Makonda amesema kweli; wengi wa viongozi wa Serikali hii ya CCM wanafanya usanii kumpa sifa Rais Samia, lakini kivitendo wanamhujumu

Makonda amesema kweli; wengi wa viongozi wa Serikali hii ya CCM wanafanya usanii kumpa sifa Rais Samia, lakini kivitendo wanamhujumu

Mkuu na kuelewa na hoja yako ina ukweli kabisa.

Tukiwa wa kweli tunapaswa kuanza kuangalia tulipo jikwaa sio tulipodondokea.

Ukweli ni kwamba Magufuli alivuruga the economic fabric and setting ya nchi yetu kwa kiasi kikubwa ndani ya muda mfupi. Madhara yake ndio yanaanza kujionyesha sasa!

Magufuli aliweka mazingira magumu ya kufanya biashara nchini, mazingira yaliyowafukuza wawekezaji wengi wa nje na ndani, wakulima, wafugaji na wavuvi

Magufuli hakufanya chochote kwenye ajira na maslahi ya wafanyakazi. Hii ndiyo nguzo ya mizunguko wa fedha.

Magufuli alianzisha miradi mikubwa mingi kwa wakati mmoja ambayo mpaka ama haijaaza kuingiza fedha au inajiendesha kwa hasara.

Magufuli alikopa kiasi kikubwa cha fedha kwenye ma benki ya ndani na nje ya kibiashara yenye riba kubwa na ya muda mfupi. Muda wa kulipa umeiva.

Magufuli aliharibu mahusiano ya kimataifa kwa namna ambayo misaada na mikopo nafuu ikasitishwa kwetu.

Magufuli alichota kiasi kikubwa cha fedha kutoka mashirika ya umma na mifuko ya kijamii kuanzisha miradi yake hiyo kiasi cha kufilisika.

Kwa Mujibu wa ripoti ya CAG ya miaka mitano 5 ya kipindi cha Magufuli, ndio kipindi ufisadi ulifika zaidi ya Trilioni 1.5 kila mwaka na deni la taifa kuongezeka mara dufu!

Bahati mbaya hayupo, ulitegemea kwa hali na mazingira haya mambo yakae sawa sawa??? Haiwezekani labda ndotoni.

Tukubali kuwa huu ndio ukweli na uhalisia wa maisha. Tulikuwa tunapiga makofi akivuruga, kwa sasa tutulie kimya maumivu yatufungue akili.
Umemaliza kila kitu kiongozi,..miradi ilikuwa mizuri lakini kwa uwezo wetu,isingewezekana twende nayo yote kwa pamoja..NEVER..na shida ndio ilianzia hapa..yote kwa yote,ACHA MUNGU AITWE MUNGU!
 
Mkuu na kuelewa na hoja yako ina ukweli kabisa.

Tukiwa wa kweli tunapaswa kuanza kuangalia tulipo jikwaa sio tulipodondokea.

Ukweli ni kwamba Magufuli alivuruga the economic fabric and setting ya nchi yetu kwa kiasi kikubwa ndani ya muda mfupi. Madhara yake ndio yanaanza kujionyesha sasa!

Magufuli aliweka mazingira magumu ya kufanya biashara nchini, mazingira yaliyowafukuza wawekezaji wengi wa nje na ndani, wakulima, wafugaji na wavuvi

Magufuli hakufanya chochote kwenye ajira na maslahi ya wafanyakazi. Hii ndiyo nguzo ya mizunguko wa fedha.

Magufuli alianzisha miradi mikubwa mingi kwa wakati mmoja ambayo mpaka ama haijaaza kuingiza fedha au inajiendesha kwa hasara.

Magufuli alikopa kiasi kikubwa cha fedha kwenye ma benki ya ndani na nje ya kibiashara yenye riba kubwa na ya muda mfupi. Muda wa kulipa umeiva.

Magufuli aliharibu mahusiano ya kimataifa kwa namna ambayo misaada na mikopo nafuu ikasitishwa kwetu.

Magufuli alichota kiasi kikubwa cha fedha kutoka mashirika ya umma na mifuko ya kijamii kuanzisha miradi yake hiyo kiasi cha kufilisika.

Kwa Mujibu wa ripoti ya CAG ya miaka mitano 5 ya kipindi cha Magufuli, ndio kipindi ufisadi ulifika zaidi ya Trilioni 1.5 kila mwaka na deni la taifa kuongezeka mara dufu!

Bahati mbaya hayupo, ulitegemea kwa hali na mazingira haya mambo yakae sawa sawa??? Haiwezekani labda ndotoni.

Tukubali kuwa huu ndio ukweli na uhalisia wa maisha. Tulikuwa tunapiga makofi akivuruga, kwa sasa tutulie kimya maumivu yatufungue akili.
Ukweli utatuweka huru ! 🙏
 
Mkuu tatizo kubwa la nchi yetu ni mifumo mibovu iliyowekwa ambayo inamfanya kiongozi yeyote mkuu kuonekana mungumtu hivyo watawala hufanya wapendavyo,hivyo suluhisho ni viongozi wa chini ku opt uchawa ili wasavaiv
Kweli kabisa !
Na mpaka sasa bado wakubwa hawajaliona hili na kuazimia kulifanyia marekebisho kwenye Katiba. !!
Lakini mimi naamini iko siku atakuja kupatikana Kiongozi Mkuu atakaye wasulubu wenzake kupitia madaraka yake aliyonayo kwa mujibu wa Katiba hii mpaka maji wataita mma. !!
Ndipo watakapolia na kusema laiti tungejua !!
Mifano ilishajionyesha kuanzia 2016 !
Kwamba kumbe akipatikana Mwamba Nchi inaweza ikanyooka !!
🙏🙏🙏
 
Kila awamu zilizopita bidhaa zilipanda bei , lakini tunachojiuliza ni kwamba zilipanda kwa kiasi gani ?
Je kwenye awamu hii watu wamepandisha sana bei za bidhaa kuliko awamu zilizopita ?
Ni kweli Kila awamu, bidhaa mbalmbali zilipanda.

Swali la kujiuliza, je upandaji huo wa bidhaa ulikuwa katika Hali halisi?

Ndiyo maana, Mimi nimetoa mfano wa bidhaa 2 zilizopanda maradufu bei zake, nazo ni bei ya sukari, iliyopanda Kwa almost 100% na nauli za mabasi nayo ni almost 50%

Ukiangalia bei ya sukari, utaona kuwa kuna baadhi ya watu, ambao wamesababisha "scarcity" ya bidhaa hiyo ili ipande.

Tukija Kwa upande wa nauli za mabasi, tujikumbushe sababu kuu walizotoa hao wamiliki wa mabasi, wakati wanawaomba LATRA kupandosha nauli hizo, sababu kuu walizotoa ni kupanda Kwa bei ya mafuta ya petroli katika soko la dunia.

Swali la kuwauliza hao LATRA ni kuwa, mafuta yameshuka bei Katika soko la dunia, je kuna uhalali Gani wa kuendelea kutumia bei hizo hizo za nauli wakati bei za mafuta ya petroli zimeshuka??
 
Pengine mtu mbaye anabeba vichwa vya habari kwa sasa kuliko mtu mwingine yoyote hapa nchini kwa sasa ni Paul Makonda aka Bashite.

Watu wanajiuliza maswali mengi, iweje mtu huyu huyu, kwenye utawala wa awamu ya 5, chini ya Mwendazake, alionekana kuwa ni mhalifu mkubwa, leo hii kwenye utawala wa awamu ya 6 aonekane kama shujaa na mtetezi wa wanyonge?

Kabla sijalijibu swali hilo, hebu tuangalie harakati anazofanya Katibu huyu wa uenezi wa CCM, katika kipindi hiki.

Anaitisha mikutano ya hadhara kwenye maeneo mbalimbali nchini na kusikiliza kero za wananchi na kujaribu kuzitatua papo kwa papo

Amekuwa ni mwiba kwa viongozi wa serikali hii ya CCM, ambao wameonekana wazi kuwa hawatatui matatizo ya wananchi kwa wakati na badala yake hao viongozi kila uchao, wamebaki kumsifia kinafiki Rais Samia Suluhu Hassan!

Hebu tujaribu kuangalia matatizo sugu ambayo watanzania hivi sasa wanakabiliana nayo:-

1. Tatizo la kukatika katika kwa umeme, kusiko na ratiba maalum, licha ya viongozi waliopo madarakani kutuhakikishia sisi wananchi kuwa tatizo hilo linatokana na mabwawa yetu yanayozalisha umeme kukauka.

Mungu naye amewaheleleza viongozi wa serikali hii ya CCM, kwa kuleta mvua ya El nino hadi mabwawa hayo yanayozalisha huo umeme wetu kufurika maji, lakini tunaendelea kushuhudia mgao wa umeme mkali kuliko wakati wowote, tokea nchi yetu ipate uhuru wake!

2. Kuna tatizo la kupaa kwa bei ya sukari, ambayo hivi sasa kuna baadhi ya maeneo hapa nchini, bidhaa hiyo inapatikana kwa bei ya mara dufu ya bei elekezi ya shilingi elfu 3 kwa kilo moja

3. Upandaji mkubwa wa nauli za daladala na mabasi yaendayo mikoani, ambako kumeleta maisha magumu sana kwa wananchi wanyonge wa nchi hii, kwa kisingizio cha upandaji wa bei ya mafuta ya petroli duniani, wakati katika hali halisi, mafuta hayo yameendelea kushuka kwa mwezi wa 3 mfululizo!

Nimemsikia Makonda katika hotuba yake ya majuzi huko mkoani Iringa, akiwaambia wananchi wa huko kuwa viongozi wengi wa serikali hii, wanapenda kumsifia Rais Samia, wakati kivitendo hawamsaidii Rais huyo, kutokana na kutoshughulikia matatizo yao ya msingi wanayokabiliana nayo hao wananchi

Hayo ni baadhi tu ya matatizo sugu wanayokabiliana nayo wananchi, huku viongozi wao hawachukui hatua yoyote ya kuyatatua na badala yake, wamekuwa wakiendelea kumpa sifa zilizopitiliza kwa Rais wetu Samia Suluhu Hassan, kuwa anaupiga mwingi katika awamu yake na wengine wakitia "chumvi" kuwa ni Rais ambaye amefanya makubwa, kuliko Rais yeyote katika awamu zilizopita!

Hivi kiongozi unapata wali ujasiri wa kumsifu Rais Samia, kuwa amefanya makubwa kuliko Rais yeyote wa awamu zilizopita, wakati katika hali halisi, yeye Samia ndiye amefeli pakubwa kuliko Rais yeyote wa awamu zilizopita??

Lakini jibu ni moja tu, hao viongozi wanakuwa wanafiki na kujipendekeza kwa Rais Samia, kutokana na ubovu wa Katiba yetu, ambayo imempa madaraka makubwa mno ya kimungu-mtu Rais wetu, ambapo kila kiongozi a serikali hii, inabidi ajipenddkeze kwake ili asimsahau katika teuzi za maelfu ya ajira za serikalini!

Sasa swali kubwa wanalojiuliza wananchi, je huyu ni ndiye Bashite ambaye tulimzoea wa wakati wa awamu ya 5, ambaye alikuwa anazivunja sheria za nchi waziwazi, kwa mfano kuvamia kituo cha televisheni cha Clouds na askari wenye hunduko na vitendo vingine vingi vya uvunjaji wa sheria au huyu Makonda wa uongozi wa awamu ya 6, amekuja kivingine kabisa?

Jibu ambalo mimi naweza kulitoa, baada ya kutafakari kwa kina kwa muda mrefu, ni kuwa huyu Makonda wa sasa ni kiumbe kipya, ambaye ametubu madhambi aliyoyafanya hapo siku za nyuma na hivi sasa amezaliwa upya kwa mara ya pili!

Hata kwenye mafundisho ya dini, yanasema mtu ambaye anatubu dhambi zake za awali na kuamua kuwa ni kiumbe kipya, basi hata Mungu atakuwa amemsamehe dhambi zake
Wanaomuita mhalifu ni Chadema bila ushahidi.

Makonda amekuwa heavyweight awamu ya 5 na Sasa awamu ya 6
 
Tatizo lipo Kwa Rais mwenyewe kupenda kusifiwa kuliko uhalisia wa matokeo ya kazi anayofanya,
 
Wanaomuita mhalifu ni Chadema bila ushahidi.

Makonda amekuwa heavyweight awamu ya 5 na Sasa awamu ya 6
Unasemaje wanaomuita mhalifu ni Chadema pekee?

Hivi nani asiyejua kuwa yeye Makonda, aliingia kwenye kituo Cha habari Cha Clouds TV, akiwa na askari wenye mitutu, ambapo ni kitendo Cha jinai??

Hivi ni nani asiyefahamu kuwa hata kwenye nchi za wenzetu, walibaini uhalifu wa huyu Bashite, hadi nchi ya Marekani, kumpiga marufuku kukanyaga katika ardhi ya nchi hiyo, yeye na familia yake, Kwa kile walichokiita kuwa yeye Makonda, anawanyima Raia wa nchi hii kuishi??

Hivi kweli umewaelewa wamarekani Kwa kusema kuwa Makonda, anawanyima raia wake haki ya kuishi??
 
Kama unamuona Makonda is doing a Good Job, he is mentally OK upstairs, then you are done and you are at liberty to think so, but subject people's opinion as I have done! Usijiweke katika level ya proletariats Najua wewe hauko hivyo lakini....... Hao anaowatukana mawaziri etc wanaogopa kumjibu kwa kutetea ugali wao.
Anyway, my thinking is on these lines as expounded by Philosopher, and Psychologist Askofu Bagonza in his post copied here below!!
ALL IN ALL NISAMEHE KAMA YOU WERE NOT PLEASANT WITH MY EARLIER COMMENT, MY APOLOGIES!
Anaandika kwa Ufasaha: Askofu Dr Benson Lwakalinda BAGONZA
[emoji116][emoji116][emoji116][emoji116][emoji116]
MAKONDA: Ni Tatizo, Dalili au Suluhisho?

Paul Makonda ni zaidi Katibu Mwenezi wa chama Tawala. Tumewahi kuwa nao wengi na wapo wengi wa vyama vingine. Hakuna kama Makonda uzuri na kwa ubaya. Kwa nini?

1. Kama Makonda ni tatizo basi halina suluhisho. Kwa sababu ndani ya chama tawala huyu ndiye ameonekana. Na kama huyu ndiye bora zaidi, waliobaki wana hali gani?

2. Kama Makonda ni dalili ya tatizo basi dalili huwa hazina tiba. Tusubiri ugonjwa wenyewe ndipo tujue tiba. Mgonjwa anayetetemeka kwa homa, kumfunika blanketi zito si kutibu ugonjwa. Ni kusaidia mayai ya vimelea yaanguliwe na mgonjwa atakuwa na hali mbaya zaidi.

3. Kama Makonda ni Suluhisho basi ni lile la “Bomoa yote tutajenga kesho”. Mchelea mwana kulia hulia yeye mwenyewe. Yeye amekuwa suluhisho zaidi ya dawa ya rangi mbili inayoua vimelea vyote mwilini.

AMESAIDIA SANA:

- Sasa tunajua hali yetu si njema. Hakuna utawala wa sheria wala wa mfumo.

- Sasa tunajua hasara za kukaa gizani. Ukikosa upinzani bungeni na mabarazani, ukakosa uhuru wa habari, ukakosa wana harakati huru, unastawisha CHAWA kila mahali.

- Sasa tunajua wananchi wanaona bora dikteta kuliko demokrasia, yaani bora shibe ya gerezani kuliko njaa ya uraiani.

- Sasa tunajua wenye shida wanataka mtu si taasisi wala mfumo.

- Sasa tunajua kila suluhisho linazaa tatizo. Ukifuga mbwa mkali wa kulinda wezi, kuna siku atakuzuia wewe usiingie nyumbani kwako.

- Sasa tunajua hakuna bunge huru, hakuna mahakama huru, hakuna DPP huru, hakuna AG huru - ila kuna Chama huru.

HEKIMA: Kuna mbwa akiwinda na kukamata mawindo, huwezi kumfukuza eti anaharibu ngozi. Atakula kitoweo chote na mwenye mbwa atakula mchicha siku hiyo.
- Sio wote wanaoogopa kumjibu Makonda, ndio maana Bashe alimjibu, na hiki ndicho nilichozungumzia kwenye my first comment uliyojibu kwa namna uliyoona kwako inafaa, hope hapa nimekuonesha vizuri nini nilikuwa namaanisha na umeelewa.

- Makonda amepewa kazi ya kukitangaza chama chao, kumkejeli humu JF wakati kule field tunaona watu wanaojitokeza kumsikiliza, hata kama mtawaita wajinga, na Makonda mumuone mjinga, lakini huo ndio ukweli, ana watu wanaomfuata na kumsikiliza, ndio wenye matatizo yao wanaotaka misaada, huu ni mfano wangu wa pili nilioandika kule juu ukaishia kujibu ulivyoona inafaa.

- Lastly, unasema your way of thinking ni kama ya Askofu Bagonza, hapo aliposema sasa wananchi wanapenda dikteta zaidi ya demokrasia hope upo nae pamoja!.
Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Kama unamuona Makonda is doing a Good Job, he is mentally OK upstairs, then you are done and you are at liberty to think so, but subject people's opinion as I have done! Usijiweke katika level ya proletariats Najua wewe hauko hivyo lakini....... Hao anaowatukana mawaziri etc wanaogopa kumjibu kwa kutetea ugali wao.
Anyway, my thinking is on these lines as expounded by Philosopher, and Psychologist Askofu Bagonza in his post copied here below!!
ALL IN ALL NISAMEHE KAMA YOU WERE NOT PLEASANT WITH MY EARLIER COMMENT, MY APOLOGIES!
Anaandika kwa Ufasaha: Askofu Dr Benson Lwakalinda BAGONZA
[emoji116][emoji116][emoji116][emoji116][emoji116]
MAKONDA: Ni Tatizo, Dalili au Suluhisho?

Paul Makonda ni zaidi Katibu Mwenezi wa chama Tawala. Tumewahi kuwa nao wengi na wapo wengi wa vyama vingine. Hakuna kama Makonda uzuri na kwa ubaya. Kwa nini?

1. Kama Makonda ni tatizo basi halina suluhisho. Kwa sababu ndani ya chama tawala huyu ndiye ameonekana. Na kama huyu ndiye bora zaidi, waliobaki wana hali gani?

2. Kama Makonda ni dalili ya tatizo basi dalili huwa hazina tiba. Tusubiri ugonjwa wenyewe ndipo tujue tiba. Mgonjwa anayetetemeka kwa homa, kumfunika blanketi zito si kutibu ugonjwa. Ni kusaidia mayai ya vimelea yaanguliwe na mgonjwa atakuwa na hali mbaya zaidi.

3. Kama Makonda ni Suluhisho basi ni lile la “Bomoa yote tutajenga kesho”. Mchelea mwana kulia hulia yeye mwenyewe. Yeye amekuwa suluhisho zaidi ya dawa ya rangi mbili inayoua vimelea vyote mwilini.

AMESAIDIA SANA:

- Sasa tunajua hali yetu si njema. Hakuna utawala wa sheria wala wa mfumo.

- Sasa tunajua hasara za kukaa gizani. Ukikosa upinzani bungeni na mabarazani, ukakosa uhuru wa habari, ukakosa wana harakati huru, unastawisha CHAWA kila mahali.

- Sasa tunajua wananchi wanaona bora dikteta kuliko demokrasia, yaani bora shibe ya gerezani kuliko njaa ya uraiani.

- Sasa tunajua wenye shida wanataka mtu si taasisi wala mfumo.

- Sasa tunajua kila suluhisho linazaa tatizo. Ukifuga mbwa mkali wa kulinda wezi, kuna siku atakuzuia wewe usiingie nyumbani kwako.

- Sasa tunajua hakuna bunge huru, hakuna mahakama huru, hakuna DPP huru, hakuna AG huru - ila kuna Chama huru.

HEKIMA: Kuna mbwa akiwinda na kukamata mawindo, huwezi kumfukuza eti anaharibu ngozi. Atakula kitoweo chote na mwenye mbwa atakula mchicha siku hiyo.
- Sio wote wanaoogopa kumjibu Makonda, ndio maana Bashe alimjibu, na hiki ndicho nilichozungumzia kwenye my first comment uliyojibu kwa namna uliyoona kwako inafaa. Hope hapa nimekuonesha vizuri nini nilikuwa namaanisha na umeelewa. Hao watu wawili wana mgogoro kati yao lakini wanakuwa connected na kumsifia Samia, hivyo wote wanabaki salama.

- Makonda amepewa kazi ya kukitangaza chama chao, kumtukana matusi ya nguoni kama mnavyofanya, au kumsifia kwa wale wanaomsifia, wote mnaonesha anafanikiwa kwenye kazi anayoifanya ya kukitangaza chama chake, ndio malengo ya kazi aliyopewa.

- Lastly, unaposema unafikiria kama Askofu Bagonza, hope inamaanisha uko pamoja nae hata pale anaposema wananchi sasa wanataka kuongozwa kidikteta zaidi ya kidemokrasia!.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Ni kweli Kila awamu, bidhaa mbalmbali zilipanda.

Swali la kujiuliza, je upandaji huo wa bidhaa ulikuwa katika Hali halisi?

Ndiyo maana, Mimi nimetoa mfano wa bidhaa 2 zilizopanda maradufu bei zake, nazo ni bei ya sukari, iliyopanda Kwa almost 100% na nauli za mabasi nayo ni almost 50%

Ukiangalia bei ya sukari, utaona kuwa kuna baadhi ya watu, ambao wamesababisha "scarcity" ya bidhaa hiyo ili ipande.

Tukija Kwa upande wa nauli za mabasi, tujikumbushe sababu kuu walizotoa hao wamiliki wa mabasi, wakati wanawaomba LATRA kupandosha nauli hizo, sababu kuu walizotoa ni kupanda Kwa bei ya mafuta ya petroli katika soko la dunia.

Swali la kuwauliza hao LATRA ni kuwa, mafuta yameshuka bei Katika soko la dunia, je kuna uhalali Gani wa kuendelea kutumia bei hizo hizo za nauli wakati bei za mafuta ya petroli zimeshuka??
Hapa kwetu bei hupanda tu !
Huwa hazishuki ! Sijawahi kusikia nauli zimeshuka !
 
Hilo la kutubu dhambi Mimi simo.hilo analijua muumba wetu
kwa matatizo uliyoyaorodhesha hapo kwa wengine wetu huku vijijini siyo vipaumbele vyetu.
Hata hiyo sukari hatuijui inatumiwa kwenye nini.sisi tunamahitaji yetu muhimu kama maji.huduma za Afya Nk
asanteni kwa yote
 
Ukweli unajulikana. Na utaendelea kujulikana.

This is a typical Grand art of Fabrication.
 
Mkuu;

Sukari ilianza kupanda bei kipindi gani?

Mafuta yameanza kupanda kipindi gani?

Mafuta ya kula yameanza kupanda bei kipindi gani?

Umeme ulipanda bei kipindi gani?

Nauli ilianza kupanda kipindi gani?

Muda wa maongezi ulianza kupanda kipindi gani?

Maharage na unga vilianza kupanda kipindi gani?

Gharama za matibabu yalianza kupanda kipindi gani?

Kudaiwa maiti kulianza kipindi gani?

Mkuu ujinga na upumbavu wetu huo hauondoi ukweli kuwa tuliishi kipindi hiko tukishuhudia upandaji huo!

Tuambizane ukweli! Tuachie unafiki!
Maswali yako yanaonesha dalili ya kama haukuwepo Nchini ndiyo umekuja toka ughaibuni..

Bahati mbaya sana jamii haiwezi kuweka rekodi ya tarehe ya kila bidhaa ilipopanda bei,nadhani unataka kutumia kichaka hicho kuficha udhaifu wa baadhi ya watu.

Kuanzia bajeti mpya ya serikali 2021/2022 ndiyo karibia kila bidhaa ilipoanda bei kwa kiwango cha juu ( utajua aliekua kiongozi mkuu alikua nani)

Utakumbuka ni kipindi hicho hicho kuna mtu alikua anasisitiza kuwa "kila kitu kitapanda bei" huku akisema ni kwa sababu ya covid...ndipo wafanyabiashara wengi wakaanza kupandisha bei za bidhaa maradufu..

Utakumbuka ni kipindi hicho Waziri mkuu aliingilia kati akamuagiza waziri wa viwanda Dr.Ashantu kupitia FCC wafanye uchunguzi ni kwanini bei za bidhaa zimepanda sana, FCC wakaja na majibu ya kuwa "hakuna sababu za msingi zilizofanya bidhaa kupanda bei"

Baada ya hapo yule yule aliesisitiza kuwa bidhaa zitapanda bei kwa sababu ya covid,akaja tena na maneno kuwa bidhaa zitapanda kwa sababu ya ukraine.

Kila awamu ya uongozi,bidhaa zilipanda bei,ila kwa kiasi gani zimepanda na sababu zilizosababisha upandaji huo ndiyo jambo la mjadala...

Kabla ya bajeti ya 2021/2022 ( kwa baadhi ya maeneo)
1:- Nomdo 12 mm, tulinunua elfu 19, ilipanda hadi elfu 28
2 :- Bati 30G, bando moja tulinunua laki 220,ilipanda hadi 350
3:-Mafuta ya kula ikawa gumzo
4:-Sabuni kila unavoenda dukani utakuta bei mpya
5:-kwa kifupi ni kila kitu
 
Hapa kwetu bei hupanda tu !
Huwa hazishuki ! Sijawahi kusikia nauli zimeshuka !
Bei zinapaswa kushuka, kama gharama za bidhaa hizo zimeshuka katika soko la dunia au soko la ndani.

Ukiona bei hazishuki, kutokana na factors hizo 2, ujue kuwa kuna hujuma
 
Bei zinapaswa kushuka, kama gharama za bidhaa hizo zimeshuka katika soko la dunia au soko la ndani.

Ukiona bei hazishuki, kutokana na factors hizo 2, ujue kuwa kuna hujuma
Kabisa
 
Makonda ananikumbusha Sauli wa kwenye biblia,toka kuwa mtesi mpaka kuwa mtetezi akiitwa baadae Paul.

Tumuelewe tu,watu ubadilika.
Sauli wa Tarso [emoji1], na baadaye akabatizwa na kuitwa Mt Paulo.

Kweli umewaza mbali sana mkuu.
 
Makonda anachokifanya ni sawa, kuchukua chupi ya baba ake iliyotoboka na kuitembeza mtaani.
Manake mambo anayosema leo anawavua nguo wazazi wake ambao CCM,hivyo akimariza ziara ajiandae kuwa barozi Malawi au Zambia, CCM hawana utamaduni wa kujivua nguo.
Kwahiyo kwakua amewavua nguo wenzake ajiandae kukutana na Kisanga kabla ya 2025.
Manake wazee wa kuchutama wamechutama.
 
Pengine mtu mbaye anabeba vichwa vya habari kwa sasa kuliko mtu mwingine yoyote hapa nchini kwa sasa ni Paul Makonda aka Bashite.

Watu wanajiuliza maswali mengi, iweje mtu huyu huyu, kwenye utawala wa awamu ya 5, chini ya Mwendazake, alionekana kuwa ni mhalifu mkubwa, leo hii kwenye utawala wa awamu ya 6 aonekane kama shujaa na mtetezi wa wanyonge?

Kabla sijalijibu swali hilo, hebu tuangalie harakati anazofanya Katibu huyu wa uenezi wa CCM, katika kipindi hiki.

Anaitisha mikutano ya hadhara kwenye maeneo mbalimbali nchini na kusikiliza kero za wananchi na kujaribu kuzitatua papo kwa papo

Amekuwa ni mwiba kwa viongozi wa serikali hii ya CCM, ambao wameonekana wazi kuwa hawatatui matatizo ya wananchi kwa wakati na badala yake hao viongozi kila uchao, wamebaki kumsifia kinafiki Rais Samia Suluhu Hassan!

Hebu tujaribu kuangalia matatizo sugu ambayo watanzania hivi sasa wanakabiliana nayo:-

1. Tatizo la kukatika katika kwa umeme, kusiko na ratiba maalum, licha ya viongozi waliopo madarakani kutuhakikishia sisi wananchi kuwa tatizo hilo linatokana na mabwawa yetu yanayozalisha umeme kukauka.

Mungu naye amewaheleleza viongozi wa serikali hii ya CCM, kwa kuleta mvua ya El nino hadi mabwawa hayo yanayozalisha huo umeme wetu kufurika maji, lakini tunaendelea kushuhudia mgao wa umeme mkali kuliko wakati wowote, tokea nchi yetu ipate uhuru wake!

2. Kuna tatizo la kupaa kwa bei ya sukari, ambayo hivi sasa kuna baadhi ya maeneo hapa nchini, bidhaa hiyo inapatikana kwa bei ya mara dufu ya bei elekezi ya shilingi elfu 3 kwa kilo moja

3. Upandaji mkubwa wa nauli za daladala na mabasi yaendayo mikoani, ambako kumeleta maisha magumu sana kwa wananchi wanyonge wa nchi hii, kwa kisingizio cha upandaji wa bei ya mafuta ya petroli duniani, wakati katika hali halisi, mafuta hayo yameendelea kushuka kwa mwezi wa 3 mfululizo!

Nimemsikia Makonda katika hotuba yake ya majuzi huko mkoani Iringa, akiwaambia wananchi wa huko kuwa viongozi wengi wa serikali hii, wanapenda kumsifia Rais Samia, wakati kivitendo hawamsaidii Rais huyo, kutokana na kutoshughulikia matatizo yao ya msingi wanayokabiliana nayo hao wananchi

Hayo ni baadhi tu ya matatizo sugu wanayokabiliana nayo wananchi, huku viongozi wao hawachukui hatua yoyote ya kuyatatua na badala yake, wamekuwa wakiendelea kumpa sifa zilizopitiliza kwa Rais wetu Samia Suluhu Hassan, kuwa anaupiga mwingi katika awamu yake na wengine wakitia "chumvi" kuwa ni Rais ambaye amefanya makubwa, kuliko Rais yeyote katika awamu zilizopita!

Hivi kiongozi unapata wali ujasiri wa kumsifu Rais Samia, kuwa amefanya makubwa kuliko Rais yeyote wa awamu zilizopita, wakati katika hali halisi, yeye Samia ndiye amefeli pakubwa kuliko Rais yeyote wa awamu zilizopita??

Lakini jibu ni moja tu, hao viongozi wanakuwa wanafiki na kujipendekeza kwa Rais Samia, kutokana na ubovu wa Katiba yetu, ambayo imempa madaraka makubwa mno ya kimungu-mtu Rais wetu, ambapo kila kiongozi a serikali hii, inabidi ajipenddkeze kwake ili asimsahau katika teuzi za maelfu ya ajira za serikalini!

Sasa swali kubwa wanalojiuliza wananchi, je huyu ni ndiye Bashite ambaye tulimzoea wa wakati wa awamu ya 5, ambaye alikuwa anazivunja sheria za nchi waziwazi, kwa mfano kuvamia kituo cha televisheni cha Clouds na askari wenye hunduko na vitendo vingine vingi vya uvunjaji wa sheria au huyu Makonda wa uongozi wa awamu ya 6, amekuja kivingine kabisa?

Jibu ambalo mimi naweza kulitoa, baada ya kutafakari kwa kina kwa muda mrefu, ni kuwa huyu Makonda wa sasa ni kiumbe kipya, ambaye ametubu madhambi aliyoyafanya hapo siku za nyuma na hivi sasa amezaliwa upya kwa mara ya pili!

Hata kwenye mafundisho ya dini, yanasema mtu ambaye anatubu dhambi zake za awali na kuamua kuwa ni kiumbe kipya, basi hata Mungu atakuwa amemsamehe dhambi zake
Yeye mwenyewe Makonda hizo ziara zake zinamhujumu Samia kwani uozo unaoibuliwa unafanywa na wateule wake na wote ni makada wa CCM
 
Hiyo inasababishwa na upole wa kiongozi mkuu, anawapa vyeo halafu hawapi direction watendaji wake wafanye vipi majukumu yao, matokeo yake unakuta kila mmoja anaanza kwenda na njia yake, wakati mwingine inafikia wao kwa wao kupishana kauli ilimradi wabaki na sifa moja kuu, ya kumsifia mama.

Kinachotokea sasa Makonda anazunguka huko mikoani na wale wenye matatizo yao wanajitokeza mikutanoni, hawa ni haki yao kufanya hivyo kwasababu mtu ukiwa na shida mara nyingi huwezi kujali nani atakayekusaidia, ilimradi ujue yupo wa kusikiliza, basi utamfuata ukamwambie.

Wengine wanaona Makonda msanii, lakini binafsi nikitazama kile anachofanya Makonda kwa sasa, na uungwaji mkono anaopata, naona kabisa amewazidi wale wanaojiona wanajua "kufuata taratibu", waliopewa kazi ya kukinadi hicho chama chao ikawashinda, ndio maana Samia akaamua kumpa hiyo kazi Makonda, anayeonekana sasa kuifanya zaidi yao.

Baadae, kinachokuja kuyaunganisha hayo makundi mawili ni ile kauli moja tu toka kwa makundi yote, "mama anaupiga mwingi" hapo makundi yote mawili, licha ya tofauti zao kiutendaji yanabaki salama kwa mamlaka yao ya uteuzi.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Aliyewataua walaji hao kwa wingi tunaachaje kuamini kuwa naye ni mlaji?
 
Back
Top Bottom