Makonda amesema kweli; wengi wa viongozi wa Serikali hii ya CCM wanafanya usanii kumpa sifa Rais Samia, lakini kivitendo wanamhujumu

Makonda amesema kweli; wengi wa viongozi wa Serikali hii ya CCM wanafanya usanii kumpa sifa Rais Samia, lakini kivitendo wanamhujumu

[emoji1666][emoji106]
Unaamini wasaidizi wanamuangusha Samia kwanini asiwaondoe kama anaona wanamuangusha?

Mkiitwa chawa mnakuwa wakali, ukweli ni kwamba Samia amefeli kuliongoza hili taifa, ameshindwa kabisa.

Huu mgao wa umeme zaidi ya miezi sita, ajabu bado mpo mnaoona anajitahidi kurekebisha makosa ya Magufuli!.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Pengine mtu mbaye anabeba vichwa vya habari kwa sasa kuliko mtu mwingine yoyote hapa nchini kwa sasa ni Paul Makonda aka Bashite.

Watu wanajiuliza maswali mengi, iweje mtu huyu huyu, kwenye utawala wa awamu ya 5, chini ya Mwendazake, alionekana kuwa ni mhalifu mkubwa, leo hii kwenye utawala wa awamu ya 6 aonekane kama shujaa na mtetezi wa wanyonge?

Kabla sijalijibu swali hilo, hebu tuangalie harakati anazofanya Katibu huyu wa uenezi wa CCM, katika kipindi hiki.

Anaitisha mikutano ya hadhara kwenye maeneo mbalimbali nchini na kusikiliza kero za wananchi na kujaribu kuzitatua papo kwa papo

Amekuwa ni mwiba kwa viongozi wa serikali hii ya CCM, ambao wameonekana wazi kuwa hawatatui matatizo ya wananchi kwa wakati na badala yake hao viongozi kila uchao, wamebaki kumsifia kinafiki Rais Samia Suluhu Hassan!

Hebu tujaribu kuangalia matatizo sugu ambayo watanzania hivi sasa wanakabiliana nayo:-

1. Tatizo la kukatika katika kwa umeme, kusiko na ratiba maalum, licha ya viongozi waliopo madarakani kutuhakikishia sisi wananchi kuwa tatizo hilo linatokana na mabwawa yetu yanayozalisha umeme kukauka.

Mungu naye amewaheleleza viongozi wa serikali hii ya CCM, kwa kuleta mvua ya El nino hadi mabwawa hayo yanayozalisha huo umeme wetu kufurika maji, lakini tunaendelea kushuhudia mgao wa umeme mkali kuliko wakati wowote, tokea nchi yetu ipate uhuru wake!

2. Kuna tatizo la kupaa kwa bei ya sukari, ambayo hivi sasa kuna baadhi ya maeneo hapa nchini, bidhaa hiyo inapatikana kwa bei ya mara dufu ya bei elekezi ya shilingi elfu 3 kwa kilo moja

3. Upandaji mkubwa wa nauli za daladala na mabasi yaendayo mikoani, ambako kumeleta maisha magumu sana kwa wananchi wanyonge wa nchi hii, kwa kisingizio cha upandaji wa bei ya mafuta ya petroli duniani, wakati katika hali halisi, mafuta hayo yameendelea kushuka kwa mwezi wa 3 mfululizo!

Nimemsikia Makonda katika hotuba yake ya majuzi huko mkoani Iringa, akiwaambia wananchi wa huko kuwa viongozi wengi wa serikali hii, wanapenda kumsifia Rais Samia, wakati kivitendo hawamsaidii Rais huyo, kutokana na kutoshughulikia matatizo yao ya msingi wanayokabiliana nayo hao wananchi

Hayo ni baadhi tu ya matatizo sugu wanayokabiliana nayo wananchi, huku viongozi wao hawachukui hatua yoyote ya kuyatatua na badala yake, wamekuwa wakiendelea kumpa sifa zilizopitiliza kwa Rais wetu Samia Suluhu Hassan, kuwa anaupiga mwingi katika awamu yake na wengine wakitia "chumvi" kuwa ni Rais ambaye amefanya makubwa, kuliko Rais yeyote katika awamu zilizopita!

Hivi kiongozi unapata wali ujasiri wa kumsifu Rais Samia, kuwa amefanya makubwa kuliko Rais yeyote wa awamu zilizopita, wakati katika hali halisi, yeye Samia ndiye amefeli pakubwa kuliko Rais yeyote wa awamu zilizopita??

Lakini jibu ni moja tu, hao viongozi wanakuwa wanafiki na kujipendekeza kwa Rais Samia, kutokana na ubovu wa Katiba yetu, ambayo imempa madaraka makubwa mno ya kimungu-mtu Rais wetu, ambapo kila kiongozi a serikali hii, inabidi ajipenddkeze kwake ili asimsahau katika teuzi za maelfu ya ajira za serikalini!

Sasa swali kubwa wanalojiuliza wananchi, je huyu ni ndiye Bashite ambaye tulimzoea wa wakati wa awamu ya 5, ambaye alikuwa anazivunja sheria za nchi waziwazi, kwa mfano kuvamia kituo cha televisheni cha Clouds na askari wenye hunduko na vitendo vingine vingi vya uvunjaji wa sheria au huyu Makonda wa uongozi wa awamu ya 6, amekuja kivingine kabisa?

Jibu ambalo mimi naweza kulitoa, baada ya kutafakari kwa kina kwa muda mrefu, ni kuwa huyu Makonda wa sasa ni kiumbe kipya, ambaye ametubu madhambi aliyoyafanya hapo siku za nyuma na hivi sasa amezaliwa upya kwa mara ya pili!

Hata kwenye mafundisho ya dini, yanasema mtu ambaye anatubu dhambi zake za awali na kuamua kuwa ni kiumbe kipya, basi hata Mungu atakuwa amemsamehe dhambi zake
Tayari Fereshi kamtia doa jingine mama. MAHAKAMA KUU TANZANIA IMETENGUA UAMUZI WA RAIS SAMIA WA KUMSTAAFISHA KWA MANUFAA YA UMMA ALIYEKUWA DC WA TABORA BWANA KOMANYA.
 
Ukumbuke kipindi cha Mwendazake biashara nyingi zilikufa, wawekezaji wengi walisepa na viwanda vingi vilipunguza uzalishaji na hivyo matumizi ya umeme kushuka.
Mkuu Mizania,

Unadai Biashara zilikufa.

Je, ni biashara zipi hizo ili Watanzania tuzijue?

Sio hivyo tu, umedai wawekezaji wengi walisepa na hivyo kufanya viwanda vingi kupunguza , uzalishaji.

Ni sababu zipi hizo zilizo fanya Wawekezaji kusepa, na ni viwanda vipi hivyo vilivyopunguza Uzalishaji? Unayo mifano yeyote ile?

Je, unaweza kutupatia chanzo cha taarifa zako? au hayo ni maoni yako tu?
 
H
Mkuu;

Sukari ilianza kupanda bei kipindi gani?

Mafuta yameanza kupanda kipindi gani?

Mafuta ya kula yameanza kupanda bei kipindi gani?

Umeme ulipanda bei kipindi gani?

Nauli ilianza kupanda kipindi gani?

Muda wa maongezi ulianza kupanda kipindi gani?

Maharage na unga vilianza kupanda kipindi gani?

Gharama za matibabu yalianza kupanda kipindi gani?

Kudaiwa maiti kulianza kipindi gani?

Mkuu ujinga na upumbavu wetu huo hauondoi ukweli kuwa tuliishi kipindi hiko tukishuhudia upandaji huo!

Tuambizane ukweli! Tuachie unafiki!
Huna kumbukumbu wewe Mbwiga. Tuliza Makalio na chuki zako kwa shujaa
 
Mkuu;

Sukari ilianza kupanda bei kipindi gani?

Mafuta yameanza kupanda kipindi gani?

Mafuta ya kula yameanza kupanda bei kipindi gani?

Umeme ulipanda bei kipindi gani?

Nauli ilianza kupanda kipindi gani?

Muda wa maongezi ulianza kupanda kipindi gani?

Maharage na unga vilianza kupanda kipindi gani?

Gharama za matibabu yalianza kupanda kipindi gani?

Kudaiwa maiti kulianza kipindi gani?

Mkuu ujinga na upumbavu wetu huo hauondoi ukweli kuwa tuliishi kipindi hiko tukishuhudia upandaji huo!

Tuambizane ukweli! Tuachie unafiki!
Kila awamu zilizopita bidhaa zilipanda bei , lakini tunachojiuliza ni kwamba zilipanda kwa kiasi gani ?
Je kwenye awamu hii watu wamepandisha sana bei za bidhaa kuliko awamu zilizopita ?
 
Hili taifa lina watu wapumbavu sana,na kwa mwendo huu wengi wamepumbazika kwa siasa za maji taka za Bashite.

Mtu anafanya pretty issuee kabisa lakini ndo anamwangiwa sifa za kipumbavu na wapumbavu.Prof.Seithy chachange alikuwa mbele ya muda wa kuona upumbavu wa Watanzania.

Endeleeni kuimba sifa na mapambio lakini majibu yenyewe mtayapata muda sio mrefu.
Wewe ndo mpumbavu!! Acha Wizi kafanye kazi ya Umma hakuna atakayekugusa
 
Ni kweli kabisa
Sifa zinatolewa kupita hali halisi on the Ground !
Wafanye kazi zao sawasawa ili wamsaidie Mheshimiwa Rais !
Hata yeye hapendi kuvishwa vilemba vya Ukoka !
Na huyo Makonda kama kweli ametubu basi atubu kikweli kweli maana Mungu ana uwezo wa kumpindua juu chini sekunde yeyote ile !
Piga kazi Makonda, waumbue mafisadi na wabadhirifu huko Chamani na nje ya Chama !
Ukifanya hivyo tutakuunga mkono ๐Ÿ™๐Ÿ™๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ
Absolutely true
 
Mkuu Mizania,

Unadai Biashara zilikufa.

Je, ni biashara zipi hizo ili Watanzania tuzijue?

Sio hivyo tu, umedai wawekezaji wengi walisepa na hivyo kufanya viwanda vingi kupunguza , uzalishaji.

Ni sababu zipi hizo zilizo fanya Wawekezaji kusepa, na ni viwanda vipi hivyo vilivyopunguza Uzalishaji? Unayo mifano yeyote ile?

Je, unaweza kutupatia chanzo cha taarifa zako? au hayo ni maoni yako tu?
Huwezi kujibiwa ๐Ÿ™๐Ÿ™
 
"Samia ni Rais ambaye amefeli kuliko Rais yeyote kwenye historia ya Marais wa nchi yetu". Nakubaliana na mleta mada 100%.
Na kafeli kweli kweli, atahitaji kusaidiwa kijiti cha uongozi hata kwa kutumia figisu.
 
Akili nyingi za watanzania ni kama za huyu Jamaa Kuonyezha kuwa We are reach of foolish people.
What you should know is Hakuna CCM na Serikali Ni watu wajinga tu wakiona Mpishi kabadilishwa wanafikiri zitakuja mboga mpya. Kuweni na akili tunatafuta Kura zenu.
 
Mkuu Mizania,

Unadai Biashara zilikufa.

Je, ni biashara zipi hizo ili Watanzania tuzijue?

Sio hivyo tu, umedai wawekezaji wengi walisepa na hivyo kufanya viwanda vingi kupunguza , uzalishaji.

Ni sababu zipi hizo zilizo fanya Wawekezaji kusepa, na ni viwanda vipi hivyo vilivyopunguza Uzalishaji? Unayo mifano yeyote ile?

Je, unaweza kutupatia chanzo cha taarifa zako? au hayo ni maoni yako tu?
Yaap atwambiie so analopoka tuuu
 
Kila awamu zilizopita bidhaa zilipanda bei , lakini tunachojiuliza ni kwamba zilipanda kwa kiasi gani ?
Je kwenye awamu hii watu wamepandisha sana bei za bidhaa kuliko awamu zilizopita ?
Mkuu na kuelewa na hoja yako ina ukweli kabisa.

Tukiwa wa kweli tunapaswa kuanza kuangalia tulipo jikwaa sio tulipodondokea.

Ukweli ni kwamba Magufuli alivuruga the economic fabric and setting ya nchi yetu kwa kiasi kikubwa ndani ya muda mfupi. Madhara yake ndio yanaanza kujionyesha sasa!

Magufuli aliweka mazingira magumu ya kufanya biashara nchini, mazingira yaliyowafukuza wawekezaji wengi wa nje na ndani, wakulima, wafugaji na wavuvi

Magufuli hakufanya chochote kwenye ajira na maslahi ya wafanyakazi. Hii ndiyo nguzo ya mizunguko wa fedha.

Magufuli alianzisha miradi mikubwa mingi kwa wakati mmoja ambayo mpaka ama haijaaza kuingiza fedha au inajiendesha kwa hasara.

Magufuli alikopa kiasi kikubwa cha fedha kwenye ma benki ya ndani na nje ya kibiashara yenye riba kubwa na ya muda mfupi. Muda wa kulipa umeiva.

Magufuli aliharibu mahusiano ya kimataifa kwa namna ambayo misaada na mikopo nafuu ikasitishwa kwetu.

Magufuli alichota kiasi kikubwa cha fedha kutoka mashirika ya umma na mifuko ya kijamii kuanzisha miradi yake hiyo kiasi cha kufilisika.

Kwa Mujibu wa ripoti ya CAG ya miaka mitano 5 ya kipindi cha Magufuli, ndio kipindi ufisadi ulifika zaidi ya Trilioni 1.5 kila mwaka na deni la taifa kuongezeka mara dufu!

Bahati mbaya hayupo, ulitegemea kwa hali na mazingira haya mambo yakae sawa sawa??? Haiwezekani labda ndotoni.

Tukubali kuwa huu ndio ukweli na uhalisia wa maisha. Tulikuwa tunapiga makofi akivuruga, kwa sasa tutulie kimya maumivu yatufungue akili.
 
Huwezi kujibiwa ๐Ÿ™๐Ÿ™
Mkuu,

sio kwamba siwezi kumjibu, ila iko hivi kama anaona nilichosema sio kweli ama ni uongo, akanushe au apinge au asahihishe majibu yangu kwa kuweka ukweli wake hapa kutoka hicho chanzo chake ambacho anadai ni cha ukweli.

Huo ndio msingi wa mjadala wowote duniani. Nina amini ataleta hizo facts zake dhidi ya za kwangu ili kutuelimisha na kutusahihisha mapema iwezekanavyo.

Huu ni mjadala sio mpasho!
 
Kuna wakati nikikusoma huwa nakuona kama mtu aliyekaribu na kuchanganyikiwa. Hizi siasa zetu msipojua namna ya kwenda nazo, mtaishia kupata vidonda vya tumbo.

Hebu iweke hiyo level yako of thinking hapa tuione....

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Kama unamuona Makonda is doing a Good Job, he is mentally OK upstairs, then you are done and you are at liberty to think so, but subject people's opinion as I have done! Usijiweke katika level ya proletariats Najua wewe hauko hivyo lakini....... Hao anaowatukana mawaziri etc wanaogopa kumjibu kwa kutetea ugali wao.
Anyway, my thinking is on these lines as expounded by Philosopher, and Psychologist Askofu Bagonza in his post copied here below!!
ALL IN ALL NISAMEHE KAMA YOU WERE NOT PLEASANT WITH MY EARLIER COMMENT, MY APOLOGIES!
Anaandika kwa Ufasaha: Askofu Dr Benson Lwakalinda BAGONZA
๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡๐Ÿ‘‡
MAKONDA: Ni Tatizo, Dalili au Suluhisho?

Paul Makonda ni zaidi Katibu Mwenezi wa chama Tawala. Tumewahi kuwa nao wengi na wapo wengi wa vyama vingine. Hakuna kama Makonda uzuri na kwa ubaya. Kwa nini?

1. Kama Makonda ni tatizo basi halina suluhisho. Kwa sababu ndani ya chama tawala huyu ndiye ameonekana. Na kama huyu ndiye bora zaidi, waliobaki wana hali gani?

2. Kama Makonda ni dalili ya tatizo basi dalili huwa hazina tiba. Tusubiri ugonjwa wenyewe ndipo tujue tiba. Mgonjwa anayetetemeka kwa homa, kumfunika blanketi zito si kutibu ugonjwa. Ni kusaidia mayai ya vimelea yaanguliwe na mgonjwa atakuwa na hali mbaya zaidi.

3. Kama Makonda ni Suluhisho basi ni lile la โ€œBomoa yote tutajenga keshoโ€. Mchelea mwana kulia hulia yeye mwenyewe. Yeye amekuwa suluhisho zaidi ya dawa ya rangi mbili inayoua vimelea vyote mwilini.

AMESAIDIA SANA:

- Sasa tunajua hali yetu si njema. Hakuna utawala wa sheria wala wa mfumo.

- Sasa tunajua hasara za kukaa gizani. Ukikosa upinzani bungeni na mabarazani, ukakosa uhuru wa habari, ukakosa wana harakati huru, unastawisha CHAWA kila mahali.

- Sasa tunajua wananchi wanaona bora dikteta kuliko demokrasia, yaani bora shibe ya gerezani kuliko njaa ya uraiani.

- Sasa tunajua wenye shida wanataka mtu si taasisi wala mfumo.

- Sasa tunajua kila suluhisho linazaa tatizo. Ukifuga mbwa mkali wa kulinda wezi, kuna siku atakuzuia wewe usiingie nyumbani kwako.

- Sasa tunajua hakuna bunge huru, hakuna mahakama huru, hakuna DPP huru, hakuna AG huru - ila kuna Chama huru.

HEKIMA: Kuna mbwa akiwinda na kukamata mawindo, huwezi kumfukuza eti anaharibu ngozi. Atakula kitoweo chote na mwenye mbwa atakula mchicha siku hiyo.
 
Pengine mtu mbaye anabeba vichwa vya habari kwa sasa kuliko mtu mwingine yoyote hapa nchini kwa sasa ni Paul Makonda aka Bashite.

Watu wanajiuliza maswali mengi, iweje mtu huyu huyu, kwenye utawala wa awamu ya 5, chini ya Mwendazake, alionekana kuwa ni mhalifu mkubwa, leo hii kwenye utawala wa awamu ya 6 aonekane kama shujaa na mtetezi wa wanyonge?

Kabla sijalijibu swali hilo, hebu tuangalie harakati anazofanya Katibu huyu wa uenezi wa CCM, katika kipindi hiki.

Anaitisha mikutano ya hadhara kwenye maeneo mbalimbali nchini na kusikiliza kero za wananchi na kujaribu kuzitatua papo kwa papo

Amekuwa ni mwiba kwa viongozi wa serikali hii ya CCM, ambao wameonekana wazi kuwa hawatatui matatizo ya wananchi kwa wakati na badala yake hao viongozi kila uchao, wamebaki kumsifia kinafiki Rais Samia Suluhu Hassan!

Hebu tujaribu kuangalia matatizo sugu ambayo watanzania hivi sasa wanakabiliana nayo:-

1. Tatizo la kukatika katika kwa umeme, kusiko na ratiba maalum, licha ya viongozi waliopo madarakani kutuhakikishia sisi wananchi kuwa tatizo hilo linatokana na mabwawa yetu yanayozalisha umeme kukauka.

Mungu naye amewaheleleza viongozi wa serikali hii ya CCM, kwa kuleta mvua ya El nino hadi mabwawa hayo yanayozalisha huo umeme wetu kufurika maji, lakini tunaendelea kushuhudia mgao wa umeme mkali kuliko wakati wowote, tokea nchi yetu ipate uhuru wake!

2. Kuna tatizo la kupaa kwa bei ya sukari, ambayo hivi sasa kuna baadhi ya maeneo hapa nchini, bidhaa hiyo inapatikana kwa bei ya mara dufu ya bei elekezi ya shilingi elfu 3 kwa kilo moja

3. Upandaji mkubwa wa nauli za daladala na mabasi yaendayo mikoani, ambako kumeleta maisha magumu sana kwa wananchi wanyonge wa nchi hii, kwa kisingizio cha upandaji wa bei ya mafuta ya petroli duniani, wakati katika hali halisi, mafuta hayo yameendelea kushuka kwa mwezi wa 3 mfululizo!

Nimemsikia Makonda katika hotuba yake ya majuzi huko mkoani Iringa, akiwaambia wananchi wa huko kuwa viongozi wengi wa serikali hii, wanapenda kumsifia Rais Samia, wakati kivitendo hawamsaidii Rais huyo, kutokana na kutoshughulikia matatizo yao ya msingi wanayokabiliana nayo hao wananchi

Hayo ni baadhi tu ya matatizo sugu wanayokabiliana nayo wananchi, huku viongozi wao hawachukui hatua yoyote ya kuyatatua na badala yake, wamekuwa wakiendelea kumpa sifa zilizopitiliza kwa Rais wetu Samia Suluhu Hassan, kuwa anaupiga mwingi katika awamu yake na wengine wakitia "chumvi" kuwa ni Rais ambaye amefanya makubwa, kuliko Rais yeyote katika awamu zilizopita!

Hivi kiongozi unapata wali ujasiri wa kumsifu Rais Samia, kuwa amefanya makubwa kuliko Rais yeyote wa awamu zilizopita, wakati katika hali halisi, yeye Samia ndiye amefeli pakubwa kuliko Rais yeyote wa awamu zilizopita??

Lakini jibu ni moja tu, hao viongozi wanakuwa wanafiki na kujipendekeza kwa Rais Samia, kutokana na ubovu wa Katiba yetu, ambayo imempa madaraka makubwa mno ya kimungu-mtu Rais wetu, ambapo kila kiongozi a serikali hii, inabidi ajipenddkeze kwake ili asimsahau katika teuzi za maelfu ya ajira za serikalini!

Sasa swali kubwa wanalojiuliza wananchi, je huyu ni ndiye Bashite ambaye tulimzoea wa wakati wa awamu ya 5, ambaye alikuwa anazivunja sheria za nchi waziwazi, kwa mfano kuvamia kituo cha televisheni cha Clouds na askari wenye hunduko na vitendo vingine vingi vya uvunjaji wa sheria au huyu Makonda wa uongozi wa awamu ya 6, amekuja kivingine kabisa?

Jibu ambalo mimi naweza kulitoa, baada ya kutafakari kwa kina kwa muda mrefu, ni kuwa huyu Makonda wa sasa ni kiumbe kipya, ambaye ametubu madhambi aliyoyafanya hapo siku za nyuma na hivi sasa amezaliwa upya kwa mara ya pili!

Hata kwenye mafundisho ya dini, yanasema mtu ambaye anatubu dhambi zake za awali na kuamua kuwa ni kiumbe kipya, basi hata Mungu atakuwa amemsamehe dhambi zake
mbona unasema ukweli aisee ๐Ÿ’
 
Haya ya 5 kutoka chini ni mbinu nzuri ya kuwashika wanyonge.
Mkuu usipumbazwe kabisa, chui habadiliki madoa ya ngozi yake asilani.

Matatizo uliyoyaainisha yana ugumu wa kuyatatua kwa haraka pasipo mpango mkakati uliosukwa vizuri. Makonda anajua fika shida ilipo maana kwenye vikao muhimu yumo.

Mabwawa tunayotegemea ni ya muda mrefu, hayana service na yamejaa tope hivyo kina cha maji kimepungua mno, unahitaji muda kuondoa hilo tope, wakati ukiwa hautumii hilo bwawa.
Makonda anafahamu vizuri. Ndio maana hazungumzii hilo anagangamara na individual issue.

Ili uyatoe matope mabwawani unahitaji chanzo cha nishati mbadala ambacho kwa bahati kwetu ni gesi, Makonda anafahamu jinsi baba yake, Mwendazake alivyovurunda na kuvuruga mkakati okozi, mbadala na wa kudumu wa nishati ya umeme, gesi ya kupikia majumbani na viwandani kisa tu ukosefu wa asilimia 10% kwa upande wake.

Kama ni mkweli na amejinyumbua kuwa kiumbe kipya awaambie wananchi shida ilipo!!!

Ukumbuke kipindi cha Mwendazake biashara nyingi zilikufa, wawekezaji wengi walisepa na viwanda vingi vilipunguza uzalishaji na hivyo matumizi ya umeme kushuka.

Makonda anajua vizuri na alijifunza barabara kutoka kwa babake, Mwendazake kuwa mbele ya macho ya the poor illiterate masses, watumishi wa serikali are the best punching bag!!!

Kuhusu upandaji wa bidhaa na nauli sababu zake ni very varied ila the common denominator ni mafuta, dolar, mvua na government policies juu ya kodi. Mvua imenyesha nyingi kwa kipindi kirefu, kwenye process ya uvunaji wa miwa haiwezekani!
It is obvious na ilitegemea kuwepo na uhaba na penye uhaba bei hupanda!

Uagizaji wa bidhaa mbali mbali umekutana na uhaba/ukata wa dola nchini! Kigingi kingine licha ya dola kuadimika, madafu yetu yameporomoka, huku serikali imeng'ang'ania msimamo wa kubaki na kodi hata ikiwezekana kuongeza kodi mpya bila kupandisha mishahara!

Unategemea kwa mazingira haya kwa wafanyabiashara bei itashuka!

Makonda anafahamu fika yote haya! Kama ni mkweli na ni kiumbe kipya basi awaambie ukweli wananchi!!!
 
Hiyo inasababishwa na upole wa kiongozi mkuu, anawapa vyeo halafu hawapi direction watendaji wake wafanye vipi majukumu yao, matokeo yake unakuta kila mmoja anaanza kwenda na njia yake, wakati mwingine inafikia wao kwa wao kupishana kauli ilimradi wabaki na sifa moja kuu, ya kumsifia mama.

Kinachotokea sasa Makonda anazunguka huko mikoani na wale wenye matatizo yao wanajitokeza mikutanoni, hawa ni haki yao kufanya hivyo kwasababu mtu ukiwa na shida mara nyingi huwezi kujali nani atakayekusaidia, ilimradi ujue yupo wa kusikiliza, basi utamfuata ukamwambie.

Wengine wanaona Makonda msanii, lakini binafsi nikitazama kile anachofanya Makonda kwa sasa, na uungwaji mkono anaopata, naona kabisa amewazidi wale wanaojiona wanajua "kufuata taratibu", waliopewa kazi ya kukinadi hicho chama chao ikawashinda, ndio maana Samia akaamua kumpa hiyo kazi Makonda, anayeonekana sasa kuifanya zaidi yao.

Baadae, kinachokuja kuyaunganisha hayo makundi mawili ni ile kauli moja tu toka kwa makundi yote, "mama anaupiga mwingi" hapo makundi yote mawili, licha ya tofauti zao kiutendaji yanabaki salama kwa mamlaka yao ya uteuzi.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Mkuu tatizo kubwa la nchi yetu ni mifumo mibovu iliyowekwa ambayo inamfanya kiongozi yeyote mkuu kuonekana mungumtu hivyo watawala hufanya wapendavyo,hivyo suluhisho ni viongozi wa chini ku opt uchawa ili wasavaiv
 
Back
Top Bottom