Kuna aina ya kwanza ya makabila wana umoja lakini sio umoja wa kuwa tegemezi kama wachaga, wakinga, wakuria, n.k yaani kama wewe ni mgeni ukienda kwa ndugu utapokelewa vizuri tu lakini itabidi uwe umeshaweka ujio wako, ratiba yako ikoje, upo mpaka lini, mipango yako, n.k. kama ni kusalimiana ni sawa kukaa hata wiki 2 ila baada ya hapo unarudi kwenye shughuli zako, sahau kuweka kambi hapo ya kudumu. kama huna shughuli na umefika hapo labda muwe mshaelewana mwenyeji wako atakusaidia mtaji na kukuzoesha mazingira ya hapo ili nawe uanze kujitegemea uwe na pako.
Kuna aina ya pili ya makabila Ukiachana na yale makabila ambayo ni mengi ambayo hayataki kabisa ndugu kqenda kuwasalimia haga tutayazungumzia siku nyingine na haya na
Ila kuna hii aina ya tatu ya makabila, yaani mmoja akipata ajira na awe na makazi hasa nje ya mikoa waliyoyokea basi wenzake watamfata kwenda kujazana kwake... Na hii pia inahusika ukioa makabila ya aina haya basi utegemee ndugu wa mkeo kujazana hapo kwako. yani mashangazi, wajomba, watoto wa baba mkubwa, mawifi, mashemeji, n.k kati yao hawakosi hapo si chini ya nne wote wanaenda kwa mji wa mtu wao kwenda kuishi huko huko kwa mda mrefu... wanakula na kulala hapo kisa eti wamesikia anafanya benki.[emoji28][emoji28] hii kitu inafanya mtu ashindwe kujikwamua kiuchumi yaani mtu mshahara laki7 au laki 5 mnamgandaa hivyo hawezi tobo.
kwa wachagga wengi huu utaratibu amna.
Makabila haya kwangu niliyoyaona ni kama.
-Wanyakyusa
-Wazaramo
-wasambaa
-wasukuma
-Wabena
-wanyamwezi
-waha
Kuna ile kujifich nyuma ya kivuli cha undugu lakini inakuwa inazidi sasa, mtu hata maendeleo yanashuka