia baada ya kusoma biblia
 
image.jpeg


Mkuu Amavubi huko unakotaka kwenda kwenye mambo ya Anglicana,Lutheran ni kuleta mada mpya,kwanza kujadili mambo hayo inabidi uwe "umeiva" kiimani,usije "ukaasi" kanisa lako.
Kiufudi hizi dini ni "utamaduni",sisi Waafrika tuliletewa tu na wamisionari..lkn dini hutambulisha utamaduni wa mtu.Martin Luther alipoona nchi yake ya Ujrumani haitambuliki na Papa aliye Rome Italy anatoa amri ambayo mpaka wao Ujerumani wanaitii akaona ni kama "utumwa",ndio maana akasema lazima aondoe ile "Papacy Authority",kwamba kwanini kila kitu kitoke Vatican,yaani kwa lugha nyingine ni kuwa kwanini kila kitu atoe amri Mtaliano??Akaamua kuanzisha dhehebu lake na akalipa jina lake,yeye akiitwa Martin Luther basi kanisa lake liitwe "Lutheran" i.e "Of the Luther".Lengo ni kuondokana na mamalaka ya Vatican chini ya mtaliano na kukuza utaifa wao wa Ujeruman,na ndio maana makao makuu ya Lutheran yakawa Ujerumani...Ulutheri ni alama ya utamaduni wa Mjerumani,alihitaji "identity" yake na akaipata.
Mfalme George VIII wa Uingereza,akiwa muumini safi wa kanisa katoliki,akataka kuoa mke mwingine aachane na Catherine of Aragon,lkn sbb kanisa katoliki hurusiwi kuoa mke mwingine wakati mmoja yupo akakataliwa na Papa.Mfalme akaona Papa anamuingilia mpaka kwenye "ufalme" wake,akaamua kuanzisha kanisa akaliita "Anglican Church" toka neno "Anglo",maana Anglo= England,hivyo Anglican Church maana yake kanisa la England,akajitoa mikononi mwa "Papacy Authority" ili na yeye awe na kanisa lenye utamaduni wao.Anglican Church likawa kanisa la nchi,Mkuu wake ni malkia na kiongozi wake wa kiroho ni askofu wa Canterbury,hii ikawa ni alama ya Uingereza na utamaduni wao,ikawa kama wewe si Muanglicana basi huwezi kuwa Waziri Mkuu wa Uingereza,wakaweza kuanzisha kanisa la utamaduni wao...Dini ni utamaduni
Huku Afrika kuna watu walijaribu kaunzisha makanisa yenye ukristo wa kiafrika,maana waliona kabisa kuwa YESU WA AFRIKA ana tofauti sana na YESU WA ULAYA..kwamba inapswa tuwe na ukristo unaoakisi utamaduni wetu maana dini ni utamaduni,Congo ya Zaire akatokea mtu anaitwa SIMON KIMBANGU akaanzisha kanisa lake akaliita "KIMBANGUISM"...alifanya miujiza na kuponya watu na magojwa,kutibu ukoma na miujiza kibao,Kimbangu akawa na waumini wake lukuki walioukimbia Ukatoliki na Uprotestanti,hii iliwatisha wamisonary wakashitaki kwa serikali ya kikoloni,Simon akakamatwa na kushitakiwanbila kupewa nafasi ya kujitetea,kanisa lake likakuwa na kudidimiza "UKRISTO WA ULAYA" wa wakatoliki na protestanti.Waumini wake wakakamatwa na serikali ya kikoloni ya mbeligiji na wakateswa na wengine kupelekwa "exile" ili kuuwa mshikamano wao.Kimbangu alifia gerezani,dhamira yeke ilikuwa kama ile ya Martin Luther na Mfalme George VII,kuanzisha dhehebu linaloakisi utamaduni wake,yaani utamaduni wa muafrika..Isingekuwa fitna za Mkatoliki na mprotestanti kwa kushirikiana na serikali katili ya mbeligiji,leo hii Afrika nasi tungekuwaa na dini ya "YESU WA KIAFRIKA"....Kwa hiyo ndugu Amavubi bhizi dini ni utamaduni...Umasikini wetu na nguvu za ukoloni zilituzuia kuimarisha dini zinazoendana na utamaduni wa kiafarika.Kwenye picha hiyo,Simon Kimbangu ni huyo aliyevaa shuka
 
Hapo kwenye red; Hakuna dini ya Roma wala Hakuna kitu kinaitwa Roman Catholic...Ila neno Roman lilipachikwa na Anglican kipindi walipojitenga na kanisa katoliki... Naendelea kusoma maana nimeanza kusoma tuu nikakutana na makosa kibao..
.
Maneno Roman Catholic Church kwa historia yake yalianzishwa na Waingereza waliokuwa wanahoji mamlaka ya Catholic Church lililo na makao yake makuu Roma. Lakini leo hii, hata uongozi wa Catholic Church ulioko Roma, mara kadhaa, umejikuta ukitumia maneno Roman Catholic Church kujitambulisha. Kwa sababu hizi za kihistoria, huku uswazi acronyms kama vile R.C. ni rasmi.

Kwa hiyo, kuikataa phrase Roman Catholic Church kwa sababu za kihistoria ni kutenda kosa la kimantki liitwalo genetic fallacy. Ni sawa na kuikataa pete ya ndoa (alama ya upendo) kwa sababu zamani pete ilikuwa ni alama ya utumwa. Na hivyo, mtoa mada hajakosea kutumia maneno Roman Catholic Church. Tuendelee na mjadala.
 
Hii ni tafakuri yangu;
  1. Awali ilikua dini ya Roma ama Roman baadae ikasambaa duniani kote (catholic) na ikawa Roman Catholic.
  2. Martin Luther alikua na mapingamizi 95 dhidi ya dini ya Roma wakati akiwa mtumishi na akajitenga kuanzisha kanisa nchini mwake ndilo leo huitwa Lutheran yaani wafuasi wa Luther na ndio vile Wajerumani wengi ni walutheran ila imeenea duniani kote
  3. neno Anglican linamaanisha England na linashabahiana kidogo na story ya Luther na muasisi wake aliamua kuanzisha kanisa nchini mwake kupingana na urumi na kuitwa Anglican church ama church of england na baadae kusamba duniani kote ila naamibiwa huwezi kuw mtawala england kama wewe si muanglikana
  4. Baptist ni asili ya watu waliofuata ubatizo wa maji mengi kwenye bibilia na kujitenga na ule wa kunyunyizia
  5. Methododist ni vijana wasomi waliokuwa hawaridhishwi na mwenendo wa taratibu za kanisa na kanzisha taratibu bora zaidi za kuabudu (methods)
  6. Seventh Day Adventist lina taathira ya kuweka mkazo katika kuabudu siku ya saba ya juma (seventh) badala ya Jumapili lakini pia utabiri wa majirlo wa William Miller ndio neno Adventists
  7. ........................ongeza...................................
Upeo wangu wa kutafakari ila wote ni waabudu wa Mungu mmoja na wanatumia Bibilia moja.
hapo kwe ukatholiki fanyaburudie kutafiti.
kipi kilitangulia maana mm najua awali ilikuwa catholic tu.baadae baada ya kuibuka vikundi vikundi vinavoshabihiana na ukatoliki ndo wakaweka roman catholic ili kuutofautisha na wengine wanaojiita nao wakatholic.ukizingatia ukatoliki maana yake ni la wote.
hebu turudie kufukunyua hapo kwanza si kwa kubishana ila kwa kujuzana.
naomba kuwasilisha.heshimabyako mkuu.
 
Sijui kwa Kiswahili wanaitwa nini, kwa Kiingereza ni Eastern Orthodox Church (EOC), wapo hasa Ulaya Mashariki.

Greek Orthodox Church
Russian Orthodox Church
orthodox ni sehemu ya ukatholiki lkn hawapo chini ya papa.wana askofu wao.na rc wanapigana sana kuwarudisha kundini hawa.
 
kuhusu lutheran mm nnavojua luther hakuanzisha km kanisa na kulipa jina hilo rasmi.nnachojua alianzisha vuguvugu na akajitenga.baadavya yy kufa walofuata msimamo wake ndo wakajiita walutheli yaani wafuata msimamo wa luther,luther hakuliita kundi lake hivo.walobaki baada ya yy kufa ndo walijiita hivo.
anaejua zaidi ya hayo anisahihishe
 
Mkuu uko sawa kabisa, ila sasa haya makanisa siku hizi yanaota kama Uyoga
Mtu akishakariri verse zake 10 kutoka kwenye biblia basi anaanzisha la kwake nyumbani
japo yanajiita makanisa kiuhalisia si makanisa ni madhehebu.kanisa haligawanyiki.
 
Hizi dini hakuna mweusi hata mmoja mwanzilishi ila zinawaumini weusi wengi.
Na sababu ni kwamba zinasambazwa kwa juhudi na wahusika.
Biashara tu.


Wazungu kwenye hii hila walituweza.
Ba siloamu je kaka alianzisha nani?.vip Agape, Efatha .
 
orthodox ni sehemu ya ukatholiki lkn hawapo chini ya papa.wana askofu wao.na rc wanapigana sana kuwarudisha kundini hawa.

Nafahamu hilo , Mkuu.

Orthodox Church wapo chini ya Holy Synod, kundi la Maaskofu linalopiga kura kumchagua Askofu Kiongozi (Patriarch) na hawamtambui Papa wa Vatican.

Sidhani kama watarudi tena kuwa chini ya Papa wa Vatican.

Hizi "reformation movements" huwa hazirudi nyuma. Leo biblia inatafsiriwa wanavyopenda waumini. Hata wananchi waliokimbia bara la ulaya na kuja Marekani, wamehakikisha kuwa watakuwa na uhuru wa kuabudu wanavyopenda na serikali waliyoianzisha iliambiwa ijitenge kabisa na dini za watu.

Leo ulaya wanafuata siasa hiyo hiyo ya kutenga dini na serikali.

Walichokuwa hawapingi Orthodox Church na Catholic Church ni "Nicede Creed" tu.

Uongozi wa dini pia ni kama wa siasa, mtamu sana. Hamna dhehebu litaacha utamu wa kuongoza waumini wao ili litawaliwe na kiongozi mwingine wa dhehebu tofauti.

Pia, kuna matatizo ya utamaduni.
Kwa mfano, Ufilipino na nchi nyingi za Marekani ya Kusini, kuachana katika ndoa au kutoa mimba hairuhusiwi. Lakini, Italy na Spain ni rahisi kwa sababu sheria zinazofuatwa ni za serikali siyo za dini.

Pia, swala la ndoa ya jinsia moja linaleta matata sana. Madhehebu tofauti ya nchi za Kiafrika na "conservative groups" wa ulaya na Marekani wanapinga sana, lakini wanashindwa kwa sababu sheria za nchi zipo juu zaidi ya dini. Serikali wameamua kuwa kuoa jinsia unayoipenda ni haki ya binadamu, na iruhusiwe.

Nadhani, "reformation movement" nyingine inakuja. Kutakuwa na aina tofauti ya dhehebu la Anglicans kwa mfano. Wale wataotaka mabadiliko na wale wasiotaka.
 
Wakishajiengua wanaenda kunzisha nini? Mkuu unachosema ni kama vile kusema mtoto wa nyoka hawezi kuwa nyoka bali anakuwa mjusi
labda unijuze tofauti ya dhehebu na kanisa.labdavtuanzie hapo ndo tutapata jibu.
 
kuhusu lutheran mm nnavojua luther hakuanzisha km kanisa na kulipa jina hilo rasmi.nnachojua alianzisha vuguvugu na akajitenga.baadavya yy kufa walofuata msimamo wake ndo wakajiita walutheli yaani wafuata msimamo wa luther,luther hakuliita kundi lake hivo.walobaki baada ya yy kufa ndo walijiita hivo.
anaejua zaidi ya hayo anisahihishe

Jina lake siyo muhimu ila kinachofuatwa ni msimamo wa kile alichokuwa anakipinga dhidi ya Kanisa Katoliki:

The Ninety-Five Theses on the Power and Efficacy of Indulgences .

(Disputatio pro declaratione virtutis indulgentiarum)

Hajaanzisha kanisa lingine ila mwaka 1517, kachapisha kwa Kilatini "theses 95", moja wapo ni ya kupinga Papa kuwa na uwezo wa kufuta madhambi ya muumini, wakati huo, kwa kulipa fedha. Yaani, unanunua hati ya kusamehewa madhambi yako duniani.

Wale wanaofuata msimamo huo wa kupinga Theses 95 alizozibandika katika mlango wa kanisa la chuo chake ndiyo wanaitwa "Lutherans", kama wale wanaofuata msimamo wa siasa za Mao wa China wanaitwa "Maoists" na wa Lenin wa Urusi, wanaitwa "Leninists".
 
Back
Top Bottom