Makabila haya mtu ukifanikiwa jiandae kujaza ndugu tegemezi kwako ama kukuomba misaada kila mara, ukikataa unaonekana huna undugu

Me pia ni miongoni Mwa familia za aina hizo na sijawahi kujutia. Ndo asili yetu wa africa inasaidia Sana kuongeza Upendo, kutambuana, maadili na kudumisha umoja.

Sisi haturuhusu mtu ambae hana kazi ila kwa kuishi pamoja mwezi 1 au 2 ukiwa una seti mambo yako ni k2 cha kawaida. Napenda sana mfumo huo na ndo mana napenda kusaidia watu na kuishi nao
 
Hahahaha [emoji1787]

Ulimtembelea muhaya nini ukapewa za uso?
 
Duh Mimi Naona wasukuma walipaswa kuwa Namba moja, ukioo msukuma umeoa ukoo, watch out
 
Dah wabongo ni wapuuzi sana.huu pia ni uzi?? Au ubaguzi kwani mtu kuishi kwa shemeji au ndugu kuna tatizo gani.????? Mbona watu wanaishi kwa marafiki iweje ndugu iwe kero ?? Mimi nimeishi katika extended family na tumeishi poa tu.wabongo tuwe na tabia ya kubebana wazeee.nimekaa nchi flani jamaa kitoka nchi nyingine wanabebana ile mbaya wanapeana michongo ila wabongo tilikuwa tunakimbiana tunaishi kwa kuogopana kila mtu anamuona mwenzie mtu mbad.Na baya yote yanasababishwa na ulimbukeni na uchoyo.mtu anataka aishi mwenyewe tu na watoto wake.imagine umekufa watoto wako wanaishije na ww hutaki ndugu.????? Watanzania tuamke kiwekwa boarding schools sio ujinga watu tuishi pamoja humo.....yangu ni hayo salute kwa wanigeria ,rwanda ,burundi, mnapambana sana mnasaidiana
 
Hahahaa wewe Jamaa unazingua.

Samatta anaweza kumsaidia vipi mtu asajiliwe EPL au Genk?

Boeing, IMF, WB hakuna undugu kule unaingia kwa uwezo wako.
Huyo hapo dogo anaitwa kelvin Pius mtanzania kapelekwa na samata Genk,hao wengine wanachukiii halafu unakuta hata sio mfuatiliaji wa mpira
 
Mmmmmhhh!
Yaani kweli baby yaani mie nakwambia yaani??? heee! hao mbona bonge la mtaji hilo!!! wacha waje tu!! fungua bonge la shamba huko Mlandizi, waje

walime na kulisha mifugo!...kiti moto ni deal hapo mjini kwenu wacha waje tu!!

usiwanyime kula sababu hao watakula kwa jasho lao na wewe una faida juu!! ila wewe buni kazi za kufanya ..sidhani km kuna mtu atakuja kwako akubali kukaa tu wenzake wako shambani!

hata kiwanda kidogo tu cha kusindika makapi weye buni tu...fungua hata kampuni ya usafi amjumbani humo waende wao! au
 
Nilipoanza kuona invoice kutoka kwa ndugu wa upande wa baba zinakuwa nyingi, nilijifanya nina maisha magumu hatare! Simu zao zikakata.
Kama kuna mjomba au shangazi hakuwahi kunitumia hata sh elfu mbili wakati nasoma, nimesema asinijue kwenye uzee wake. Shida zake apelekee waliokula mshahara wake!
 
Hii nzuri
 
Wagogo mbona umewaacha? kama mkeo au mume mgogo muwe na kashughuri kadogo watakuja ukoo mzima bila kujali watalala wapi inanishangazaga sana.
 
Unacho we saidia, mali zenyewe ni za mpito, tutaziacha duniani hapa hapa, tenda wema na wala usitegemee malipo toka kwao wakikubadilika utaumia saana nafsi.

Mimi nakuwa kwetu familia ilikuwa ni kubwa kinyaaama, na sio kwamba mama yangu alikuwa na senti saana, la hasha maidha ya kawaiida mnooo watoto wa shangazi, watoto wa mjomba, sijui mama mkubwa, mama mdogo, wengine wazee wao wako hai, wengine umauti ushawafika, mama yangu akawachukua na kuwalea, kikipikwa chakula ni jungu kuu lisilokosa ukoko😂, si chini ya watoto 15 wamepita kwenye mikono ya mama yamgu mzazi, abarikiwe saana kwa roho ile, kila nikitazama ndugu zake sidhani kama wangeweza kutulea sisi. Wengine wamekuwa hata kumkumbuka kwa kumjulia hali hawafanyi hivyo..
 
Umenikumbusha, kuna mzee wa rafiki yangu, wao ni wale wa zee wa mapanga shaaa(wakurya)

Yupo mjini hapa kitambo, hela ya mboga haimpigi chenga, basi akaja mdogo wake kumtembelea, kama mwezi na ushehe vipi bila kuondoka, mara ikaja familia yake(mke na watoto wa mdogo wake)
Yule mzee akawasikilizia tena kama wiki 2 hivi, kilichofata akamtafutia mdogo wake chumba cha miezi 6, akamlipia, hapo atajijua akitaka kuendelea kukaa dar basi ataongeza kodi yakimshinda atarudi UKURYANI 😂
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…