Majina ya wanaCCM waliochukua fomu za Uspika

Kwa maoni yangu sababu zaweza kuwa;

1. Pamoja na uhuru uliotolewa ktk katiba bado umeacha mwanya mkubwa wa kukipa hadhi kiti cha Spika kwa vigezo/sifa za ziada mfano, kiwango cha elimu na nyanja ya ubebezi, umri, na uzoefu nk.

2. Kushushwa hadhi ya kiti chenyewe na Spika aliye jiuzulu hivyo Kila mtu kuona anao uwezo wa kuliongoza bunge maana alionekana nyakati nyingi akishindwa kufuata kanuni na kuwa kama mazoea.

3. Katika chama (ccm) inaonekana sasa ni fursa yao ya kuneemeka kwa kukusanya fedha nyingi kwa viongozi walio ktk idara ya siasa na uenezi na hii si kwamba ni demokrasia kama wanavyotaka kuhadaa watu maana ktk mchakato ndani ya chama wengi watakatwa bila kupiga kura wala maelezo ili kupata wawili/watatu wa kuzugia tu. Ndiyo maana inapigiwa promo sana ili wakachukue wengi na baadae watapigia debe kwa kuteleza kuwa huku chama kina hazina ya viongozi.

4. Baadhi ya vijana wapya wa ccm na wale waliosahaulika ktk teuzi mbalimbali wanatumia fursa hii kujitambulisha wakidhani kuwa kamati kuu/ halmashauri zitajisumbua kuwajadili jambo ambalo halipo maana tayari mteule wa kiti alishajadiliwa na kupitishwa hizi zilizobaki ni sanaa za kiitifaki tu.
 
Tulia anafaa kwani ameshapata uzoefu
 
Ni aibu , hebu waweke mavyeti yanayohitajika ili uweze kuwa spika au ni sawa na ubunge hata ukiwa zuzu unakubalika ?
 
Washaingiza kama million57 za haraka haraka...

Wameruhusiwa kula ila wasivimbiwe...
 
Mwenda. Burton Mwenda alias Mwijaku
Ila jamani watanzania kupitia zoezi hili la kujaza nafasi ya uspika, tumeonesha jinsi tusivyokuwa serious na mambo yetu. Nafasi muhimu kama ya spika inafanyiwa utani wa kiwango kile, kupitia tukio hili ni dhahiri kuwa:

1. Mambo yetu mengi ya kitaaluma mtindo ni huu huu....... tunazalisha wasomi kwa vyeti lakini practically hamna wasomi
2. Uchumi wetu ni hoi, mbali na natuaral resources endowments zote tulizonazo...... tunaendelea kupambana na madawati na vyoo karne ya 21
3. Siasa zetu ni jokes, tuna sheria ya vyama vingi lakini nchi inaongozwa na chama kimoja miaka yote na opposition imejifia na haiwezi kujenga hoja
 
Utitili huu unaonyesha ni jinsi gani hadhi ya Bunge letu imeshuka na hasa kiti cha Speaker. Hivi kweli hata kama tuna demokrasia..watu zaidi ya 50 toka Chama kimoja wanaomba ridhaa ya kupendekezwa kugombea nafasi ya Speaker? Hii inaonyesha pia Chama husika kukosa mikakati ya kutengeneza viongozi na kujidhalaurisha.

Je Wanachama hao walio chukua form hawajui vigezo, sifa na uzoefu wa Kazi ya Speaker? Kwa kweli hii ni kuifanya nafasi ya Speaker ionekane ni very cheap na ni sehemu ya Ulaji, hasa ukizingatia mafao yaliyowekwa kwa nafasi hiyo akiwa kazini na akistaafu.

Labda ingalau kuwa na Bunge litakalo anza kujitambua, achaguliwe Speaker toka Chama cha Upinzani...na wapiga kula wenyewe ambao ni wengi ni kutoka chama kimoja, onyesheni mabadiliko kama wawakilishi wa wananchi. Msifuate Siasa za Uchama Bungeni, fuateni Siasa za maendeleo ya Watanzania kwa ujumla wake.
 
Kwenye hiyo list yako sijaona jina la Dr. Kasheku mzee wa wediwide open free viza.....
 
Mlinga na Mwijaku sasa huu ni utani, hawa wameionaje hii position ya Speaker? Hatari sana.
 
Jibu ni lahisi sana, Ajira na mafao kedekede wakistaafu... ndio hilo tu ingawaje wanasisitza wengine wajiajiri ili hali wote hao wanataka waajiliwe na bunge...
 
Kampuni kama Ferrari au Lamborghini wana uwezo wa kutengeneza magari ya kumuuzia kila multi millionaire duniani.

Lakini kulinda brand zao ata model ambazo ni nyingi azizidi 9000 na hiyo unakuta kwa mwaka walikuwa wakitengeneza 1000 tu kusambaza duniani.

Kuna model zingine magari ayafiki 20 duniani na production imesimama bei ya gari $4.5 million na kuna watu duniani hiyo sio hela ya kuwanyima usingizi; lakini wakizitaka awapati. Brand protection ni muhimu.

Mradi katiba imesema speaker sio lazima awe mmbunge bali mtu mwenye sifa za kuwa mmbunge; achilia mbali hao kina Mwijaku bali kila mmbunge, msomi na mfanyakazi wa serikali anadhani anayo sifa ya kuwa mmbunge.

Nchi zilizoendelea ata kama na wao takwa la kikatiba kama letu, sahau kuwa speaker if you are not a seasoned house member.

Hata USA na U.K kumbe kikatiba kugombea nafasi za leader of their houses sio lazima uwe member; lakini tokea kuanzishwa kwa nyumba zao aijawahi tokea leader kutokuwa member of the house. Sasa tujiulize hizo houses zina miaka mingapi.

Na hizo nchi sio kwamba zinawasomi wa sheria waliobobea bali zinawahusika walioshape legal thinking duniani.

Leo kuna constitutional lawyers huko wameajiriwa ndani ya vyama vya siasa wanajua kanuni za kuendesha bunge na administration law za nchi yao kushinda house member yeyote, leave alone outsiders. Lakini wanajua leader of the house traditionally ni nafasi za seasoned house members.

CCM mnaaribu nchi na kushusha viwango vya hadhi ya nafasi muhimu serikalini. Kuna watu walitakiwa ata kuchukua form za speaker waogope kwa ukubwa wa nafasi yenyewe.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…