Makabila haya mtu ukifanikiwa jiandae kujaza ndugu tegemezi kwako ama kukuomba misaada kila mara, ukikataa unaonekana huna undugu

Umetokosea sana wanyakyusa tutoe hatustahili kukaa kwa hiyo list yako hapo.

Hiyo familia uliyoiona ukaifanyia research ni shida zao ila sio kigezo Cha kujumuisha wote.

Kwetu ni mwiko mkwe kwenda kwa mwanae pasipo SABABU maalumu.
Hizo mambo sanasana kwenye mikoa yenye njaa Green City chakula Cha kutosha kama wapo hata kwenye kabila zingine hawakosekani ila sio kutuweka kwenye kabila za kupiga camp kwa ndugu zao.
Mma nakamo!!!
NB: Angalia sifa za mkoa wa mbeya kijiografia na kiuchumi.
 
Umewasahau wasukuma, wazigua na wanyantuzu(hawa hata uwe na chumba kimoja, mjomba ake bibi yako naye atakuja kujibanza hapo hapo).
 
Hahahaa wewe Jamaa unazingua.

Samatta anaweza kumsaidia vipi mtu asajiliwe EPL au Genk?

Boeing, IMF, WB hakuna undugu kule unaingia kwa uwezo wako.
 
Katika hali ya kawaida inaweza kuwa kero kwako lakini katika jicho la kibinadamu na kama Mungu amekujaalia kipato basi jitahidi kuwasaidia ndugu zako katika namna ambayo hutawadhalilisha au kuwakwaza...........

Zipo namna nyingi za kuwasaidia ndugu bila kugombana au kukwazana nao....kila mmoja ana jinsi yake ya kuyaendea maisha na kutafakari mambo yake......Kuna baadhi ya watu akili zao zimechangamka katika kuziona fursa na kuzifanyia kazi....lakini pia wapo watu ambao akili hazifanyi kazi mpaka ziamshwe kwa matendo au matukio ni hali kawaida kimaumbile kwani hatuwezi kufanana..........

Kama Mungu amekunyooshea mambo yako na una nafasi ya kumsaidia ndugu yako au hata jamaa yako wa karibu usisite kufanya hivyo kwa namna yoyote Ile ambayo itamfaa.........

Kweli maisha ni magumu vipato vyetu Wakati mwingine havikidhi mahitaji yetu lakini haimaanishi kuwa tuwatupe ndugu zetu.........

Wapo watu ambao ni wachache wa fadhila na wapo watu ambao ni wenye kushukuru na kukumbuka fadhila.....hupaswi kuhangaishwa na hayo kwani moyo wa mtu ni kiza kinene fanya wema wako kwa kadri ya uwezo wako.......

Mafanikio na hali nzuri za maisha zisitupe viburi na jeuri na kuona kuwa hatuwahitaji.....huo ni upofu wa fikra na ubinafsi......maisha ni kutegemeana na kusaidiana kwani hakuna mwanadamu anayejitegemea kwa kila kitu........asio kufaa kwa hili basi atakufaa kwa lile.......

Tuufanye wema kama kiunganishi na tuukatae ubaya kama utenganishi......


Ukubwa au udogo wa Dunia inatokana na wewe unavyoishi na binadamu wenzio......
 
Hapo Kwa wazaramo naomba mlete mzungu aongeze sauti
 
Mkuu huwezi kuongea jambo bila uthibitisho

Sample yako ni ya watu wangapi uliyoitafiti?

Eneo lako la utafiti ni wapi na lina ukubwa gani

Umetumia methodolojia gani kwenye utafiti wako?

Ukishindwa kuyajibu maswali hayo baasi tutaconclude kwamba umeamua kuleta ugomvi wako binafsi na mkeo kwenye mitandao ya kijamii sisi hautuhusu

Umefanya "over generalization'
 
Sio tabia ya wabena . Wabena umetuonea
 
Pogoro kabila la hovyo sana, kwenye ngoma kaka na dada wanagongana tu, na kwenye chakula /Kitoweo hawachagui, nyani, sokwe, yote twende
Sasa Kama kwa ndugu sio wachoyo na kwa watu Baki je? Sindio wanakigawa bure bure?
 
Pole
Pole ndg mpogoro, but sio wote ila wengiwao!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…