Makarani wa sensa hawatalipwa malipo yaliyobaki kama hawatafikisha kaya 100 kila mmoja

Makarani wa sensa hawatalipwa malipo yaliyobaki kama hawatafikisha kaya 100 kila mmoja

Kingsmann

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2018
Posts
4,805
Reaction score
17,850
Mtakwimu mkuu wa serikali NBS, Dr. Albina Chuwa amewatahadharisha makarani kuwa hawatalipwa kiasi cha malipo kilichobaki endapo hawatafikisha kaya 100 kila mmoja, wakati akieleza mwenendo wa zoezi hilo tangu kuanza kwake mpaka hivi sasa. Amesema lengo ni kuhakikisha watu wote wanahesabiwa.

Dr. Chuwa amesema kama kuna karani amehesabu eneo lenye kaya pungufu, kuanzia 50-60 anatakiwa kwenda katika eneo jingine. "Karani asijikute kwamba eneo lake la kuhesabu watu lina kaya 50-60, akakaa akarelax, hapana, tulisema kwamba kama eneo lina kaya 50 au pungufu yu 50, lazima atakwenda kwenye eneo lingine, atakwenda kwenye eneo lingine, atakwenda katika eneo lingine, katika ileile kata, au kata nyingine kwa ajili ya kuharakisha kumaliza kazi hii mapema".

Zoezi hili la sensa litaendelea kwa siku 7 nchini, na sensa ya majengo itafanyika kwa siku 3.



Chuwa NBS.jpeg
 
Nilijua tu. Hao ndio MABOSS wa Tanzania. Kazi zao huwa Ni kuwatishia watu huku wao hawajui chochote kinachoendelea.

Kifuatacho hapo Ni KUPIKA DATA kumfurahisha huyo a mpuuzi kama wanavyopika data za chanjo.
 
Nimesikia kwa mijini makarani wamepangiwa kaya 150@, Sasa hizi kaya 50 zitakazobakia inakuwaje?
 
Naona bado hao makarani wanaweza kufanya mchezo ilimradi wafikishe hizo kaya 100, hii sensa maandalizi yalifanyika muda mrefu lakini utekelezaji wake unavyokwenda ni kama vile hapakuwepo na maandalizi.
 
Wajiandae kupata idadi ya watu Watanzania mara 2 ya uhalisia..

Kwa maana si kila eneo linafika idadi hiyo..

Vijijini kule kupata kaya 100 si mchezo, unaweza ukatembea kilomita nyingi sana ndipo ufikishe idadi hiyo..
 
Wajiandae kupata idadi ya watu Watanzania mara 2 ya uhalisia..

Kwa maana si kila eneo linafika idadi hiyo..

Vijijini kule kupata kaya 100 si mchezo, unaweza ukatembea kilomita nyingi sana ndipo ufikishe idadi hiyo..
Idadi ya Kaya wanaijua kutokana na Anwani za makazi. Hata idadi ya makarani imepangwa kulingana na idadi hiyo ya kaya
 
Mtakwimu mkuu wa serikali NBS, Dr. Albina Chuwa amewatahadharisha makarani kuwa hawatalipwa kiasi cha malipo kilichobaki endapo hawatafikisha kaya 100 kila mmoja, wakati akieleza mwenendo wa zoezi hilo tangu kuanza kwake mpaka hivi sasa. Amesema lengo ni kuhakikisha watu wote wanahesabiwa.

Dr. Chuwa amesema kama kuna karani amehesabu eneo lenye kaya pungufu, kuanzia 50-60 anatakiwa kwenda katika eneo jingine. "Karani asijikute kwamba eneo lake la kuhesabu watu lina kaya 50-60, akakaa akarelax, hapana, tulisema kwamba kama eneo lina kaya 50 au pungufu yu 50, lazima atakwenda kwenye eneo lingine, atakwenda kwenye eneo lingine, atakwenda katika eneo lingine, katika ileile kata, au kata nyingine kwa ajili ya kuharakisha kumaliza kazi hii mapema".

Zoezi hili la sensa litaendelea kwa siku 7 nchini, na sensa ya majengo itafanyika kwa siku 3.

View attachment 2336056

View attachment 2336058
Ni jukumu la karani kujipangia eneo lolote lile la kufanya kazi!? Mbona huyu Bi. Chuwa anakuwa mropokaji bila hata kuangalia uhalisia wa mambo? Kweli nchi yetu ina viongozi wenye vichwa vigumu sana.
 
Wajiandae kupata idadi ya watu Watanzania mara 2 ya uhalisia..

Kwa maana si kila eneo linafika idadi hiyo..

Vijijini kule kupata kaya 100 si mchezo, unaweza ukatembea kilomita nyingi sana ndipo ufikishe idadi hiyo..
Nilifanya sensa ile ya mwaka 2012 tena KWA uweledi Sana hapo ilikuwa manually!na madodoso yetu kitaa safi KABISA!

Nakumbuka nilikuwa chuo mwaka wa pili!nikiwa field ndio nilishauriwa niombe na kweli nikapata!kulikuwa hakuna cha uvccm wala makada ndio wapewe KAZI ile!!

Kinachoendelea ni sarakasi za kufa mtu!kuanzia upigaji Hadi kulazimishana idadi ya kaya kuliko uhalisia!!

Hadi Sasa sijahesabiwa na Ndio màana sikuomba hii KAZI nikijua kuna sarakasi KIBAO!!

""Rasimu ya Warioba irudi mezani SASA iwe KATIBA MPYA"!
 
Mtakwimu mkuu wa serikali NBS, Dr. Albina Chuwa amewatahadharisha makarani kuwa hawatalipwa kiasi cha malipo kilichobaki endapo hawatafikisha kaya 100 kila mmoja, wakati akieleza mwenendo wa zoezi hilo tangu kuanza kwake mpaka hivi sasa. Amesema lengo ni kuhakikisha watu wote wanahesabiwa.

Dr. Chuwa amesema kama kuna karani amehesabu eneo lenye kaya pungufu, kuanzia 50-60 anatakiwa kwenda katika eneo jingine. "Karani asijikute kwamba eneo lake la kuhesabu watu lina kaya 50-60, akakaa akarelax, hapana, tulisema kwamba kama eneo lina kaya 50 au pungufu yu 50, lazima atakwenda kwenye eneo lingine, atakwenda kwenye eneo lingine, atakwenda katika eneo lingine, katika ileile kata, au kata nyingine kwa ajili ya kuharakisha kumaliza kazi hii mapema".

Zoezi hili la sensa litaendelea kwa siku 7 nchini, na sensa ya majengo itafanyika kwa siku 3.

View attachment 2336056

View attachment 2336058
Na watafikisha tu 100, hata kama hazifiki kaya 100 kwa kila karani
 
Hapa hawa makarani tusubiri kelele za vilio vyao haya ni mazingira ya dhulma yanaandaliwa,Rai yangu kwa makarani wajiandae kisaikolojia kwa chochote kitakachowakuta,waliyopokea ndiyo stahiki yao iliyobaki ni tozo watakatwa.
 
Hapa watu watapika data, ila vijijini huko kufikisha hizo kaya 100 ni kazi pevu...
 
Ili zoezi lilishafeli leo siku ya 5 bado siku bado siku 2 zoezi lifike tamati. Kuna mahali wamekosea ili swala

Hadi jana walikua wamehesabu almost watu million 30+
 
Back
Top Bottom