Pre GE2025 Makonda: Tutawapa kila kitu CHADEMA lakini kura hawatopata

Pre GE2025 Makonda: Tutawapa kila kitu CHADEMA lakini kura hawatopata

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
"Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) walitegemea tutawaletea Polisi na tutawapiga mabomu, nimwambie kaka yangu Freeman Mbowe awamu hii imebadilika, tutawapa kila kitu lakini kura hamtapata.

Wako bararani wanatembea, wanazurura wanaona raha na kwa kuwa wengine ni wagonjwa tumewapelekea magari ya wagonjwa Ambulance ili kutoa msaada itakapotokea dharura." - Katibu wa NEC Itikadi, Uenezi na Mafunzo Paul Makonda akiwa Makuyuni Monduli Arusha

Ameongeza kuwa "Wakati wao wanaandamana Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameelekea nchini Indonesia kwenye vikao vya Kimataifa kutafuta fedha za miradi ya maendeleo."

Source - CloudsTv
Tutawapa kila kitu maana yake nini?
Mimi kwa ufahamu wangu haki wanayopata Chadema na vyama vingine vyote ikiwemo CCM vinatokana na katiba, sheria,kanuni na miongozo tuliojiwekea wpte kama nchi.
Sasa huyu bwana division 0 aliekosa hata D mbili haya kayatoa wapi?...ila CCM safari hii mmepatikana
 
.... kasoro kura. Hii kauli ni fupi lakini imebeba ujumbe mzito ndani yake, kwamba wao ndio wenye maamuzi nani ashinde kwa kura ngapi, na yupi afuatie kwa kura ngapi.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app

Wamejimilikisha nchi ...... CCM ni sawa na Mkoloni.

Wakoloni walifikiri watatawala milele ..... same as hawa Wakoloni wetu weusi!!
 
Back
Top Bottom