Afisa Ustawi wa Jamii wa Jiji la Dar es Salaam, Joyce Maketa, amesema kwamba miongoni mwa mambo yanayovuruga ndoa hadi kupelekea wanandoa kuachana inasababishwa na wanaume kuomba mahusiano kinyume na maumbile.
Kauli hiyo ameitoa hii leo Septemba 6, 2022, jijini Dar es Salaam, kwenye kipindi cha SupaBreakfast ya East Africa Radio mara baada ya taarifa kuonesha kwamba kila mwezi ndani ya jiji la Dar es Salaam takribani ndoa 300 zinavunjika.
"Kumekuwa na mahusiano mapya (Kwa wanandoa) yanayopelekea wakati mwingine kuomba kuwa na mahusiano kinyume na maumbile hicho kimekuwa ni moja ya kitu ambacho kimekuwa kikivuruga ndoa nyingi na watu mwisho kuachana, tuachane na hizo tabia tunazozi-copy na tuishi maisha yanayompendeza Mungu,"amesema Joyce
====
Haya yanajiri baada ya kamati ya Bunge ya huduma na Maendeleo ya jamii kutoa ripoti Septemba 5, 2022 iliyoelezea kuwa mkoa wa Dar es salaam unaongoza kwa uvunjifu wa ndoa nyingi nchini ambapo wastani wa ndoa 300 huvunjika kila mwezi.
Kamati hiyo ilibaini pia kuwepo kwa mmomonyoko mkubwa wa maadili na ukatili mkubwa wa kijinsia hasa ule unaohusisha watoto.
EATV
Huenda Tanzania🇹🇿 ikawa ndio nchi pekee duniani ambayo raia wake hata hawaelewi wanataka nini, wao ni bora liende tu. Hawa hawa wabunge wanashangaa ndoa kuvunjika kwa sababu feki waliyoitoa ndio waliokuwa mstari wa mbele kumtetea shilole pale aliyopitia mchakato dume kwenye ndoa yake.
Jike shupa ni mdau wa hii mambo na ninasema wazi tu kwa ujasiri kwa sababu ndiye aliyekuwa akihamasisha wanawake, tena wake za watu watoe KWA MPALANGE kwa waume zao kulinda ndoa zao. Hakuna mbunge hata mmoja aliyekemea hili isipokuwa ukawa ni msemo maarufu uliopokelewa na kukubalika katika jamii. Leo hii eti bunge linadanganywa kuwa ndoa zinavunjika kwa sababu ya wanapenda nyuma!!?
Watanzania wanaongoza kwa usahaulifu duniani. Ni majuzi tu madam Amba Rutty alijizolea umaarufu kwa kutoa nyuma, halafu ghafla tunamuona akiwa shule ya msingi kuhamasisha watoto kujitambua. Haya mambo yako wazi tu wala sio siri.
Tazama wasanii wa bongo fleva, nyimbo zao nyingi zimejaa huu ubaradhuli. Watu wake kwa waume huziimba kwa madaha huku wadada wakitingisha makalio wanapofika kwenye vesi husika. Hawa ndio kioo cha jamii ya wajinga, tena wanapewa publicity kubwa sana. Hutembelea mashuleni kuhamasisha mtoto wa kike kujitambua, hawa hawa mabaradhuli.
Kwenye mitandao ya kijamii zimejaa video za kina mama zinazo hamasisha ngono kinyume na uumbaji. Kama unabisha basi wewe ni mgeni hapa duniani. Kwa kuanzia pitia thread mbalimbali humu humu JF. Mijitu inatamba kwa jinsi gani inakula uchafu jalalani, halafu wadada na wao wanaringia kudhalilishwa kimaumbile.
Leo hii kamati ya Bunge inataka kutuaminisha kwamba wanawake wa Tanzania ni exceptionally holy kiasi kwamba wako tayari kupewa talaka ili kulinda nyuma zao? Tena mnataka tuamini kwamba wanaume wamefikia hatua kwamba ni heri ndoa ivunjike kuvunjika kuliko kukosa nyuma ya mke? Kwa jinsi ilivyo, wanaume wengi hupenda kuwafanyia ushenzi huu wanawake ambao SI WAKE ZAO, mpaka pale mke wake atakapoonyesha dalili za uhitaji ama kutoa ushirikiano pale anapofanyiwa "dodoso". Wanaume licha ya kupenda ukakasi huu bado wanaamini kuwa ni tendo la aibu sana kubainika kwamba anamtumia mkewe kinyume na maumbile, hivyo hawako tayari kutengeneza mazingira ya mke kuwatuhumu ama kwa ndugu, ama hadharani.
Wisho nadhani kamati hii kuliko kuhoji makahaba ingejikita mahakamani kutafuta TAKWIMU za sababu zinazopelekea ndoa kuvunjika, tuone kama kuombwa nyuma ingeibuka kinara!!