MAKALA: Mambo muhimu ya kuzingatia kuhusu kodi kwa mtu anayeanza biashara

Asante

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Shukrani sana kwa somo nimependa sana kuelimishwa juu ya kodi maana watu hukwepa kulipa kodi kumbe wakati mwingine ni kukosa elimu juu ya ulipaji kodi.
 
Mkuu apo umeeleweka vema isipokuwa changamoto zipo njiani ukibeba mzigo wanataka efd receipt ata ukiwaambia mauzo ni chini ya 14 milion hawaelew
 
Mkuu apo umeeleweka vema isipokuwa changamoto zipo njiani ukibeba mzigo wanataka efd receipt ata ukiwaambia mauzo ni chini ya 14 milion hawaelew
Jambo unalotakiwa kufanya ni kuwapeleka kwenye duka ulilonunua mzigo. Na wao wakifika kwa mhusika alietoa risiti ambaye kwa mwaka anauza chini ya mil 14 wataona hali halisi na vlvl watafanya crosschecks zao kujiridhisha.
Lakini tambua mauzo ya mil 14 kwa mwaka ni kama 39,000 kwa siku (360 siku). Ss kwa duka lililopo mjini kidg hii inaleta ukakasi tuwe wakweli jamani. Kuna biashara ambazo hazina mauzo ya kila siku hili lawezekana lkn kwa biashara za mauzo ya kila siku mmh
 
Maswali yangu ni kama ifuatavyo....
1. Unaweza pata TIN ya biashara na makadirio yake kwa biashara ambayo unahitaji kufungua miezi sita ijayo? Nikimaanisha kodi ianze kuhesabiwa baada ya kuanza biashara ingawa TIN imeombwa miezi 6 nyuma?
2. Ili kupata leseni ya biashara halmashauri mfano biashara ya bucha unahitaji viambatanisho gani?
 
Naam Mkuu Trayvess Daniel
Nashukuru kwa maswali yako mazuri. Majibu ni hivi
1. Kulipa kodi wakati huu ili itumike wakati ujao
Unapoomba TIN ya biashara ina maana ya kwanza na inatafsirika umeshaanza biashara hata kama bado hujaianza biashara hiyo kivitendo. Hivyo basi kike kitendo cha wewe kupata TIN ya biashara inahalalisha wewe kulipa kodi kwa wakati husika na haitaweza kutumika tena kwa wakati ujao.
Unachoweza kufanya ni Kuomba TIN lakini isiwe kwa ajili ya biashara bali kwa mambo mengine kwa mfano kuombea leseni ya udereva nk ambapo utakuwa na TIN hy. Ukiona umeanza biashara utaenda kuibadilisha matumizi na kuwa TIN ya biashara ambapo utakadiriwa na kulipa makadirio husika kwa wakati huo ulioanza biashara.

2. Vielelezo vya kupata leseni kwa biashara ya bucha
Kwa biashara hii utatakiwa kuambatanisha vielelezo hivi
1. TIN 2. mkataba wa pango 3. Cheti cha uthibitisho wa kulipa kodi 4. Kujaza fomu ya manispaa ya maombi ya leseni 5. Cheti cha afya na uthibiti cha TFDA 5. Kopi ya kitambulisho chako
 
Kwanza naomba nikupongeze kwa somo zuri unalolitoa kuhusu Kodi na taratibu zake

Kiongozi mimi nina swali japo ntaanza kwa maelezo kidogo

Mwezi wa tisa mwaka 2015 nilifanya mchakato wa kuomba TIN kwa ajili ya biashara yangu ya Library na kuitumia TIN hiyo kupata Leseni ya biashara na kupata line kihalali za Tigo Pesa na M-Pesa maana ndio biashara niliyotaka kufungua.

Japo wakati wa makadirio nilibishana nao pale waliponikadiria kodi kubwa maana mwenyewe najua kabisa biashara yangu ya Library haina uwezo wa kuingiza milioni 4 na zaidi kwa mwaka.
Walikataa kubadilisha makadirio yao ya kodi ya 150,000 kwa mwaka waliyonikadiria nikakubali kishingo upande na baada ya muda nikapewa TIN yangu
Ila kiukweli kabisa mpaka sasa ninavyoandika sijawahi kulipa kodi yao waliyonikadiria maana biashara haizalishi kiasi cha kuweza kulipa kodi.
Kati ya 2016 mpaka 2017 mwishoni nilibanwa sana na majukumu ya chuo na maisha japo biashara yangu ya Library ilikuwa inaendelea kama kawaida
Mwaka jana mwezi wa pili ndio nilienda manispaa kuomba Leseni ya biashara na nikapewa na nikaanza kufatilia line za Tigopesa na M-Pesa

So maswali yangu ni kama ifuatavyo:
1. Je naweza kwenda TRA na kuomba wanikadirie upya??
2. Huku uswahilini serikali za mitaa zinatushinikiza tuchukue kitambulisho cha mjasiriamali na mimi nimechukua je naweza kwenda TRA na kuomba kuisitisha matumizi ya TIN namba yangu?
Ntashukuru nikipata msaada wa kielimu hapo.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole sana Mkuu Ramzy Classic kwa changamoto. Anyway maisha lazima yaendelee.
Majibu yako ni
1. Kwa mwaka 2015, TIN na makadirio
Kwa wakati huo baada ya "kulazimishwa" kulipa kiasi ambacho si stahiki kutokana na biashara yako ambayo wewe binafsi umesema mauzo hayakuwa yanazidi mil 4 kwa mwaka, ungeandika barua kwa meneja wa hilo tawi ulilopata huduma juu ya kupinga makadirio hayo.

LAKINI ANGALIZO HILI LIZINGATIWE
Suala la kuandika barua ya kupinga litakuwa sawa kama na kama tu wakati wa mahojiano ulisema kiwango ambacho Afisa wa kodi akifanya hesabu za mauzo kwa mwaka kinakuwa chini ya mil 4. Hivyo basi kama mauzo ulisema mwenyewe yanakuja zaidi ya mil 4 hiyo ni kosa lako mwenyewe, ulitakiwa ulipe

2. Malipo ya kodi toka 2015......2019
Kama hujaenda kutoa taarifa zozote TRA tambua penati itabaki pale pale kwa muda wote huo ambapo ni sh 225,000 kwa kila mwezi unaoongezeka toka mwezi wa malipo ya kodi. Hivyo tarajia ukienda kukutana na faini hii. Sio nakuogopesha usiende laaah bali tatizo hutatuliwa kwa kukabiliana nalo. Nakushauri nenda kaangalie hali halisi naamini utasikilizwa na kusaidiwa kutatua changamoto hii.

3. Kukadiriwa upya mwaka huu 2019
Ndiyo utakadiriwa upya lkn viporo vya madeni yako vipo pia. Kila mwaka makadirio mapya hufanyika.

4. Kitambulisho vya mjasiriamali
Kama biashara yako ni ndogo sana bhasi ni vema ununue hicho kitambulisho na pia uende TRA kutoa taarifa juu ya mabadiliko ya hali ya kibiashara kuwa biashara yako imekuwa ndogo sana. Nenda na kitambulisho hicho kama ushahidi wa biashara yako ni ndogo sana na hapo elezea na hali halisi ya wakati huo wa makadirio makubwa ambayo hayaendani na biashara yako
 
Shukran Kiongozi kwa maelezo yaliyojitosheleza

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Shule tosha mkuu barikiwa
 
Tunashukuru sana kwa elimu yako lakini ninaomba ufafanuzi kidogo hapo kwenye bidhaa zilizosamehewa VAT.
Umeeleza vyakula ambavyo havijasindikwa na ukatoa mfano wa unga wa mahindi,nilitaka kujua kama unga tunaouona ukichakatwa kwenye hivi viwanda vidogovidogo na kufungashwa kwenye viroba kama pale Tandale DSM kama nao upo kwenye msamaha wa VAT.
Thnx
 

Asante kwa kufuatilia mada zetu gimmy's

Mahindi kama mahindi as a raw material hayana VAT. Lkn kama yakibadilishwa ie processed na kuwa unga na muuzaji akawa ana kiwango au anazidi mil 100 ya mauzo yake kwa mwaka bidhaa hii ya unga itachajiwa VAT

NOTE: Niwie radhi kwa mkanganyiko wa mfano uliokuwa haupo sawa ie unga vs mahindi. Samahani sana
 
Wazo tu
Suala la kodi hili naona linahitaji elimu sana kwa watu ili kuelewa na kuepuka kuumizwa. Kama kuna kundi la watu wa masuala ya kodi naomba niunganishwe au liundwe kundi la whatsapp la masuala ya kodi tu. Namba ya ofisi yetu ni hii 0755411455
 
Wazo tu
Suala la kodi hili naona linahitaji elimu sana kwa watu ili kuelewa na kuepuka kuumizwa. Kama kuna kundi la watu wa masuala ya kodi naomba niunganishwe au liundwe kundi la whatsapp la masuala ya kodi tu. Namba ya ofisi yetu ni hii 0755411455
Kweli itapendeza tutapata kujifunza zaidi kuhusu kodi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umuhimu wa kutunza kumbukumbu kwa wafanyabiashara binafsi katika kodi

Tujitahidi sana kuweka kumbukumbu hata kama biashara yako si kubwa kwani inakusaidia badala ya kukadiliwa utafanyiwwa hesabu na kujulikana wazi watakiwa ulipe kiasi gani. Kwa mujibu wa Sheria ya Usimamizi wa Kodi (kifungu cha 35, utunzaji wa kumbukumbu) kuna namna nzuri na za wazi kabisa katika ukokotoaji wa kodi.
Mfano
Mfanyabiashara A ameuza kwa mwaka mzima mauzo ya mil 4,500,000 na haweki kumbukumbu. Makadirio ya kodi atatakiwa kulipa sh 150,000 kwa mwaka

Mfanyabiashara B ameuza kwa mwaka mil 4.5 kwa mujibu wa kumbukumbu zake ie risiti. Huyu malipo yake ya kodi itakuwa 3% ya mauzo yanayozidi mil 4.
Hii ni kwamba
Kodi=4,500,000-4,000,000
Kodi=500,000*3%
Kodi=15,000
(Rejea ukurasa wa 9, kitabu cha Kodi na Ushuru mbalimbali 2018/19)

Na kuboresha vizuri kumbukumbu zako za mauzo nunua mashine ya kielektroniki ie ELECTRONIC FISCAL DEVICE EFD ambayo kwa sasa bei yake kati ya TZS. 580,000 hadi TZS. 590,000, kila ukiuza toa risiti nawe mnunuzi dai rositi pia. Kwani hii inakusaidia kuwafikishia rekodi za mauzo yako Mamlaka ya mapato kila unapotuma Z-Report.
Naambatanisha kitabu
1. Kodi na Ushuru mbalimbali 2018/2019, toleo la Julai, 2018 TRA
2. Umuhimu wa utunzaji kumbukumbu. Nimekutoa ktk mtandao nimeona ni kizuri kwa kujifunza zaidi juu ya uwekaji sahihi wa kumbukumbu. Afrolink-Tz CL si waandishi wa kitabu hiki
3. Kushauri kununua na kutumia EFD mashine haina maana sisi ni wadau au wauzaji wa mashine hizo laah hasha bali tumeshauri ktk kusaidia kuona njia bora zaidi za kulipa kodi halisi kutokana na mauzo yetu, hivyo tusihusishwe na kulazimisha au kutangaza manunuzi ya mashine hizoView attachment KUTUNZA KUMBUKUMBU ZA BIASHARA.pdfView attachment kodi-na-ushuru-July-18-19 (1).pdf
 
Tunakumbushana tu
Kwa wafanyabuashara wenye sifa za kuwasilisha mahesabu ya mizania, ritani TRA, muda wa uwasilishaji unaisha 30.06.2019 kwa mwaka wa fedha 2018. Je tayari mahesabu yako yameshakadiriwa? Wahi muda kabla ya muda haujakuwahi!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…