Makabila yanayopatikana Morogoro na wilaya yanakopatikana

Makabila yanayopatikana Morogoro na wilaya yanakopatikana

Shukrani mkuu kwa nyongeza, wangindo wanapatikana Kilosa. Hivi kuna tofauti Kati ya Wabena na Wabena manga? Nadhani kiuhalisia moro inatakiwa kuwa namba moja kwa kuwa na MAKABILA mengi
Kiuhalisia nyingi ni Kama koo. Mfano wandwewe wana ukaribu na Wangoni. Hali kadhalika Wabenamanga na Wabena.
 
Morogoro geographically ndio mkoa unao pakana na mikoa mingi Tanzania,Ruvuma,Iringa,Pwani,Tanga na Lindi
 
Shukrani mkuu kwa nyongeza, wangindo wanapatikana Kilosa. Hivi kuna tofauti Kati ya Wabena na Wabena manga? Nadhani kiuhalisia moro inatakiwa kuwa namba moja kwa kuwa na MAKABILA mengi
Wabena manga ndio Waluguru. Wabena, Kinga na Wahehe ndio wamezaa Waluguru. Kwa Mfano Majina kama Luvanda ni Kibena lakini Kiluguru ni Luwanda, Kibiki ni Mbiki Kiluguru, Mwenda kibena na Mwenda Kiluguru, Mabena kibena na Mbena au Kibena Kiluguru, Mgera Kibena na Mgera Kiluguru, Mzeru Kihehe na Mzeru Kiluguru, Anofu Kibena na Anogha. Kisaki Kinga na Kisaki Kiluguru, Fungo Kinga na Fungo Kiluguru. Kwahiyo Waluguru ni Wabena waliopotea. Wakaguru ni Mchanganyiko wa Waluguru na Wagogo. Wapogoro ni Mchanganyiko wa Waluguru na Wandendeule wa Namtumbo Songea.
 
Morogoro ni mkoa mojawapo wenye MAKABILA mengi hapa nchini. Zifuatazo ni wilaya na MAKABILA yake

1. Halmashauri ya Morogoro: hii wilaya maarufu kama Morogoro Vijijini, makabila yanayopatikana ni; Waluguru, Wakwere, Wakutu, na Wazaramo

2. Morogoro Mjini: hapa wenyeji ni Waluguru.

3. Wilaya ya Kilosa: Wenyeji hapa ni Waluguru, Wakaguru, Wasagara, na Wazigua japo sio wengi, Wavidunda,

4. Mvomero: Waluguru, Wazigua (Wazigua wanapatikana kwa wingi hasa Turiani), Wasagara.

5. Kilombero; Wanapatikana Wandamba, Wapogoro, Wambunga, Wabena ( wanapatikana eneo kunaitwa Mbingu Ifakara)

6. Ulanga; Wapogoro

7. Malinyi; wanapatika Wapogoro na Wandamba .

Kama kuna kabila nimelisahau nitashukuru mkinikumbusha...maana morogoro kuna makabila mengi na mengine sio maarufu sana. Ahsanteni
Kwa sasa na wasukuma nao wameingia huko Malinyi halafu Upande wa Ulanga kwenye maeneo kama Sali, Ruaha na Mwaya kuna hadi wangindo from Lindi.
 
Back
Top Bottom