MAKALA: Mambo muhimu ya kuzingatia kuhusu kodi kwa mtu anayeanza biashara

MAKALA: Mambo muhimu ya kuzingatia kuhusu kodi kwa mtu anayeanza biashara

Hapo kwenye kulipa kodi kabla sijaanza biashara,ndio panapoumiza sana kwa nini waniambie nilipe kiasi flani wakati sijajua kama ntauza au sitauza?
Unaambiwa kwa sababu zifuatazo
1. Maelezo yako ya msingi juu ya mauzo utakuwa umesema mauzo kwa mwaka akifanya hesabu yanazidi mil 4
2. Unatakiwa kulipa kodi kwa awamu nne, awamu ya kwanza utalipa ndani ya siku 90 toka kukadiriwa hvy bhasi km biaahara sio una haki ya kurudi TRA kujaza fomu ya marekebisho lkn ile awamu ya kwanza uilipe
3. Kuanza biashara ni mchakato, hvy bhasi ina maana tyr umeshajipanga. Vinginevyo omba TIN isiyo ya biashara
 
MKUU, Utaratbu wa kulipia hiyo witholding Tax (kodi ya zuio) na ushuru wa stempu, inakuwaje ikiwa jengo ni la kwangu na sikupanga?
 
Mkuu Mr coffee
1. Ieleweke wazi kuwa malipo ya kodi hayana uhusiano na mtaji wako bali mauzo (kwa biashara ndogo) au faida yako (biashara kubwa)

2. Changamoto kubwa iliyopo ni "lugha ya biashara" kwa tuliowengi hatuwezi au hatuielewi vema. Ipo wazi kabisa kuwa mauzo chini ya mil 4 kwa mwaka hutakiwi kulipa kodi. Tatizo linakuja ktk mahojiano na yule anaekukadiria kodi kwn maswali anayokuuliza juu ya mauzo na ww maelezo unayotoa juu ya biashara yako akifanya hesabu zinazidi zaidi ya mil 4 kimauzo UTAKAPOKUJA ANZA KUFANYA BIASHARA. Hivyo unalipa kama malipo ya awali 'advance payment' ambayo una haki ya kutoa maelezo au kuirekebisha baadae kama mambo hayapo sawa
Shukrani ndg.
 
MKUU, Utaratbu wa kulipia hiyo witholding Tax (kodi ya zuio) na ushuru wa stempu, inakuwaje ikiwa jengo ni la kwangu na sikupanga?
Iwapo jengo ni la kwako utalipa kodi ya jengo ambayo ulishakadiriwa na manispaa yako husika. Malipo kwa nyumba nyingi za kawaida ni kuanzia elfu Tsh 10,000 kwa mwaka. Hivyo hautalipa kodi ya zuio wala ushuru wa stempu
 
MAKALA: SEHEMU YA KWANZA
Habari zenu wanajukwaa
1. Utangulizi
makala hii inahusu masuala ya kodi kwa wanaoanza biashara lakini vilevile itagusa sheria na biashara kwa ujumla wake. lengo ni kuzidi kuelimishana kwa wasiofahamu na vilevile kukumbushana kwa wenye ufahamu na kuongezeana elimu kwa michango mbalimbali itakayoletwa kutoka kwa wanajukwaa.
2. Biashara na aina zake
Biashara ni kununua na kuuza, kuzalisha mali na kuuza, utaalmu, wito na makubaliano ya kipekee yenye nia ya kupata faida kwa kifupi ili nisiwachoshe.
kwa mujibu wa Sera ya Taifa ya mwaka 2003 ya kuendeleza wajasiriamali wadogo, wa kati na wakubwa, biashara zimegawanyika katika makundi manne:
1. Biashara ndogo sana
Ina idadi ya waajiriwa kuanzia mmoja hadi wanne, na Mtaji wake ni kuanzia Sh 1 hadi 5mil

2. Biashara ndogo
Ina idadi ya waajiriwa 5 hadi 49, na mtaji wake ni kuanzia mil5 hadi mil 200

3. Biashara za kati
Ina idadi ya waajiriwa 50 hadi 99 na mtaji ni kati ya mil 200 hadi mil 800

4. Biashara Kubwa
Ina idadi ya waajiriwa zaidi ya 100 na mtaji zaidi ya mil 800.

Vingezo vingine vinavyotumika na Mamlaka ya Mapato kuweka madaraja ya walipa kodi ni kulingana na kiasi cha mauzo kwa mwaka au kiasi cha kodi kinacholipwa kwa mwaka

3. SHERIA ZA KODI
Shera hizi zinamgusa anaeanza biashara:
1. Sheria ya kodi ya mapato ya mwaka 2004
2. sheria ya kodi ya Ongezeko la thmani (VAT) ya mwaka 2014 kwa anefuzu kusajiliwa
3. Sheria ya ushuru wa stempu ya mwaka 1972
4. sheria ya usimamizi wa kodi ya mwaka 2015
Sheria hizi zinasimamiwa na Mamlaka ya Mapato (TRA) kupitia kodi za ndani

A: Sheria ya Kodi ya Mapato
Kodi ya mapato hutozwa kwa mtu ambaye mapto yake yanatokana na vyanzo mbalimbali km vilivyoainishwa ktk sheria kama vile
a) Biashara yoyote na kwa muda wowote inapofanyika
b) Ajira yoyote afanyayo mtu
c) Uwekezaji ktk rasilimali. Mfano nyumba, ardhi na hisa
d) Vyanzo vinginevyo vya mapato vya kutozwa kodi ya zuio "Final Withholding Tax. Mf: Kodi ya malipo ya pango, malipo ya gawio kutoka ktk kampuni kwa Mtz, Riba itokanayo na benki na malipo kutokana na maliasili (mrahaba)

B: Mapato yatokanayo na biashara
kwa mujibu wa sheria ya kodi ya mapato ya mwaka 2004 ikarejewa mwaka 2006, Mapato yanayotozwa kodi kutokana na biashara ni Faida au Ziada itokanayo na biashara kwa mwaka wa mapato. Mapato hayo ni pamoja na:
1. Faida kutokana na mauzo ya bidhaa au huduma za biashara
2. Malipo anayolipwa mfanyabiashara kwa masharti ya kufanya au kutofanya biashara kulingana na makubaliano ya upande wa pili
3. Zawadi au Takrima anazolipwa mfanyabiashara kutokana na shughuli zake za biashara
4. Kiasi cha mapatoyanayohusiana na biashara ambayo vinginevo yangekuwa mapato ya uwekezaji ktk rasilimali kwa mtu anayefanya biashara ya kupangisha nyumba`

Inaendelea.......
B: Taratibu za kufuatwa na mtu anaeanza biashara kupata namba ya utambulisho wa mlipa kodi (TIN) pamoja na malipo ya kodi na mengineyo:

Mtu anaeanza biashara atatakiwa kuomba TIN kutoka TRA ambapo vielelezo hv vitahitajika
1. Fomu za maombi ya TIN kwa mtu binafsi (zinatolewa TRA)
2. Barua ya utambulisho wa Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa (hutolewa na TRA)
3. Mkataba wa pango kwa aliepanga eneo la biashara au kielelzo cha umiliki wa eneo la biashara kama hati, ofa au karatasi za malipo ya kodi ya majengo
4. Kopi ya kitambulisho cha Taifa, Leseni ya udreva, paspoti ya kusafiria au kitambulisho cha kupigia kura
5. Picha ndogo ya paspoti saizi

Mhusika utaulizwa juu ya biashara yako "business assessment". baada ya hapo utaambiwa kiasi cha kodi utakayostahili kulipa kutokana na mauzo ya biashara unayofanya au unayotarajia kuifanya. baada ya maelezo haya taratibu nyingine zitaendele na hatimaye utapata TIN.
Kwa leo naomba tuishie hapa sehemu ya kwanza kutokana na majukumu. Tutaendelea sehemu ya pili
Matarajio ni kuwa wengi wetu tutaisoma makala hii na kuelewa vizuri kwani inawezekana kuwa malalamiko mengi hutokana na wafanyabiashara au/na wanaofikiria kufanya biashara kutoelewa vizuri sheria na kanuni.
 
Mkuu kwaiyo risiti isiyo ya efd inahusisha hadi biashara zenye mauzo ya million 4?
 
Mkuu kwaiyo risiti isiyo ya efd inahusisha hadi biashara zenye mauzo ya million 4?
Nakushauri usome makala imeelezea vema sana suala la EFD usione uvivu
Ila kwa kifupi tu ni kuwa biashara yyt inayofikisha mauzo ZAIDI YA MIL 14 KWA MWAKA unatakiwa kutoa risiti za kielektroniki ie EFD receipts. Hivyo biashara yenye mauzo chini ya mil 14 hustahili kutoa risiti za kielektroniki bali UTOE RISITI YA KUANDIKWA KWA MKONO ambayo itaonesha TIN yako, Jina lako na bidhaa na bei pia
 
Unaambiwa kwa sababu zifuatazo
1. Maelezo yako ya msingi juu ya mauzo utakuwa umesema mauzo kwa mwaka akifanya hesabu yanazidi mil 4
2. Unatakiwa kulipa kodi kwa awamu nne, awamu ya kwanza utalipa ndani ya siku 90 toka kukadiriwa hvy bhasi km biaahara sio una haki ya kurudi TRA kujaza fomu ya marekebisho lkn ile awamu ya kwanza uilipe
3. Kuanza biashara ni mchakato, hvy bhasi ina maana tyr umeshajipanga. Vinginevyo omba TIN isiyo ya biashara
TIN isiyo ya biashara ndo ipoje? Unakua hulipii chochote baada ya kupewa TIN ama?
 
TIN isiyo ya biashara ndo ipoje? Unakua hulipii chochote baada ya kupewa TIN ama?
Ni TIN isiyohusiana na masuala ya biashara.
Mifano:
1. TIN ya kuombea leseni ya udreva
2. TIN ya kulipia kodi ya jengo

Kwa mfano unapotaka leseni ya udreva, utapata hy Non-Business TIN. Itakusaidia kulipa ze kodi stahiki tu kwa mfano unapoomba au ku- 'renew' leseni ya udreva utalipia. Ukitaka kuanza biashara unatoa taarifa inabadilika inakuwa business TIN hivyo utalipa kodi ya mapato kama kawa!
 
Ni TIN isiyohusiana na masuala ya biashara.
Mifano:
1. TIN ya kuombea leseni ya udreva
2. TIN ya kulipia kodi ya jengo

Kwa mfano unapotaka leseni ya udreva, utapata hy Non-Business TIN. Itakusaidia kulipa ze kodi stahiki tu kwa mfano unapoomba au ku- 'renew' leseni ya udreva utalipia. Ukitaka kuanza biashara unatoa taarifa inabadilika inakuwa business TIN hivyo utalipa kodi ya mapato kama kawa!
Nimekupata mkuu,ubarikiwe sana
 
asante kwa somo zuri, naomba ufafanuz jinsi ya kupata TIN TRA kwa kundi la kampuni, taasisi . na hiyo kodi inayokatwa kwa kampuni kutokana na faida inakatwa kwenye gross profit au net profit
Asante Mkuu Laki Si Pesa
Tukirejea katika swali lako la kuhutaji mwongozo wa kupata TIN kwa upande wa kampuni, taasisi nk. Hili limegawanyika kutokana na 'legal entity' ya taasisi/kampuni husika.

A: Kampuni yenye ukomo wa shea ie limited company
Kupata TIN ya kampuni yenye ukomo utaanda vielelezo vifuatavyo:
1. MEMARTS ithibitishe kwa mwanasheria/mahakamani
2. Cheti cha Usajili ie Certificate of Incorporation vema ukithibitisha kwa mwanasheria/mahakama japo kwa sasa mfumo wa usajili wa BRELA na TRA kwa kampuni umeunganishwa hivyo namba ya usajili ya Cheti ndiyo itakuwa namba ya TIN ya kampuni na maelezo yanatumwa TRA pia ukisajili
3. TIN za wanahisa/wamiliki wote wa kampuni
4. Mkataba wa kisheria wa pango
5. Uwepo japo Mkurugenzi mmojawapo wa kampuni hii ni lazima
6. Barua ya utambulisho toka kwa Afisa Mtendaji(barua hii hutolewa na TRA)
7. Fomu za maombi ya kufungua TIN ya kampuni (hutolewa TRA)
8. Fomu za kujaza kwa ajili ya TIN ya kila mwanahisa (hutolewa TRA)
9. Fomu ya makadirio ya kodi kwa ajili ya kampuni (hutolewa TRA)
10. Kama una mshauri wa kodi/mkaguzi wa mahesabu/?mwanasheria(jambo jema hili) andika barua ya kum-'appoint' kwn kadhia zozote watahusika wao kwa niaba ya kampuni yako. Vlvl ndani ya fomu za maombi ya TIN kuna jedwali huonyesha kama unao ujaze maelezo yao kama jina, TIN. Barua hii lazima uliomu'appoint' asaini na mhuri agonge kuonyesha amekubali
11. Passport size ya kila mwanahisa
12. Mnaweza mkaweka na 'Resolution letter' (tafsiri isiyo rasmi barua kuu ya maelezo ya kampuni na kuridhia kwa bodi ya kampuni kufungua TIN. Pia barua hii inasaidia kuweka wazi mnaanza au mnafanya biashara gani kwn MEMARTS huwa na idafi kubwa ya biashara ambazi kampuni inazifanya na inatarajia kuzifanya hapo baadaye)

B: TIN ya ushirikiano "Partnership TIN"
Mahitaji yanafanana na ya mwanzo kwa baadhi ya mambo. Mahitaji yake ni
1. TIN ya kila mshiriki
2. Mkataba wa ushirikiano ie Partnership Deed
3. Mkataba wa kisheria wa pango
4. Fomu za maombi ya TIN kwa ushirikiano
5. Passport size 2 kwa kila mshiriki
6. Fomu ya makadirio ya kodi kwa ushirikiano
7. Na mengine km barua ya appointment ya tax/auditor/lawyer etc

N. K (hii mada ndefu kuweka kila taasisi na mahitaji yake). Naomba uridhike na hizi chache kwanza au uende moja kwa moja kwa taasisi unayotaka.

Tukirejea katika swali la pili juu ya kodi za kampuni:
Ikumbukwe taasisi na makampuni hutakiwa kulipa kodi kubwa 'corporate tax' ya 30% kutoka katika faida ghafi ie Operating Profit.
Faida hii hupatikana baada ya kuandaa mahesabu ya mizania kwa muda ulioona wafaa kwa wakati huo inaweza ikawa ndani ya miezi 6,12,14 lkn si miezi 24 kwa wakati mmoja etc etc kwani statement itaweka wazi hayo mahesabu ni ya muda gani. Hivyo bhasi baada ya kukokotoa mahesabu yako ya faida utatoa 30% ya kodi. Na kama umepata hasara bhasi hutalipa. Suala la namna gani uta'compansate' kodi ya makadirio uliyolipia itaoneshwa ndani ya mahesabu ya mizania
 
Mkuu, Naomba kuhuliza swali, JE kuna uwezekano wa kufuatilia leseni ya biashara kabla ya kupata TIN number kwa maana nilifika TRA kuanza hatua za awali za kupata Hiyo namba ya mlipa kodi lakini baada ya kukinzana kwa hoja kati yangu na bwana mmoja wa TRA ambaye alikuwa akinioji kuhusu biashara yangu,ambaye alilenga kunipa makadirio makubwa. Akaniambia nianze biashara, nitunze kumbukumbu then baada ya mwezi nirejee waangalie biashara yangu.

Je, ni naweza kupata leseni ya biashara?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu Mr coffee
Hautaweza kupata laseni ya biashara kabla ya kupata TIN kutoka TRA. Hii ni kwa sababu TIN ndiyo namba yako maalumu ya utambulisho wa mlipa kodi mosi, pili katika taratibu za kupata leseni ni lazima uambatanishe TIN na cheti cha mlipa kodi msafi ie Certificate of Tax Clearance hivyo utakosa cheti hiki pia. Na kubwa zaidi ktk mlolongo wa kuanza biashara au hata ukiwa huna biashara kuwa na TIN ni haki yako
Ushauri wangu
1. Ulitakiwa umsikilize huyo afisa wa kodi na kumshauri atembelee biashara yako
AU
2. Ukubali hayo makadirio, then ulipe awamu ya kwanza halafu uandike barua ya kuomba makadirio yarwjewe kwa kuwa ni makubwa kuliko kipato kinachozalishwa na biashara
ANGALIZO
Huyo afisa kusema ukaanze biashara halafu baada ya mwezi upeleke rekodi haijakaa sawa vinginevyo akuandikie barua rasmi kuwa huyu Mr coffee afanye biashara bila TIN then tutampa baada ya muda. Kwa sbb kama TRA wakipita utaonekana sio mlipa kodi. Watu wa manispaa leseni wakipita utaonekana we unafanya biashara bila kulipa ada ya leseni. Haya yote ni makosa kisheria ambayo utawajibika wewe mwenyewe

(Punguza ubishi[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]joking)
Mkuu, Naomba kuhuliza swali, JE kuna uwezekano wa kufuatilia leseni ya biashara kabla ya kupata TIN number kwa maana nilifika TRA kuanza hatua za awali za kupata Hiyo namba ya mlipa kodi lakini baada ya kukinzana kwa hoja kati yangu na bwana mmoja wa TRA ambaye alikuwa akinioji kuhusu biashara yangu,ambaye alilenga kunipa makadirio makubwa. Akaniambia nianze biashara, nitunze kumbukumbu then baada ya mwezi nirejee waangalie biashara yangu.

Je, ni naweza kupata leseni ya biashara?

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
[emoji23][emoji23][emoji23] Hawa maafisa ovyo sana eti ananidanganya na kuniona lofa sana, kwa kuniambia TRA wanachukua 800 Tsh ikiwa mtu anauza 15000tsh kwa siku ...
harafu aka malizia na neno tu! !!
Mbaya zaidi akajifanya anakorogakoroga mahesabu mengi ili nisimuelewe, mwisho wa siku ni kabakia pale pale ya kuwa makisio yake mengi kwangu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]hili kweli ttz maana wanajua kila mtu binafsi huwa haelewi masuala ya kodi na mahesabu. Ss akikutana na mwelewa ndo mvutano unapoanza kwa sbb yeye anatakiwa abaki na kusimamia sheria, kanuni na taratibu za kodi tu na sio maneno na vitisho vingi
[emoji23][emoji23][emoji23] Hawa maafisa ovyo sana eti ananidanganya na kuniona lofa sana, kwa kuniambia TRA wanachukua 800 Tsh ikiwa mtu anauza 15000tsh kwa siku ...
harafu aka malizia na neno tu! !!
Mbaya zaidi akajifanya anakorogakoroga mahesabu mengi ili nisimuelewe, mwisho wa siku ni kabakia pale pale ya kuwa makisio yake mengi kwangu.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom