Pre GE2025 Makamba: Hata kama hatumkubali Rais Samia, ni wetu

Pre GE2025 Makamba: Hata kama hatumkubali Rais Samia, ni wetu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Kama MoU aina legal obligation, mbona serikali iliwalipa ‘Symbion Power’ zaidi ya billion tsh 350 mara tu baada ya Samia kuingia madarakani.

Tena ile MoU ya Symbion na serikali ilikuwa option tu na rahisi kuvunja wameshindwa kesi (ambayo awakwenda kujitetea), hawaku-challenge, wakawalipa Symbion na kuwapa kibali cha kuendelea kuzalisha umeme juu.

Sio kila MoU uwezi shitakiwa wasikariri mambo.

Halafu wanajiaminisha vitu vichwani mwao wanadhani wote kweli tunaamini Magufuli aliharibu uhusiano wa kimataifa kisa alikuwa aendi kwenye mialiłko tu. Hizo fikra zinaishi kwenye vichwa vyao tu, sio kila mtu wa kuamini every nonse running in their heads.
Usimlete Magufuli hapa, gharama ya kurekebisha uovu wake ni kubwa mno. Ni vizuri Syombion Power walilipwa bila kwenda kwenye arbitration tribunal
 
Usimlete Magufuli hapa, gharama ya kurekebisha uovu wake ni kubwa mno. Ni vizuri Syombion Power walilipwa bila kwenda kwenye arbitration tribunal
Unafahamu hata madai ya Symbion yalikuwa nini?

Ngoja nikusaidie hawakua na mkataba wa kuendelea kuzalisha umeme muda wao ukiisha, bali MoU ambayo haipo public.

Madai yao kwa uelewa wana MoU (hivyo chances za kuongezewa muda) walifanya maamuzi ya uwekezaji wenye thamani ya dollar million kadhaa wakijua watapata extension (that’s not a contract) and probably a set trap ya kufungua kesi ya madai mbeleni wakikosa contract extension.

Huo uwekezaji could be challenged ni maamuzi yao (mainly ilikuwa kubadili uzalishaji wa mafuta kwenda kwenye gas) kama kwenye MoU hamna kitu kama hiko.

Halafu nani kathibitisha gharama halisi za madai yao na justification zilizokuwa kwenye MoU. Magufuli hakurenew contract wamefungua kesi alijipanga kwenda mahakamani, kafa mmelipa halafu mnataka kumlaumu yeye.

Kesi zingine mnazoshindwa mnapeleka watu uelewa wao wa contract mdogo wote tumesikiliza ile ya Indiana iliyofanyika NY kwa arguments zile ilikuwa washindwe tu.

Magufuli ataongelewa kwa sababu ni wao ndio wanamrudisha kwenye mijadala kama wameamua kusafiri si wao mpaka waseme yule mwingine alifanya abc za kutunga, mtu kama Makamba na Napę ndio wanaofanya Magufuli aishi.

Makamba hawezi tetea kitu bila ya kumtumia Magufuli negatively katika hoja yake.
 
Waziri Januari Makamba amesema hata kama hatumkubali Samia ni wetu hivyo tunatakiwa kuacha siasa hasa kuhusu ziara zake nje ya nchi kwani zimeleta manufaa makubwa kwa nchi.

Waziri Makamba ameyasema hayo leo 6.6.2024 akizungumzia ziara ya Rais Samia nchini Korea

Zaidi sikiliza hii link mpaka mwisho

Well said ,kumbe mnajua hili ,akaaaa mmeanza kujishtukia kumbe ,sisi wa Ngorongoro tutakulaani na hatukupendi hataa kidogo
 
Unafahamu hata madai ya Symbion yalikuwa nini?

Ngoja nikusaidie hawakua na mkataba wa kuendelea kuzalisha umeme muda wao ukiisha, bali MoU ambayo haipo public.

Madai yao kwa uelewa wana MoU (hivyo chances za kuongezewa muda) walifanya maamuzi ya uwekezaji wenye thamani ya dollar million kadhaa wakijua watapata extension (that’s not a contract) and probably a set trap ya kufungua kesi ya madai mbeleni wakikosa contract extension.

Huo uwekezaji could be challenged ni maamuzi yao (mainly ilikuwa kubadili uzalishaji wa mafuta kwenda kwenye gas) kama kwenye MoU hamna kitu kama hiko.

Halafu nani kathibitisha gharama halisi za madai yao na justification zilizokuwa kwenye MoU. Magufuli hakurenew contract wamefungua kesi alijipanga kwenda mahakamani, kafa mmelipa halafu mnataka kumlaumu yeye.

Kesi zingine mnazoshindwa mnapeleka watu uelewa wao wa contract mdogo wote tumesikiliza ile ya Indiana iliyofanyika NY kwa arguments zile ilikuwa washindwe tu.

Magufuli ataongelewa kwa sababu ni wao ndio wanamrudisha kwenye mijadala kama wameamua kusafiri si wao mpaka waseme yule mwingine alifanya abc za kutunga, mtu kama Makamba na Napę ndio wanaofanya Magufuli aishi.

Makamba hawezi tetea kitu bila ya kumtumia Magufuli negatively katika hoja yake.
Mkuu umepuyanga sana kwenye hili la mikataba. Laiti Magufuli angepewa kipaji cha kuwa msikivu basi angemsikia Tundu Lissu alivyoshauri. Lakini akaamua kummiminia marisasi. Kuna hizo kesi 3 tunalipa billions na zingine zitakuja tutalipa tu!

Hivi are you seriously defending Magufuli kwenye kujurupuka? Umesahau alivyo handle issue ya Hermanus Steyn yule mkulima wa SA mpaka ndege yetu ilakamatwa Joburg?? That was a madman running a country, muache tu huko huko jehanam
 
Toka maktaba :

BREAKING: Rais Magufuli AMTUMBUA Waziri January Makamba Rais John Pombe Magufuli leo Jumapili, Julai 21, 2019 ...

1717689055183.png

Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na kurugenzi ya mawasiliano ya rais na kutiwa saini na mkurugenzi wake Gerson Msigwa

Hata hivyo taarifa ya ikulu haijatoa sababu zilizopelekea rais Magufuli kumwondoa kazini Januari Makamba.

Za ziada
TOKA MAKTABA :
2019 17 July

Viongozi wengine wastaafu wa CCM na wa Serikali waliostaafu na walioko madarakani, kwamba eti mnamhujumu Rais...


NJAMA ZA NAPE, KINANA na MAKAMBA DHIDI YA MWENYEKITI WA CCM RAIS MAGUFULI ZAVUJA KUPITIA KUNASWA KWA MAONGEZI YA SIMU KATI YA NAPE NAUYE NA ABDULRAHMAN KINANA


View: https://m.youtube.com/watch?v=VACtkPNb1tM
 
Waziri Januari Makamba amesema hata kama hatumkubali Samia ni wetu hivyo tunatakiwa kuacha siasa hasa kuhusu ziara zake nje ya nchi kwani zimeleta manufaa makubwa kwa nchi.

Waziri Makamba ameyasema hayo leo 6.6.2024 akizungumzia ziara ya Rais Samia nchini Korea

Zaidi sikiliza hii link mpaka mwisho

Endelea kumsukia deal la kupewa PhD ya sita
 
Waziri Januari Makamba amesema hata kama hatumkubali Samia ni wetu hivyo tunatakiwa kuacha siasa hasa kuhusu ziara zake nje ya nchi kwani zimeleta manufaa makubwa kwa nchi.

Waziri Makamba ameyasema hayo leo 6.6.2024 akizungumzia ziara ya Rais Samia nchini Korea

Zaidi sikiliza hii link mpaka mwisho

Nani kasema hamtaki???
 
Mkuu umepuyanga sana kwenye hili la mikataba. Laiti Magufuli angepewa kipaji cha kuwa msikivu basi angemsikia Tundu Lissu alivyoshauri. Lakini akaamua kummiminia marisasi. Kuna hizo kesi 3 tunalipa billions na zingine zitakuja tutalipa tu!

Hivi are you seriously defending Magufuli kwenye kujurupuka? Umesahau alivyo handle issue ya Hermanus Steyn yule mkulima wa SA mpaka ndege yetu ilakamatwa Joburg?? That was a madman running a country, muache tu huko huko jehanam
Tafuta habari za kina kuhusu hizo kesi kuanzia ya mkulima Stein, mwenyewe kwanza hakuwa hata na habari za shamba ni wapambe tu ndio waliofungua kesi zama za JK.

Hayo mambo tumejadili sana humu wapingaji wa maamuzi ya serikali kipindi cha Magufuli walikuwa wanapotosha tu. But given the background ya kesi zenyewe ni upigaji mtupu.
 
Waziri Januari Makamba amesema hata kama hatumkubali Samia ni wetu hivyo tunatakiwa kuacha siasa hasa kuhusu ziara zake nje ya nchi kwani zimeleta manufaa makubwa kwa nchi.

Waziri Makamba ameyasema hayo leo 6.6.2024 akizungumzia ziara ya Rais Samia nchini Korea

Zaidi sikiliza hii link mpaka mwisho

Hii kauli haina afya kwa eliemteua,kumbe anajua boss wake hakubaliki basi amwambie face by face
 

Historia ya Mikwaruzano ndani ya Kambi za CCM​

Muktasari Chama kurejeshwa mikononi mwa CCM Asilia :​

“Hakuna sababu ya kutoa shutuma hizo kwa sababu walioharibu ni CCM na anayetengeneza ni CCM,” alisema Kinana jana alipokuwa na Rais Magufuli mjini Muheza wakiwa njiani kwenda Tanga na kisha kuwahoji wananchi juu ya kile wanachokitaka nao kujibu ‘ndiyoo’ kisha akasema kinachotakiwa ni maendeleo na si kitu kingine

Kurejea kwa kada halisi wa chama​

CCM ni chama cha kikada - hata kama sasa baadhi ya matendo na maneno ya wafuasi na viongozi wake hayatoi picha hiyo. Katika chapisho lake mashuhuri la What is to Done lililochapwa mwaka 1902, Vladmir Lenin - Baba wa Mapinduzi ya Urusi ya mwaka 1917, alieleza kuhusu umuhimu wa kuwa na chama cha kikada - cha kimapinduzi, kitakachokuwa na uwezo wa kulinda mapinduzi dhidi ya adui zake.

Mwanasiasa V.I Lenin alieleza kuhusu umuhimu wa kutengeneza wanachama maalumu - kadrovyy sostav (makada) - akitohoa kutoka neno la lugha ya Kifaransa Cadre, waliopikwa vyema kiitikadi na kijeshi. Kazi ya makada ilikuwa ni kuwa na uwezo wa kufanya siasa na wakati huohuo kuwa tayari kukilinda endapo kutatokea changamoto zinazohitaji mbinu za kijeshi.

Makada ni watu waliokuwa wakiaminika kwamba hata kama watabaki watano tu, wanaweza kukifufua chama na kukirejesha kilipokuwa.

Hiyo ndiyo sababu ya CCM - iliyoundwa kimapinduzi, kutengeneza wanachama waliopitia pia mafunzo ya kijeshi kama Jakaya Kikwete, Andrew Shija, Moses Nnauye, Yusuph Makamba, Edward Lowassa, Kinana na wengine. Katika muktadha huu, ni vigumu kuona ni kwa vipi Kinana angekataa kuitikia wito wa Mwenyekiti wake, Rais Samia, wa kutaka kukirejesha chama katika njia yake.

Novemba 2012, Kinana aliitwa tena na aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM wakati huo, Jakaya Kikwete, kuwa Katibu Mkuu katika wakati ambao chama tawala kilikuwa kinapitia mitihani mikali ndani na nje ya chama. Ndani ya chama, wafuasi wa Lowassa walianza kuonesha waziwazi kampeni za kutaka awe mrithi wa Kikwete kwenye urais na uenyekiti, wakati nje Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kilikuwa kimetoka kupata mafanikio makubwa kwenye Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010.

Kinana alishika ukatibu mkuu baada ya jitihada za 'kukinyoosha' chama chini ya Katibu Mkuu, Wilson Mukama kuanzia April 2011 kutozaa matunda.

Ni Kinana aliyesifiwa kwa kufanikiwa kubadili upepo na kurejesha umaarufu wa CCM kiasi cha kupata ushindi katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 - ambapo John Magufuli alimshinda Lowassa aliyekuwa amehamia Chadema baada ya kuihama CCM. Lowassa sasa amerejea chama tawala.

Kinana, mbunge wa zamani wa Arusha Mjini ni kiongozi anayefahamika utendaji wake wa kazi na anayekifahamu chama vilivyo. Alipokuwa Katibu Mkuu wa CCM kati ya Novemba 2012 hadi Mei 2018 alipoomba kupumzika, ilikuwa ikifahamika kwamba hakuwa akichukua mshahara kutoka CCM kama ilivyokuwa kwa watumishi wengine wa chama. Ni kama vile alijitolea kufanya kazi za chama.

Askari, Mwanadiplomasia, MwanaBunge, Mwanasiasa na Mfanyabiashara​

Kinana ni mtu mwenye kofia nyingi. Ni askari aliyepitia mafunzo ya kijeshi kufikia cheo cha Kanali. Ni mwanadiplomasia aliyewahi kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wakati wa utawala wa Rais Ali Hassan Mwinyi.

Ni MwanaBunge aliyewahi kuwa mbunge na baadaye Spika wa Bunge la kwanza la Afrika Mashariki mwak 2001.
Ni mwanasiasa aliyewahi kushika vyeo vya kisiasa kama mbunge, waziri na Katibu Mkuu wa chama. Mtu wa mipango na mtekelezaji wa mikati, kwani aliongoza kampeni nne za urais kwa mafanikio; mwaka 1995 na 2000 akiwa Meneja wa Kampeni mgombea wa CCM Benjamin Mkapa, pia meneja wa kampeni wa Jakaya Kikwete mwaka 2010 kabla ya kusimamamia kampeni za Magufuli 2015 akiwa Katibu Mkuu.

Kadhalika ni mfanyabiashara aliyewahi kuwa kwenye bodi kadhaa za mashirika ya umma na sekta binafsi. Sifa yake kubwa ni kwamba anaweza kuvaa kofia yoyote kati ya hizo pale anapotaka au inapobidi.
Kofia zake hizo zimemfanya kuwa mmoja wa viongozi wenye wigo mpana wa marafiki ndani na nje ya nchi - kuanzia marais, wafanyabiashara maarufu, wanasiasa wa vyama tawala na upinzani na watu wa kawaida ambao wamekuwa muhimu kwake kwa kumwongezea maarifa na taarifa katika majukumu yake tofauti.

CCM Mpya, CCM ya zamani​

Baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020, niliandika uchambuzi kupitia BBC Swahili Mwisho wa zama za 'kizazi cha zamani CCM' - BBC News Swahili, ambao niliueleza uchaguzi huo kama mwisho wa zama za kizazi cha akina Kinana ndani ya CCM.
Utawala wa Rais Magufuli ulikuwa na uhusiano usio na afya na waliokuwa wakijulikana kama wenye CCM - akina Kinana, na kuna wakati Katibu Mkuu huyo wa zamani na Yusuph Makamba walifikishwa katika Kamati ya Maadili ya chama kukiwa na tishio la kuwafukuza uanachama.

Kinana alipewa karipio na kuwekwa chini ya uangalizi kwa miezi 18. Makamba alisamehewa lakini Waziri wa Mambo ya nje wa zamani Benard Membe alifukuzwa uanachama. Baadaye Kinana na Membe walisamehewa.

Kurejea kwa Kinana kuna maana zaidi ya moja ndani ya CCM. Kwanza ni kurejea kwa mtu anayeweza kukirudisha chama katika misingi yake na kukizimua ikibidi - kazi aliyofunzwa kama kada, kuandaa kizazi kipya cha viongozi wajao wa chama hicho na kukitayarisha chama kwa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.

Mwaka 2020, CCM ilitumia zaidi nguvu za dola kushinda uchaguzi kuliko ushawishi kwa wapiga kura na inaonekana Rais Samia hataki kujirudia kwa siasa za namna hiyo.

Kulikuwepo tuhuma nyingi za viongozi wa vyama vya upinzani dhidi ya CCM kunufaika na nguvu za dola. Hata hivyo, viongozi wa CCM mara kadhaa walikanusha tuhuma hizo na kuwataka wanaodai kuonewa kufungua kesi mahakamani.

Uzoefu wa Kinana ni mtaji mkubwa kwa CCM. Katika historia ya vyama vingi nchini Tanzania; kuna chaguzi mbili zinazotajwa kuwa ngumu zaidi kwa CCM - ule wa mwaka 1995 dhidi ya NCCR Mageuzi ya Augustine Mrema na wa mwaka 2015.

Mtindo wa Kinana wa kufanya kazi ni CCM kutoionea haya serikali na kuwa msemaji wa kero za wananchi. Muda si mrefu, tutaanza kuona viongozi wa CCM wakiwa wasemaji wa kero za wananchi pengine kuliko hata vyama vya upinzani.

Pengine huu ni wakat iwa vyama vya upinzani kukaa chini na kuangalia kama mipango yao inaendana na mabadiliko haya ya 'upepo' ndani ya chama tawala.
Kinana alizaliwa Arusha Mei mwaka 1951. Alijiunga na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) mnamo mwaka 1972 na kulitumikia hadi mwaka 1992 alipostaafu.

Ni msomi wa shahada ya kwanza katika Sayansi ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa aliyoipata katika Chuo Kikuu cha Ljubljana katika iliyokuwa Yugoslavia na Shahada ya Uzamili katika Uongozi na Utawala aliyoipata katika Chuo Kikuu cha Harvard nchini Marekani.

Katibu Mkuu huyu wa zamani wa CCM ni mtu asiyependa kuanika maisha yake binafsi na familia yake hadharani lakini inajulikana kuwa ana mke, Rahma, na watoto.

Makala toka BBC

Membe afukuzwa CCM, Kinana aonywa, Makamba asamehewa.​


kinaa.jpg

Kamati kuu ya Halmashauri kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi imemvua uanachama kada wake Bernad Membe huku ikitoa karipio kwa katibu mkuu mstaafu Abdulrahman Kinana na ikimsamehe katibu mkuu mwingine mstaafu Yusufu Makamba.

Katibu wa itikadi na uenezi wa halmashauri kuu ya chama hicho Humprey Polepole amesema uamuzi huo wa kamati kuu umefikiwa ikiwa ni utekelezaji wa katiba ya chama hicho kulingana na makosa ambayo makada hao watatu walituhumiwa kuyafanya.
Kinana apewa karipio, awekwa chini ya uangalizi miezi 18.
 
Back
Top Bottom