Makato ya HESLB: Rais Samia tunaomba mrudishe makato ya 8%, pia yazingatie sheria ya kubaki na 1/3 ya basic salary

Pamoja sana kiongozi.
 
Bodi hawakati hela ya mtu, hela anakata mwajiri wako halafu ndio anaipeleka HESLB, wewe banana na mwajiri wako akupe hela yako ambayo amekukata bila utaratibu
Unachokitetea hapa hata hukijui, au unatetea uongo. Kuna wanufaika kibao walimaliza madeni yao zaidi ya miaka 5 iliyopita.

Mwaka huu wa 2023 wamepewa madeni mapya ya kulipa. Na wanakatwa 15% kwenye basic salary yenye mikopo lukuki.

Mabaya zaidi hao HELSB wewakiulizwa wanatoa sababu za kipuuzi puuzi tu. Halafu unasema mwajiri ndiye anayepeleka hayo madeni!
 
Bodi hawakati hela ya mtu, hela anakata mwajiri wako halafu ndio anaipeleka HESLB, wewe banana na mwajiri wako akupe hela yako ambayo amekukata bila utaratibu

Kwan lazima kubishana na hujui kitu mzee
 
Utakuta jitu kutoka hifadhi ya lumumba linapinga tu kisa wewe ni mwana mageuzi.

Hii hoja ni ya msingi sana maana wanao umizwa na hii sheria gandamizi ni watanzania wote.

Hongera sana kwa kuibua hoja ya msingi sana kiongozi.
 
Mama ajatukwanza popote kwenye issue ya bandari iko sahihi , mtakuja kumshukuru badaye kwa kubinaifusisha badari anapenda maendeleo ya Tanganyika, isipo kua wengi ni slow learners.
Kuwakaribisha wawekezaji siyo dhambi bali dhambi ni njia iliyotumika ya kuvizia ndiyo watu wanaona kuwa kuna kasoro
 
Fuata upepo wa kisuri suri
 
Serikali kwenda kinyume au kukiuka mkataba waliosainiana wanafunzi wa vyuo na bodi ya mikopo, kwa nini hamkujipanga na kwenda mahakamani kupinga? Mkataba ulikuw8% ni kukiuka Sheria kuifanya 15%
 
Mwalimu tafuta tuu plan B mshahara hautokaa ukutoshe... uza hata juisi walimu mnaikera sana serikali wanaona mnamalizia makusanyo
 
Utapeli mtupu walitangaza kuongeza pesa kutoka shilingi 8,500/= kwenda shilingi 10,000/= lakini uhalisia bado ni 8,500/= kwa mjibu iwa barua walizoandikiwa wanafunzi wanaotarajiwa kujiunga Oktoba 2023
 
Kuna taasisi za ajabu sana hapa Duniani, bodi ya elimu ya juu HESLB ya Tanzania pamoja na bima ya afya NHIF ya Tanzania.
Sijui huko Bungeni wanaongelea mambo gani kuhusiana na bima ya afya.
 
Utakuta jitu kutoka hifadhi ya lumumba linapinga tu kisa wewe ni mwana mageuzi.

Hii hoja ni ya msingi sana maana wanao umizwa na hii sheria gandamizi ni watanzania wote.

Hongera sana kwa kuibua hoja ya msingi sana kiongozi.
Asante mkuu. Pamoja sana.
 
Sijatetea kitu na kweli inawezekana sijui kitu lakini Nadhani hujanielewa vizuri kuhusu nafasi ya mwajiri kwenye makato yoyote unayokatwa kwenye mshahara wako. Wengine tulikuja kupata muafaka baada ya kutishia kumshtaki mwajiri na bodi mahakamani ndio taarifa zikakaa sawa, mana mtu unakatwa na deni badala ya kupungua linaongezeka, sasa unaponiambia mwajiri hahusiki nakuwa sikuelewi vizuri
 
Kwan lazima kubishana na hujui kitu mzee
Sidhan kama tupo humu kuoneshana nani anajua sana, lengo ni kuoneshana njia zinazoweza hilo tatizo kutatuliwa, kwani wengine mwajiri wao amewasaidia kuondokana na hilo janga la kubambikiwa deni la HESLB ambalo halina uhalisia, kuna watu walikuwa wanakatwa badala ya deni kupungua ajabu likawa linaongezeka, lakini kwa kushirikiana na mwajiri wakaweka taarifa sawa. Nafasi ya mwajiri ipo kuhakikisha mtumishi wake anatendewa haki
 
Usione aibu mwalimu...walimu nikama mahouse boi/girl mnafanya vizuri kulea watoto wetu hatuwachukii kiukweli
Kwa hiyo na wazazi wako waliokuzaa (hawa ndiyo walimu wako wa kwanza kabisa kukufundisha kula, kunya, kuvaa nguo, kupiga mswaki, kuoga, kusalimia, kuheshimu wakubwa zako, nk) nao ni ma house boy/girl wako siyo!!!

Kama wewe kweli ni mzazi, basi utakuwa na akili za kitoto kama walivyo hao watoto wako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…