Major Claude NDIKUMANA wa jeshi la Burundi, akamatwa akiwa mzima na M23 huko Kivu kusini

Inafikirisha sana. Yan M23 wanaweza kuwa na utu kiasi hicho kwa mtu ambaye ni adui yao? Hatima yake itakuwaje? manake sijawahi sikia kama M23 wanachukuaga POWs.
 
Kwahiyo baada ya mkuu kupigwa risasi ya mguu walinzi wakaamua kuokoa maisha yao na kutokomea kusikojulikana.

Hawa M23 ni moto wa kuotea mbali ukienda kichwa kichwa unarudishwa kwenu bendera iko juu ya jeneza
Mpaka sasa watu wanajua wanapigana na M23 kwa shinikizo la uongozi wao tu, lakini ukweli wanaujua kuwa si mgambo. Kila mmoja lazima ajiokoe. Lakini pia, kumbuka. Kwenye kurushiana risasi, haiwezekani walinzi wote wakakimbia, pengine na adversary lazima apoteze. Huyo ni mtu mkubwa jeshini ujue
 
Unefafanua vyema mkuu. Sasa imeeleweka.
 
Inafikirisha sana. Yan M23 wanaweza kuwa na utu kiasi hicho kwa mtu ambaye ni adui yao? Hatima yake itakuwaje? manake sijawahi sikia kama M23 wanachukuaga POWs.
Kumbuka hawa wanahitaji attention ya ulimwengu mzima. Wasipotumia akili ya ziada wameisha. Pili, ukiachilia mbali hawa. Wanajeshi wa SAMIDRC waliokamatwa mateka, M23 imekuwa ikiwahudumia, japo na serikali zao kwa sasa zina budget kwa ajili yao. Mara mbili, jitihada za kuwanasua ziligonga mwamba. Na bado wanaishi vizuri tu.
 
Major anavaa gunboots πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€
Sasa kinacho washangaza ni nini? Jeshini kuna mgao hadi wa gumboots, kuna mazingira hayafai kuvaa buti za kawaida
 
Ina mana M23 wanayo mindombinu (infrastructure) kwa ajili ya kuwahifadhi mateka wa kivita au
 
Nionavyo mimi hapa tunarushiwa madongo. Hebu cheki majibu ayatoayo mleta mada utagundua kitu.
Wala usisite kuuliza mkuu. Ninalolijua ntajibu, nisilolijua ntasema sijui, ninalo na shaka nalo, ntahakikisha nakutafutia taarifa za uhakika kwanza.
 
Mmmh! Mkuu; Hizo gum-boots walimsaidia kuzisafisha matope halafu wakampa nafasi ya kuoga na kuvaa kombati safi kabla ya kumpiga picha? Aisee mbona mnatulisha matango pori??
Ni kawaida mateka kupewa matunzo mazuri hasa akiwa na faida
 
Ina mana M23 wanayo mindombinu (infrastructure) kwa ajili ya kuwahifadhi mateka wa kivita au
Mkuu, M23 unayoambiwa ni waasi, ni tofauti na uijuayo.

-Nimesema hapo juu, lazima iwazibe watu midomo. Ikikamata na kuua, kuna uwezekano wa kutumiwa wanaoizidi uwezo. Hivyo lazima ihakikishe watu wanaiamini. Ukilinganisha na miaka au siku za nyuma, sasa hivi utasikia wasitishe mapigano, hakuna aliyewahi kuomba waachie maeneo waliyokwisha twaa.

Hivyo sasa, hawa wakikamatwa, usafiri upo wa uhakika, ni Bukavu mjini(kwa Kivu kusini), au Goma, huko Kivu kaskazini. Huduma za afya huko zinaendelea, na hospitali za jeshi kwenye kambi zinatoa huduma kama kawaida.
 
Sasa kinacho washangaza ni nini? Jeshini kuna mgao hadi wa gumboots, kuna mazingira hayafai kuvaa buti za kawaida
Buti za jeshini sio sawa na zile za machinga japokuwa zaweza kufanana maumbile. Za jeshi huwa na design/mabaka-mabaka kama zilivyo kombati zao au ni za ngozi sio plastiki.
 
Ni kawaida mateka kupewa matunzo mazuri hasa akiwa na faida
Hata asipokuwa na faida mkuu. Kumbuka M23 ni tishio ukanda wa wasio na uwezo, lakini wale wazee wa mbali wakisema waingie, hana ubavu huo. Ndio maana inahakikisha ulimwengu utambue kuwa lengo lake siyo kuua. Na wewe ukijua watu wako wanapata huduma kama binadamu wengine, huwezi kuwa na attention kubwa. Mfano hai, hata South Africa bungeni, walisema wanaishukuru M23 kwa moyo wa huruma dhidi ya wanajeshi wake, ambao waliua wenzao, lakini inawahudumia.
 
Waw! Kumbe M23 wamejipanga. Hivi mkuu; itakuwaje ile deal ya DRC na Marekani wakianza utekelezaji??
 
Buti za jeshini sio sawa na zile za machinga japokuwa zaweza kufanana maumbile. Za jeshi huwa na design/mabaka-mabaka kama zilivyo kombati zao au ni za ngozi sio plastiki.
Hapana hakuna gunboots za ngozi..
okwi BOBAN SUNZU muelekeze huyu jamaa
 
Waw! Kumbe M23 wamejipanga. Hivi mkuu; itakuwaje ile deal ya DRC na Marekani wakianza utekelezaji??
Haiwezekani.

Na ikitokea imewezekana,

Maji na mafuta vitakuwa tayari vimeshakaa kila kimoja mahara pake.
Toka jana, ofisi ya raisi wa Angola, mpatanishi katika maswala ya mzozo wa DRC, ilitangaza kuwa rais wa DRC sasa yupo tayari kuzungumza na M23.
Ili jambo hilo lifanyike, ni kwamba plans zote za nje zinatakiwa zisitishwe, wanajeshi hao wa nchi mbali mbali, kwanza watoke( Hapa nisiende mbali, kama yeye sasa ndo anaomba mazungumzo na M23, subiri tuone orodha ya matakwa ya M23 ili ikae nae).

Kingine, kuwa rais hakumpi mamlaka ya kuuza nchi. Nchi haongozi raisi peke yake, ana kamati zake za ushauli. Hivyo wote hao hawawezi kuridhia kitu kama hicho, huku wanajua anaenufaika ni nani.

Na mbaya zaidi,kumbuka kuna wachina kwa makubaliano, Canada kwa makubaliano,USA kwa makubaliano(si kwamba hawapo). Russia ndo hivo. Hawa watu wote ukitaka wakae sehemu moja unategemea nini?

Tena kumbuka,DRC ina watu wana hela chafu. Na kwa sasa,M23 imekuwa na influence kubwa sana. Ukiangalia vitu vinavyoendelea kwenye maeneo yake,na ukiambiwa ni pesa za Congo, hawawezi kukubali michezo ya hivyo.

Matajiri hao,na wenyewe wana uwezo wa kuendesha migodi.
Kilichopo,huko Katanga, ni km60 tu kutoka ilipofika M23. Ndipo kuna mgodi wake. Je,anauachia hivi hivi uende? Japo haimaanishi atauendeleza! Ndo maana hapa subiri wazungumze ndo utajua inakuwaje.
Kumbuka tu kuwa wasaliti wa ile serikali ni wengi sana. Iwe upande wa jeshi na upande wa siasa. Jama kwa sasa nguvu ya ndani hana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…