boaz mwalwayo
JF-Expert Member
- Jan 27, 2015
- 6,287
- 4,738
Kwa mujibu wa sheria ya karma, hakuna laana yoyote inayoweza kumpata mtu aliyenunua mali kihalali hata kama mali hiyo ni ya wizi au dhuluma, ila laana humpata yule aliyedhulumu, hivyo kwa case ya containers za Makando, laana itamhusu anayetoza kodi vitu vya bure vya masikini waalimu wetu!.
P.
Hii imefafanuliwa vizuri Sana ktk Mada zinazohusiana na hili jambo mkuu, taratibu na sheria ambazo bunge letu tukufu liltunga ndo zinazofanya kodi idaiwe. Ushauri bunge linaanza tarehe ngoja wapeleke hoja ya dharula kuhusu hivyo vifaa tuirekebishe haraka tumpe akagawe shuleni. Fuata taratibu la sivyo utapata ngiri Sana.Mambo mengine yanatia kinyaa!
Makonda ali-mobilize watu(diaspora) kuchangia samani za shule. Wito ukaitikiwa kwa kuchangia na kuzisafirisha hadi Dar. Aliye-mobilise ni Makonda, ametumiwa Makonda akazikabidhi katika shule za serikali.
Suala hapa kama serikali ina wasiwasi na nia hii ya Makonda basi ifuatilie konteina moja moja kuhakikisha mizigo yote inagawiwa mashuleni na si vinginevyo!
Mara nyingi mizigo mingi inayotumwa kutoka nje kwenda kwenye taasisi za serikali jina la mtu wa kufuatilia (Attn. so and so) huandikwa! Hii inakuwa rahisi kwa mtumaji kupata uthibitisho wa mizigo kufika!
Sasa ni nini watu wenye PhD kinawachanganya hapa?
How sure u are Makonda ana nia njema? Yan ww umejuaje kua ana nia njema? Niko interested kutaka kujua.Kwanza kwa mlio walimu mtanielewa ninaposema waziri kakurupuka wala hazijui changamoto za elimu
ukisikiliza kwa umakini kwenye hotuba yake ya juzi utagundua kabisa aelewi anachokiongea...
Anaongelea maswala ya elimu bure kitu ambacho ni nje kabisa ya mada ya makontena
swala hapa ni vifaa kwa ajiri ya kusaidia elimu ya dsm ambayo ina changamoto nyingi ikiwa na mrundikano wa wanafunzi na mambo kibao
Makonda inawezekana kuna sehemu alikosea katika mchakato huo lakini serikali walitakiwa kuwa wajanja wangeruhusu kwanza vitu viingie ndio waanze kuvimonitor wapate ushahidi wa kutosha ndio waje kumtuhumu.
matokeo yake wananchi nao wameyabeba na kusahau watoto wao ndio wanakaa chini milele
mimi niko na ushahidi kabisa nilienda shule moja na taasisi fulani kutoa msaada wa computer lakini unakuta walimu stafu viti tu vya kukalia haviwatoshi hii ni aibu kama mwalimu hana kiti stafu mwanafunzi je darasani itakuwaje?
tukiweka siasa pembeni Makonda yupo sahihi kabisa na ana nia njema ingawa anaweza kuwa kafanya makosa kutumia jina lake kwa ushauri mbovu wa watendaji waliopo chini yake lakini naamini tatizo letu la elimu ni kubwa mno kuliko jina la makonda kuwa kwenye makontenana hili swala tunalibabe kishabiki sana kama kawaida yetu...
kwamba mimi ni chadema Gambo akifiwa na mzazi wake nashangilia, mimi ni ccm Sugu akipata msiba nashangilia upuuzi mtupu.
Hivi waziri anavipiga mnada vitu vya shule za dsm watu tunashangilia leo halafu kesho jangwani secondary inakuwa ya mwisho tunaanza kumponda makonda ...
Hivi vitu vikinunuliwa na wafanya biashara sisi wananchi wa kawaida tutafaidika vipi direct kama ambavyo tungeviona kwenye shule zetu? namimi naongeza na alaaniwe kabisa atakae vinunua.
"Form four wanakaribia pia kuanza mtihani msisahau kuleta mrejesho hapa wa shule za umma"
Makosa ya Makonda:-Mkiendekezi hii tabia, ipo siku mtu ataingiza mizigo yake kwa style hii ambayo kwanza hakuna mwenye uhakika kama vifaa hivyo vyote kweli vinawafia walengwa au ni janja tu.
Na kwa jinsi jambo hili linavyokwenda mpaka sasa, ni dhahiri unahitajika uchunguzi wajulikane ni kina nani walituma vifaa hivyo na shule gani hasa zilizolengwa kupewa hiyo misaada.
Hili jambo lina ukakasi unaohitaji uchunguzi maana huenda si kila kifaa kitaenda kutolewa kama msaada.
Na nikwambie tu, vifaa hivyo vingekuwa vimeingizwa na mtu kutoka upinzani, vingeshapigwa mnada siku nyingi tena huyo Makonda angeweza hata kuingilia viuzwe haraka japo kisheria hahusiki.
Tena namshauri waziri Mpango awe makini na kama kuna mtu atamshinikiza atoe msamaha,basi ahakikishe mtu huyo anatoa agizo kwa njia ya maandishi vinginevyo ajiuzulu kwani ipo siku anaweza kuja kujikuta anawajibika kwa matumizi mabaya ya madaraka na kuikosesha serikali mapato.
Wanasiasa sio watu, hawachelewi kukugeuka.
Tukumbuke sheria tunatunga wenyewe na kuzipitisha kwa mbwembwe.
Swali: Iweje leo tuzione chungu?
Tunavuna tulichopanda.
Hapana mtazoea, haki lazima tuisimamia changie mlipe kodi, siasa mwaka kesho kutwa, hapa kodi tuBusara inayotumika kusamehe wakwepa kodi ,itumike pia kwenye makontena haya ili walimu wasiendelee kukaa chini na kukalia viti vichafu.
Kama tatizo ni sheria hata mikutano ya vyama vya siasa ipo kikatiba lakini imepigwa marufuku na watu wameelewa
Sent using Jamii Forums mobile app
DAH U MADE MY DAYHilo dua lilikwenda kwa Mungu kwa jina gani?
Una akili sanaMkuu Techinically umeandika jambo zito na lenye kuhitaji akili zinaoongozwa na utaifa kwanza.
Ni kweli kabisa RC alikosea kwa kutotengeneza mazingira ya kuhakikisha huo mzigo unakombolewa bandarini, kabla hata meli haijaondoka kutoka huko ilipotoka.
Tunafanya masikhara kwenye mambo ya maana na tunapenda kujifanya tupo makini kwenye mambo ya kipuuzi. Tumeukumbatia ujinga mpaka tunashindwa kutofautisha kati ya akili zenye faida na ujinga wenyewe.
Hizo furniture zingeleta kitu fulani kipya kwenye shule za Dar lakini kama kawaida siasa za kipumbavu ndio zinapewa nafasi.
Yaani muagize nje wanufaike wa nje halafu huku msilipe kodi, raisi alichasema Tanzania ya viwanda hakusema maana yake muagize viti nje alimaanisha muwape mafundi wa ndani ajira humuhumu, walipe kodi humhumu, mgawanjo wa hayo mapato yafanyike humhumu nchi isonge. Msaidieni harambee mlipe kodi, tuwape mameza yenu. Hamtaki tunauza na laana hatupati hata mmu hawatugusi. Manake wengine wameenda hija saudia, wengine juzijuzi Jerusalem kwa hiyo hizo laana zitakuwa Zabibu kwa watakanunua tu. Akilaani kule meza yako inajaa Zabibu zingine unawapa wenzio. Msihofu kabisa nunua meza za makonda tujenge nchi yetu.Jamani eh. Kodi nayo ikilipwa si itaingia uko uko katika kusaidia elimu, kununua madawa hospitalini, kujenga miundombinu n.k sasa kwanini isilipwe ili ata watu wasio wakazi wa Dar es Salaam wafaidike
Sent from my SM-G610F using Tapatalk
Yaani nyie msihangaike kodi italipwa, chapeni kazi mlipe kodi tumefunga hayo.hivi vitu ni vya Hotel yake ya Mwanza mambo ya kusema eti ni vifaa vya shule ni uongo ingekuwa kweli ni siku nyingi sana angekuwa amevitoa
Sent using Jamii Forums mobile app